Je, inawezekana kila kitu ni mpango wa Mungu?

Je, inawezekana kila kitu ni mpango wa Mungu?

Ukishasema mtazamo utabaki kuwa ni mtazamo tu na uthibitisho ni kitu kingine,yawezekana huo mtazamo ndio ukawa ukweli wenyewe au sivyo.
Mtazamoulioukweliukipimwa kuthibitishwa utaonekana kuwa ukweli?
 
Mkuu unajuaje kiongozi wasasa ni maridadi? Unaweza kujua miaka kumi ijayo huyu wasasa atazalisha kitu gani?


Kama huyu wa sasa ameweza kuleta maendeleo kwa kipindi hiki kifupi tu na bado ana nia ya kuleta zaidi ya hapa, sasa jiulize tutakuwa wapi baada ya miaka 10 ijayo? Kumbuka si Mwinyi wala Mkapa na Kikwete walijaribu kuleta maendeleo hapa nchini kwani kila mmoja wao alikuwa bize kulitaifisha hili taifa. Hatujawahi kuwa na rais maridadi kama huyu tuliyenaye na ndiyo maana waafrika wengi wanamlilia akatawale kwao.
 
Unazidi kuongea pumba tu,sijui ukileta imani Jf.. ndio nini sasa?!!!

Kama nina uhuru wa kuamini sasa tatizo liko wapi kuja kujadili imani yangu hapa JF?

Au kuna aliyekulazimisha kuamini kile anachoamini? wewe ukiona mtu anasema kuna Mungu(imani) unaweza kuacha kujadili maana hauamini,sio kukataza watu wasijadili imani.

Suala la Mungu ni imani na wewe kitendo cha kujadili hapa unajadili imani,hauwezi kulitoa hili jambo kwenye imani kisa wewe unajadili au linajadiliwa JF.
Mungu hajadiliwi kama imani tu JF, anajadiliwa mpaka kama fact.

Ukitakakujadii habari za Mungu kamaimani nenda kwenye nyumba yako ya ibada (kanisani, msikitini etc) au kaa kwako umjadili, sitakufuata.

JF ni public square.

Mungu wako hayupo,unaweza kutengeneza imani kwamba yupo, lakinihilo halimaanishi yupo.

Hayupo.

Ndiyo maana huwezi kuthibitisha kwamba yupo.
 
Hadi hapo haujaona kuna utofauti kwamba kuna uthibitisho na Mtazamo na ndiyo kitu nachokizungumzia hapa?
Katika set theory kuna union, intersection, set na subset.

Unaweza kuwa na mtizamo uliosubset ya uthibitisho, maana yake, mtazamo wote upo ndani ya uthibitisho.

Kama vile unavyoweza kuwa na mkoa wa Dodoma ulio katika nchi ya Tanzania.

Maana yake ukiwa katika sehemu yoyote ya mkoa wa Dodoma, upokatika nchi ya Tanzania.

Sasa wewe unachosema ni kwamba, mtizamo hauwezi kuwa ndani ya uthibitisho.

Unasema kwamba mkoa wa Dodoma ni mkoa wa Dodoma tu, hauwezi kuwa ndani ya Tanzania, kwa sababu wenyewe ni mkoa wa Dodoma.

Mimi nakwambia Bunge la Tanzania lipo Dodoma, hivyo lipo nchini Tanzania.

Wewe unabisha, unasema Bunge halipo nchini Tanzania, lipo Mkoa wa Dodoma.
 
Mungu hajadiliwi kama imani tu JF, anajadiliwa mpaka kama fact.

Ukitakakujadii habari za Mungu kamaimani nenda kwenye nyumba yako ya ibada (kanisani, msikitini etc) au kaa kwako umjadili, sitakufuata.

JF ni public square.

Mungu wako hayupo,unaweza kutengeneza imani kwamba yupo, lakinihilo halimaanishi yupo.

Hayupo.

Ndiyo maana huwezi kuthibitisha kwamba yupo.
Wewe kama nani hapa JF hadi uzuie kujadili imani???
 
Mimi nina visa viwili tu naomba unieleze kwamba kama si Mungu nini.
1.Kisa cha Tundu Lisu kupigwa risasi idadi ile then asifiwe utasema Mungu hajahusika kumuepusha na kifo?!
2. Kuna Bwana mmoja sitomataja lakini yupo hadi sasa alitekwa yaan alikua ndani ya basi walipofika sehemu flani basi likasimamishwa porini wakaamuru abiria wote kushuka,theni wakapanda wote isipokua huyo bwana,basi likaja gari lenye vioo vyeusi akasafirishwa huku anatajiwa makosa yake na kwamba mwisho wake umefika. Alivyofikishwa mahali flani akashushwa porini akakabidhiwa kwa jamaa,theni gari likageuza yule aliyekuwa amepangiwa kumumaliza jamaa kumbe wamesoma naye UDSM akasikitika sana akamwambia mshikaji kweli Una Mungu yaani ni wewe ndo umeletwa nikumalizie..ndo akawa amepona.
Kwa visa hivi eti hakuna mkono wa Mungu?
Mkuu watu wakila wakivimbia wanabana pua na kusema hakuna Mungu, kwanza tu jinsi watu wanvyo kutana na wenza wao wa ndoa ni ajabu tupu.
 
Kwa nini Bwana Mungu na si Bibi Mungu?

Huoni Bwana Mungu ni mfumodume wa watu tu wamejipangia?
Enenda zako Shetani wewe! imeandikwa; "kila dhambi watakazofanya wanadamu chini ya jua watasamehewa, lakini dhambi ya kumtukana ROHO MTAKATIFU haitasamehewa kamwe, siyo katika ulimwengu huu wala ule ujao".

