Je, Kanisa Katoliki ndiye mnyama wa nne duniani wa Unabii wa Daniel na Ufunuo?

Je, Kanisa Katoliki ndiye mnyama wa nne duniani wa Unabii wa Daniel na Ufunuo?

Hakuna kanisa lililo sahihi yote yana mambo ya kipagani. MUNGU atamhurumia Jacob tu.... Na ataingia AGANO tena na uzao wake tu... Na wote waliohusika ANADili nao sambamba


USIWE MBISHI SANA KANISA LA MUNGU HALIWEZI KUANGUKA.

TAFUTA KUJUA HAPO KWENYE UFUNUO 12.
JE HAO WALIOSALIA NI AKINA NANI??????
WAZISHIKAO AMRI ZA MUNGU
NA KUWA USHUHUDA WA YESU.....

Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu;
UFUNUO 12.17.
 
Umeandika ANDIKO lefu la kunishtumu na sijaona Cha maana ulichokiandika.
Baada ya kujenga hoja kwa Maandiko unakuja kumshambulia mtoa hoja.

Sambulia hoja Kwa Maandiko na si mtoa hoja kwa umbea.

Lete REFERENCE YOYOTE YA WEMA WA CATHOLIC CHURCH BIBLICALLY MSIDANGANYWE.

FICHA UJINGA.

NAKUSHAURI SOMA
SOMA.
SOMA..... ELIMU ELIMU ELIMU

Lakini Nimefundishwa MITABU CHA METHALI

Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye.

Mithali 26:4
Hiyo mithali unayong'ang'ana nayo ni nani aliiandika ikasomeka kimpangilio hivi?
 
Mnyama wa kitabu cha Ufunuo

Watu wengi hawafahamu kuwa mnyama ni nani, na wengi wamejihusisha naye bila wao wenyewe kujua kama wanashiriki na mnyama. Lakini Mungu hajatuacha gizani, hivyo, kwa kupitia neno lake (Maadiko Matakatifu) tunaweza kumfahamu mnyama huyu aliyelezwa katika kitabu cha Danieli na Ufunuo.

Tunapaswa kuyaacha maandiko yajitafisiri yenyewe; kwa maana “hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.” 2Petro 1:20-21. Hatupaswi kumuacha mtu flani atafsri unabii kwa jinsi yake mwenyewe, badala yake tunapaswa kuiacha Biblia ijitafsiri yenyewe.

Katika Danieli 7 wametajwa “wanyama wanne” ambao wanawakilisha falme nne. Kumbuka mmyama wa 4 aliyetajwa katika Danieli 7 ndiye mnyama aliyetajwa katika kitabu chote cha Ufunuo. Hivyo hapa tutaangalia sifa za mnyama wa nne wa kitabu cha Danieli, na mnyama wa kitabu cha Ufunuo, kisha tutaangalia ni wapi hapa duniani ambapo sifa za mnyama zinatimizwa kikamilifu.

1. Mnyama atakuwa na uwezo wa kisiasa na kidini (kanisa na serikali).

Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona MWANAMKE, AMEKETI JUU YA MNYAMA mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.”

Mwanamke au bibi-arusi katika unabii huwakilisha kanisa.

Ufunuo 21:2 “…Yerusalemu mpya…umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.”

Ufunuo 21:9 “…Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.”

Mnyama huwakilisha taifa au ufalme

Danieli 7:17 “Wanyama hao…wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani”

Danieli 7:23 “…Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia…”

Kutokana na Ufunuo 17:3, mnyama huyu ana mwanamke aliyeketi juu yake, na kwa sababu unabii unatafisiri mwanamke kama kanisa, na mnyama kama taifa. Je kuna taifa au serikali ambayo imechanganywa pamoja na kanisa kama kitu kimoja? Ndiyo! Vatican, ni serikali au taifa ambalo limechanganywa pamoja na kanisa la Romani Katoliki kama kitu kimoja, na kuongozwa na mtu mmoja ambaye ni Papa.

2. Mnyama atakuwa na kanisa & serikali vimekaa juu ya milima 7.

Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana…mwenye VICHWA SABA na pembe kumi.”

Vichwa saba katika unabii vinawakilisha milima saba.

Ufunuo 17:9 “Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo.”

