Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

 
Mkuu Kalunya , mpaka uliopo kati ya Nguvu na Asili ni UPI? Maana kwangu Asili ni kisawe tu cha neno Nguvu.

Ni nini hasa kilifanya uwepo wa nguvu mbili, yaani Hasi na Chanya? Yaani Shetani na Mungu?
 
Hakuna Uchawi ulio mkuu hapa duniani kupita ule uliomo katika hoja za neno IMEANDIKWA....

Ukiashavalishwa huo Uchawi, Utumwa hautapotea kichwani mwako.
 
Mtumishi nimekuelewa kwanza Mimi namkubali zaidi mtu aliyekuwa gizani au aliyekuwa mtumishi wa shetani na akaacha na akaamua kumtumikia Mungu,huyu ndie mtumishi sahahi ambae Bwana amemuita sababu alikuwa kwa shetani akiamini ndie nguvu kuu kuliko Yesu,katika misukosuko yake shetani akashindwa kumsaidia na kumuokoa dhidi ya kombora toka kwa Yesu akageuka sasa kama shetani mwenyewe niliyekuwa namuabudu namtegemea amekula kona kaniacha nipambane na hali yangu dhidi ya Yesu, au walipokuwa wakienda kwenye nyumba za watu wa Mungu wanakuta moto wa gesi,mlima mkubwa,barafu,nk au walipokuwa wanaenda mahospitalini kuchukua vitoto vichanga vyenye ulinzi wa Mungu awasogei yaani wanakutana na moto wa kwann mtu huyu asione kumbe Yesu ndie mwenye nguvu zaidi kuliko shetani, kama shetani mwenyewe anakimbia. Utapambana vipi na shetani kama umjui vizuri anavyotenda Kazi, ukitaka kumjua adui ni vyema umjue. Kuwa mtumishi wa Mungu kwa kujifungia tu kwenye elimu ya Ukristo pekee bila kujifunza elimu zingine wewe bado ni mchanga, utajua vipi sasa utendaji Kazi wa ulimwengu wa roho, maana huwezi ongoa roho kama uujui vizuri ulimwengu wa roho. Hawa waliokuwa watumishi wa shetani wanaujua vizuri tena in deep zaidi ulimwengu wa roho kuliko mtu aliyepata elimu tu ya darasani bila vitendo. Zipo shuhuda za watu walikuwa gizani leo ni watumishi au ni Wakristo wazuri zaidi ya waliozaliwa kwenye Ukristo baada ya kuijua kweli,Tazama mtume Paulo kabla ndie aliyewaua Wakristo wengi sana kabla ajakutana na nguvu ya Yesu akiwa kwa shetani akiamini ndie nguvu kuu kuliko,baada ya kupata wongofu akawa Mkristo ndie aliyeanzisha makanisa mengi Sana na ndie aliyechangia Sana kuenea kwa Ukristo asia ndogo na ulaya mashariki,mtu alikuwa mchawi na jambazi Sugu ameua maelfu leo anamuhubiri Kristo akinifundisha ubaya wa dhambi kwann nisimuamini zaidi. Mimi nazungumzia elimu ya ulimwengu usioonekana tena elimu ya jumla sio category ya Christianity au Quran. Ukitaka kuujua ulimwengu usioonekana ambao upo pande mbili wa giza na nuru usijifungie tu kwenye elimu yako tu jifunze pia imani zingine wao wanasema nini.
Sijasema wanadamu wote Wana nguvu ya imani sawa ,nimesema mwanadamu kiasili ana asilimia moja, asilimia ya nguvu ya imani upanda au ushuka kulingana na mtu anavyotumika na upande aliouchagua.Wapo watu Wana nguvu kuliko majini kulingana na jinsi walivyojitoa kwa shetani, na kuna watu Wana nguvu ya imani asilimia 90 karibia ya Jesus.
Watu watajuaje madhara ya dhambi uchawi, wizi, nk kama wasipofundishwa na kupata shuhuda, mtu aliekuwa kwa shetani akatoka ni rahisi kwa anaetaka kuingia kwa shetani kusita sababu tayari anajua madhara kabla ya kuingia. Hio Efeso 3.20 tayari hapo ushataja nguvu kuu ambayo mwanadamu kajiunganisha nayo, sasa kama huna nguvu uliyojiunganisha nayo utasemaje unayo nguvu, maana nguvu yeyeto ni lazima itoke kwenye asili ya hio nguvu. Si Quran na Biblia pekee ndo zina habari kuhusu ulimwengu usioonekana, zipo elimu zingine zimeeleza kwa kina zaidi.
Yesu Kristo alikuja kuwakomboa watu watakao kukomolewa dhidi ya nguvu za giza so alikuja kuhubiri juu ya ufalme wa Mungu baada ya kuona wanadamu wanaangamia, wanateswa, akasema Mimi ndie njia ya uzima na kweli kwa jina langu mtazishinda nguvu za giza. Hapa Yesu kaongea kwa ujumla, sasa utazishindaje nguvu za giza kama ujui zitendavyo kazi Ili umshinde adui ni lzm umjue adui. Yesu hakufundisha kuhusu nguvu za giza lakini mwanadamu anateswa na nguvu za giza.
Waliokuwa watumishi wa shetani kama Sauli to Paulo ndio watumishi sahihi maana walikuwa kwenye giza wakidhani wapo kwenye nuru, baada ya kuijua Nuru ya kweli huwa watumishi wa kweli na sio watumishi wa sadaka. Mimi nimezungumza uKuu wa jina la Yesu kwa elimu ya jumla ikiwemo hata walio nje ya Ukristo.
Mtumishi usijifungie kwenye Ukristo pekee soma pia elimu zingine Ili uimarishe imani yako. Binafsi kupitia elimu zingine nje ya Biblia nimejifunza hakuna jina jingine kuu lenye nguvu kuliko jina la Yesu kwa ushahidi wa hata elimu zingine.
 
