Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Wacheni kudanganyana, someni Biblia...

Mathayo 7:
21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
 
Kuna dini ina uhusiano wa karibu na mapepo na mashetani, wao ni wapinga Kristo, watapinga kila kitu, watasema Yesu hajawahi kuponya wala kutoa pepo, ili tu aonekane sana na yule karani wa mama mfanyabiashara ambaye alioa katoto ka miaka tisa
umeambiwa ushuhudie yesu amekutendea Jambo gani seems like hakuna alichokutendea imebidi uhamishie mada upande wa pili. pole mkuu maumivu yako hayana dawa unaumia watu kumpinga Yesu wakati wapo watu waliishi nae na walimuona live kipindi Cha uhai wake na walimpinga hata huyo unaemuita karani hajakuepo maana unaumizwa na uwepo wa huyo karani utafikiri yeye na wafuasi wake ndo walimgonga misumari na kumtundika kwenye mti Mungu mtoto wenu.
 
Yesu ndio chanzo cha uzima wangu, nilishawahi kugongwa na treni, licha ya kwamba gari yangu iliharibiwa kabisa lakini mimi binafsi nilitoka nikiwa mzima kabisaaaaaaaaa
 
Ajali ya treni nilipatia hapo Kamata nikitoka kwenye soko la Kibasila miaka mitano nyuma
 
Yataje mapenzi ya Mungu yanahotajwa kwenye mistari hiyo uliyoiweka
 

Movie nzuri sana ile,jamaa alisimamia imani yake mpaka mwisho...
 
Katika hali ya kustaajabisha mwanzoni mwa mwaka 2012, nyumbani kwetu tuliingia vita ya kiroho kati yetu sisi na jirani aliye kua mganga wa kienyeji (R.I.P)

Yule mganga ilifika kipindi akamtupia pepo la uchizi dada angu awali katika kustaajabu hali kama ile tulianza kwenda hospital kujua hali yake ki afya kama amepatwa na maralia kali au kuna kingine, tulimkuta ana maralia ringi 15 akatumia sindano ya dozi lakini hakutengemaa.

Tuliona ile vita si ugonjwa wa maralia ikabidi tumfanyie maombi maarumu kanisani alikaa siku tatu pale kanisani yale mapepo machafu yalimtoka na kawa safi mpaka leo.

Baada ya mwaka mmoja vita ikarud kwa mama hii haikudumu sana. Naye pia alirushiwa pepo la uchizi akawa anacheka cheka tu kwakua tayari iliwahi kutokea kwa sister tuliingia moja kwa moja kwenye maombi tukitumia mamlaka tuliyo pewa na Mungu kupitia jina la Yesu kristo tukafurumisha mapepo wachafu wakatajana mpka walio watuma wakaondoka.


Miezi michache mbele yule mganga alianza kuugua ugonjwa ambao ulisababisha kifo chake.

Hakika Yesu ni Mkuu alitutendea Makuu bila gharama yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Sasa liondoweni pepo CCM Kama unasema kweli
 
Nilikuwa na interview kwenye taasisi moja kubwa ya umma, hapa nchini; mara ghafla mida ya saa 9 usiku nikiwa usingizini nikasikia sauti ikiniamsha amka uombe maana Kristo amekusudia kukupa hii kazi, hitaji lako la kazi Mungu amelisikia na anakwenda kukutendea muujiza, amka uombe, usiache kuomba

Kweli nikaamka, nikakuta kwenye radio kuna maombi yanaendelea ya kuombea watu wanaokwenda kwenye interview siku inayofuata

Nikafuatilia hayo maombi hadi alfajiri yalipokwisha

Nilikwenda kwenye hiyo interview najiamini sana; nilishinda hiyo interview bila rabsha yoyote, kwenye Oral interview niliulizwa maswali mawili tu...nieleze nitafanya nini kipya nikipewa hiyo kazi na swali la pili ningependa nilipwe mshahara kiasi gani..

Mwaka wa 4 huu sasa niko kazini, maisha yamebadilika; JINA LA KRISTO YESU NA LIHIMIDIWE!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…