Je, hili gonjwa lililompata mshikaji wetu ni karma au uchawi?

Je, hili gonjwa lililompata mshikaji wetu ni karma au uchawi?

Tego hilo.... na hakuna wakulitoa zaid ya bwana J. Jamaa atahangaika dunia nzima halitatoka had ayamalize na bwana J.
Jamaa tatizo lake anashindwa kuja kum face bwana J moja kwa moja ili amuombe msamaha na yaishe. Badala yake amekuwa akipayuka payuka na kutema vitisho kuwa akija gundua kuwa kuna mkono wa J basi na yeye atalipiza kisasi, nahisi hapo ndo jamaa anapoharibu na kuharibikiwa zaidi.
 
Habari zenu wana JF wenzangu.. Ama baada ya salam naomba nijielekeze kwenye mada husika. Kuna rafiki yang mmoja anaitwa J (nimekatiza jina lake kwa sababu ya heshima na usalama wake). Sasa huyo J na yeye anamshikaji wake ambae walipanga nae nyumba 1 mitaa fulani (jina kapuni) J aliowa mwaka uliyopita, akamleta mkewe hapa jozi ili waishi nae pamoja. Kabla hata miezi 6 ya ndoa haijaisha, J akaanza kulalamika kuwa mkewe anaonekana hana uaminifu na ndoa yao. Kuja kuchunguza tukagundua kama kuna ukweli fulani, ikabidi mimi na yule rafiki yake na J tuwe kama wasuluhishi wa ugomvi wao mara kwa mara. J akaona hali inazidi kuwa mbaya ikabidi ampe talaka mkewe kwa kushauriwa na yule rafiki yake mungine, na kumrudisha nyumbani. Kama walivyosema waswahili kuwa "kikulacho kipo nguoni mwako" baada ya miezi miwili ya talaka, yule rafiki yake na J akamchumbia yule aliekuwa mke wa J kimya kimya, na kufunga nae ndoa tena kimya kimya. Waswahili walishasema kuwa "la kuvunda halina ubani". Baada ya ndoa kabla jamaa hajamfikisha hapa huyo mkewe ambae alikuwa shemeji yake, taarifa zikaanza kusambaa na kutufikia mimi na J mwenyewe. J alipomuuliza jamaa, akakataa akisema eti huo ni uzushi tu na kwamba kamwe hawezi kufanya uchafu kama huo katika maisha yake. Ghafla jamaa akahama nyumba mpaka mtaa, yani akahamia mbali na mahali ambapo itakuwa ngumu kuonekana. Baada ya kuhama, mara mkewe akafika, kuchunguza ikaonekana kweli jamaa kamuowa shemeji yake aliekuwa mke wa J. Jamaa siku ya kwanza katwanga kinu cha mkewe kwa masham sham na furaha tele kama kawaida, siku ya pili pia mchana na usiku inasemekana katwanga fresh, ya tatu mtwangio wa jamaa ukagoma, yani ukalegea ukawa hausimami hata ukiubust na jeki. Jamaa amejitahidi kwa kadri awezavyo kurudisha uhai wa mtwangio wake imeshindikana. Sasa jamaa ameanza kulalamika kwa watu, kuwa eti aliekuwa rafiki yake kipenzi ndugu J amemroga ili kumkomoa, na kwamba atafanya kila awezalo kuujua ukweli na kulipiza kisasi kwa yeyote aliemsabishia yeye fedheha mbele ya mkewe. Ila wenye kujua kinachoendelea tunahisi hii inaweza kuwa ni karma ya kujaribu kupindua meza ya mwenzake (J) na kwamba karma hiyo itamtafuna hadi aende kumuangukia muhusika, na kuomba msamaha. Sasa wana JF wenzangu, nyinyi hili swala mnalionaje? Ni karma hii, au kuna uchawi umetumika hapo? Sababu J mwenyewe nikimuuliza, anasema binafsi hafahamu hata huo uchawi huwa unaptikana vipi na unatumikaje. So wengi hatuelewi zaidi nini kinaendelea mpaka jamaa kuwa vile. Karibuni ndugu kwa michango yenu. Ushauri: Wabongo wenzangu wa kiume tuachane tamaa, Mungu kaumba wanawake wengi kwa ajili yetu, kwahiyo tujiepushe kuchukuliana wanawake au wake wenyewe kwa wenyewe.
Mwambie aende Tunduru Barabara ya kwenda Namtumbo vijijini vya jiran Kuna wajuz wa hyo kitu jamaa alipigwa hyo na mchepuko alikuwa akienda kw mke wake goma usingiz mzito akirud kwa mchepuko hatar kama kanywa red bull jamaa akastuka wajuz wa hayo Mambo wakasaidia Sasa yupo pouwa...
 