Reactions: _ly
Mkuu Kalunya , mpaka uliopo kati ya Nguvu na Asili ni UPI? Maana kwangu Asili ni kisawe tu cha neno Nguvu.

Ni nini hasa kilifanya uwepo wa nguvu mbili, yaani Hasi na Chanya? Yaani Shetani na Mungu?
Asili ni chanzo na nguvu ni uwezo wa kufanikisha jambo.
Ili nguvu iwepo ni lzm iwepo chanzo cha nguvu hio negative au positive.
Nguvu na asili vinategemeana nguvu haiwezi fanya Kazi kama hakuna asili.
Hakuna dhambi bila shetani. Hakuna wokovu bila Mungu.
Mungu kaumba dunia na kaweka vitu vyote vinavyoonekana na visivyoenekana, kaweka misingi ya ulimwengu. Shetani alikuwa kwa Mungu baada ya kulewa sifa na kuzijua siri akaingiwa wivu na tamaa ya kutaka kuumiliki ulimwengu. Mungu akaona hila ya shetani akamfukuza toka mbinguni pamoja na malaika zake waliomuasi Mungu. shetani akaweka bifu na vita ya kupambana na Mungu. Shetani ni mpinzani wa Kazi ya Mungu ulimwengu akaanzisha nae sheria zake kupitia zile za Mungu ambazo zinaitwa dhambi mfano ua, zini, iba, uwongo, abudu mizimu, tumainia waganga wa kienyeji, na vyote kinyume na Mungu. So nguvu nyanya zinatoka kwa Mungu na hasi kwa shetani na hizi nguvu uoenekana kupitia matendo.
 
Yesu ndio chanzo cha uzima wangu, nilishawahi kugongwa na treni, licha ya kwamba gari yangu iliharibiwa kabisa lakini mimi binafsi nilitoka nikiwa mzima kabisaaaaaaaaa
Kwanini asikuepushe kabisa na tukio hilo, mpaka amekuacha ugongwe, upata hasara ya gari.

