Je, huyu Rais wetu wa sasa ni Vasco Da Gama mwingine? Ziara za nje zimekuwa nyingi sana kama enzi za Awamu ya Nne

Je, huyu Rais wetu wa sasa ni Vasco Da Gama mwingine? Ziara za nje zimekuwa nyingi sana kama enzi za Awamu ya Nne

Yule jiwe a.k a mzimu wa sukuma gang ndiyo amesababisha yote haya. Aliua biashara zote kubwa na ndogo kwa kupora fedha za watu. Vyanzo vyote vya Kodi vikafa. Akawa anakopa hovyo tena kwa siri kubwa mikopo ya kibiashara ambayo riba zake ni kubwa.

Mama hana namna lazima asafiri ili apate mikopo, maana nchi imeachiwa matatizo na madeni makubwa na jiwe.

Asante mama endelea kuinusuru nchi.
Hapa ndiyo umeweka vizuri na ndipo watanzania wenye akili ya kawaida hawajui.

Miradi ile ailyoanzisha Magufuli haina funding. Asipoimaliza watamlaumu
 
Awamu ya nne tulishudia Jakaya Kikwete akifanya ziara za nje huku akisahau kabisa masuala ya ndani ya nchi yake mpaka akapachikwa jina Vasco Da Gama.

Awamu hii nayo naona ni mwendo uleule. Juzi alikuwa Ulaya. Leo yupo Uarabuni.

Hii ishu ya Uarabuni asingeweza kuwakilishwa hata na balozi!
View attachment 2131649View attachment 2131650

Ni ushamba nao huu kujadili mambo kama haya. Kama kuna faida kwa nchi kujifungia Dodoma sio sifa. Tujue tu mtawala wa Dubai hawezi kukutana na Bashe
 
Kusafiri is one thing (na kama delegation sio kubwa sana huenda tusiumie sana)...., BUT......

Mimi kinachotisha zaidi ni urahisi / unafuu wa hio Mikopo tunayopewa au hizo fursa uwekezaji tunaoingia...,

Sababu bila transparency ni ngumu kujua kama tunapiga au tunapigwa....
 
Awamu ya nne tulishudia Jakaya Kikwete akifanya ziara za nje huku akisahau kabisa masuala ya ndani ya nchi yake mpaka akapachikwa jina Vasco Da Gama.

Awamu hii nayo naona ni mwendo uleule. Juzi alikuwa Ulaya. Leo yupo Uarabuni.

Hii ishu ya Uarabuni asingeweza kuwakilishwa hata na balozi!
View attachment 2131649View attachment 2131650
Kusafiri kwa Mama na Vasco Dagama km unavo muita, ni kuthaminiwa adhimu sana, ....huwezi mtu yeyote pata mwaliko ukiwa mjingamjinga ivi tu!!! hii ni dhamana ya nchi ile anayo kwenda kule,,

kwa akili zako za shule ya kata hiyo unadhani ni hela yako ya Madafu, iliyo jaa majasho ya kulima mchicha Bonde la Msimbazi. ambayo hata kodi hulipi unashindia bondeni msimbazi kukwepa na kuogopa --kamata kamata ya kodi!!

wewe umeweka tu naniliu yako hiyo nyuma ya key board yenye Rubber band tano hapo hujui kitu!! ngoja wenye akili tukuelimishe!! kinacho msafirisha Mama ni tunu yake ya jinsi alivo yeye km yeye!! pamoja na akili zake! Busara zake! Hekima zake! mchango wake!!

Yaani kifupi hawa wa hivi! ni maajaliwa tena mnooo na jumuia za kimataifa!! utameza chupa bureeee!! hata Mama akitoka kwenye kiti hicho leo, atakula shavu Dodo, kwenye jumuiya za kimataifa na alianza kitambo sana tu kujulikana kiivo!!

si unamuona yule demu katotot ka Malecela kalivo pangua gia pamoja na mtima nyongo wa jiwe?? so!! Mama kukubalika kimataifa! ni km ilivo kuwa kwa binti malecela !

kwa hiyo anaalikwa na wao! kwa hela zao! kwa ndege zao, chakula chao, Magari yao Hotel zaoo!!! akawagawie busara bure wewe Mkaanga chips na muuza mchicha unalialia nini?? unatujazia saver tu hapa bureee!...ni wazi pasi shaka kuwa....

Wewe hata, Chrismass, kitcheni party, Birth day tena za jiranizako, za ndugu zako, rafikizo ulio soma nao, pamoja na kuwapa michango yako ya hela taslimu!! hualikwagi ng'ooo, unaonekana kirahisi sana,

labda uwalie timing katkati ya sherehe, kama mie muongo kataa!! pamoja na kutoa michango yako miingi kufanikisha shughuli hiyoi!!

maajabu ukiwashtua sasa??? ''jamani inakuwaje? mbona ivi? utajibiwa kirahisi tu ''shemeji tulikusahau jamani tuwie radhi'' .....kuna sufulia ya pilau imebaki ngoja tukupakulie ukale na watoto'' ndo mkoga hivi!

Mwaliko wa Mama! Vasco D. ni wao km wao! Nyotaile Babu weye!!! na huyo Vasco bado mpaka leo ni mialiko tu kwa kwenda mbele!! ukiona vepe saga chupa kunywa!! Jiwe hakuwahi kualikwa akanuna akawa anamzodoa!! Boss wake wa zamani!!

wakati wote walikuwa Mawaziri bila hiana huyo Vasco dagama akamuweka jiwe kwenye Baraza lakela Mawaziri bila hiana, kuumbe jiwe alikuwa nyoka tu yule!!! anamzodoa Mzee wawatu!...

