Je, hili limekukuta kuachwa na bus kisha ukatumia bodaboda kulifukuza bus

Je, hili limekukuta kuachwa na bus kisha ukatumia bodaboda kulifukuza bus

Nilikua napenda mabasi yanayokimbia boda niliyopanda ikaharibika wakati tunaenda ile kushuka na kutafuta nyingine nikapata sasa nafika tu stendi ndo ile chuma inaondoka ile asubuhi hamna magari hivi jamaa akasema naikuta ile tuondoke ??😂😂😂


Boda inakimbia nimeishikilia kwa nyuma machozi yanatoka ila hayashuki chini yanatiririka kwenye masikio 😂😂😂😂

Jamaa amekakamaa moyoni nasema tukiyumba hapa hawapati hata leso basi likasimama nikampa jamaa li 10k hata sikukumbuka chechi nikakaa kwenye gari naona watu pembeni yangu wanacheka 😂😂😂

Kumbe wanacheka machozi yalipo😂
 
Habari ya uzima wana JF moja kwa moja niingie ktk mada bila ya kupoteza muda Je..? umewahi kuachwa na bus au kuchelewa kufika stendi kwaajili ya safari na ukakuta bus limesha ondoka kisha ukatumia bodaboda kufukuzia bus embu tueleze ilikuaje na gharama za kulifukuza zilikua kiasi gani.


Mimi niliachwa na bus enzi zile stendi ipo ubungo nilikua naelekea dodoma na bus ya Al-Saedy tiketi iliandikwa safari inaanza saa 10:00 asubuhi nafika pale majira ya saa 3:50 asubuhi naambiwa gari imeshaondoka muda si mrefu nilivurugwa ikabidi nichukue namba za konda akaniambia hawako mbali nichukue bodaboda wao wataenda mdogomdogo, chap nikavuta bodaboda nikaanza kuifukuzia nilikuja kuipata kibaha bodaboda ananiambia gharama yake nilibaki hoi ni bora ningeongezea kidogo nipande bus nyengine ikawa mzozo ila konda akalipa kwa kumuahidi nikifika dodoma nitamlipa maana pale sikua na kitu, nilipofika dodoma nikamkimbia sikumlipa kitu.


Je wewe ilishawahi kukutokea tueleze ilivyokua ...
Mimi nimeexperience kinyume

Nishawahi kukata tiketi gari la kuelekea Dodoma (nadhani ilikuwa alsaedy au super champion)
Nimekata tiketi saa 2 na walisema litaondoka saa 2 ½, kibaya naingia ndani nakuta abiria kama watano tu nikasema leo nimeyakanyaga

Nimejaribu kwenda Kwa konda akawa anakazia abiria wapo wengi tu wametoka nje na akanionyesha kitab Chao Cha tiketi kweli kilikuwa kinakaribia kujaa


Tukikaa kwenye gari kuanzia saa 2 hadi saa 5, kibaya zaidi gari lilikuwa lipo limewashwa likazimwa na wakalipaki pembeni kabisa kuonesha hakuna ratiba ya kuondoka

Kuna jamaa mmoja, akawafuata makonda akawaka sana na akawaambia wamrudishie nauli yake huku wengine tupo kimya tu tunasapoti kimoyomoyo


Jamaa wakataka kumrudishia Hela yake akagoma akasema yeye atakuwa wa mwisho kupewa, yaani Hela Kila mtu apewe nauli yake ili akapande gari lingine

Jamaa wakapagawa wakaamua kuanza safari.


NILICHOJIFUNZA
1. Hutakiwi kuwasikiliza maagent vishoka maana waliniongopea gari kama kimbinyiko, shabiby nk zimejaa kumbe uongo

2. Sikuwahi kukata tiketi mpaka niingie ndani ya gari nijirishishe kuwa lina abiria wa kutosha

3. Kusafiri na kampuni za uhakika sio magari mabovumabovu /ya zamani
 
Happy Nation iliniacha Moshi kila bodaboda akimpigia honi dereva asimame akajifanya hamnazo hadi Himo.
Kulikuwa na vitu vyangu vya thamani kwenye bus hilo.
Wapuuzi sana
Duhh inamaana waliingia nizani ndio ukawaoata bila ya mizani ya himo ungeendelea kumfukuza, lakini boda alikuambia umlipe kiasi gani?
 