Je hapa duniani kuna kanisa na serikali vimekaa juu ya milima saba?

“Ni ndani ya mji wa Roma, uitwao Mji wa vilima saba, hivyo eneo lote la Serikali ya Vatican limewekewa mpaka kikamilifu.” –The Catholic Encyclopedia, p 529.

“Je vilima saba vya Roma ni nini?

Roma inajulikana kuwa imejengwa juu ya vilima saba. Roma ilisemwa imepatikana wakati Romulus na Remus, wana mapacha wa Mars, walifika katika futi ya kilima Palatine na wakauanzisha mji, Vilima sita vingine ni Capitoline (kiti cha serikali), Quirinal, Viminal, Esquiline, Caelian, na Aventine.” –Geography.about.com

ENCYCLOPÆDIA BRITANNICA
Vilima saba vya Roma

“…kundi la vilima juu au kuhusu ambapo mji wa Roma wa zamani ulijengwa. Mji wa awali wa Romulus ulijegwa juu ya kilima Palatine (#1) (Kilatini: Mons Palatinus). Vilima vingine ni Capitoline, (#2) Quirinal, (#3) Viminal, (#4) Esquiline, (#5) Caelian, (#6) na Aventine (#7) (Vinavyojulikana kimoja kimoja kwa kilatini kama Mons Capitolinus, Mons Quirinalis, Mons Viminalis, Mons Esquilinus, Mons Caelius, na Mons Aventinus).” –http://www.britannica.com/seo/s /seven-hills-of-rome/

Kwa hiyo unabii huu wa Ufunuo 17:3, unaonyesha wazi kuwa mwanamke aliyeketi juu ya mnyama, amekaa juu ya vilima saba vya mji wa Roma. Kwa vyovyote, ni Vaticani na kanisa la Romani Katoliki ambavyo vimekaa juu ya milima saba, na kutimiza unabii huu. Danieli 7:23 inasema mnyama wa mwisho (Roma) anatofautiana na wanyama wengine watatu waliopita. Kwa hakika hakuna taifa wala ufalme mwingine ambao una kanisa na serikali, harafu kwa wakati huo huo umekaa juu ya milima saba. Ila ni kanisa la Romani Katoliki pekee.

3. Mnyama atatoka baharini

Ufunuo 13:1 “Kisha nikaona mnyama AKITOKA KATIKA BAHARI, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.”

Bahari katika unabii huwakilisha watu/jamaa, mataifa, lugha.

Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.”

Ukatoliki wa Romani ulitokea ulaya ya magharibi pamoja na makutano ya “watu/jamaa, mataifa, na lugha.” Na kwa wakati huu kanisa la Romani Katoliki lina idadi kubwa ya “watu, mataifa, na lugha,” kuliko kanisa jingine lolote duniani mwote. Na sasa, baada ya kuanzishwa kanisa moja duniani, Juni 26, 2000, Papa alichaguliwa kama kiongozi wa makanisa yote ambayo yameungana na lake. Hii ilifanya kanisa liongezeke mara mbili. Na hivi karibuni, makanisa yote pamoja na yasiyo ya Kikristo yatatangaza kwamba Papa ni kiongozi wao mwema.

Na Juni, 2008 mataifa 174 katika mataifa 192 duniani, yana serikali zao zikiwakilisha Vatican. Hivyo, kanisa la Romani Katoliki linatimiza unabii huu kwa ukamilifu.

4. Mnyama atatawala miaka 1260. (kabla hajapata jeraha la mauti).

Danieli 7:25 “Naye atanena maneno kinyume chake aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataadhimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake KWA WAKATI, NA NYAKATI MBILI, NA NUSU WAKATI.”

Ufunuo 12:6 “Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko mda wa SIKU ELFU NA MIA MBILI NA SITINI.”

Ufunuo 13:5 “Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake MIEZI AROBAINI NA MBILI.”

Danieli 7:25 inaonyesha muda ambao angetawala mnyama, kama wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati. Ufunuo 13:5 inauonyesha mda huu wa utawala wa mnyama, kama miezi 42, miezi 42 = miaka 3 na 1/2. Hivyo, ukiangalia kwa makini hapa utaona kuwa, wakati = mwaka 1, na nyakati mbili = miaka 2, na nusu wakati = nusu mwaka.

