u upumbavu wa kudhani imani yako ni bora kuliko kuliko ya mwingine, iliniganya ninunue bibilia nisome ili niwe najibu kwa mstari, humu tulikua na akina mgeni na wakristo wengine wenye majina fulani ya kishoga.
Lakini mwisho wa Siku tulikubaliana, Uwe Muislam uwe mkristo maisha ni yale yale Shida raha tunaziishi wote, bila kujali imani yako.
Hivyo kubisha hapa ni upumbavu tu, imani yako kama ndiyo bora kwanini ulalamikie kupanda kwa mafuta, kwanini Mungu wako asikurahishie eneo hilo, ili tabu muachie wasiamini kwenu.
Mtu anafunga Ramadhini yake kwa imani yake, alafu anatokea mjinga mmoja, anakosoa kupitia bibilia, huu si ujinga, yeye hafungi kupitia bibilia yako.
Kitabu chenu nimempa rafiki yangu John Ndongo, Ujinga uishie Mbali, Mungu hawezi kukuacha Salama ikiwa huheshimu wengine, Maana kwa mkosaji nini yeye mwenye uwezo wa kumuonyesha njia sahihi nae ndiye mwenye Kuhukumu.
Ila mkilianzisha sikai ki
Yesu alionya, lakini Paulo hakusikia:
"Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na wakawararua."
Yaliyosemwa yamekuwa. Kwa kitendo cha Paulo kuwaingiza mapagani wa Kizungu katika dini ya Yesu sharia ya Mwenyezi Mungu ikaambiwa ni laana, ikatolewa ruhusa kula nyamafu, nguruwe na damu, na kila kiuzwacho sokoni bila ya kutia wasiwasi wo wote katika dhamiri.
Tohara aliyoamrishwa Ibrahimu na Mwenyezi Mungu na Manabii wote wakaifuata mpaka mwenyewe Yesu na wanafunzi wake, Paulo aliipuuza kuwaridhi makafiri. Imani za kipagani za mungu mwana na utatu zilizoenea katika mila za Mithra, Osiris, Attis n.k. zikaingizwa katika dini ya Kikristo.
Katika ufalme wa mbinguni Yesu ana yakini kuwa hatokuwa nao ila wana wa Israili tu. Injili ya Mathayo inasema:
Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
Mathayo 19.28
Hata katika maombi yake inaonyesha kuwa Yesu alikuwa anajua mipaka yake na uwezo wake.
Madai ya kuwa yeye ni mwombezi, mbali kuwa ni mwokozi, wa ulimwengu mzima ni kumsingizia jambo ambalo mwenyewe hakulidhania.
Kumpa mtu cheo asichokuwa nacho ni kumtukana, ni kumvika kilemba cha ukoka, kama Mayahudi walivyotaka kumkejeli kwa kumvika taji la miba.
Cheo alicho nacho kwa hakika si kidogo. Kuwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa Mitume na Manabii watukufu ni jambo kuu kweli kweli.
Kuwa mtumishi wa Mwenyezi Mungu mwenye kupendeza si utukufu mdogo.
Na Yesu alitafakhari nao, na alitafakhari kuwa yeye hakutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa Ki-Israili.
Na hayo si kwa upungufu wo wote kwa upande wake, ila ni kuutumikia ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa kuulinda usiharibiwe na washirikina mpaka ufike wakati wa kuja huyo atayekuwa kazi yake ni kuitangazia risala ya Mungu kwa ulimwengu mzima.
Katika Injili ya Yohana ananukuliwa Yesu kusema:
Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa.
Yohana 17.9
Ni jambo linalojuulikana katika historia - na hata ukisoma katika Biblia kitabu cha Matendo ya Mitume utaona - ya kuwa Ukristo kwanza haukuhubiriwa kwa mataifa mengine mpaka alipoingia Paulo.
Na yeye alipingwa vikali sana kwa kutoa shauri hiyo na wanafunzi wake Yesu waliomwona na wakawa naye siku zote na wakajifunza vilivyo mafunzo yake na makatazo yake ya kwenda kuwahubiria watu ambao bado ni makafiri.