Mimi nimeexperience kinyume

Nishawahi kukata tiketi gari la kuelekea Dodoma (nadhani ilikuwa alsaedy au super champion)
Nimekata tiketi saa 2 na walisema litaondoka saa 2 ½, kibaya naingia ndani nakuta abiria kama watano tu nikasema leo nimeyakanyaga

Nimejaribu kwenda Kwa konda akawa anakazia abiria wapo wengi tu wametoka nje na akanionyesha kitab Chao Cha tiketi kweli kilikuwa kinakaribia kujaa


Tukikaa kwenye gari kuanzia saa 2 hadi saa 5, kibaya zaidi gari lilikuwa lipo limewashwa likazimwa na wakalipaki pembeni kabisa kuonesha hakuna ratiba ya kuondoka

Kuna jamaa mmoja, akawafuata makonda akawaka sana na akawaambia wamrudishie nauli yake huku wengine tupo kimya tu tunasapoti kimoyomoyo


Jamaa wakataka kumrudishia Hela yake akagoma akasema yeye atakuwa wa mwisho kupewa, yaani Hela Kila mtu apewe nauli yake ili akapande gari lingine

Jamaa wakapagawa wakaamua kuanza safari.


NILICHOJIFUNZA
1. Hutakiwi kuwasikiliza maagent vishoka maana waliniongopea gari kama kimbinyiko, shabiby nk zimejaa kumbe uongo

2. Sikuwahi kukata tiketi mpaka niingie ndani ya gari nijirishishe kuwa lina abiria wa kutosha

3. Kusafiri na kampuni za uhakika sio magari mabovumabovu /ya zamani
huwa vishoka wanatumia maneno ya ushawishi ukiwasikiliza imekula kwako, ila hiyo point ya kutokata tiketi mpaka uingie ndani ya bus ni muhimu zaidi.
 
Sijawah kutana na kadhia hiyo.. Maana akili yangu hata nikilala saa 8 usiku na niwe na ratba ya kuamka saa 10 Kamili alfajili basi ni uhakika saa kumi kasoro 10 au 5 ntashituka. Ingawa nina mpwa wangu huyo Kama kuachwa na mabasi basi katika maisha yake haipungui mara 10 na Mbanga zake ni hzo hzo za kufukuzia ba Bodaboda, Nilishamshaur aache kukata tiket badala yake awah stend mapema na apande basi analolikuta.

Shuhuda
Kuna siku nilikuwa nasafir toka DSM Kwenda Sumbawanga enzi hzo tunatokea Ubungo na basi la Majinja, Kuna Vijana wawili waliachwa na hilo basi na wakaanza fukuzia kwa boda mpaka pale walipotukuta maeneo ya Kibamba, Dogo mmoja alichanganyikiwa kias kwamba ile kafika tuu kwenye basi ni mbio hadi ndani na helmet kichuani, Sasa Boda kwa sautiii Naomba Helmet,,, dogo sina helmet yako banaaa.. yalikuwa majibizano ya sekunde kadhaa mpaka mim nilipoenda kumvua yule dogo helmet na kumrushia Boda aliyekuwa chin
 
Habari ya uzima wana JF moja kwa moja niingie ktk mada bila ya kupoteza muda Je..? umewahi kuachwa na bus au kuchelewa kufika stendi kwaajili ya safari na ukakuta bus limesha ondoka kisha ukatumia bodaboda kufukuzia bus embu tueleze ilikuaje na gharama za kulifukuza zilikua kiasi gani.


Mimi niliachwa na bus enzi zile stendi ipo Ubungo nilikuwa naelekea Dodoma na bus ya Al-Saedy tiketi iliandikwa safari inaanza saa 10:00 asubuhi nafika pale majira ya saa 3:50 asubuhi naambiwa gari imeshaondoka muda si mrefu nilivurugwa ikabidi nichukue namba za konda akaniambia hawako mbali nichukue bodaboda wao wataenda mdogomdogo, chap nikavuta bodaboda nikaanza kuifukuzia nilikuja kuipata kibaha bodaboda ananiambia gharama yake nilibaki hoi ni bora ningeongezea kidogo nipande bus nyingine ikawa mzozo ila konda akalipa kwa kumuahidi nikifika Dodoma nitamlipa maana pale sikuwa na kitu, nilipofika Dodoma nikamkimbia sikumlipa kitu.