Kwa hiyo, wakati nyakati mbili nusu wakati = miaka 3 na nusu ya Danieli 7:25, au miezi 42 ya Ufunuo 13:5, au siku 1260. Mahesabu haya yanathibitishwa katika Ufunuo 12:6 ambapo inasema, “Yule mwanamke (kanisa) akakimbilia nyikani…wamlishe huko mda wa siku 1260.” Kwa hiyo miaka 3 na 1/2 = miezi 42 au siku 1260 ambazo mnyama angetawala kabla hajapata jeraha la mauti.

Bado, wengine watakataa na kusema, hapana, miezi 42 haiwezi kuwa sawa na siku 1260, kwa sababu miezi mingine haina siku 30. Lakini katika unabii mwezi 1 = siku 30. Mwanzo 7:11 inasema, mvua za garika zilianza siku ya 17 ya mwezi wa pili, na Mwanzo 8:3, 4. inasema kuwa maji yakapunguka mwishoni mwa siku 150, harafu safina ikatua siku ya 17 ya mwezi wa saba. Hizo ni miezi 5 tangu mvua zilipoanza. Kama ukigawanya siku 150, kwa miezi 5, utapata siku 30 kwa kila mwezi. Hivyo, miezi 42 ikizidishwa kwa 30 jibu litakuwa 1260. Kwa hiyo wakati, nyakati mbili, na nusu wakati, ni sawa na miaka 3 na nusu, au miezi 42, au siku 1260. Kwa hakika, Ufunuo 12:6 inathibitisha mahesabu haya inaposema kuwa watoto wa Mungu watakimbilia nyikani kwa muda wa siku 1260 wakati wa utawala wa mnyama (upapa).

Katika unabii siku 1 ni sawa na mwaka 1,

Ezekieli 4:6 “…siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagiza.”

Hesabu 14:34 “…siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka…”

Kutokana na Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34, ni hakika kwamba siku 1260 ni sawa na miaka 1260 ambayo Upapa ungetawala na kuwadhofisha watakatifu. Je hii ilitokea? Je unabii huu ulitimia? Au Je kuna ushahidi wowote unaothibitisha kuwa unabii huu ulitimia?

Kwanza kabisa tunatakiwa kujua ni lini kanisa la Romani Katoliki lilipata nguvu zote za kutawala kama “mwanamke juu ya mnyama” (kanisa na serikali), na kutawala kisiasa na kidini kwa wakati mmoja kama Ufunuo 17:3 inavyosema.

“Vigillius…alikalia kiti cha upapa (538 B.K.) chini ya ulinzi wa jeshi la Belisarius.” –History of the Christian Church, Vol. 3, p. 327

Hiistoria inathibitisha kuwa upapa umeanza utawala wake kama “kanisa na serikali” mwaka 538 B.K. juu ya amri ya mfalme Jastinian, na chini ya ulinzi wa jeshi la Belisarius. Na unabii unasema mnyama (upapa) atatawala miaka 1260 kabla haujapata jeraha la mauti.

Ukiongeza miaka 1260 katika mwaka ambao kanisa la Romani Katoliki lilianza kutawala kisiasa na kidini, mwaka 538 B.K., utapata 1798 B.K. Hivyo, unabii unasema utawala wa kwanza wa mnyama ungeisha 1798 B.K. Je utawala wa mnyama uliisha mwaka huo 1798 B.K?

“Katika mwaka 1798 Generali Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica 1941 edition

Kwa hakika, hizo ni miaka 3 na 1/2 au wakati, nyakati mbili, na nusu wakati, ambazo ni miezi 42 au siku 1260 za unabii ambazo mnyama angetawala kisha angepata pigo la mauti au kuchukuliwa mateka. Je mnyama alipata pigo la mauti mwaka huo 1798 B.K?

5. Mnyama atapokea jeraha la mauti.

Ufunuo 13:3 “Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake lake la mauti likapona…”

Ufunuo 13:10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga…”

Kama tulivyoona huko nyuma baada ya mnyama kutawala miaka 1260 angepata jeraha la mauti na kuuawa kwa upanga (upanga = vita). Baada ya mnyama kumaliza utawala wake wa miaka 1260, ambao ulianza 538 B.K. hadi 1798 B.K., Napoleon alimtuma Generali/Jemedari wake Berthier pamoja na jeshi lake, kwenda Roma kuuondoa utawala wa upapa.