Ukristo tuuonao na ulioenea ulimwenguni sio Ukristo aliofundisha Yesu. Wa Yesu ulitoweka na mwenyewe na wafuasi wake wa mwanzo wa kabila la Kiyahudi. Paulo kaufuja Ukristo.
Kauli zinazonukuliwa kwa kudai kuwa ni ushahidi kuwa Yesu mwenyewe alitaka mafunzo yake yakafundishwe kwa ulimwengu wote yamo katika Injili ya Mathayo 28.19-20, Injili ya Luka 24.46-49 na Marko 16.15. Mathayo inasema:
Basi, enendeni, mkwafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Mathayo 28.19-20
Luka anatwambia:
(Yesu) akwaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya. Na tazama, naweletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kueni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
Luka 24.46-49
Na Injili ya Marko inasema:
(Yesu) akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
Marko 16.15
Je, imekuwaje?
Yesu ni kigeugeu?
Mbona huku anawakataza wanafunzi wake wasende kuwahubiria ila kabila kumi na mbili za Israili, na huku anawaambia nendeni kuwahubiria Injili ulimwengu mzima.
La, Yesu si mbabaishi, wala si kigeugeu.
Hebu natuziangalie vilivyo hizo amri mbili, moja ya kuwa mafunzo yake wasifunzwe ila wana wa Israili tu, na ya pili ni hii ya kuwa watu wote wafunzwe dini.
Vipande vyote vitatu tulivyonukulu mwishoni havitaji mambo ya Yesu alipokuwa na maisha yake ya uhai wa kidunia, lakini vyaeleza mambo yaliyotukia baada ya "kufufuka kutoka wafu" kama inavyosimuliwa na Injili zote tatu.
Yajuulikana kuwa Injili ya mwanzo kuandikwa ni Injili ya Marko. Hizo nyingine ziliandikwa baadae, na labda ujuzi wao ulitegemea hiyo hiyo Injili ya Marko.
Yajuulikana vile vile kuwa maneno yote yaliyohusu kufufuka Yesu kutokana na wafu, pamoja na hayo maamrisho ya kwenda kuihubiri Injili "kwa kila kiumbe", kinyume na maamrisho yake yote ya kuwa asihubiriwe ila Muisraeli tu - maneno hayo yote hayakuwamo katik Marko ya asli, bali yaliongezwa baadae.
Encyclopaedia Brittanica, nakla ya 11, jalada 17, sahifa 730, yasema ya kuwa kipande chote hicho kiliongezwa baadae, yamkini mwanzo mwanzo wa karne ya pili, kuchukua maneno yaliyopotea, au yaliyoonekana kuwa ni mapungufu.
Kama nilivyosema mwanzo
w a l e j a m a a (Yahaya mpe MIC) wamewapoteza sana,na inaonekana mna program maalum yakufanya upotoshaji.Nimegundua uwezo wenu sasa naomba uniruhusu nikufundishe kama mtoto wa darasa la kwanza,nimeona jinsi ninavyokuelezea huelewi una lengo lako,najua kabisa unajua unachokifanya na unawajua na ndugu zako mnaoshirikiana nao kuweka sumu,ndiyo sababu,huna vitu vyako wewe kama wewe,mambo mengi unayoyaandika tukiyatafuta tunayakuta mitandaoni yanafanana.Hii inaonyesha umekalilishwa au umepewa maswali fulani ndiyo sababu hutoki na haujibu maswali yangu ila unaendelea kuleta maswali yako.Unashindwa kujibu maswali yangu kwa sababu haya ninayoukuuliza huna desa.
Sasa nirudi nikufundishe kwa technique nyingine kama hii nayo hautailewe basi tutaendelea kukuombea
Mfano wa kwanza:Wewe ni mfanya kazi, mnafanya kazi ya kusambaza mboga mikoa ya Tanzania,boss anatoa maelekezo mwezi huu wa nne,tutapeleka mboga Arusha peke yake ,msipeleke maeneo mengine.Sawa ?Sawa boss.Maagizo haya yanarekodiwa kwenye vitabu ya kwamba boss alisema tutapeleka mboga Arusha peke yake.