Je wewe ilishawahi kukutokea tueleze ilivyokua ...
Mimi nilikuwa nafukuzia shabiby ,Dodoma_Mbeya nililikuta sehemu inaitwa Iringa road jamaa kadai elfu ishirini!Wakati huo Dodoma _Mbeya Tsh28,000Hatari na nusu mkuu,Hawa bodaboda ndo maana wanapata ukilema,Mungu anawaona.
 
Niliwahi kuachwa na basi la Taqwa lililokuwa linafanya safari za Nairobi Dar es salaam. Nililazimika kukodi taxi kulifukuzia kutoa Nairobi kwa Dollar 100 wakati huo. Hata hivyo tulilikuta basi limeishavuka mpaka wa Namanga tayari kuelekea Arusha.
 
Sijawah kutana na kadhia hiyo.. Maana akili yangu hata nikilala saa 8 usiku na niwe na ratba ya kuamka saa 10 Kamili alfajili basi ni uhakika saa kumi kasoro 10 au 5 ntashituka. Ingawa nina mpwa wangu huyo Kama kuachwa na mabasi basi katika maisha yake haipungui mara 10 na Mbanga zake ni hzo hzo za kufukuzia ba Bodaboda, Nilishamshaur aache kukata tiket badala yake awah stend mapema na apande basi analolikuta.

Shuhuda
Kuna siku nilikuwa nasafir toka DSM Kwenda Sumbawanga enzi hzo tunatokea Ubungo na basi la Majinja, Kuna Vijana wawili waliachwa na hilo basi na wakaanza fukuzia kwa boda mpaka pale walipotukuta maeneo ya Kibamba, Dogo mmoja alichanganyikiwa kias kwamba ile kafika tuu kwenye basi ni mbio hadi ndani na helmet kichuani, Sasa Boda kwa sautiii Naomba Helmet,,, dogo sina helmet yako banaaa.. yalikuwa majibizano ya sekunde kadhaa mpaka mim nilipoenda kumvua yule dogo helmet na kumrushia Boda aliyekuwa chin
nilicho note hapa kutoka kwako ni kukata tiketi siku hiyohiyo ya safari, ila kuna badhi ya mikoa inahitajika ukate kabla ya tarehe ya tukio mfano mikoa ya kaskazini kipindi cha mwishoni mwa mwaka
 
Mimi nilikuwa nafukuzia shabiby ,Dodoma_Mbeya nililikuta sehemu inaitwa Iringa road jamaa kadai elfu ishirini!Wakati huo Dodoma _Mbeya Tsh28,000Hatari na nusu mkuu,Hawa bodaboda ndo maana wanapata ukilema,Mungu anawaona.
😁😁 ukamuachia na laana huyo bodaboda, na wakati mwengine dereva wa bus au konda anafosi umpe hiyo pesa ambayo haina uhalisia nikama kamchezo fulani hivi
 
Niliwahi kuachwa na basi la Taqwa lililokuwa linafanya safari za Nairobi Dar es salaam. Nililazimika kukodi taxi kulifukuzia kutoa Nairobi kwa Dollar 100 wakati huo. Hata hivyo tulilikuta basi limeishavuka mpaka wa Namanga tayari kuelekea Arusha.
Duhh juhudi zako hazikuzaa matunda pole sana
 
Habari ya uzima wana JF moja kwa moja niingie ktk mada bila ya kupoteza muda Je..? umewahi kuachwa na bus au kuchelewa kufika stendi kwaajili ya safari na ukakuta bus limesha ondoka kisha ukatumia bodaboda kufukuzia bus embu tueleze ilikuaje na gharama za kulifukuza zilikua kiasi gani.