“Katika mwaka 1798 Generali Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica 1941 edition

Napoleon alipomtuma Generali wake Berthier kwenda kumuondoa Papa madarakani, hapo ndipo jeraha la mauti lilipompata mnyama, na mwaka uliofuata 1799 B.K. Papa alikufa. Hii ndiyo sababu watoto wa kikatoliki katika parokia hufundishwa kuwa Napoleoni alikuwa mpinga Kristo.

“Nusu ya Ulaya walidhani…kwamba pamoja na papa upapa ulikuwa umekufa.” –Joseph Rickaby “The Modern Papacy” Lectures on the History of Religion, Lecture 24, (London Catholic Truth Society, 1910), p. 1

Lakini unabii ulisema kuwa jeraha hili lililompata mnyama lingepona. Je jeraha hili lilipona? Je utawala wa upapa ulipoondolewa madarakani na Generali Berthier ulipata nguvu zake tena?

6. Mnyama atapona jeraha lake la mauti.

Ufunuo 13:3 “Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, NA PIGO LAKE LA MAUTI LIKAPONA. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule.”

Kama tulivyoona, upapa ulipata jeraha la mauti mwaka 1798 B.K. Vaticani ilibaki kama kanisa tu bila nguvu za kisiasa, na unabii ulisema jeraha hili lingepona. Je jeraha la mauti lilipona? Baada ya jeraha la mauti kutokea miaka kadhaa badaye katika mwaka 1929 B.K. Italia ikautambua mji wa Vaticani kama serikali ya kujitegemea, hii ilimfanya papa kuwa na nguvu tena kama mtawala wa kisiasa na kidini. kama unabii ulivyosema kwamba jeraha la mauti lingepona, na upapa ungerudishiwa tena uwezo wake wa kanisa na serikali kwa pamoja. Hebu angalia magaziti yaliyotoa taarifa hiyo jinsi waandishi wake walivyotumia lugha ya unabii bila ya wao wenyewe kujua.


Kusaini kwa Mussolini na (Kadinali) Gasspari mkataba wa kihistoria wa Romani

“Suala la Romani usiku huu lilikuwa ni jambo lililopita, na Vaticani ilikuwa katika amani na Italia…katika kuweka sahihi kwenye mkataba wa kukumbukwa kuponya jeraha la miaka mingi, uchangamfu wa kupindukia ulionyeshwa na pande zote.” –The San Francisco Chronicle. Feb. 11, 1929

Papa Amekuwa Kiongozi Wa Serikali Tena

“Roma, Juni 7.–Kutoka saa 5 kamili asubuhi hii kulikuwa na mtawala mwingine wa serikali ya kujitegemea duniani. Katika mda huo waziri mkuu Mussolini, kama waziri wa mambo ya nje Italia akimuwakilisha mfalme Victor Emmanuel–waziri mkuu wa kwanza Italia kuvuka kizingiti cha chini cha mlango wa Vaticani–akibadilishana na kadinali Gasspari, wakala wa serikali ya upapa, akimuwakilisha papa Pius XI, makubaliano ya mikataba yalisainiwa katika ikulu ya Lateran Feb. 11. Kwa kitendo hicho rahisi mtawala wa serikali ya kujitegemea ya mji wa Vaticani amekuwepo.” — New York Times July 7, 1929

Hivyo, unabii huu ulitimia kikamilifu na jeraha la mauti lililoupata upapa 1798 B.K. lilipona kabisa tangu 1929 B.K. mpaka leo kanisa la Romani Katoliki lina nguvu za “kisiasa na kidini” au “mwanamke juu ya mnyama.” Kwa kumaliza sehemu hii tunagundua kwamba mnyama huyu ndiye aliyekuwako, naye hayuko, na sasa yupo.


7. Mnyama aliyekuwako, naye hayuko, naye yuko.

Ufunuo 17:8 “Yule mnyama…alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari…”

Mnyama aliyekuwako: ni kanisa la Romani Katoliki tangu lilipoanza kutawala kama “kanisa & serikali” 538 B.K. na likaendelea mpaka. Napoleon alipomtuma Berthier kwenda kuuondoa utawala wa upapa. 1798 B.K.

