Je, Hatuna Wanawake wa kutosha kukidhi 50/50 au kuna kosa?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kila nipatapo fursa, huwa naendeleza zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" ambazo zina lengo la kukuza uzalendo na kulisaidia taifa letu, kusaidia nchi yetu, kusaidia serikali yetu na kusaidia viongozi wetu waweze kutuongoza vizuri kwa kuangazia maeneo yenye changamoto ili zitatuliwe. Makala ya leo ni hoja na swali.

Hoja ni "Kufanya Kosa Si Kosa, Kosa Kurudia Kosa", hoja hii inakuja kwasababu hatuongozwi na malaika, tunaongozwa na binadamu, katika kuongoza huko, huweza kufanyika makosa ya hapa na pale. Hivyo hata kukifanyika makosa, kufanya kosa sii kosa, kosa ni kurudia kosa.

Hoja hii inakuja kwa tangu rais Samia ashike usukani, juzi ndio amefanya uteuzi wake mkubwa wa kwanza wa viongozi wengi kwa mpigo. Kwenye uteuzi huu, kuna idadi ndogo ya wanawake, na ndipo kwenye swali, "Jee ni kweli Tanzania hatuna wanawake wa kutosha wenye sifa za uongozi kustahili uteuzi?. Kwa maoni yangu japo uteuzi huu una walakin ya idadi ndogo ya wanawake, yaani gender imbalance, Rais Samia hajafanya kosa, bali akirudia idadi ndogo hivi kwa ma DC, RAS, DED na ma DAS, then, litakuwa ni kosa!.

Lazima tukubali, tukatae, kwenye gender balance kule nyuma, kuna makosa yalifanyika. Sasa ni jukumu letu sisi tuliobahatika kuyaona makosa hayo ya nyuma, ambayo Rais Samia ameyarithi, tumsaidie, rais Samia, kwa kuyaangazia makosa hayo, ili rais Samia asiyarudie makosa ya nyuma kwa spirit ile ile ya kufanya kosa sii kosa, kosa kurudia kosa, kwenye uteuzi wa maRC kuna kosa la gender balance, kwa vile sasa wanakuja ma RAS, wanakuja ma DED, wanakuja ma DC, wanakuja ma DAS, tumsaidie Tanzanite Lady wetu, Mama Samia, huko mbele, tusirudie makosa!.

Kabla haujasoma hoja za bandiko hili, naomba nikupe homework ndogo ya kusoma bandiko langu hili

Kwenye bandiko hilo nilisema
Kwa vile Mama Samia amejitanabaisha wazi yeye ni kama JPM, kwenye upande wa uteuzi wa JPM, we had gender problem, Mama Samia, asiiendeleze.

Uteuzi wa JPM, Kwa mfano idadi ya mawaziri wanawake ni 4 tu kati ya 19, hii ni asilimia 21%. wanaume ni asilimia 79%. Kwenye Baraza la Mawaziri la Samia, lina mawaziri 25, wanawake ni 6 ambao ni asilimia 24% wanaume 19 ambao ni asilimia 76%. Hivyo hapa gender imbalance imeendelezwa!.

Kwenye uteuzi wa Wakuu wa Mikoa, kati ya wakuu wa mikoa 26 wa Magufuli, wanawake ni 4 tu ambao ni asilimia 15% wakati wanaume ni 21 ambao ni asilimia 85%!. Sasa rais Samia anapita mule mule, alikopita JPM kwenye uteuzi wa wakuu wa mikoa wa Samia ameteuwa ma RC wanawake 4 tu kati ya ma RC 25, hii ni asilimia 16% ndio wanawake na wakati wanaume ni 21 ambao wanafanya asilimia 84%!.

Kwenye wakuu wa wilaya, kati ya wakuu wa wilaya 134 wa Magufuli, wanawake ni 25 tu ambao ni asilimia 18%, wakati wanaume ni 109 ambao ni asilimia 82%. Na kwa upande wa Wakurugenzi, kati ya wakurugenzi wa halmashauri na wilaya 185 wa Magufuli, wanawake ni 33 tu!, ambao ni asilimia 17% tuu, wanaume asilimia 83%.

