Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Ukiamua kuilazimisha akili yako kutafuta vikasoro kwenye jambo huwezi kosa
kulingana ndio maana yake nyengine ?, mbona unazunguka mbuyu au kiswahili kinakupiga chenga?
 
Yesu si Mungu nje ya imani ya Ukristo.

Tutazame Biblia inasema nini katika jambo hili?

Mt Paulo katika barua yake ya kwanza kuwapelekea Wakorintho aliandika:
Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
1 Wakorintho 15.15

Juu ya kuwa Paulo anaambiwa ya kuwa akiamini kuwa Masihi (yaani Kristo) na Mwenyezi Mungu ni kitu kimoja hapa anasema: "Tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo."

Ikiwa Mungu kamfufua Kristo, hawawezi kuwa wote wawili hao ni mtu mmoja.

Mmoja alikuwa ni mtenda, mfufuaji, na wa pili alikuwa ni mtendwa, mfufuliwa. Kama Kristo ni Mungu mwenye uwezo wa kufufua basi maelekeo ni kusema: "Kristo kajifufua", sio kafufuliwa.

Mwenye kufufuliwa ni mfu asiyejiweza kitu.

Katika kitabu cha Matendo ya Mitume inasimuliwa kuwa Mt Stefano alisema aliyoyaona yaliyo mbinguni. Alisema:
Tazama! naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
Matendo 7.56

Mwana wa Adamu ndiye Yesu, na kwa jina hilo ndio mwenyewe akipenda kujiita, sio Mwana wa Mungu. Hapo basi huko mbinguni Stefano anasema anamwona Yesu kakaa mkono wa kulia wa Mungu.

Mwenye kukaa mkono wa kulia wa fulani hawezi kuwa ndiye yule yule fulani. Hayo ni maelezo ya mbinguni.

Ni wazi basi kwa ushahidi wa Biblia kuwa Yesu hakuwa Mungu mbinguni kama alivyokuwa si Mungu duniani.

Yesu alipokimbilia kwenye Mlima wa Zaituni na huku akisakwa na Mayahudi alijitenga na wanafunzi wake. Huko faraghani aliomba hivi:


Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.
Luka 22.42-43

Hapa tunaona mambo matatu muhimu:

Yesu anamwomba Mungu. Yesu anamwabudu Mungu. Wawili hao ni mbali mbali, na vyeo vyao ni mbali mbali. Yesu ni mtumwa mnyonge mwenye kuomba na kuabudu. Na Mungu ni Mwenyezi Mungu mwenye uwezo wote na mwenye kustahiki kuabudiwa pekee, hata na Yesu, mwenye kutakiwa msaada pekee, hata na Yesu.

Mapenzi ya Mungu ni mbali na yale ya Yesu. Yesu hataki kuuliwa, ananyenyekea na kuomba kwa Bwana wake: "uniondolee kikombe hiki" cha mauti.

Yesu hana azma hata chembe ya kufa msalabani, kifo cha mhalifu, kifo cha laana kama maadui zake Mayahudi walivyoazimia kumpatilisha nacho. Lakini anakiri kuwa ni mapenzi ya Mungu sio yake yeye yatendeke. Yeye hana hila wala nguvu za kuzuia kudra ya Mwenyezi Mungu.

Yesu, Mwana wa Adamu, anakata tamaa. Imani inampunguka. Kavunjika moyo. Ikabidi "Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu."

Jee, yaelekea kuwa Yesu ndiye Mungu? Yaelekea kuwa yeye na Mungu kuwa ni sawa? Kama upo wasiwasi wo wote wa kujibu hayo, mwenyewe Yesu anajibu kama anavyo hadithiwa na Yohana kuwa kasema:
Baba ni mkuu kuliko mimi.
Yohana 14.28

Na mwishoni naye yupo mslabani:
Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
Mathayo 27.46

Yafaa hapa tujiulize: Yesu akimlilia Mungu gani hapo msalabani ikiwa naye mwenyewe ni Mungu?

Au nini alikusudia aliposema: "Mungu wangu naye ni Mungu wenu"?

Maneno hayo kama yanaonyesha cho chote basi yanaonyesha unyenyekevu wa Yesu mbele ya Mungu wake.

La kustaajabisha ni kule kukata tamaa kwake na kuvunjika moyo. Huwaje mtu wa imani, licha ya nabii na mwana pekee wa Mungu, akate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Ama kuwa Mungu akate tamaa na Mungu, na kumyayatikia: "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha", ni jambo ambalo halimkiniki kuwa.