…naye hayuko tokea 1798 B.K. mpaka kusaini kwa mkataba uliofanyika katika ikulu ya Lateran katika mwaka 1929 B.K. Vaticani ilikuwa kanisa tu bila uwezo wa kiserikali.

…naye yu tayari kutoka 1929 B.K. mpaka leo kanisa la Romani Katoliki lina nguvu za kisiasa na kidini, “kanisa & sesikali” au mwanamke juu ya mnyama.

8. Mnyama atabadili majira na sheria za Mungu.

Danieli 7:25 “…naye ataadhimu kubadili majira na sheria…”

Unabii huu ni ushahidi ulio wazi sana ambao karibu kila mtu hawezi kusumbuka kuelewa kwamba ni kanisa gani hapa duniani lililobadilisha sheria za Mungu. Ni kanisa moja tu la Romani Katoliki ndilo lililobadilisha sheria za Mungu kama Danieli 7:25 inavyodai kuwa. Kanisa la Katoliki limebadilisha sheria ya pili inayozuia kuchonga sanamu ya kitu chochote kile (angalia Kut 20:4). Katika katekism kanisa limeirarua amri ya 2 kisha likaigawa amri ya 10 katika sehemu mbili ili kuonyesha amri 10 zote. Lakini Je ni nani hapa duniani anayedai kuwa anauwezo wa kubadili amri za Mungu?

“Papa anauwezo wa kubadili majira, kubadili sheria, na kuachana na mambo yote, hata maagizo ya Kristo!” “Papa anayo mamlaka na mara nyingi ameyatumia, kuachana na amri ya Kristo.” –Decretal, de Tranlatic Episcop. Cap. (The Pope can modify divine law.) Ferraris’ Ecclesiastical Dictionary.

“Papa ni wa mamlaka kuu na nguvu kiasi kwamba anaweza kurekebisha, kuelezea au kutafsiri hata sheria za Mungu…Papa anaweza kurekebisha sheria ya Mungu, kwa sababu nguvu zake si za mwanadamu, bali ni nguvu za Mungu, na hutenda kama mwakilishi wa Mungu juu ya dunia.” –Lucius Ferraris,Prompta Ribliotheca, “Papa,” art. 2, translated.

Tangu kwamba papa ana mamlaka na maranyingi ameyatumia kubadili majira na sheria za Kristo, Je alibadili sheria ya Sabato? Je kanisa katoliki liliibadili Sabato ya siku ya saba ya wiki kwenda siku ya kwanza ya wiki? Kwa hakika kanisa lenye linakubali!

“Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –H.F. Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons

“Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” –Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

“Swali: Siku ipi ni siku ya Sabato?
Jibu: Jumamosi ni siku ya Sabato.
Swali: Kwanini tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi?
Jibu: Tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi kwa sababu kanisa katoliki, katika balaza la Laodikia (364 BK) liliihamisha kutoka Jumamosi kwenda Jumapili.” –The Convert’s Catechism of Catholic Doctrine,p. 50, 3rd ed.

“Kanisa la Romani (Katoliki) liliigeuza amri ya nne kwa kuiondolea mbali Sabato ya neno la Mungu, na kuanzisha Jumapili kama siku ya mapumziko.” –Nicholas Summerbell, History of the Christian Church, 3rd edition, 1873, p. 415 [Christian Church (Christian Connection)].

“Na ni wapi tumeambiwa katika maandiko kwamba tutunze siku ya kwanza kabisa? Tumeamriwa kutunza siku ya saba; lakini hakuna sehemu yoyote tuliyo amriwa kutunza siku ya kwanza. Sababu ya kutunza siku ya kwanza ya wiki kitakatifu badala ya siku ya saba ni kwa sababu ile ile kwamba tunatunza mambo mengine mengi, siyo kwa sababu ya Biblia, lakini kwa sababu kanisa, limeyaingiza [limeyaamuru].” –Isaac Williams, Plain Sermons on the Catechism, vol 1, pp. 334, 336 [Anglican].

