Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
VeraCity (au Veracity) maana yake ni UKWELI.
Nimeamua kutumia jina hili kama kielelezo cha mwelekeo ninauotaka au ninaoamini na kuutumia.Uongo kwenye serious forums kama JF unaondoa maana nzima ya kuwepo kwa forum yenyewe.
nilipokuwa sec nilikuwa na ma frnds zangu watatu, tulikatiana hivyo vijina vya ajabu ajabu tu kama hivyo, mie ndio nikakatiwa Nyamayao.
MTM = initials representing majina yangu matatu, M la kwanza, T la pili na M la baba yangu!!
Duuu,,,................................Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?
Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.
Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.
Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.
Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.
Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.
Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.
Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?
Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.
Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.
Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.
Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.
Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.
Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.
Nyie hapo juu mnazo double ID na nimefanikiwa kuwagundua kwamba:
1. WomanOfsubstance = veracity
2. Babra = Nyamayao
3. De Novo = MTM
Kaazi kwelikweli!
Mkaa Mweupe: kwa kawaida mkaa ukiwa umepoa rangi yake ni nyeusi ila ukikolea moto huwa na rangi nyeupe, hapo kuushika yataka moyo. Ndivyo nilivyo.
Duuu,,,................................
Niliwahi kufanya kazi Na maprofessor wa Harvard miaka ya 2004 moshi, nikazinguana na mabosi zangu walikua wananilipa vizuri sana kipindi hicho kazi yenyewe nilipata kibahati then nikaacha kazi kwa hasira, nikaingia mtaani nikahustle saana tuu kwa 2 years then nikaishi porini huko tanga kwa mwaka mmoja maji ya madimbwi kuoga ilikua ishu no phone no what msosi ilikua ishu nikarudi mjini nikapigwa miezi sita jela nikatoka nikaenda znz mwaka 1 porini kabisa huko kizimkazi kwenda hta town ilikua ishu nikateseka na wachina kinoma tulikua tunajenga mi kama kibarua then,,,, mwaka jana nikaingia mjini mambo yakaanza kwenda saafi....noti ikakubali na hapo nikafikiriiiiiiaaa weeeee nikagundua kweli "maishapopote" Hiyo avatar ni picha ya arnold schwazernegger akiwa gym miak ile eee kipindi kile akiwania mr olympius then nikaangalia mtiririko wa maisha yake hadi sasa amekua gorvenor bado naamini
maisha popote...........na sikati tamaaa!!!!!!!!!!!
Nyie hapo juu mnazo double ID na nimefanikiwa kuwagundua kwamba:
1. WomanOfsubstance = veracity
2. Babra = Nyamayao
3. De Novo = MTM
Kaazi kwelikweli!
Mkaa Mweupe: kwa kawaida mkaa ukiwa umepoa rangi yake ni nyeusi ila ukikolea moto huwa na rangi nyeupe, hapo kuushika yataka moyo. Ndivyo nilivyo.
me na jinsia mbili
Na haya mengine je?
Fugwe, kikwetu ni Kobe. Kobe kwa asili yake ni mnyama mstaarabu sana, anapenda amani, na nimkaa kimya. Katika ukimya wake tunaamini kikwetu anautumia kutafakari mambo yaliyopo na yale yanayokuja. Ukimchokoza hawezi kulipiza kisasi bali anajificha kwa kutumia gamba lake gumu. Kuhusu 'Avatar' yangu, hilo ni kaburi alimozikwa Baba wa Taifa hayati MWL NYERERE, napenda yale yote aliyofanya mazuri, aliyotuasa tusiyafanye, watu aliowakataa katu wasipewe uongozi kama watapewa watakuwa kama mbwa mwenye njaa aliyekabidhiwa nyama ailinde. Hao si wengine ni akina Bazil Mramba na Mwenzake Lowassa.
KAITABA, ni uwanja wa mpira upo mkoani Kagera, mama yangu mzazi alikuwa bosi enzi hizo, akiwa anakagua gwaride uwanjani hapo akashikwa na uchungu,
Alipopelekwa chumba cha faragha uwanjani hapo nikazaliwa mimi,
Wakati niko school A level nilikuwa napenda sana mambo ya diplomasia na nilikuwa na dream kwamba siku moja nami niwe balozi wa Tanzania katika nchi yoyote.
Wenzangu walinipachika jina la Ambassador na wakanishauri nisome International Relations. Matokeo yake? Sikuwa hata balozi wa nyumba kumi! I still treasure and honor my friends, and ofcourse my dream...... With due respect....
NGALIKIHINJA
NGALI = ASIYE NA
KIHINJA = JIKO
Nilijipa jina hili kwa kumkumbuka mzee fulani tulikuwa tunaishi naye jirani nikiwa mdogo. Huyu mzee alikuwa ananihamasisha sana nijiunge na kundi lililokuwa linacheza ngoma ya kwetu. Vile vile alikuwa hajibu kitu kama utamsemesha lugha ya kiswahili huku akijuwa kuwa unafahamu lugha ya kijijini kwenu ambayo naye anaifahamu. Hayupo duniani hivyo kwa kumkumbuka yeye nikaamua kutumia jina lake la utani.
Shishi.....jina nililitunga kutokana na jina la kitoto nililopewa na mama. nilizaliwa hospitali moja mji wa Embu, Kenya, wakati huo kulikuwa na muziki ukifana sana ukiitwa' shiro murata' kwa kikikuyu inamaanisha 'shiro mpenzi'... 'shiro my love '. sasa pale spitali manurse wakaniita shiro. mama aliporudi nyumbani kawaambia dada na kaka zangu (am the fifth born) kuwa mtoto anaitwa shiro.....basi jina likashika mpaka wa leo naitwa shiro...basi ndio nami nikalifanyia mutation kidogo tu...ikawa shishi!
Hili jina limeshika kabisa ijapokuwa silitumii officially...watu wengine hawajui kuwa nina majina mengine!!!
Isha Lubuva kwa Kirangi inamaanisha Mwana wa Lubuva kama Wamasai wanavyoitwa Ole Saitoti, Ole Mollel, Ole Lokoine au Waarabu wanavyoitwa El Faid n.k. Aidha unaweza kutumia mkato na kuita Sha Lubuva. Mimi ni mtoto wa Mzee Lubuva. Lubuva inamaanisha mabua yanayobakia shamba baada ya kuvuna na marehem Bibi yetu alipatwa na uchungu na kumzaa Mzee lubuva kwenye (mabua) shamba ambalo tayari lilishavunwa ndipo akaitwa Lubuva. Ingekuwa alizaliwa nyakati za leo angekuwa na aka yake ya LbV