Kwa uthibitisho ulio wazi Biblia inatwambia kuwa Yesu si Mungu, wala Mungu si Yesu
 
Desmond Doss alikua ni mwanajeshi kutokea Marekani, alishiriki Vita Ya Pili Ya Dunia kama mtoa huduma ya kwanza. Kipindi chote cha vita alikataa kushika bunduki au kuua adui kutokana na imani yake (alikua ni msabato). Vitani aliweza kuokoa wanajeshi takribani 75 na kupokea medali nyingi za heshima. Alifariki mwaka 2006, Filamu inayohusu maisha yake inaitwa Hacksaw Ridge (2016) iliigizwa na Andrew Garfield
Ukishasema filamu iliigizwa na basi hamna uhalisia hapo ni maigizo ilitakiwa filamu ya matukio iliyorekodiwa hayo matukio yakimtokea siyo ujinga
 
Nini according , sikiliza clip hii


Ni kwa mtazamo wake yeye na si kwa mtazamo wa waamini.
Ni SAwa na wanazuoni wasemao uislamu ulianzishwa na mapadre watano walioasi ukatoliki wakipinga suala la kutooa.
 
Ni kwa mtazamo wake yeye na si kwa mtazamo wa waamini.
Ni SAwa na wanazuoni wasemao uislamu ulianzishwa na mapadre watano walioasi ukatoliki wakipinga suala la kutooa.
Si kwa mtazamo Wake yeye ni Hao walioziandika biblia ndiyo wanaosema
 
Ni kwa mtazamo wake yeye na si kwa mtazamo wa waamini.
Ni SAwa na wanazuoni wasemao uislamu ulianzishwa na mapadre watano walioasi ukatoliki wakipinga suala la kutooa.


Aramai ilikuwa ndio lugha iliyokuwa ikitumiwa na Mayahudi huko Palestina. Kwa hiyo, inaaminika kuwa Yesu na wanafunzi wake walizungumza na kufundisha kwa Kiaramai. “Simulizi za kwanza ya mdomo za matendo ya Yesu na kauli zake bila shaka zilisambaa kwa Kiaramai.

Hata hivyo, Injili nne ziliandikwa kwa ukamilifu wake kwa maneno mengine, Kiyunani ya kawaida, lugha iliyokuwa ikitumika katika dunia ya Kistaarabu ya Mediterania, ili kutumikia wengi katika Kanisa, ambayo ilikuwa ni ya Kiyunani (wenye kuzungumza Kigriki) badala ya Kipalestina.

Mabaki ya Kiaramai yalikuwepo katika Anaajiyl za Kiyunani.

Kwa mfano, katika Marko 5: 41, “Kisha akamshika mkono, akamwambia, ‘Tal’itha cu’mi’, maana yake, ‘Msichana mdogo, nakuambia amka’”.

Pia Marko 15: 34: “Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, ‘Eloi, Eloi, lama sabachthani?’ maana yake, ‘Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?’” (Encyclopedia Americana, Mj. 3, uk. 654).



Injili ya Marko katika Agano Jipya, japokuwa inachukuliwa na wanazuoni wa Kanisa kuwa ndio kongwe kabisa kati ya Anaajiyl, haikuandikwa na mwanafunzi wa Yesu. Wamehitimisha wanazuoni wa Biblia, kutegemea na dalili zinazopatikana katika Injili, kuwa Marko mwenyewe hakuwa mwanafunzi wa Yesu. Zaidi ya hayo, kulingana na wao, haijulikani kamwe huyu Marko alikuwa nani kwa uhakika.

Mwandishi wa kale wa Kikristo, Eusebius (325 BI), alipokea kuwa mtunzi mwengine wa zamani, Papias (130 BI), alikuwa wa kwanza kuinasibisha Injili kwa John Mark (Yohana Marko), mwandani na mfuasi wa Paul (Paulo).

Wengine wametoa rai kuwa huenda alikuwa mwandishi wa Petro na ilhali wengine wanaona kuwa huenda alikuwa mtu mwengine kabisa.



Hiyo ndiyo hali ya Injili nyingine.

Japokuwa Mathayo, Luka na Yohana yalikuwa majina ya wanafunzi wa Yesu, waandishi wa Injili hizo waliokuwa na majina ya wanafunzi hao mashuhuri, lakini ni watu wengine ndio waliotumia majina yao ili maelezo yao yapate kusadikika.

Kwa hakika, Injili zote zilisambaa hapo awali bila majina.

Baadaye majina yenye kuaminika yalipatiwa kama watunzi wa Injili hizo na watu wasiojulikana katika kanisa za awali.