Mimi niliachwa na bus enzi zile stendi ipo Ubungo nilikuwa naelekea Dodoma na bus ya Al-Saedy tiketi iliandikwa safari inaanza saa 10:00 asubuhi nafika pale majira ya saa 3:50 asubuhi naambiwa gari imeshaondoka muda si mrefu nilivurugwa ikabidi nichukue namba za konda akaniambia hawako mbali nichukue bodaboda wao wataenda mdogomdogo, chap nikavuta bodaboda nikaanza kuifukuzia nilikuja kuipata kibaha bodaboda ananiambia gharama yake nilibaki hoi ni bora ningeongezea kidogo nipande bus nyingine ikawa mzozo ila konda akalipa kwa kumuahidi nikifika Dodoma nitamlipa maana pale sikuwa na kitu, nilipofika Dodoma nikamkimbia sikumlipa kitu.


Je wewe ilishawahi kukutokea tueleze ilivyokua ...
10:00 umemaanisha saa 4 asubuhi, ila 3:50 umemaanisha saa tatu asubuhi

Rekebisha kuwe na consistency
 
Niliwahi kuachwa na basi la Taqwa lililokuwa linafanya safari za Nairobi Dar es salaam. Nililazimika kukodi taxi kulifukuzia kutoa Nairobi kwa Dollar 100 wakati huo. Hata hivyo tulilikuta basi limeishavuka mpaka wa Namanga tayari kuelekea Arusha.
Mbona kama chai mkuu🤣
 
Hiki kitu nlikitambua baada ya kuwa nimefanya makosa ila nilijifunza. Mwaka jana mwishoni nilikata tiketi mtandaoni ya kwenda Mwanza kwa bus la kampuni ya Happy Nation, tiketi ilionesha bus linatoka pale Shekilango saa tisa kamili.

Nimefika Shekilango saa tisa kasoro nikiwa na bodaboda naambiwa bus limetoka hapa sasa hivi, nikaanza kulikimbiza lakini silipati, nikaenda mpaka Mbezi silioni maana nilikuwa natizama plate number za mabus ya kampuni hiyo ninayopishana nayo.

Kufika Mbezi naambiwa limeondoka nikaanza kulifukuza tena ila nikawa nashangaa mbona magari ninayoyapita hayana hii plate number?

Nikaja kugundua baadae kuwa plate number ya kwenye tiketi haikuwa plate number ya basi liliondoka😂😂😂😂,nikapanda bus lingine la kampuni hiyo mpaka Moro ndio nikakutana na bus la Mwanza, ila mpaka napata hilo bus lao jingine lililonifikisha Moro nilikuwa nimeshatoboka kinoma.

Na tangu hiyo siku nimeagana na safari kwa kutumia kampuni ya HAPPY NATION hata bure.
bila ya kugundua kama plate namba nitofauti ungefika mpaka morogogoro na hiyo bodaboda
 
Natoka zangu Mbulu kwenda Babati, usafiri ni land cruiser, tumefika maeneo ya Magugu kuna abiria akawa anashuka, me nimekaa siti ya mbele pembeni ya dereva, kwa jinsi gari ilivyojaa na yule abiria anayeshuka kakaa nyuma kabisa, nikasema na mimi nishuke chap ninunue maji ya kunywa. Nikakikimbia duka la karibu chapchap nikapata Maji. Dah! Ile kurudi kwenye gari naiona cruiser ileee ishaishia. Kwenye gari nimeacha begi langu lina vitu vya muhimu Sana. Magugu na Babati sio mbali, zipo bajaji zinaenda. Nikachukua bajaji nikitegemea nitaikuta tu ile cruiser stand nichukue vitu vyangu. Hao, tukaanza safari na bajaji kufika maeneo ya daraja la Kiongozi, naiona ile cruiser kwa mbali imepaki kando ya barabara na abiria wameshuka. Nikaona baadhi yao wanaisimamisha ile bajaji ili kutaka kupanda.Nikashangaa!! Kumbe cruiser imezingua asee, naona boneti iko juu, gari imechemka haiwezi endelea. Haha! Nikasema dah! Kumbe ni Mungu kaniepusha na ile gari, nikamwomba dereva bajaji nichukue begi langu pale, kisha haooo mpaka Babati. Abiria wa ile cruiser walikosa nafasi sababu bajaji nyingi zinazopita hapo zinakua zimeshajaza kutokea Magugu.
 
Back
Top Bottom