Uchaguzi 2020 Je, hii ndiyo sababu ya NEC kutochapisha fomu za wagombea Urais kwa "Alphabetical order"?

Uchaguzi 2020 Je, hii ndiyo sababu ya NEC kutochapisha fomu za wagombea Urais kwa "Alphabetical order"?

Kutakuwa na wakala wa CCM anayewatolea macho wapiga kura ambao ni wanachama wa CCM. Ukimchagua Lissu lazima utaonekana tu unavyomtafuta kule chini. Hivyo mwanaccm itambidi apige tu pale juu kama akishindwa kujilipua.

Nahisi washaambiwa OLE WAO. ...
 
Hivi hili suala mbona sielewi. Yaani mtu umepanga kwenda kumchagua Lissu, halafu unafika kituoni unamkuta Magufuli amewekwa picha yake wa kwanza. Basi tu kwasababu Magufuli yupo wa kwanza unaghairi kumchagua Lissu, ambaye picha yake ipo mwisho, unaweka tick kwa Magufuli. Like seriously.
Tupe sababu moja kuu ya kutofuata mpangilio wa alfabeti kama ilivyo kawaida.
 
Uxuri mgombea wangu wa chauma nimeona alipo nikifika sina cha kukawia

sent from HUAWEI
Una undugu na "delicious" au Elton John!?
Hii "uxuri" ndio nini?
Halafu wewe ndio unakuwa wa kwanza kuandika/kusema, "ooh Chadema wanasapoti ushoga"!
 
Nape alikuwa sahihi alipodukuliwa simu yake alikuwa akisema tuna Rais mshamba.
Huu ni ushamba wa hali ya juu sana kudhani CCM wakikaa pale juu basi watu hawataona wengine au? Ushamba tuu.
Tuko kwenye kizazi ambacho wasiojua kusoma na kuandika wamebaki wachache sana kama siyo kuisha kabisa.
Sasa hivi mtu anaenda kupiga kura akijua anaenda kuchinja, hata kama wageuzie karatasi Lissu awe ukurasa wa pili tutamtafuta tuu
 
na sisi tunasema usihangaike we check jina la mwisho tu. Wamempiga chura teke.
ila haya mambo ya sijui wepesi wa kuonekana yanafanya waTz tuonekane akili zetu sio,hivi kabisa umesikiliza sera,umefanya maamuzi,halafu unaenda pale unatiki Jiwe katili kwa sababu ya uvivu wa kumtafuta Lissu. Duuh
 
Na sisi tunawaambia usihangaike kusoma majina, angalia wa mwisho kabisa chini ya karatasi
2020-10-24_7-53-00 RDDD-.gif
 
Kama ni kweli nia ilikuwa kumpoteza Lissu basi huyo aliyetoa wazo hilo hana kazi, angemuweka katikati hapo ingewapa shida mtu kutafuta na macho yenyewe haya ya siku hizi unaona kama huoni ingekuwa shida ila hii ya mwisho unaambiwa yule wa mwisho ndio mwenyewe, rahisi sana. kawaida mtu ukimpa karatasi anataka kuona wa juu halafu sababu wa Tz tunapenda umbea tunapenda kuona nani wa mwisho huku..
 
"Wewe siku ya kupiga kura wala usihangaike kuangalia majina yote ya wagombea. CCM tupo juu kabisa ya wagombea wote, utamuona Mama Samia Suluhu, utamuona baba mmoja ana kaupara kazurikazuri hivi. Weka tiki hapo. Usihangaike kuangalia wagombea wengine, wale hawakuhusu. Angalia jina la juu ambapo CCM tupo mwanzo"
Na kwa masikitiko makubwa nchi hii bado inao watu wengi wajinga kabisa wanaosikiliza upuuzi kama huo na kufanya walivyoelekezwa.

Halafu tunasema kama taifa tunaendelea bado tukiwa na watu wajinga wengi kiasi hicho!
 