Taaangu akiwa Bulldozer Jiwe hakuwahi kuitwa popote asiwazuge kwa sababu hkn aliye taka kimeo!! hata sura yake tu ilifubaa!!..anagalia vasco dagama alivo changamkiwa pale south!! kuliko jiwe !!! Piga ua galagaza....Mmama kazia hapo hapo!!! wapelekeee!! wapelekeee!!

Mki ---Mind...Ardhi ipo!! itawameza tu!!.... mwendo mdundo Mwake humo humoooo!!!!!!! mwana!!!!!! hakuna kupindisha!!!!! Moto mchibuyu!!!!! Mama ni sisi na sisi ndo Mamaaa!!! Aksante Zanzibar!!!
 
Yaani akili za kimasikini kabisa, ndiyo maana waarabu wanaona waislamu wa africa ni wajinga. Hivi kuna nchi iliwahi endelea kwa mikopo toka mataifa yaliyoendelea????
Hili swali zuri tungemuuliza Mwendazake, miaka 5 trilioni 40 za mkopo! Tena kwenye mabenki ya kibiashara! Exim mojawapo.

Tena walimfuata humu humu.
 
Hivi kuna nchi iliwahi endelea kwa mikopo toka mataifa yaliyoendelea????
Maweee acha hasira Mbarbara yooote hayoo bongo!! mighorofa hiyo unazani nini ??? ni mikopo tuliyo kopa zamani!!! hiyo Elimu yako achana nayo!! mkijua kuitumia inakulipa! nani asiyekopa na akawa tajiri???
 
Pumbavu zako, wakati wa kikwete alisafili sana sasa nini kilitokea cha aajabu hapa tanzania?
Sema hata kimoja?
Kama ni kuonana na wafanya biashara alionana nao saana wote wa ulimwenguni lakini nchi bado ni masikini.
Sasa huyu ataonana na yupi ambae kikwete hakuonana nae?
Jamani Maghorofa yooote hayo??viwanda , fursa nyingi wkt wa kikwete, watu walienda mpaka china huko kufanya biashara mweee!! wengine walikuwa wana lewa china, wanakamatwa hovyo ajili ya kushiba fursa za kikwete!! Barabara za Lami mikoani huko mpaka jikoni, loool!!! ......wewe sema tu MUNGU kakupiga kofi!!! mkwere hoyeeee!!

sasa chazea tena fursa ya mama ukome milele!
 
Yule jiwe a.k a mzimu wa sukuma gang ndiyo amesababisha yote haya. Aliua biashara zote kubwa na ndogo kwa kupora fedha za watu. Vyanzo vyote vya Kodi vikafa. Akawa anakopa hovyo tena kwa siri kubwa mikopo ya kibiashara ambayo riba zake ni kubwa.

Mama hana namna lazima asafiri ili apate mikopo, maana nchi imeachiwa matatizo na madeni makubwa na jiwe.

Asante mama endelea kuinusuru nchi.
Hopless kabisa wewe huku swaiba yako anenjoy tu na midege aliyenunua Rais wetu mpendwa!

Mnaenjoy infrastructure wakati mpaka kilembwe chako atakuja lipa madeni ya sasa.
 
Yaani akili za kimasikini kabisa, ndiyo maana waarabu wanaona waislamu wa africa ni wajinga. Hivi kuna nchi iliwahi endelea kwa mikopo toka mataifa yaliyoendelea????
Hilo swali ungewauliza marais wetu watano waliomtangulia SSH.
 
Kama karudi juzi Mama anasema eti kuna hela sijui umoja wa Ulaya eti ni za kuchangamkia, ni moja ya kauli mbaya kabisa kutolewa na kiongozi ambaye nchi yake ina rasilimali nyingi kuzidi nchi nyingi za Ulaya. Yaani anatuaminisha sisi ni maskini, yaani kweli anaamini hivyo????? Yaani badala ya kufanya kama Dkt Magufuli ili tujiamini tujifunge mkanda ili nchi yetu iweze kujitegemea yeye anaendekeza eti mikopo mikopo, dah basi tu
Kuwa na rasilimali ni kitu kimoja, hizo rasilimali kubadilisha hali ya uchumi wa nchi ni suala jingine tofauti kabisa.

Angeamua tufunge mikanda, watu wangekuja kulalamika humu humu JF.
 
Wewe sio mjinga, ni mpumbavu.

Mama asisafiri maana tunaweza kutangazia watalii kupitia redio ya wasafi na clouds😂 na sisi tutaendelea kupata $3B kwa mwaka.

Kwasababu ni gharama sana Mama kusafiri😂😂 haya ndiyo mawazo yenu ya kitoto.

Nchi haina muda wa kuogopa madongo ya washamba wachache kama huyu
 
Mama asisafiri maana tunaweza kutangazia watalii kupitia redio ya wasafi na clouds😂 na sisi tutaendelea kupata $3B kwa mwaka. Kwasababu ni gharama sana Mama kusafiri😂😂 haya ndiyo mawazo yenu ya kitoto. Nchi haina muda wa kuogopa madongo ya washamba wachache kama huyu
Lack of sense is a big problem
 
Back
Top Bottom