Kwa trend reading, kama ni kweli kabisa Samia ni kama Magufuli, then you know what to expect, kwenye uteuzi wa ma DC na Wakurugenzi. Jameni hili ni kosa, lisiachwe liendelee!, ili tufikie gender balance ya 50/50.

Kwa vile hatukumpangia JPM nini cha kufanya, hivyo nilisisitiza tangu mwanzo, hata Mama Samia, tusimpangie, lakini huku kutompangia hakumaanishi tunyamaze tuu, pale tunapoona mapungufu mahali, au mambo yanakwenda ndivyo sivyo, tunawajibu wa kumshauri ili kumsaidia.

Katika safari ya kuelekea gender balance ya 50/50 katika uongozi, mimi siamini kuwa Tanzania hatuna wanawake wa kutosha hadi uteuzi wa wanawake uwe that low!.

Kwa maoni yangu, naamini uteuzi huu wa ma RC ni mama Samia, ameendelea kubeba some luggages na baggages za mtangulizi wake. Hilo ni kosa!. Kufanya kosa si kosa, kosa kurudia kosa!. JPM alifanya kosa kwenye gender balance.

Gender balance kwenye baraza la mawaziri hatuwezi kulaumu, kwasababu ili mtu uwe waziri ni lazima kwanza uwe mbunge, ikitokea hakuna wanawake wa kutosha kujaza nafasi za kufikia kiwango cha 50/50, hili litaeleweka, kwasababu Mama Samia, ameingia na kuwakuta wabunge tayari wapo, ikitokea wabunge wote hadi wa viti maalum, hawana sifa za uwaziri, hatuwezi kulaumu, kwasababu sio kosa lake. Huwezi tuu kujiteulia watu hawana sifa ili tuu kutimiza gender balance. Lakini kwenye ma RC, ma DC , ma RAS, ma DAS ns na DED, yaani Wakurugenzi, haiwezekani Tanzania ndani ya hii milioni 60, wakakosekana wanawake wenye sifa.
Hitimisho
Naamini rais Samia, kaletewa majina na kuongeza wachache tuu, hivyo sasa tunamuomba, kwenye ma DC, ma RAS, ma DED na ma DAS, awatendee haki wanawake wa Tanzania.

Nisimalize bila kumpongeza Mama Samia kwanza kwa ku heal the nation kwa kutenda haki, na pili ni pongezi kwa kuyaishi maneno yake ya kuteua yoyote hata kutoka upinzani.

Tanzania ni yetu sote,
Mungu mbariki Mama Samia.
Mungu ibariki Tanzania.

Paskali
Update
Hoja za bandiko hili, zimejibiwa jana na Rais, Mama Samia wakati akiapisha majaji, amesema ataongeza nafasi za wanawake kwenye teuzi zote zijazo

Hii ni habari njema, hivyo mabandiko kama haya, yanasaidia.

P
 
CCM iondoke kwanza ndio nchi hii itaweza kufanya mabadiliko ya maana kuanzia kwenye katiba na kwenye maeneo mengine.

Kwenye teuzi, Mama Samia hana jipya na anaharibu tu na hata haya mambo ya wanawake kupewa nafasi hayana maana.

Covid 19 wamethibitisha wanawake ni mzigo hivyo hawastahil kubebwa.
 
Japo wametumia Neno kuteua bali lilichofanyika ni kubadilisha tu vituo vya kazi! Hakuna jipya! Kwa hio kwa mtazamo wangu hajafanya chochote kile cha kushangaza, the same kwa DCs huenda akafanya hivyo hivyo na ni kwa sababu huwezi kuweka team mpya yote, huenda hapo mbeleni akabadilisha mdogo mdogo.

Kama Jiwe mlimpa muda wa kutupoteza na huyu pia tumpe muda tube kuona hapo mbeleni
 
Nashangaa nikiona mwaume naye anahangaika na mambo ya ajabu ya 50/50 na namuona kichwani kuna tatizo haswa, hivi Tanzania haina maendeleo sababu hatuna 50/50? kwanini asiteue wanawake wote kama wanauwezo? mkimaliza mambo ya 50/50 mtahamia kwenye dini, makabila, ukanda, mikoa, wilaya, kata, vijiji na koo, mambo ya kijinga sn, mbona hakuna 50/50 kwenye kutoa matumizi nyumbani? wacheni Rais afanye kazi yake tutakuja kumuuliza 2025
 
Kwanza teuzi/uhamisho ni gharama kubwa sn kwa mtu mmoja siyo chini ya milioni 20 ambayo ni madarasa 2.
 
