Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

hA-HA-HA BAK!...Kisa cha kuitwa binti maringo...yaani hata OPP hajakosea kabisa ni kwa sababu ya miondoko yangu na jinsi ninavyongea plus mapozi!....hahaha kwenye kula kama nipo na men ndiyo naweka mapozi ila kama nipo alone napakia bila mapozi aisee!....

Mhhh! naona miondoko yako itakuwa inafanana fanana na ile ya Naomi Campbell au Tyra Banks ambayo inawapagawisha sana njemba wengi. Nilicheka sana siku moja nadhani hapa jamvini dada mmoja aliandika kwamba mumewe anampandishia sana eti anatembea kishamba maana Mumewe anataka atembee kama Naomi Campbell...mhhhhh! Njemba nyingine zina makuu kweli kweli! ukakasirike na kuja juu eti kisa mkeo hatembei kama Naomi Campbell! Hizi ndoa zina matatizo ya kila aina.

Naona kwenye msosi ukiwa mwenyewe wala hujivungi, maringo yote unaweka pembeni na kufukia kama kazi ha ha ha ha ha ha 🙂 Ahsante sana kwa kujibu Binti Maringo.
 
Mhhh! naona miondoko yako itakuwa inafanana fanana na ile ya Naomi Campbell au Tyra Banks ambayo inawapagawisha sana njemba wengi. Nilicheka sana siku moja nadhani hapa jamvini dada mmoja aliandika kwamba mumewe anampandishia sana eti anatembea kishamba maana Mumewe anataka atembee kama Naomi Campbell...mhhhhh! Njemba nyingine zina makuu kweli kweli! ukakasirike na kuja juu eti kisa mkeo hatembei kama Naomi Campbell! Hizi ndoa zina matatizo ya kila aina.

Naona kwenye msosi ukiwa mwenyewe wala hujivungi, maringo yote unaweka pembeni na kufukia kama kazi ha ha ha ha ha ha 🙂 Ahsante sana kwa kujibu Binti Maringo.



hahahaha huyo mwanaume kiboko sasa si angemfundisha mkewe jinsi ya kutembea?...uongo mbaya kuna wale wanatembea kama wanapandisha mlima Meru au wanafunza (ki-Nyalu tunaitwa makegete)...

aah ule mwendo wa Naomi au Tyra bana kama hujui unaweza kuanguka ila i am blessed naupatia maana nikipita na hilo badunka donkie kila mtu anageuza shingo lake!.....weeh!
 
hahahaha huyo mwanaume kiboko sasa si angemfundisha mkewe jinsi ya kutembea?...uongo mbaya kuna wale wanatembea kama wanapandisha mlima Meru au wanafunza (ki-Nyalu tunaitwa makegete)...

aah ule mwendo wa Naomi au Tyra bana kama hujui unaweza kuanguka ila i am blessed naupatia maana nikipita na hilo badunka donkie kila mtu anageuza shingo lake!.....weeh!

BM, kumwambia mkewe atembee kama NC ni rahisi sana lakini sidhani kama yule njemba angeweza kumuonyesha bila kupiga mweleka wa nguvu. Kama unaiweza miondoko ile ya NC na TB basi hongera zako.

Huwa naangalia mara moja moja 😉 kile kipindi "American's next model" cha Tyra na nimeshawaona mabinti wakipiga mweleka au kukaribia kufanya hivyo pale walipoonyeshwa na Tyra au yule shoga jinsi ya kutembea kama Tyra.
 
Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?

Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.

Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.

Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.

Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.

Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.

Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.






[ame="http://www.youtube.com/watch?v=adKf6G2bOnc"]
pixel-vfl73.gif
[/ame]




pixel-vfl73.gif





 

HAHAHAHAHAHAHAHA Mzizi Mkavu umenifurahisha sana Mkuu. Umeenda kuutafuta huo wimbo mpaka umeupata 🙂 Ahsante sana Mkuu kwa juhudi zako. Naam, mtu chake apendacho hakina hila machoni, huridhika kuwa nacho japo hakina thamani.
 
