Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Kama Che Guevara?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi jina langu laanza na herufi "J"ushaitamka tayari sasa ni "Jay"
kuwa nina maarifa kiasi fulani basi jamaa fulani wakawa wananiita "Mtaalam" hivyo basi "Jay Mtaalam" naweza kukufanya ukabadili fikra,nikakufanya useme unachokifikiri japo mimi nitjifanya sijui haya kidogo ili nijue fikra zako,watu hufikiri sijui muda mwingine kumbe nawasoma ajili zao kwa sababu ni wabishi..nawasubiria mwishoni.
 
Hili jina natumia maana napenda sana kufanya Kazi kwenye Off Shore Rig, na nilipenda kujiita hivi tukisafiri tukiwa maeneo yenye hali ya hewa mbaya sana watu wanatapika mimi nakuwa nipo vizuri na ndio muda wangu wa kufurahia ubaharia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ni mbenamanga?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaaha,
 
Mtaani kulikuwa na majina mengi ya jumaa hivyo kutofautisha waliniita jumaa kizinga(kizinga ni kirefu cha kizingani. Na ni Jina LA kijiji kinachopatikana mtimbwani.Ukifika mtimbwani unaingia ndani kidogo unakuta kijiji jangwakuu kisha kizingani. Na aliishi hapo bibi yangu mzaa mama.Na kipatikana jijini Tanga njia ya kwenda horohoro mpakani) na Mpemba nilikaa Sana unguja niliporudi Nikawa naongea kipemba nikawa pia naitwa jumaa Mpemba. Nikaunga kizingampemba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…