Vitabu


Watunzi

Gospel of Matthew (Injili ya Mathayo)


Hajulikani (“Japokuwa yupo Mathayo aliyetajwa katika orodha tofauti za wanafunzi wa Yesu… mwandishi Mathayo kwa kiasi kikubwa hana jina” (The New Encyclopaedia Britannica, Mj. 14, uk. 824).

Gospel of Mark (Injili ya Marko)


Hajulikani (“Japokuwa mtunzi wa Marko huenda akawa hajulikani…” (The New Encyclopaedia Britannica, Mj. 14, uk. 826).

Gospel of Luke (Injili ya Luka)


Hajulikani (“Sheria ya Muratori inamtaja Luka, tabibu, mwandani na mfuasi wa Paulo; Irenaeus anamuonyesha Luka kuwa ni mfuasi wa Injili ya Paulo. Eusebius anamuweka Luka kuwa ni tabibu wa Antiocha, ambaye alikuwa na Paulo ili kuipatia Injili mamlaka ya kiutume” (The New Encyclopaedia Britannica, Mj. 14, uk. 827).

Gospel of John (Injili ya Yohana)


Hajulikani (“Kutokana na dalili za ndani, Injili hii iliandikwa na mwanafunzi mpenzi ambaye jina lake halijulikani” (The New Encyclopaedia Britannica, Mj. 14, uk. 828).

Acts (Matendo)


Mtuzi wa Luka (The New Encyclopaedia Britannica, Mj. 14, uk. 830.)

I, II, III John (1, 2, 3 Yohana)


Mtunzi wa Yohana (The New Encyclopaedia Britannica, Mj. 14, uk. 830).
 
Katika Injili za Mathayo, Marko na Luka, Yesu ameitwa mara 22 kwa jina la "Mwana wa Mungu", lakini hata mara moja yeye mwenyewe hakujiita kwa jina hilo.

Katika Mathayo 27.43 yanatajwa maneno ya wakuu wa makuhani wa Kiyahudi pamoja na waandishi na wazee waliokuwa wakimdhihaki, si maneno yake yeye Yesu.

Hao walikuwa wakimzulia kuwa anadai uwana wa Mungu, na anadai kuwa ni Mfalme wa Israeli.

Sana waliokuwa wakimwita Mwana wa Mungu walikuwa ama wendawazimu, wenye pepo wachafu, au askari wa Kirumi ambao tokea hapo wao ni washirikina, mapagani.

Mwenyewe Yesu alikuwa daima akipendelea kujiita mwana wa Adamu kwa Kiebrani, lugha yake, Bin Adam, yaani ni binaadamu, mtu tu.

Katika Injili jina hili la Yesu kuitwa mwana wa Adamu limetajwa yapata mara 80.

Mahasimu zake wa Kiyahudi walimzulia kuwa alidai kuwa ni Mfalme wa Mayahudi ili kumchongea kwa watawala wa Kirumi, na kuwa alidai kuwa ni Mwana wa Mungu ili apate kuchusha kwa Mayahudi.

Katika Injili ya Yohana, ambako maneno ya maelezo yamewekwa kwenye mdomo wa Yesu, injili zote nyengine zinaeleza kuwa wenye kutumia maneno kama 'Mtakatifu wa Mungu', au 'Mwana wa Daudi', au 'Mwana wa Mungu' si Yesu bali wengineo.

Jina pekee alilokuwa mwenyewe Yesu daima akilitumia ni 'Mwana wa Adamu'...

Katika kitabu cha Matendo ya Mitume inasimuliwa kuwa Mt Stefano alisema aliyoyaona yaliyo mbinguni. Alisema:

Tazama! naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.

Matendo 7.56



Mwana wa Adamu ndiye Yesu, na kwa jina hilo ndio mwenyewe akipenda kujiita, sio Mwana wa Mungu.

Kazi imeisha, usirudie tena kusema uwongo kwamba Yesu hakujiita mwana wa Mungu
 
Kitambo tu mbona ameungana nao kwa kuwatumia malaika zake waovu Ili kuwaingia wanadamu watende matendo maovu Ili kumuabudu.
Malaika waovu huwa nao wana sifa kama za malaika wengine wao wamebadilika?
 
Kazi imeisha, usirudie tena kusema uwongo kwamba Yesu hakujiita mwana wa Mungu

Lugha ya Yohana ni ya namna ya peke yake.

Injili tatu za mwanzo, Mathayo, Marko na Luka zinamweleza Yesu ni binaadamu.

Lakini Yohana amepindukia mipaka hapa kwa kumweleza Yesu kuwa ni "Neno" kwa maana aliyoipata kutokana na waandishi wa Kigiriki, sio kutokana na maandishi ya Kiyahudi.