Uu nani wewe unayeweza kumjadili MUNGU kama vile uwajadilivyo wanadamu wenzako??? Hivi kweli kinyago cha udongo kinaweza kumjadili yeye aliyekichonga?? Hivi chombo cha udongo kinaweza kumjadili yeye aliyekifinyanga??
 
Jibu nindiyo, BWANA MUNGU anajua kama utatenda dhambi kabla hata hujaitenda. Mfano mzuri BWANA MUNGU alijua kama Kaini anataka kumuua ndugu yake na ndiyo maana alimwambia hivi; "dhambi iko inakuotea mlangoni nayo inakutamani wewe, lakini yakupasa uishinde".

Kama Kaini angemsikiliza BWANA MUNGU na akaamua kuishinda dhambi, basi asingemuua Abeli.
Kwahiyo kila kitu ni mpango wa Mungu?
 
Katika set theory kuna union, intersection, set na subset.

Unaweza kuwa na mtizamo uliosubset ya uthibitisho, maana yake, mtazamo wote upo ndani ya uthibitisho.

Kama vile unavyoweza kuwa na mkoa wa Dodoma ulio katika nchi ya Tanzania.

Maana yake ukiwa katika sehemu yoyote ya mkoa wa Dodoma, upokatika nchi ya Tanzania.

Sasa wewe unachosema ni kwamba, mtizamo hauwezi kuwa ndani ya uthibitisho.

Unasema kwamba mkoa wa Dodoma ni mkoa wa Dodoma tu, hauwezi kuwa ndani ya Tanzania, kwa sababu wenyewe ni mkoa wa Dodoma.

Mimi nakwambia Bunge la Tanzania lipo Dodoma, hivyo lipo nchini Tanzania.

Wewe unabisha, unasema Bunge halipo nchini Tanzania, lipo Mkoa wa Dodoma.
Hoja yangu mtazamo ni mtazamo na uthibitisho ni uthibitisho.

Sasa wewe ulitoa mfano hapa et umeliona kabisa jua linawaka halafu useme et kwa mtazamo wako jua linawaka,kwanini utumie neno mtazamo na sio kusema tu jua linawaka maana ni kweli jua linawaka?
 
Enenda zako Shetani wewe! imeandikwa; "kila dhambi watakazofanya wanadamu chini ya jua watasamehewa, lakini dhambi ya kumtukana ROHO MTAKATIFU haitasamehewa kamwe, siyo katika ulimwengu huu wala ule ujao".

Uu nani wewe unayeweza kumjadili MUNGU kama vile uwajadilivyo wanadamu wenzako??? Hivi kweli kinyago cha udongo kinaweza kumjadili yeye aliyekichonga?? Hivi chombo cha udongo kinaweza kumjadili yeye aliyekifinyanga??
Unahubiri na kukemea, lakini hujathibitisha Mungu yupo bado.
 
Hoja yangu mtazamo ni mtazamo na uthibitisho ni uthibitisho.

Sasa wewe ulitoa mfano hapa et umeliona kabisa jua linawaka halafu useme et kwa mtazamo wako jua linawaka,kwanini utumie neno mtazamo na sio kusema tu jua linawaka maana ni kweli jua linawaka?
Kwa sababu inawezekana unafikiri unaliona jua linawaka, kumbe unaangalia TV nzuri sana ambayo imewekwa kama dirisha kukuonesha jua linawaka.
 
Katika set theory kuna union, intersection, set na subset.

Unaweza kuwa na mtizamo uliosubset ya uthibitisho, maana yake, mtazamo wote upo ndani ya uthibitisho.

Kama vile unavyoweza kuwa na mkoa wa Dodoma ulio katika nchi ya Tanzania.

Maana yake ukiwa katika sehemu yoyote ya mkoa wa Dodoma, upokatika nchi ya Tanzania.

Sasa wewe unachosema ni kwamba, mtizamo hauwezi kuwa ndani ya uthibitisho.

Unasema kwamba mkoa wa Dodoma ni mkoa wa Dodoma tu, hauwezi kuwa ndani ya Tanzania, kwa sababu wenyewe ni mkoa wa Dodoma.

Mimi nakwambia Bunge la Tanzania lipo Dodoma, hivyo lipo nchini Tanzania.

Wewe unabisha, unasema Bunge halipo nchini Tanzania, lipo Mkoa wa Dodoma.
Unaanza kunichosha tu,tatizo ulazimisha mtazamo uwe ndio uthibitisho wakati tumeshaona kuna uthibitisho na Mtazamo.

Mimi kwa mtazamo wangu naweza kusema wewe ni mwanamke lakini pengine sio mwanamke ni mwanaume, uthibitisho ndiyo utafanya niweze kujua bila shaka kuwa wewe ni mwanamke au mwanaume.
 
Wapi nimesema nazuia kujadili imani?

Tatizo hata kusoma hujui, unataka kujadili uwepo wa Mungu!
We ndio hujui unachokieleza.

Unvyosema nikajadili kanisani au msikitini,maana yake nini? ina maana hapa hautaki pajadiliwe imani bali ni huko msikitini na kanisani tu.
 
Kwa sababu inawezekana unafikiri unaliona jua linawaka, kumbe unaangalia TV nzuri sana ambayo imewekwa kama dirisha kukuonesha jua linawaka.
Vizuri sana na ndiyo maana nasema kuna mitizamo na uthibitisho.
 
Back
Top Bottom