Je, huu ni wakati sahihi kwa kanisa Katoliki kubadilika na kuendana na kasi ya makanisa ya Kilokole?

Je, huu ni wakati sahihi kwa kanisa Katoliki kubadilika na kuendana na kasi ya makanisa ya Kilokole?

Walikataa kumzika ndugu yangu,ikabidi nimuite shekhe aje kufanya ibada ya mazishi hapo ndio wakajua duniani kuna vichaa wa aina nyingi.

Pia kama umezaa haujafunga ndoa mtoto anaweza asibatizwe haya mambo zamani hayakuwepo.

Naongea hivi For Good sake wanalipoteza kanisa pasipo kujua kwamba linapotea.
Kikatoliki mtoto anabatizwa kwa imani ya wazazi wake.Sasa kama wazazi wake mnalegalega si bora wasubiri mtoto awe mkubwa abatizwe kwa imani yake mwenyewe?
 
Kanisa katoliki linaunganisha waumini wake wote kwa njia ya jumuiya, ukiwa mshiriki mzuri utajikuta unajenga ukaribu na waumini wengi sana wa kanisa unalosali, maana unakuta mkusanyiko wa jumiya kadhaa unaunda kanda ambapo idadi ya kaya inaongezeka na kuzidi kujenga ukaribu wa waumini. Ila kwenye swala la michango hapo kwa kweli itabidi tu ufuate imani yako ya kutoa kama sadaka au lah.
 
Kikatoliki mtoto anabatizwa kwa imani ya wazazi wake.Sasa kama wazazi wake mnalegalega si bora wasubiri mtoto awe mkubwa abatizwe kwa imani yake mwenyewe?
Sisi wakati tunabatizwa miaka hiyo hakukuwapo na ubaguzi wa namna hiyo haya mambo yameanzishwa hivi karibuni nakwambia .

Kanisa linapoteza waumini pasipo kujua mfano wewe ni mRC mke wako sio sababu RC haliwezi batiza mtu hasiye kwnye jumuia hivyo hapo wife anapata power ya kumbatiza huko kwenye kanisa lake ambalo sio Katoliki.
 
Dini /imani ni ulevi mbaya kuliko cocaine.
Ili kuwa mfuasi mzuri wa dini inakupasa usifikiri Wala usiulize chochote uwe Kama kondoo.

Catholic kuna msemo wa kilatini unasema" Roma locuta causa finita "Roma ikisema kesi/mjadala umefungwa.

Yani hupaswi kuhoji wala kujihoji Kwa mfano Kwanini nichangie ujenzi wa shule ambayo ada yake ni kubwa kiasi kwamba wale waumini kindaki ndaki hawawezi kusomesha hapo watoto
 
wa RC bana, Mungu Ana tuona[emoji4][emoji4][emoji4]
d76ff5f4ba6741ba9757a22babba1df9.jpg
 
Sisi wakati tunabatizwa miaka hiyo hakukuwapo na ubaguzi wa namna hiyo haya mambo yameanzishwa hivi karibuni nakwambia .

Kanisa linapoteza waumini pasipo kujua mfano wewe ni mRC mke wako sio sababu RC haliwezi batiza mtu hasiye kwnye jumuia hivyo hapo wife anapata power ya kumbatiza huko kwenye kanisa lake ambalo sio Katoliki.
Katoliki hii misukosuko haijaanza leo.Watapoteza waumini wengi lakini kanisa halitakufa.Kama wanafanya kazi za shetani basi litakufa lkn kama wanafanya kazi ya Mungu basi halitakufa kamwe
 
Siku hizi mi swala la michango tu ndio silielewi, wanajumuia wakigonga hodi kwako hata kama unaumwa usidhani ni kukujulia hali, wanaijia michango....
Na ni michango ya aina nyingi
Unasali kigango gani mpendwa[emoji3][emoji3]?
 
Ndugu, kwa upendo kabisa, nakushauri utafute kumjua Mungu zaidi kuliko kuwa na karibu na kanisa huku ukiishi kwa hofu.
Ukimfahamu Mungu kwa undani hizo hofu za kutengwa na hujui atakaekuzika zitaondoka. Unachotakiwa kuhofia ni kuishi sawa sawa na mapenzi ya Mungu sababu yeye ndio anafahamu kuhusu kuishi kwako na baada ya kufa kwako.

