Je, hili limekukuta kuachwa na bus kisha ukatumia bodaboda kulifukuza bus

Je, hili limekukuta kuachwa na bus kisha ukatumia bodaboda kulifukuza bus

Natoka zangu Mbulu kwenda Babati, usafiri ni land cruiser, tumefika maeneo ya Magugu kuna abiria akawa anashuka, me nimekaa siti ya mbele pembeni ya dereva, kwa jinsi gari ilivyojaa na yule abiria anayeshuka kakaa nyuma kabisa, nikasema na mimi nishuke chap ninunue maji ya kunywa. Nikakikimbia duka la karibu chapchap nikapata Maji. Dah! Ile kurudi kwenye gari naiona cruiser ileee ishaishia. Kwenye gari nimeacha begi langu lina vitu vya muhimu Sana. Magugu na Babati sio mbali, zipo bajaji zinaenda. Nikachukua bajaji nikitegemea nitaikuta tu ile cruiser stand nichukue vitu vyangu. Hao, tukaanza safari na bajaji kufika maeneo ya daraja la Kiongozi, naiona ile cruiser kwa mbali imepaki kando ya barabara na abiria wameshuka. Nikaona baadhi yao wanaisimamisha ile bajaji ili kutaka kupanda.Nikashangaa!! Kumbe cruiser imezingua asee, naona boneti iko juu, gari imechemka haiwezi endelea. Haha! Nikasema dah! Kumbe ni Mungu kaniepusha na ile gari, nikamwomba dereva bajaji nichukue begi langu pale, kisha haooo mpaka Babati. Abiria wa ile cruiser walikosa nafasi sababu bajaji nyingi zinazopita hapo zinakua zimeshajaza kutokea Magugu.
Bila ya kupata hitilafu chuma ungeikuta babati hiyo, nazile cruiser zinapakia mizigo mpaka kwa mbele zinanyanyuka hivi hamuogopi
 
Nilikuwa naenda Arusha nimekata kilimanjaro express Enzi hizo zipo moto
Nmefika mapema kabisa nikapanda kwenye gari nikatulia gari ikaanza safari
Tunafika mbezi wanakagua ticket naambiwa nmekosea gari Ile niliyopanda inaenda Tunduma
Wakanishusha nirudi pale shekilango nikapande ya arusha ya saa kumi na mbili maana nilikuwa nmekata ya saa 11 alfajiri na ilishaondoka ilikuwa inapita njia ya bagamoyo.. nikachukua boda hadi shekilango tena
Ikabidi nipande ya saa 12 nilikuta nayo ndyo inatoka wakanipa siti
Tangu hapo nikajifunza kusoma namba ya gari kabla sijapanda.
 
Nilikua napenda mabasi yanayokimbia boda niliyopanda ikaharibika wakati tunaenda ile kushuka na kutafuta nyingine nikapata sasa nafika tu stendi ndo ile chuma inaondoka ile asubuhi hamna magari hivi jamaa akasema naikuta ile tuondoke ??[emoji23][emoji23][emoji23]


Boda inakimbia nimeishikilia kwa nyuma machozi yanatoka ila hayashuki chini yanatiririka kwenye masikio [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Jamaa amekakamaa moyoni nasema tukiyumba hapa hawapati hata leso basi likasimama nikampa jamaa li 10k hata sikukumbuka chechi nikakaa kwenye gari naona watu pembeni yangu wanacheka [emoji23][emoji23][emoji23]

Kumbe wanacheka machozi yalipo[emoji23]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nilikuwa naenda Arusha nimekata kilimanjaro express Enzi hizo zipo moto
Nmefika mapema kabisa nikapanda kwenye gari nikatulia gari ikaanza safari
Tunafika mbezi wanakagua ticket naambiwa nmekosea gari Ile niliyopanda inaenda Tunduma
Wakanishusha nirudi pale shekilango nikapande ya arusha ya saa kumi na mbili maana nilikuwa nmekata ya saa 11 alfajiri na ilishaondoka ilikuwa inapita njia ya bagamoyo.. nikachukua boda hadi shekilango tena
Ikabidi nipande ya saa 12 nilikuta nayo ndyo inatoka wakanipa siti
Tangu hapo nikajifunza kusoma namba ya gari kabla sijapanda.
ndio uzuri wa kusafiri na kampuni yenye mabus mengi
 
Mbona kama chai mkuu🤣
Mkuu napata faida gani kuleta chai humu?.... Kama huamini basi ni wewe ila habari ndio hiyo, tena inaendana na mada hii.
 
Yeye kaandika saa 4:00 wewe unaandika saa 10:00 ?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] wewe kweli pacha wangu nilitaka kuandika sentensi hii kama ilivyo ila nikaona uzi tayari una komenti nyingi itakuwa tayari wameshamwambia wengi nikaona niache tu
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] wewe kweli pacha wangu nilitaka kuandika sentensi hii kama ilivyo ila nikaona uzi tayari una komenti nyingi itakuwa tayari wameshamwambia wengi nikaona niache tu
Nimegundua mleta mada ali-edit, aliandika 10:00
 
Hiki kitu nlikitambua baada ya kuwa nimefanya makosa ila nilijifunza. Mwaka jana mwishoni nilikata tiketi mtandaoni ya kwenda Mwanza kwa bus la kampuni ya Happy Nation, tiketi ilionesha bus linatoka pale Shekilango saa tisa kamili.

Nimefika Shekilango saa tisa kasoro nikiwa na bodaboda naambiwa bus limetoka hapa sasa hivi, nikaanza kulikimbiza lakini silipati, nikaenda mpaka Mbezi silioni maana nilikuwa natizama plate number za mabus ya kampuni hiyo ninayopishana nayo.

Kufika Mbezi naambiwa limeondoka nikaanza kulifukuza tena ila nikawa nashangaa mbona magari ninayoyapita hayana hii plate number?

Nikaja kugundua baadae kuwa plate number ya kwenye tiketi haikuwa plate number ya basi liliondoka😂😂😂😂,nikapanda bus lingine la kampuni hiyo mpaka Moro ndio nikakutana na bus la Mwanza, ila mpaka napata hilo bus lao jingine lililonifikisha Moro nilikuwa nimeshatoboka kinoma.

Na tangu hiyo siku nimeagana na safari kwa kutumia kampuni ya HAPPY NATION hata bure.
Inaonesha wenye mabasi ni waswahili, mleta mada nae alifika dakika 15 mapema lakini basi lilishaondoka. Hawazingatii muda wanaondoka tu kwa mihemko.
 
Mkuu napata faida gani kuleta chai humu?.... Kama huamini basi ni wewe ila habari ndio hiyo, tena inaendana na mada hii.
HAkuna shida mkuu, ila nauli ya basi ilikua ngapi kipindi hiko
 
Back
Top Bottom