Je, hili gonjwa lililompata mshikaji wetu ni karma au uchawi?

Je, hili gonjwa lililompata mshikaji wetu ni karma au uchawi?

Hauzijui nyonyo? Nyonyo ni zao maarufu Tanzania, hutumika pia kutibu malaria.
Oh unazungumzia yale majani fulani ambayo ina vimatunda kama vya miba miba hivi mkuu? Au nimekosea kuifananisha
 
Akili za kuambiwa changanya na zako usikute huyo jamaa ambaye amechukuliwa mke ni wewe kwahiyo jamaa kaamua kueneza uongo kwamba jogoo hasimami ili ufurahi usimfuatilie tena huku akiendelea kufaidi tunda la Ex wife wako
 
Akili za kuambiwa changanya na zako usikute huyo jamaa ambaye amechukuliwa mke ni wewe kwahiyo jamaa kaamua kueneza uongo kwamba jogoo hasimami ili ufurahi usimfuatilie tena huku akiendelea kufaidi tunda la Ex wife wako
Hapana mkuu, huyo aliechukuliwa mke sio mimi. Mimi nina mke na watoto wawili mkuu.
 
Jina jingine ni mbarika, kwahiyo wewe mpaka unazeeka unajua vinaitwa vimatunda fulani hivi kama vya miba miba!
Ya mkuu, ki ukweli huu mti sikuwahi kuufatilia sana, ndomaana hata uliponambia jina lake sikufahamu. Shukran kwa mchango wako uliotukuka mkuu.
 
Mchumba au Mke wa mtu ni sumu na sumu inazidi hasa pale unapotembea nae ukijua kbs huyu ni mchumba au mke was mtu utagundulika tu. Tujiepushe na ambavyo sio vya kwetu
 
Mchumba au Mke wa mtu ni sumu na sumu inazidi hasa pale unapotembea nae ukijua kbs huyu ni mchumba au mke was mtu utagundulika tu. Tujiepushe na ambavyo sio vya kwetu
Ya ni kweli mkuu, ndio maana waswahili walisema "mke wa mtu ni sumu".
 
Habari zenu wana JF wenzangu.. Ama baada ya salam naomba nijielekeze kwenye mada husika. Kuna rafiki yang mmoja anaitwa J (nimekatiza jina lake kwa sababu ya heshima na usalama wake). Sasa huyo J na yeye anamshikaji wake ambae walipanga nae nyumba 1 mitaa fulani (jina kapuni) J aliowa mwaka uliyopita, akamleta mkewe hapa jozi ili waishi nae pamoja. Kabla hata miezi 6 ya ndoa haijaisha, J akaanza kulalamika kuwa mkewe anaonekana hana uaminifu na ndoa yao. Kuja kuchunguza tukagundua kama kuna ukweli fulani, ikabidi mimi na yule rafiki yake na J tuwe kama wasuluhishi wa ugomvi wao mara kwa mara. J akaona hali inazidi kuwa mbaya ikabidi ampe talaka mkewe kwa kushauriwa na yule rafiki yake mungine, na kumrudisha nyumbani. Kama walivyosema waswahili kuwa "kikulacho kipo nguoni mwako" baada ya miezi miwili ya talaka, yule rafiki yake na J akamchumbia yule aliekuwa mke wa J kimya kimya, na kufunga nae ndoa tena kimya kimya. Waswahili walishasema kuwa "la kuvunda halina ubani". Baada ya ndoa kabla jamaa hajamfikisha hapa huyo mkewe ambae alikuwa shemeji yake, taarifa zikaanza kusambaa na kutufikia mimi na J mwenyewe. J alipomuuliza jamaa, akakataa akisema eti huo ni uzushi tu na kwamba kamwe hawezi kufanya uchafu kama huo katika maisha yake. Ghafla jamaa akahama nyumba mpaka mtaa, yani akahamia mbali na mahali ambapo itakuwa ngumu kuonekana. Baada ya kuhama, mara mkewe akafika, kuchunguza ikaonekana kweli jamaa kamuowa shemeji yake aliekuwa mke wa J. Jamaa siku ya kwanza katwanga kinu cha mkewe kwa masham sham na furaha tele kama kawaida, siku ya pili pia mchana na usiku inasemekana katwanga fresh, ya tatu mtwangio wa jamaa ukagoma, yani ukalegea ukawa hausimami hata ukiubust na jeki. Jamaa amejitahidi kwa kadri awezavyo kurudisha uhai wa mtwangio wake imeshindikana. Sasa jamaa ameanza kulalamika kwa watu, kuwa eti aliekuwa rafiki yake kipenzi ndugu J amemroga ili kumkomoa, na kwamba atafanya kila awezalo kuujua ukweli na kulipiza kisasi kwa yeyote aliemsabishia yeye fedheha mbele ya mkewe. Ila wenye kujua kinachoendelea tunahisi hii inaweza kuwa ni karma ya kujaribu kupindua meza ya mwenzake (J) na kwamba karma hiyo itamtafuna hadi aende kumuangukia muhusika, na kuomba msamaha. Sasa wana JF wenzangu, nyinyi hili swala mnalionaje? Ni karma hii, au kuna uchawi umetumika hapo? Sababu J mwenyewe nikimuuliza, anasema binafsi hafahamu hata huo uchawi huwa unaptikana vipi na unatumikaje. So wengi hatuelewi zaidi nini kinaendelea mpaka jamaa kuwa vile. Karibuni ndugu kwa michango yenu. Ushauri: Wabongo wenzangu wa kiume tuachane tamaa, Mungu kaumba wanawake wengi kwa ajili yetu, kwahiyo tujiepushe kuchukuliana wanawake au wake wenyewe kwa wenyewe.
Tego hilo.... na hakuna wakulitoa zaid ya bwana J. Jamaa atahangaika dunia nzima halitatoka had ayamalize na bwana J.
 
Back
Top Bottom