Kauli hii haikutajwa katika Injili hizo tatu za mwanzo wala katika vitabu vyote vya Agano la Kale.

Katika karne ya sita kabla ya Yesu kulizuka katika maifalasufi wa Kigiriki nadhariya ya kuwa uumbaji wa ulimwengu haukuzuka ovyo lakini kwa mpango wa kiakili, na ulimwengu wote unaendeshwa kwa kufuata sharia maalumu.

Sharia hii au akili hii au mpango huu waliuwita "Logos", maana yake ni "Neno".

Tunaona tamko hilo linatumika katika "Bio-logy" "Geo-logy" "Psycho-logy", kwa maana ya "ilimu".

Katika zile zile zama za Yesu alikuwako mwanachuoni wa Kiyahudi katika mji wa Iskandaria katika Misri ambaye alikuwa ni mwanachuoni katika ilimu za Kiyahudi na vile vile ni mtaalamu katika falsafa za Kigiriki.

Alijaribu kutaka kueleza mafunzo ya Kiyahudi kwa kutumia hoja za falsafa za Kigiriki. Yeye alitumia hii kauli ya Logos au "Neno"

kwa kueleza ile hekima na busara ya Mwenyezi Mungu katika kuumba. Myahudi huyu akiitwa Filo.

Yohana aliitumia lugha ya huyo Filo na kuingiza ndani yake mawazo ya kipagani akachanganya falsafa ya Kigiriki kwa kumuambatishia Yesu, na kumfanya yeye Yesu ndiye "Logos" au "Neno" na hilo "Neno" lilikuwapo tangu mwanzo, na hilo "Neno"lilikuwa pamoja na Mungu, bali ndilo khasa likawa ni Mungu.

Haya yote hayakusemwa kabisa na Injili zote zilizotangulia, wala Yesu mwenyewe hakuyadai, wala wanafunzi wake hawakupata kumdaia. Tena Yohana alizidi kusema:

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Yohana 3.16

Tunaona kwa mara ya kwanza Yesu kuitwa Mwana wa Mungu wa pekee. Lakini hata kulitumia neno "Mwana wa Mungu" kuna maana gani khasa?

Tukiipitia Biblia na kufungua sahifa zake tutaona kuwa jina hilo limetumiliwa kwa watu wengi licha Yesu.

Katika Agano la Kale ambalo lote limeandikwa hata kabla ya Yesu hajazaliwa tunakuta mifano kama hii:

Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6.1-2


Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani?
Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni,
Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,
Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
Ayubu 38.6-7

Tena itakuwa ya kwamba hesabu ya wana wa Israeli itafanana na mchanga wa bahari, usioweza kupimwa wala kuhesabiwa; tena itakuwa, badala ya kuambiwa, Ninyi si watu wangu, wataambiwa, Ninyi ndio wana wa Mungu aliye hai.
Hosea 1.10

Ni dhaahiri tunaona ilikuwa ni jambo la kawaida hata kwa waandishi wa Kiyahudi wanaoamini Mwenyezi Mungu mmoja kutumia maneno kama "wana wa Mungu" kwa kukusudia "vipenzi vya Mungu", au "waja wa Mungu", yaani watu wema.

Mwanachuoni wa Biblia wa Kitaliana, Marcello Craveri, aliyeandika kitabu chake, Maisha ya Yesu (The Life of Jesus), anaamini kuwa neno hilo "Mwana wa Mungu" limegeuka maana kwa kupitiwa na miaka ya makosa ya kufasiri. Ameandika:

"Kwa hakika, Agano la Kale limetumia neno ebed Yahweh, ambalo maana yake ni 'mtumishi wa Mungu', 'mtumwa wa Mungu', 'khaadimu wa Mungu'. Matini ya Kigiriki ya Septuagint imeipa tafsiri ambayo yaweza kuwa na maana mbili, (Pais Theou), hali ya kuwa pais, kama neno puer laweza kuwa maana ya 'mvulana mdogo' au 'mtumwa'.

Baada yake ilikuwa ni wepesi kuliondoa neno pais lenye maana ya 'mvulana' likatiwa neno (hyos)ambalo maana yake ni 'Mwana'."
 
Sababu ipo nguvu kuu ya utendaji ndani ya jina la Yesu. Hayo majina mengine hayana nguvu ya kutenda chochote.
Tatizo hakuna jina moja wazungu wanamwita Jesus na waswahili wanamwita Yesu na lugha zengine wanamwita vyengine pia sasa hapo tutasemaje ni jina moja?
 
Back
Top Bottom