Hivyo, kanisa la Romani Katoliki liliibadili sheria ya Sabato na kuwaamuru watu watunze jumapili badala yake. Na mwaka 1582. Papa Gregory XIII, alianzisha kalenda mpya. Kwa vyovyote, ni Vaticani ndiyo ilitimiza unabii huu kwa ukamilifu kabisa, hakuna jumuiya, wala shirika, wala sehemu yoyote ya kidini au isiyo ya kidini ambayo imetimiza unabii huu, kama ilivyo Vaticani. Ni kanisa la Romani Katoliki pekee ambalo lilibadili sheria, na majira, na kuamuru siku ihesabiwe kuanzia saa sita usiku kinyume na Maandiko yanayothibitisha kuwa siku huanza kuhesabiwa jioni.

Mwanzo 1:5 “Mungu akaiita nuru Mchana, na giza Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.”


9. Mnyama atanena maneno ya makufuru juu ya Mungu.

Danieli 7:25 “Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu…”

Ufunuo 17:3 “…nikaona mwanamke ameti juu ya mnyama…mwenye kujaa majina ya makufuru…”

Ufunuo 13:1 “…nikaona mnyama…mwenye…vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.”

Ufunuo 13:5 “Naye akapewa kinywa cha kunena makuu, ya makufuru…”

Kukufuru katika Biblia inaelezewa kama hali ya mtu kujifanya yeye mwenyewe kama Mungu.

Yohana 10:33 “Wayahudi wakamjibu, kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwamadamu wajifanya mwenyewe u Mungu.”

Je nani hujiita na kujifananisha na Mungu hapa duniani?

“Papa siyo mwakilishi tu wa Yesu Kristo, yeye ni Yesu Kristo mwenyewe, amejificha chini ya uficho wa mwili.” –Catholic National July 1895.

“Kwa kuwa wewe u mchungaji, wewe u tabibu, wewe u mwongozaji, wewe u mkulima, hatimaye wewe u Mungu mwingine duniani.” –Labbe and Cossart’s “History of the Councils.” Vol. XIV, col. 109

“Tunapachukulia juu ya dunia hii sehemu ya Mwenyezi Mungu…” –Pope Leo XIII Encyclical Letter of June 20, 1894,

Katika “The Bull Unam Sanctam” iliyotolewa na Papa Boniface VIII inasomeka kama ifuatavyo…
“Papa wa Roma huukumu watu wote, lakini yeye haukumiwi na mtu. Tunatangaza, kutetea, kuelezea, na kutamka; kutawaliwa na Papa wa Roma ni kwa kila kiumbe cha mwanadamu muhimu kwa ajili ya wokovu ambao ulisemwa na Kristo ‘Ameviweka vitu vyote chini ya miguu yake’ inaonekana vizuri imethibitishwa kwangu…Nina mamlaka ya Mfalme wa Wafalme. Mimi ni yote katika yote na juu ya yote, hivyo basi, Mungu Mwenyewe na mimi, kasisi wa Mungu tuna usawa mmoja, na ninaweza kufanya yote ambayo Mungu anaweza kufanya.”

“Mwokozi mwenyewe ni mlango wa zizi la kondoo; ‘Mimi ni mlango wa kondoo’. kwenye zizi hili la Yesu Kristo, hakuna mtu anayeweza kuingia mpaka awe ameingizwa na Papa mtawalawa na ni pale tu kama wameunganika naye ndipo wanadamu wanaweza kuokolewa, kwa sababu Papa wa Roma ni kasisi wa Kristo na ni mwakilishi wake kwa nafisi duniani.” –(Pope John XXIII in his homily to the Bishops and faithful assisting at his coronation on November 4, 1958).

Kudai kuwa Mungu duniani Biblia inathibitisha kuwa ni kukufuru ju ya Mungu aliye hai. Kufuru nyingine ni kudai kuwa na uwezo wa kusamehe dhambi.

Marko 2:7 “Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi ispokuwa mmoja, ndiye Mungu?”

Je makuhani wa kanisa la Romani Katoliki hudai wana uwezo wa kusamehe dhambi?

“Kuhani kiukweli kabisa husamehe dhambi kwa uwezo aliopewa na Kristo.” -Joseph Devarbe’s Catechism, p. 279

“Dhambi zinaweza kusamehewa kupitia sakramenti pekee…wote makuhani na sakramenti ni vifaa ambavyo Kristo anavitumia kukamilisha msamaha ndani yetu na neema ya utakaso.” -Catechism of Trent, p. 115.