Mama Joe, inaelekea Joe ni mtoto wa mama na inaelekea anapendwa sana kuliko waliomfuatia... 🙂
Of coz i have a special feeling for him, but not mama's boy. Why? First born ni kama mnakua pamoja: kwake unajifunzia mtoto anazaliwa vipi, kula, anataka nini so kwa pamoja mie na yeye tunaweza kufanya malezi ya wenzie. Kwa vile sijajua mziwanda atakuwaje so as far as my children are concerned he remain special.
 

Well, here you have it....somebody has done the job for me..!!

"Yebo Yebo is a type of cheap plastic sandals which is common among in Tanzanians, particularly in the rural areas. Usually they are worn by women, men and children alike who have low income and cannot afford shoes or better quality sandals.

Urban poor people in Tanzania also go for Yebo Yebo as multipurpose shoes because they are cheap and easily available. At one time yeboyebo referred to one of the big football clubs in Tanzania whose team had been losing matches regularly. "

My Reason to use the name: Most of the time I feel that is how our Government is treating us (the citizens) of Tanzania. I/We are like Yebo Yebo, they can do what ever they wish, whenever without ever considering the People.
 
well, here you have it....somebody has done the job for me..!!

"yebo yebo is a type of cheap plastic sandals which is common among in tanzanians, particularly in the rural areas. Usually they are worn by women, men and children alike who have low income and cannot afford shoes or better quality sandals.

urban poor people in tanzania also go for yebo yebo as multipurpose shoes because they are cheap and easily available. At one time yeboyebo referred to one of the big football clubs in tanzania whose team had been losing matches regularly. "

my reason to use the name: most of the time i feel that is how our government is treating us (the citizens) of tanzania. I/we are like yebo yebo, they can do what ever they wish, whenever without ever considering the people.

.......pia sekondari za kata
 
Of coz i have a special feeling for him, but not mama's boy. Why? First born ni kama mnakua pamoja: kwake unajifunzia mtoto anazaliwa vipi, kula, anataka nini so kwa pamoja mie na yeye tunaweza kufanya malezi ya wenzie. Kwa vile sijajua mziwanda atakuwaje so as far as my children are concerned he remain special.

Naam Mama Joe, Children who are 1st born are very special.
 
BabaUbaya= Ukicheka na nyani utavuna mabua Ubaya ubaya tu teh teh teh Lol .... but nipo simple ile mbaya Pakajimmy anajua hilo!!!!
 
Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?

Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.

Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.

Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.

Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.

Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.

Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.


Dadii = means dad,,, am a family man!! kifupi namkubali sana merehemu baba wa taifa Mungu amlaze mahari pema peponi,,,,, alikuwa baba haswa,,, naitunza familia yangu katika misingi yake Mwl Julius kama alivyoitunza Tanzania kabla ya Mafisadi kuharibu kila kitu pumbavu....... sana hawa.
 
Well,jina langu kama lilivyo 'Sumu Baridi'...nilipachikwa na Marehemu Bibi yangu (mzaa mama),nikutokana na hali yangu ya ukimya,wa kuangalia mambo kwa macho hata yawe ya kuumiza vipi,ni mtu wa kuyachukuwa masuala ya kuya scrutinize,then maamuzi huya chukua mara nyingi pale watu wanapodhani nimesahau,na wao kusahau BUT kishindo kinachotokea ni balaa,unless my Late Grandma had other interpretations to that name...
 
Mi mentor wangu ni muanzilishi wa Goldman Sach, ni majina ya baba na mkwe. Why I admire this shirika ni kwamba wanapiga kazi masaa yasiyopungua 14 per day nikawaza hivi sisi wa tz tungewaiga najua tungekuwa mbali sana, kwa hiyo mi kama individual napiga kazi whatever the time come rain come shine if there is job
 
Mimi pia kwa wale waliotazama filamu ya analyze this
ya robert deniro
mtakumbuka kuna sehemu aliulizwa na daktari wake..
What do u do????
Akajibu ..what do i do???am the boss.....i dont do anything..
It was so funny....

nimeipenda sana hiyo ...lol
 
Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?

Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.

Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.

Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.

Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.

Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.

Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.

Nimegundua kila binadamu huwa na aghalabu majina matatu,jina la kurithi,jina unalopewa na wazazi na jina unalojipa mwenyewe,na katika haya majina tunayojipa wenyewe mara nyingi yanatokana na mazingira au hali fulani na ni majina ambayo inawezekana yakawa yanaanzishwa na sisi wenyewe,marafiki au hata wale wasio marafiki (maadui)zako.Majina haya huwa yanabadilika mara kwa mara,naweza sema ni majina ambayo huzaliwa,huishi naa hatimaye hufa kutokana na sababu mbalimbali.....Kwa mfano mimi nilikuwa mfatiliaji mkubwa sana wa Jambo to Jamii forums lakini nikiwa kama guest msomaji tu, sikuwa mchangiaji wa mada yoyote ile kutokana na right za Guest..hivyo nilipoamua sasa nataka kuwa member wa Jamiiforums lengo langu likiwa ni kupata fursa ya kuchangia na kutoa mawazo yangu yaani "KUONGEA"Then jina "NALONGA"likazaliwa ikiwa ni neno kutoka katika kabila moja nchini lenye maana "NAONGEA".
 
Gudboy: hili ni jina la ni wimbo flan wa jamaa Niki wa 2 naupenda sana kwa sababu vitu vingi alivyoimba vinareflect maisha yangu. Mfano pale aliposema gudboy akiwa na kitu moyoni hafichi anasema, hakuna ubaya kama kufanya mabaya mbele ya watoto wanaotuiga leo ili wakafanye mema kesho, kubalehe ni mtihani na wengi wamefail, nani kasema shujaa azaliwi guest, fanya kazi ujenge urafiki na hizi hela, sina chuki za CCM kwenye ubongo wa Lipumba, utajiri wa kwanza ni kuwa na marafiki, simtongozi mwanafunzi kumharibia maisha, usimwache anayekupenda mapenzi yakamfunga jela, wingi wa mashori sio kipimo cha urijali kama mwanaume wa kweli nyumbani wapate ugali, gudboy huamka mapema.

hii ni kati ya mistari katika wimbo huu ambao nauzimia ile mbaya, maana nami ni gudboy mazee

Gudboy sijakuelewa vizuri.
 
Chimunguru ni Jina langu halisi lipo kwenye cheti changu cha ubatizo naitwa Chimunguru Chiziwa. NALIPENDA JINA HILI sababu sipendi tumia SLAVE NAMES, naamini ntakuwa nimetumia jina la asili yangu. Babu yangu alikuwa akiniambia miaka hiyo yuko hai, EEeh mnyanga, mtombo, chiziwa, mchoramiti, chimunguru, kateke manji tupuuze. Ntakuja wambia maana ya huu usemi.


Nakukumbusha tueleze maana yake!
Heri ya mwaka 2011.
 
Kwa Muda sasa nimekuwa obsessed na Identity ya mwanadamu haswa ktk self consciousness. Hapo nikaangukua ktk essays za philosopher John Locke ( Locke's general theory of Identity) hapo nikajitambua na kuthamini sana Origin yangu ( Uafrica na Utanzania wangu) ila conflict inayonisumbua kichwa kama wengi wetu ni hali za kisiasa na maendeleo ya uchumi, selfishness, greediness, uonevu ktk haki(injustices), ignorance etc etc. Waafrica wengi hawana huruma na wenziwao, hawana huruma na mali ya nchi yao, upendo, hari na nchi au bara lao llililojaaliwa na kwa ujumla hawajitambu. Wee need to understand who we are, ili tujijali, tujitetee na kutetea waliotuzunguka, let's be Loyal na nchi zetu Ukereketwa ukereketwa wajameni! tuijali nchi yetu. LoyalTzCitizen

 
Back
Top Bottom