Ulimkosea nini mpaka akakuacha, unaingia kwenye ajali, iliyekupa hasara.

Yesu kwako anakulinda wewe tu, mali zinajilinda zenyewe.
 
Unatofautishaje Maangamizo ya Uchawi na yale ya Mungu?

Wachawi wanaua watoto wadogo, sawa na Mungu katika maandiko.

Unatofautishaje?
Wachawi wanauwa watoto wadogo ambao hawana ulinzi wa damu ya Yesu Kristo kwa ajili ya Kazi za kichawi au kujiimalisha kichawi au kumtolea sadaka shetani afurahi Ili awape kile watakacho.
Watoto wachanga ni bidhaa ghali Sana kwa wachawi ikiwemo kutengeneza mafuta ya upako,na Kazi zingine.
Tofauti ya maangamizo ya kichawi na ya Mungu.
Mungu amchukui mtu ambae ajamaliza miaka yake aliyopangiwa kuishi.Wachawi uua mtu asiye na ulinzi wa Mungu kwa interest zao kama ni kuwafanya misukule kwa Kazi za dukani, mashambani, kafara ya utajiri, vyeo, madaraka, matambiko, kufanya Kazi kuzimu, au kuwala nyama, nk. Kuna vifo vya aina mbili cha Matakwa ya wachawi na cha Matakwa ya Muumba.
 
Kwanini asikuepushe kabisa na tukio hilo, mpaka amekuacha ugongwe, upata hasara ya gari.

Ulimkosea nini mpaka akakuacha, unaingia kwenye ajali, iliyekupa hasara.

Yesu kwako anakulinda wewe tu, mali zinajilinda zenyewe.
Ili uKuu wake ujihidhirishe kwake na hata kwa wengine wapate shuhuda ya kwamba ukimtumaina Yesu Kristo hawezi kukuacha yatima.
Je wajua ya kwamba katika usafiri wa mabus hata abiria mmoja tu akisali na kuomba ulinzi wa damu ya Yesu Kristo bus haliwezi onekana kwenye radar za wachawi barabarani Ili litolewe kafara.
 
Ni mpaka upibuliopo kati ya Asili/Chanzo na Nguvu? Maana kwangu bado hicho ni Kitu kimoja.

Unasema ili kuwa na Nguvu ni lazima kuwe na Chanzo, na kwa mujibu wako umedai Mungu ni Positive Energy na Shetani ni Negative. Je, ndio kusema kwamba kuna kilicho juu ya Mungu? Yaani ASILI?

Lakini pia, ni nini kinakufanya uipersonalize Nguvu, iwe hasi au chanya? Nguvu inavaaje Sifa na kuenenda kwa mihemko ya kibinadamu, amabayo kwa wazi kabisa inatambulika kuwa ni zao LA mwili?

Shetani akalewa Sifa, Mungu akaona/akamfukuza....nk.. Kwanini unazivisha hizi nguvu sifa za kibinadamu?

Kwangu Ukamilifu uko katika Umoja, ni kutokuwa na upande wa Pili.

Unachokiita keo kuwa Dhambi, vyote vimeshawahi kufanywa na Mungu wa vitabuni, je naye ataandikiwa hizo dhambi?

Mkuu, IPO Nguvu moja tu nayo ndiyo ASILI, ukiamua kuiita Mungu au Shetani ni sawa tu. Ila cha kuzingatia UNAPOITII INATENDA, na UNAPOIKIUKA INATENDA VILEVILE.
 
Kwanini asikuepushe kabisa na tukio hilo, mpaka amekuacha ugongwe, upata hasara ya gari.

Ulimkosea nini mpaka akakuacha, unaingia kwenye ajali, iliyekupa hasara.

Yesu kwako anakulinda wewe tu, mali zinajilinda zenyewe.
Alilala.
 