Mnafanya kazi ya kupelaka mboga Arusha,baadaye siku za mbele boss anawaagiza pelekeni mboga miko yote ya Tanzania.Taarifa hii pia inarekodiwa ya kwamba boss aliagiza tupeleke mboga Tanzania yote.
Hapa shida yenu kwa kuwa boss alisema mwanzoni tutapeleka Arusha tu,mnapinga maagizo yake ya kuepeleka mikoa mingine.Pia hamtaki kukubali kwamba katika kujifunza kuna formal way na informal.Hamuwaamini wanafunzi wa Yesu ya kwamba walichokiandika ni kweli Yesu alisema?Kwa lugha zingine mimi leo nije nikubishia wewe juu ya somo mlilofundishwa Ijumma iliyopita pale ulipoenda kuswali.Nikatae ya kwamba mlichofundishwa siyo hicho,yaani mtu amabaye hakuwepo anabisha na na watu waliokuwepo?Huyu mtu akili yake iko sawa?
Biblia huwa haijipingi isipokuwa sisi ndiyo tunashindwa kuelewa ,sasa ukisema Paulo ameleta mafundisho mapya?
Nokusaidie katika ukristo wa kweli hatufanynhudumamkwa akili zeti wenyewe yupo anayetuonhgoza katika huduma hiyo.Paulo alichaguliwa na Mungu kwa kazi maalum,kwa hiyo hakuna sehemu alienda kufanya kazi kwa matakwa yake mwenyewe.
Mfano wa pili:Baba yako ametoa maelekezo kwamba nataka mfanye usafi wa ndani ya nyumba tu ndicho nilichopanga,sawa?Sawa baba.Alichokisema kikaandikwa kwenye vitabu vya kumbukumbu.Baada ya mwezi anawaagiza enendeni mtaani,mpite kila nyumba mfanye usafi nje ya nyumba hizo.Hili agizo la pili linachelewa kutekelezwa,linakuja kufanyiwa kazi baadaye.Je ni sahihi mtu akikubishia akakuambia wewe Baba alisema tufanye usafi nyumbani kwetu na siyo kwingine?Mtu huyu anyebisha pasipo kuwa na hoja za msingi ni wewe na hao ndugu zako.Hoja zenu ni dhaifu sana hazina ushadhidi zaidi ya kutumia technique za ujanjaujanja kuwachanganya watu,kisha unawafanya waone unachosema wewe ni sahihi.
Soma Matendo 13:2
"Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu aliwaambia, “Nitengeeni
Sauli na Barnaba
kwa kazi maalumu niliyowaitia.”
Sasa Mungu mwenyewe anasema atengewe Sauli(Paulo) amemwita kwa
kazi maalum,wewe huna hata umri wa miaka 120 unabisha kwa sababu ya document na vitabu vilivyojaa mawazo ya wanadamu vinavyopotosha kweli?
Mathayo 28:19 Yesu anawaagiza waende wakawafundishe mataifa wote...Wewe na wenzako mnataka wabaki na maelekezo ya mwanzo ya kufanya kazi kwa Wayahudi?Unachokifanya ni kama mfanyakazi anakataa maagizo mapya anayopewa na boss wake na kung'ang'ania alichoambiwa jana?Samahani umeajiliwa au umejiajili?Nisije niaka naongea na kukupa mifano ambayo ni giza kwako?Amacho hamjuini kwamba Yesu alikuwa na kazi anaifanya hivyo alikuwa anatoa maelekezo,leo atatoa maelekezo haya na kesho mengine ili lengo la kuja kwake litimie.Sasa kitendo chenu cha kung'ang'ania tu amelekezo fulani ili mtimize agenda yenu ya siri hatuwezi kunyamaza,taratibu watu wataujua ukweli na nitaendelea kuweka wazi technique zenu mpaka ndugu zako watampokea Yesu awe Bwana na mwokozi wao.