Apige namba hii tumpe dawa arudishe heshima ya ndoa 0746852145, ni dawa ya kisukuma hii, lazima kieleweke
Japokuwa jamaa amekuwa adui mkubwa wa rafiki yangu, lkn kwa huruma wang nitawapa ujumbe huu rafiki zake ili wamfikishie kwa faida zake mwenyewe. Shukran kwa msaada wako mkuu.
 
Mwambie aende Tunduru Barabara ya kwenda Namtumbo vijijini vya jiran Kuna wajuz wa hyo kitu jamaa alipigwa hyo na mchepuko alikuwa akienda kw mke wake goma usingiz mzito akirud kwa mchepuko hatar kama kanywa red bull jamaa akastuka wajuz wa hayo Mambo wakasaidia Sasa yupo pouwa...
Ok mkuu ngoja nitafikisha ujumbe huu kwa muhusika. Ila swala hili limefanyika nje ya nchi sasa sijui kama atahitajika kufunga safari kwenda Tunduru au mtaalam atatumia tiba ya fimbo ya mbali kumponya jamaa. Shukran kwa mchango na msaada wako wa kutatua tatizo linalomsibu jamaa.
 
Chai ya pilipili kichaa na tangawizi kali!
J aliyeacha mke ni bwege tena zoba!
Huko Sauzi si ndiyo kuna mabingwa wa uchawi, wenyewe wanaita ancestors, a calling. Sijui nini! Sangoma walioshukiwa na roho!
 
Chai ya pilipili kichaa na tangawizi kali!
J aliyeacha mke ni bwege tena zoba!
Huko Sauzi si ndiyo kuna mabingwa wa uchawi, wenyewe wanaita ancestors, a calling. Sijui nini! Sangoma walioshukiwa na roho!
Hahaha 😂😂😂 mkuu sauzi hakuna wachawi bali kuna matapeli ya kichawi. Waganda na baadhi ya wazimbabwe wamekuwa wakipiga pesa ndefu kupitia uchawi fake. J nae aliacha mke baada ya kuona mienendo ya mkewe haieleweki. Hakujua mapema kuwa mkewe anazuzuliwa na rafiki yake.
 
Hahaha 😂😂😂 mkuu sauzi hakuna wachawi bali kuna matapeli ya kichawi. Waganda na baadhi ya wazimbabwe wamekuwa wakipiga pesa ndefu kupitia uchawi fake. J nae aliacha mke baada ya kuona mienendo ya mkewe haieleweki. Hakujua mapema kuwa mkewe anazuzuliwa na rafiki yake.
Bwege wacha wamuolee!
Yaani mwanaume uliyekamilika unakuwa na urafiki WA kike na mwanaume mwenzako, mpaka unamlilia mkeo ana matatizo, anakuambia muache, nawe unamtii!??

Huko Rainbow nation huko!
 
Atajuta.
Hapo waganga feki atujaanza yetu.

Mwambie nipo mganga mzuri nitamtibia hata akiwa mbali...awe na mbuzi na debe la mchele,wa kyela, ndoo ya mafuta ya kupikia kama sadaka.
Malipo baada ya kupona.
 
Kwani huyo J si kamuacha huyo mwanamke! Amfungue mwenzake bhn sometimes sio kila ushauri tunabeba tu
 
Unamshauri mwenzako amuache mke wake halafu unaenda kumuoa

Ndio ukome siku nyengine


Halafu mkipata matatizo mseme msaidiwe msisingizie rafiki zenu
 
Mawili akaombe msamaha na mke aachane nae, maan kuachana na mke bila kwenda kuomba msamaha haitasaidia unaweza kwenda kwingine hali ikawa hivyo hivyo. Hivyo la kwanza akatubu toka moyoni uchafu wake na iwe fundisho maishani mwake
 
Acheni kulala na wake za wanaume wenzenu, katika vitu vinaweza kukubadilishia maisha kabisa ni kulala na mke wa mwanaume mwenzako.

Kuna watu wanaijua revenge Acha kabisa, kuna wanaume wanajua kutoa revenge sio poa. Binafsi mke wa mtu NEVER!
 
Atajuta.
Hapo waganga feki atujaanza yetu.

Mwambie nipo mganga mzuri nitamtibia hata akiwa mbali...awe na mbuzi na debe la mchele,wa kyela, ndoo ya mafuta ya kupikia kama sadaka.
Malipo baada ya kupona.
Hahaha 😂🤣🤣 baada ya kusoma comment yako, nimejikuta nacheka mwenyew kama chizi 😂😂
 
Back
Top Bottom