Je, huu ni wakati sahihi kwa kanisa Katoliki kubadilika na kuendana na kasi ya makanisa ya Kilokole?

Sasa kama umejitenga na kanisa unategemea nini ?
Elewa kiswahili mtu hajajitenga anaenda kanisani kama kawaida na kutoa sadaka ila hayupo kwenye jumuia.Au anaenda kanisani kila jumapili na yupo kwenye jumuia ila akitoka kanisani anaenda kwenye uponyaji kwa Lusekelo au Mwamposa n.k .Mtu huyo anatengwa.
 
Sina shaka na mengine yote....
Ila michango imekua too mucha aseee too much, sijui labda hali mbaya ndio maana naona hivi.
 
NI UPUUZI ,wabadilike waendane na maagizo ya yesu na si makanisa ya kilokole.

usiabudu sanamu.

usiombe kwa jina lingine isipokuwa la Yesu
 
Walikataa kumzika ndugu yangu,ikabidi nimuite shekhe aje kufanya ibada ya mazishi hapo ndio wakajua duniani kuna vichaa wa aina nyingi.

Pia kama umezaa haujafunga ndoa mtoto anaweza asibatizwe haya mambo zamani hayakuwepo.

Naongea hivi For Good sake wanalipoteza kanisa pasipo kujua kwamba linapotea.
 
Sasa kama huendi jumuiya sindio unajitenga mwenyeye.
 
Walikataa kumzika rafiki yangu kisa alikuwa hashiriki sana jumuiya, tukaenda KWA walokole wakamzika

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
 
This is the best answer for his question...
 
Kanisa liliopo miaka 2000 iliyopita wewe hii uje ulipoteze! Hatari
 
Dini ni njia ya kuwatawala watu na kupata pesa, wanachokifanya ni kuwalazimisha watu watii matakwa yao, na waendelee kupata pesa, fikiri ktk nyakati hizi na ugumu wa uchumi bado wanawataka watu waende jumuiya kila jumamosi, kila siku kuna ibada kuanzia saa kumi na mbili asubuhi, jumapili kuna ibada, siku za Katikati kuna maombi. Huyu mtu saa ngapi ataweza kwenda kutafuta kipato kwa ajili yake na familia au kusoma, kufanya utafiti? walizoea miaka iliyopita watu walikua wanafanya kazi serikalini na kwenye mashirika ya umma, walikua na muda mwingi wa kupoteza, na hii ni sababu nyingine iliyosababisha mashirika kufa, hata sasa watu wanategemea miujiza na sio kufanya kazi, ndio maana utakuta kijana anasoma ila anaenda kukemea ili afaulu mtihani na si kuweka juhudi kwenye kusoma, Akiajiriwa anakemea sio kufanya kazi kwa bidii na kujifunza. Nchi Jirani kuweka sheria kila Mchungaji awe na digirii wako sahihi. ni wakati wa kila mtu kusimama na kuangalia masla Yake na familia yake, kwani maumivu ni yako mwenyewe. hata wachina hawana dini na angalia maendeleo yao.
 
Marehemu Ana waswaasa huwenda asizikwe kikamilifu ktk ibada zote za heshima ofu yako ndio hyo .....nakuakikishia utazikwa vzr Sanaa na kusherekewa maisha yako Apo duniani
 
Alitoka martin luther miaka ya 1500 huko na bado kanisa lipo sembuse wewe? Ondoka tena nakusha

Hapana mtoto wana batiza bora tu uwe na jumuiya.
 
Wakristo woote inabidi tuwe kitu kimoja haya madhehebu hayana umuhimu kabisa coz sis sote ni wafuasi wa Jesus tubadilike mi binafsi huwa nasali makanisa yoyote ili mradi tunamwabudu Yesu huu udhehebu unatenganisha tu hauna maana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…