Kitu kingine nikusaidia ukawaambie na jamaa zako wale wanafunzi hawakujiita wao Wakristo bali waliitwa kwa mara ya kwanza kwenye mji unaitwa Antiokia(uko Uturuki ya sasa) kwa hiyo jamaa walipeleka injili mpaka Turkey wewe unasema kwa Wayahudi peke yao?Unapingana na Biblia na unapingana na historia.Hivi na Damscas ni Isarel?Jamaa walifika huko,tatizo humjui Mungu wetu na jinsi anavyofanya kazi.Kama ingekuwa siyo mapango wake injili iende kwa watu wengine angewazuia.Na kama ulikuwa hujui hata hayo makanisa 7 ya kwenye ufunuo yako Uturuki ,sasa mnapojadili muwe na hoja zenye nguvu.
,kama ambavyo mnang'ang'ani tuwape ushahidi wa wapi Yesu alijiita mwenyewe mwana wa Mungu?Mmekuwa kama mmejitoa ufahamu,unajua watu wana majina ,mara nyingi mtu anaitwa jina lake na watu wengine mara chache anajiita mwenyewe.
Biblia ni kitabu kizuri ,naamini unajua maana ya a.k.a (inawezekana hujui,nikifupi cha "also known as") ingekuwa leo yamkini Yesu angeiwa Mwana wa Mungu ak.a Mwana wa Adam.ak.a Mwana wa Daudi, kumbe kwa lugha nyingine a.k.a ilianza siku nyingi Sauli a.ka. Paulo.Sasa nyie shida yenu siielewi inaonekana kuna kitu mnataka mkifikie lakini ni kuambie hamtaweza kwa sababu Mungu wa Israel ni mkuu.Kama ambavyo taifa la Israel limeendelea kuwepo( pamoja na Iran kusem ni uvimbee ambao unaweza ukatumbuka muda wowote )ili uwe ushahidi wa habari zake zilizojaa kwenye biblia pamoja na chuki za mataifa wanayomzunguka ingawa siku hizi wamegundua wanaanza kushirikiana naye ,wewe tu bado umekomaa na madesa yako.
Je Yesu ni kigeugeu?Yesu siyo ,hajawahi na hatawahi ,shida ni nyie mnaolazimisha mambo yawe mnavyotaka nyie kwa makusudi yenu ambayo hamuwezi kuyaweka hadhalani,lakini najua unayajua au unatumiwa ila huyajui .
Nikuulize kitu,wewe unaamini nini katika Biblia ?Kipi kiko sahihi ambacho kiko ndani ya Biblia?
Naomba pia urudi shule ujifunze nini maana ya "passive na active speech" inaonekana katika Biblia hamtaki kutambua "passive speech".Ila mnaposoma magazeti yanaandika "mwanzo wa kunukuuu..." mwisho wa kunuuu" au mkiangalia TV mtangazaji akisema "namnukuu" hayo mnayakubali ila ya Kwenye biblia yamepotoshwa.Waandishi wakiandika Rais alisema "......." Mnakubali ila Biblia ikiandika "Yesu alisema..."Mnakataa.Kazi kwelikweli
Kuna maswali niliuliza usidhani nimesaahau nahitaji jibu,
1.Je huwa mnavaa pete za ndoa?Na kama huwa mnavaa,mnavaa zaidi ya pete moja?Kama huwa hamvai zile pete wanavaa wakubwa wenu zinakazi gani?
2.Ulisema Yesu siyo mwana wa Mungu yeye mwenyewe alijiita mwana wa Adam,nilikuuliza Yesu anakuwaje ni mwana wa Adam wakati tunajua alizaliwa na bikra Maria kwa uwezo wa Roho Mtakatifu?Naamini mnaijua Biblia vizuri kuliko sisi ndiyo sababu nataka jibu kutoka kwako mwananzuoni.lakini pia pita Mathayo moja,juu ya ukooo wa Yesu ameitwa tena Yesu mwana wa Daudi,mwana wa Abraham,tusaidie majibu mwananzuoni wetu ila usikimbie,taratibu tutaelewana.