Yesu alizikwa na Yusufu wa Arithmataya na hakukuwepo na Ibada ya maziko. Sasa wewe ni nani unayeogopa kutengwa??
Muamini Mungu tu kwa kila jambo, hata wasipokuzika, Manispaa watakuzika. Sidhani kama Mungu ataangalia umezikwa vipi ila atahukumu matendo yako. Mpendeze Mungu na hayo mengine muachie yeye atakufanyia njia kwani Mungu anaweza yote.
Ooh Yesu mwema, ahsante kwa ajili ya huyu mtumishi wako...👏👏👏
 
Ndugu, kwa upendo kabisa, nakushauri utafute kumjua Mungu zaidi kuliko kuwa na karibu na kanisa huku ukiishi kwa hofu.
Ukimfahamu Mungu kwa undani hizo hofu za kutengwa na hujui atakaekuzika zitaondoka. Unachotakiwa kuhofia ni kuishi sawa sawa na mapenzi ya Mungu sababu yeye ndio anafahamu kuhusu kuishi kwako na baada ya kufa kwako.

Yesu alizikwa na Yusufu wa Arithmataya na hakukuwepo na Ibada ya maziko. Sasa wewe ni nani unayeogopa kutengwa??
Muamini Mungu tu kwa kila jambo, hata wasipokuzika, Manispaa watakuzika. Sidhani kama Mungu ataangalia umezikwa vipi ila atahukumu matendo yako. Mpendeze Mungu na hayo mengine muachie yeye atakufanyia njia kwani Mungu anaweza yote.
Umenena vyema 🙏
 
Kanisa Katoliki la Mitume linaanzia katika ngazi ya familia. Kama ukibatizwa katika ukatoliki, wewe una jukumu la kuitangaza injili kuanzia kwako, halafu unaenda jumuiya, kanda, parokia, jimbo n.k. Makanisa yanaendeshwa kwa zaka na sadaka, michango ya ujenzi n.k. Sasa wewe jumuiya huenda, kazi iliyopewa na Bwana wetu Yesu Kristu ya kutangaza injili unaofanyika wapi? Huko Kanisani unaotaka kumpeleka mtoto akabatizwe kanisa liliota kama uyoga? Nani analipia umeme? Padre anakula nini? Anavaa nini? Atakuja je kuzika huyo marehemu wako? Wewe ndio mlinzi wa usiku hapo Kanisani! Hivi kama sio kujenga makanisa waumini wote inabidi tutoke huko tuliko Mbagala, Gongolamboto, Tegeta, Kimara, Kigamboni wote twende Msimbazi na St. Joseph au St Peter? Hujui Jumuiya ndio zinajenga makanisa mapya?

Mimi nakuruhusu kwenda unaotaka iwe kwa Mwaiposa, Kakobe, Lusekelo. Wakifa itarudi maana mmiliki hatakuwepo!
 
Alitoka martin luther miaka ya 1500 huko na bado kanisa lipo sembuse wewe? Ondoka tena nakushauri uende kwa Mwamposa
Unajua shida ya wanadamu wakionja kitu wanataka wote tuonje hapo ndio mtihani sasa, Kwani Katoliki anasalisha kwa kushindana na kanisa lingine au wao ndio wanashindana na Kanisa Katoliki?
 
Wakristo woote inabidi tuwe kitu kimoja haya madhehebu hayana umuhimu kabisa coz sis sote ni wafuasi wa Jesus tubadilike mi binafsi huwa nasali makanisa yoyote ili mradi tunamwabudu Yesu huu udhehebu unatenganisha tu hauna maana
Nategemea kuwa kama wewe mkuu. Natamani nimjue zaidi Mungu kwa sasa najiona mweupe kwenye maswala hayo aisee.
 
Hilo kanisa halimjui Muumba wako kiujanja2 zaidi watu wanalewa, hawamjui R/Mtakatifu, wanaabudu madoli; mbingu wataisikia bombani hao. Ndiyo maana hata c-19 imeua sana makasisi wao hata nguvu ya kuifukuza hakuna! Sasa si mnapoteza muda wenu bure!
 
Kwani umelazimishwa kuendana nao! Nenda kwa masanja
SANAMU inaleta laana kwa nchi, tubadilike na haya mambo wazungu tena mabeberu wataliano walotuletea bila kuhoji.
chanjo zao hatutaki, sijui tujitegemee, ila mamisanamu yao tunayaabudu mavitu hata hayana pumzi,
 
Back
Top Bottom