Tofauti na miaka mingine ya Uchaguzi Mkuu, mwaka huu Tume ya Uchaguzi Tanzania(NEC) imechapisha form ya kupigia kura kwa ngazi ya Urais wa JMT isiyo na mfumo rasmi wa mpangilio wa alfabeti.

Hii ni tofauti na form ya Urais wa Zanzibar chini ya ZEC ambayo imechapishwa kwa kufuata alfabeti. Form ya ngazi za wabunge na madiwani pia imefuata mtiririko huohuo.

Hii inaweza kuonekana jambo dogo machoni pa wengi, lakini katika fitna na mbinu za ushindi, Chama Cha Mapinduzi hapa kimecheza karata mahiri kwani mshindani na mpinzani mkubwa wa Mgombea Urais wa CCM ndugu Lissu amewekwa chini kabisa kwenye mpangilio wa Wagombea wote wa Urais.

Na kwa kuthibitisha hilo, mgombea Urais wa CCM akiwa Hedaru-Same amenukuliwa akisema:

"Wewe siku ya kupiga kura wala usihangaike kuangalia majina yote ya wagombea. CCM tupo juu kabisa ya wagombea wote, utamuona Mama Samia Suluhu, utamuona baba mmoja ana kaupara kazurikazuri hivi. Weka tiki hapo. Usihangaike kuangalia wagombea wengine, wale hawakuhusu. Angalia jina la juu ambapo CCM tupo mwanzo"

View attachment 1607811

Akaenda mbali zaidi akaongezea

View attachment 1607812

"Watu wa Hedaru, huu ndio mfano wa karatasi ya kupigia kura. Mimi na Mama Samia Suluhu tupo mwanzo kabisa kwenye karatasi ya kupigia kura. Ukifika tu unaweka tiki kwangu, unachukua kwa Mbunge Mathayo na diwani. Hayo majina mengine huko usiangalie, tena kama majina ya huko chini usiangalie kabisa, unaweza kupofuka"

Hii ni mbinu nzuri ya ushindi, kuna maeneo watu hawajibiidishi na kutafuta jina la mgombea mshindani wa CCM, watatazama jina la mwanzo na kuweka tiki.

Na ili kuiboresha mbinu yao, sasa CHAMA CHA MAPINDUZI kimetoa karatasi ya mfano wa kupigia kura na mshindani wao mkuu amekatwa na haonekani, hii ni hatua ya mwanzo ya "kumuondoa" mgombea mwenye ushindani na chama chao na NEC inawajibika kutoa tamko kama "karatasi ya Mfano" ya kupigia kura inapaswa kuhaririwa kwa maslahi ya chama kimoja cha siasa, maana kutoa "karatasi ya mfano" isiyofanana na "karatasi rasmi" kwa kumkata mmoja wa wagombea inaleta maswali mengi.

Hii ni wiki ya lala salama, tunapohubiri amani, tukumbuke kuwa AMANI NI ZAO LA HAKI...Tutendeane haki ili kudumisha amani ya nchi.​

View attachment 1606918
Mbinu za ushindi bwashee
 
Wamekosea sana kumuweka JPM pamoja na hawa wasio hata na chembe ya uzalendo. Wamekosea sana

Sijui unawezaje kupima uzalendo wa mtu usiyemjua vizuri. Wote wawili Lissu na JPM huwajui zaidi ya kuwasikia tu jinsi wanavojieleza au kuelezwa!! Ninyi ndio pia hupima imani au dhambi za watu kwa maneno na matendo yao - huku hamjui mioyo yao. Uzalendo ni jambo lisilopimika!! Uhalifu ndio hupimika. Ingekuwa bora ukataja uhalifu wa Lissu na kumuita ni mhalifu.

Nchi hii ina tatizo la ujinga zaidi kuliko njaa na maradhi!! Wewe ni kielelezo cha ujinga.
 
Back
Top Bottom