“Haya mamlaka ya jaji (Judicial authority) yatajumuisha hata uwezo wa kusamehe dhambi.” –[The Catholic Encyclopaedia Vol 12, -article “Pope” pg 265]

“Na Mungu mwenyewe analazimika kufungwa na hukumu ya kuhani wake na ama kutokuomba msamaha au kuomba msamaha, kutokana na kama wanakataa kutoa ukamilifu, unaotoa toba inayoridhisha.” –Liguori, «Duties and Dignities of the Priest», p.27

10. Mnyama ana jina lenye namba 666.

Ufunuo 13:17 “tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, ispokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.”

Ufunuo 13:18 “Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinaadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.”

Biblia inatuambia kuwa hesabu au namba ya jina la mnyama ni 666

Kanisa la Romani Katoliki hudai kuwa Papa ni kichwa cha kanisa au mwakilishi wa Yesu.

“Maneno yaliyoandikwa katika kofia (miter) ya Papa ni haya, ‘VICURIUS FILII DEI’. ambayo ni ya kilatini kwa ajili ya ‘KASISI WA MWANA WA MUNGU’. Wakatoliki huchukulia kwamba kanisa, ambalo ni jumuiya ya kuonekana, lazima liwe na kichwa cha kuonekana. Kristo, kabla ya kupaa kwake kwenda mbinguni, alimteua M.t. Petro kuwa kama mwakilishi wake…hata hivyo Askofu wa Roma, kama kichwa cha kanisa, alipewa jina ‘KASISI WA YESU.'” –Our Sunday Visitor, (Catholic Weekly) “Bureau of information,” Huntington, Ind., April 18, 1915.

Kwa hiyo “VICARIUS FILII DEI” ndilo jina linalotumiwa na mamlaka ya Upapa na kumthibitisha Papa kama kichwa cha kanisa.

Helufi za kilatini zinaweza kutumika pia kama namba, na siku hizi hujulikana kama “Namba za Kirumi,” na helufi U inaweza pia kutumika kama V.


“VICARIVS FILII DEI”

(Kasisi wa Mwana wa Mungu)

V........5
I........1
C..... 100
A...... 0
R.......0
I........1
V.......5
S.......0
F........0
I.........1
L .......50
I.........1
I.........1
D........500
E.........0
I............1
Jumla= 666

Vicarius inamaanisha, katika nafasi ya
Filii Mwana
Dei Mungu
Hivyo, kanisa la Romani Katoliki linatimiza unabi huu wa hesabu ya mnyama 666 kwa ukamilifu kabisa.

11. Onyo la Mungu kwa wote walio katika kanisa katoliki.

Mungu anaoya vikali sana juu ya wale wote ambao wanashirikiana na mnyama huyu, kama wewe ni mmojawapo unapaswa kuchukua uamuzi sahihi sasa bila kupoteza muda; kwa maana hukumu itakuja juu ya mnyama na yule kahaba (kanisa Katoliki) aliyekaa juu mnyama. Hili ni onyo la mwisho la upendo na la rehema kutoka kwa Mungu.

Ufunuo 14:9-10. “Na mwingine, malaika watatu, akafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye naye atakunywa katika mvinyo ya gadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.”

Ufunuo 19:20 “Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;”

Ufunuo 18:4 “Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amemkumbuka maovu yake…Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemuhukumu ni mwenye nguvu.
Usabato ni kikundi cha itikadi
Hivyo ni kawaida yenu na itikadi zenu kila siku kuusema ukatoliki

Kati ya makundi yaliyoanzishwa Marekani baada ya utabiri wa William Miller kwamba ujio huo eti, utatokea tarehe 22 Oktoba 1844, lililoenea zaidi ni lile la Waadventista Wasabato (mwanzo rasmi mwaka 1863) ambalo kwa sasa lina waumini zaidi ya 17 milioni duniani kote.

