Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Ni jina langu na hata picha ni yangu

Amani Iwe Kwenu
 
Ni jina langu na hata picha ni yangu

Amani Iwe Kwenu

Iwe kwako pia Mchungaji, twambie basi maana ya jina hilo. Hiyo picha mhhhhhhh! I reserve my comments hahahahahahah. Mrs hajambo?

 
M-mbabe = mtu wa undava undava hususani dhidi ya fisadi's
 
Iwe kwako pia Mchungaji, twambie basi maana ya jina hilo. Hiyo picha mhhhhhhh! I reserve my comments hahahahahahah. Mrs hajambo?


Maana yake ni Makutano yenye busura, ama Muungano wenye Busara! Mamaa Mchungaji iko haijambo. Ila sijui kala nini iko tema mate sana
 
Maana yake ni Makutano yenye busura, ama Muungano wenye Busara! Mamaa Mchungaji iko haijambo. Ila sijui kala nini iko tema mate sana

Hahahahahahaha labda ushajeruhi mtu LOL! ngoja tusubiri kwanza kabla hatujawapeni hongera zenu :whoo:
 
Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?

Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.

Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.

Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.

Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.

Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.

Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.

Ni mawazo mema, nia njema, pambazuko wakati wa kiza kinene kabla ya asubuhi halisi ndani ya nchi ambayo wengi wameanza kukata tamaa ya kuishi kama wenzao wengine duniani! Ni tunda jipya la kisiasa na kijamii, furaha kwa waliokosa usingizi kwa kulala kwenye vitanda vyenye kunguni, wakianza kufurahia mwanga utakaowaliwaza mpaka asubuhi itakapofika ili wawaue hao kunguni kwa jua kali lisilo na huruma.

Ubarikiwe BAK kwa swali zuri na lenye wingi wa busara ndani yake!
 
Mokoyo ni jina langu la halisi, ni jina la kikabila maana yake siijui
 
mzuanda, ni mtoto wa mwisho,na wazazi wangu wananiita hivyo most of the time wakitaka kunimwagia misifa
 
sulphadoxine ni dawa ya malaria ambaye kwa sasa aipatikani madukani,(sp)nimechagua hili jina la dawa kwa sababu ilikua inanisaidia sana kuliko hizi dawa za sasa hivi(mseto)
 
MPASUAJIPU : Hili jina nilichagua kwa sababu napenda kusema ukweli hata kama unauma.

Unajua jipu linauma sana na dawa yake ni kulipasua na kutoa taka zilzomo ndani yake.

Sipendi kuficha mambo kwani hata jipu ukilificha ipo siku litapasuka lenyewe tu likiiva.

na hisia zangu ni kuhusiana na serikali zote dhalimu na mafisadi wanaodhulumu wanyonge ni kama jipu ambalo km hatukulipasua basi kuna siku litapasuka lenyewe tu.
 
Nilikuwa nimepotea wakati sredi hii inaendelea.

Zakumi - Ni mascot iliyotumika kwenye world cup 2010, nchini Africa kusini. Nilichagua mascot hii ni kwa sababu ni chui (Leopard). Mnyama mwenye kupenda uhuru na kuwa pekee yake (solitary animal). Hawezi kufugwa. Hatabiriki. Instinctive. Territorial. Eat fresh meat. Risk taker.

Hivyo nili-create a character yenye persona za chui kama ifuatavyo:-
---Hakuna urafiki wala kujuana hapa JF (solitary animal)
---Hafuati imani au kundi la watu, yuko tayari kutetea au kupinga ideas hata kama atabaki pekee yake (hawezi kufugwa)
---Hana personal issues ana connect dots tu (Instinctive)
---Ana maeneo na topiki zake (territorial)
---Anapenda idea mpya (Fresh meat Easter)
---Mgomvi wa mawazo na haogopi kujaribu (Risk taker)
 
bob giza, kwa rangi ni kama ile kitu tanesco wanawapa raia kupitia mgao nyakati za usiku...yaani ni full masizi wa kutosha..ni ivo tuu!!
 
Tamka 'mtu be'. Ni jina walilonipa marafiki tangu nikiwa shule ya sekondari. Sababu zake zilikuwa mbili: Kwanza umbo langu la mazoezi, wenzangu walikuwa wanadai niko sawa na watu wawili. Pili nilikuwa na tabia (sijui mbaya?) ya kudai shea ya watu wawili wakati tunagaiwa nguna (ugali) kule *DH* (dining hall) la shule, kila mara nilimwambia mwanafunzi anayegawa nguna siku hiyo anijazie shea ya 'mtu be' (watu 2) kwenye sahani yangu ya bati (TG).

''E banae nigee shea ya mtu be mshkaji wangu, si unajua nimetoka kwenye tizi au vipi!''.

Basi ndio jina likashika tangu wakati huo, kuna wengine tuliosoma shule moja hadi leo hawanijui kwa jina lingine zaidi ya Mtu B.

Kwenye nyota umenkumbusha Dodoma Hotel(DH).
 
Back
Top Bottom