Adui wa mwanamke hajawai kuwa mwanaume hata siku moja Adui wa mwanamke ni mwanamke mwezie

Kingine hyo 50/50 ni uongo tu hyo sera haitekelezeki si kwa Tanzania tu Dunia nzima haiwezekani ata walioleta sera hii wameshindwa kuitekeleza kwa vitendo.
 
Wanawake wenyewe hawaaminiani hao wanaume watawaamini saa ngapi? inaonekana mfumo dume umeshaingia kwenye vichwa vya wanawake, nao wanafikiria kama wanaume hata wakipewa nafasi wanaangalia kwanza wanaume.
 
Nilidhani ingelikuwa busara kuzungumzia ubora wa waliyoteuliwa kuliko kuzungumzia habari ya usawa wa kijinsia , kwani wanaenda kuzaa huko ?[emoji12]

Hata kilichompa shavu Madam wenda kikawa ni weredi na utulivu wake wa kiakili kiasi cha kuaminika kuwa anaweza akamfaa MzeeBaba na siyo jinsia yake .

Nadhani kilichotazamwa ni weredi na siyo gender balance mkuu #Mayala .
 
Huwa tunahangaika na vitu vidogo vidogo ili mradi tuonekane tunaenda sawa na dunia, swala la teuzi za rais halijawahi oumwacha kiongozi yeyote salama, wapo walioshutimiwa kuteua kisinda, kirafiki au kindugu waliporoka.
Cha muhimu walioteuliwa wawe na uwezo bila kujali jinsia ila tukitaka kufanya gender balance hatutafika popote, kama wanawake wana uwezo wateuliwe hata asilimia 90 lakini tusiteue ili mradi tuonekane rumefanya teuzi kukishi haja.
 
Kilochofanyika sio uteuzi ni uhamisho wa vituo vya kazi.
Lakini pia suala la 50/50 linalenga kumridhisha nani? Mfumo wa dunia wenyewe hata kutoka maandiko matakatifu hakuna mahali wanawake na wanaume wanawekwa kwenye mizani sawa. Imeandikwa mwanamke atakuwa msaidizi. Hata kuumbwa tu amekuwa next tena baada ya kuona mwanaume ni mpweke (kwa wanao amini maandiko ya Biblia). Sasa hii force against nature mjue tu haitakaa iwezekane itabaki kinadharia tu.

Na angalia hata trend ya hizo asilimia ulizoweka. Kila mahali kuna angalau 80/20 mpaka 85/15. Hii ikupe ujumbe.
Tuangalie masuala mengine ya msingi nchi iende mbele sio hizi porojo za wanaharakati.
 
Mimi nataka mchakato wa Katiba Mpya urejeshwe, na hayo mambo yote unayo yalalamikia hapa yawepo kikatiba! Badala ya kuendelea na huu utaratibu wa kizamani, wa kuzienzi fikra za Mwenyekiti.
 
wapo wengi , tuanzie 50/50 kwa wabeba zege, TANESCO hasa wapanda nguzo, makondakta, walinzi hasa mgambo wa jiji, wachimba mitaronwakisha kuwa wengi tuende taratibu kwenye teuzi.
 
Daaa! Mungu amsaidie mama yetu kwa kweli.
  • Akibakiza aliowakuta kutoka kwa JPM ni kosaaa!
  • Akiteua wapya nalo ni kosaaa!
Tumsubiri mama 2025 ndipo atakuwa na timu yake. Hapo ndipo auliizwe masuala ya jinsia nk

Kwasasa muacheni mama yetu kipenzi Mhe. Samia Suluhu Hassan achape kazi kwanza mambo ni mengi na muda ni mchache.

Kazi Inaendelea kwa kishindo.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…