Yaani hata mbwa analinda mtoto wa bwana wake anaposogelewa na hatari, Ila huyo Yesu amekaa tu anaangalia mtoto mdogo akidhurumiwa uhai naye yupo tu asimpe ulinzi?

Mbwa wa namna hiyo nyumbani hufukuzwa.

Katika biblia, Mungu aliamuru kuuliwa watoto wadogo wakiume huko misri? Unatofautishaje hilo na Uchawi? Usiukimbie Ukweli. Mungu aliruhusu na kubariki Uzinzi wa mtu na watoto wake, nk...
Unatofautishaje na kazi za umuitaye shetani?
 
Kwanini asikuepushe kabisa na tukio hilo, mpaka amekuacha ugongwe, upata hasara ya gari.

Ulimkosea nini mpaka akakuacha, unaingia kwenye ajali, iliyekupa hasara.

Yesu kwako anakulinda wewe tu, mali zinajilinda zenyewe.
Ili aonyeshe ukuu wake
 
Kumbe serikali inakosea sana, Wanapo waasa madereva, kuwa tahadhari ya usalama barabarani, kumbe ajari zinasababishwa na Wachawi.

Hao wengine watapataje Shuhuda, ikiwa kuamini ajali ile amekuponya yesu inabaki kwa muumini, asiamini bila kumuona yesu akifanya uokoaji ataamini vipi.
 
Panapo original na feki nayo ipo.Watu wanashindwa tofautisha Kati ya Christianity na white magic,kuna mitume na manabii feki na original, na huu ni msiba wa dini zote hizi mbili kuna watu ni mashehe lakini ni waganga na wanawaongopea watu kwa kuwahadaa kutumia vitabu vya Mungu, ndo hao udanganywa watu kwamba kuna jini mzuri na kuna jini mbaya Ili kuwahadaa waumini, hawa wote ni washirikina tupu jini ni kiumbe kilichomuasi Mwenyezi Mungu toka lini kikawa kizuri, jini ni shetani na Kazi ya shetani ni kuuwa, shetani hana urafiki kabisa na mwanadamu hata kama atampa utajiri na mali lakini mwishoni ni lzm atamuua tu baada ya kumaliza ndugu zake.
Mfano zumarid anafanya white magic na sio Christianity, chochote kile kifanyikacho nje ya maandiko siyo cha Kikristo. Hata Yesu alionya watakuwepo Ma Yesu wengi kuwaadaa watu.
 
Serikali haishughuliki na mambo ya ulimwengu usioonekana bali unaonekana.
Yesu ni roho, Yesu ni nguvu, huwezi ona roho au nguvu katika ulimwengu wa mwili
 
Hao watoto waliouliwa na huko Misri ndo kwanza taarifa hizo napata kwako,liweke wazi hili.
Ili la uzinzi wa mtu na watoto umelipata wapi kwangu ni geni
 
KILA mtu ana utashi wake na uamua upande autakao kulingana na interest zake.Hakuna mipaka Kati ya nguvu na asili.Mwanadamu ni roho na roho ndio utenda Kazi ndani ya mwanadamu.Roho ni nguvu.dhambi ni roho chanzo ni nguvu hasi.
 
Serikali haishughuliki na mambo ya ulimwengu usioonekana bali unaonekana.
Yesu ni roho, Yesu ni nguvu, huwezi ona roho au nguvu katika ulimwengu wa mwili
Ila hakuna aneweza kuendesha gari, kanuni za usalama barabarani, Ukitegemea Yesu atakuokoa.

Yesu ni imani tu, na kupitia imani watu wamejitengenezea flusa, sasa ni matajili kuliko watu wanaojihangaisha na biashara.
 

Ni kweli hata biblia lazima ziko Za feki Na iko halisi lakini ni biblia ipi ya kweli ndio kishindo kuijua kwani Yesu hakuleta biblia wala hakuandika kitabu chochote . Wala Hakuna aliyeandika chochote kuhusu alichosema yeye wakati alipokuwepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…