Usabato lasmi ulianzishwa lasmi 1863 na huyo mzungu hapo juu 🤣🤣🤣
 
Usabato ni kikundi cja itikadi
Hivyo ni kawaida yenu na itikadi zwnu kila siku kuusema ukatoliki

Kati ya makundi yaliyoanzishwa Marekani baada ya utabiri wa William Miller kwamba ujio huo eti, utatokea tarehe 22 Oktoba 1844, lililoenea zaidi ni lile la Waadventista Wasabato (mwanzo rasmi mwaka 1863) ambalo kwa sasa lina waumini zaidi ya 17 milioni duniani kote.

Usabato lasmi ulianzishwa lasmi 1863 na huyo mzungu hapo juu 🤣🤣🤣


Mimi sijadili maswala hayo.

Mimi napenda tujadili bibilia.

Tuje na evidence za bible.

Ukija na maneno Nje ya bible na ukashambulia kanisa ninakushangaa.

NJOO NA BIBLE LETE NENO LA MUNGU.
 
Mimi sijadili maswala hayo.

Mimi napenda tujadili bibilia.

Tuje na evidence za bible.

Ukija na maneno Nje ya bible na ukashambulia kanisa ninakushangaa.

NJOO NA BIBLE LETE NENO LA MUNGU.
Mimi nimeongelea usabato ulivyoanzishwa kwani kuna ubaya hapo?
 
Sasa mkuu ipi dini au dhehebu la haki ambalo tunapaswa kuabudu maana hayo makanisa yote yamefata mpaka siku ya sabato Kwa waroma na huku tena inadaiwa hta uislam ni wao waanzilishi kimbilio la mwanadamu ni wapi
Kanisa Ni mkusanyiko wa watu, sio jengo
 
Kati ya wavaa kobazi na andazi nachagua andazi
510211862.jpg
1790656329.jpg
854703580.jpg
 
Mimi nimeongelea usabato ulivyoanzishwa kwani kuna ubaya hapo?
Ibada ya Sabato, imeanzishwa na Mungu mwenyewe , wewe ulichoweka hapo Ni historia ya usajili wa SDA, lakini pia William Miller hakuwahi kuwa SDA,

Watunza sabato wapo karne na karne , wamekuwa wanapitia transition period ,


Unawajua WAWALDENSIA ? Papa aliwaua na wengi walikimbilia milimani


Yesu aliwafundisha mitume wake kwamba hawatakiwi kufanya lolote siku ya Sabato lakini kilichoamuriwa “kisheria.” Mathayo 12:12.

Aliwaelekeza mitume wake kwamba Sabato kwa maombi ilipaswa kuangaliwa miaka 40 baada ya ufufuo wake. Mathayo 24:20 (kukimbia kwao kulitokea mwaka 66 BK).

Wanawake watauwa waliokuwa wamekaa pamoja na Yesu kwa uangaifu walitunza siku ya saba baada ya kifo chake. Luka 23:56.

Miaka thelathini baada ya ufufuo wa Kristo, Roho Mtakatifu kwa wazi anaiita “siku ya Sabato.” Mdo 13:14.

Paulo, mtume kwa Mataifa, aliita “siku ya Sabato” mwaka 45 BK. Mdo 13:27. Je, Paulo hakujua? Au tuwaamini walimu wa kisaa, wanaodai kwamba ilikoma kuwa Sabato wakati wa ufufuo wa Kristo?

Luka, mwanahistoria wa Kikristo aliyevuviwa, akiandika baadaye mwaka 62 BK, anaiita “sikuya Sabato.” Mdo 13:44.

Waongofu Mataifa waliita Sabato. Mdo 13:42.

Katika Baraza kuu la Kikristo, mwaka 52 BK, mbele ya mitume na maelfu ya wafuasi, Yakobo anaiita “siku ya Sabato.” Mdo 15:21.

Ilikuwa ni desturi kuwa na mikutano ya maombi katika siku hiyo. Mdo 16:13.

Paulo alisoma maandiko katika mikutano ya hadhara katika siku hiyo. Mdo 17:2-3.

Yalikuwa ni mazoea yake kuhubirikatika siku hiyo. Mdo 17:2.

Kitabu cha Matendo ya Mitume hutupatia kumbukumbu ya yeye kuendesha mikutano themanini na nne katika siku hiyo. Angalia Mdo 13:4, 44, 16:13, 17:2, 18:4, 11.
 
Ibada ya Sabato, imeanzishwa na Mungu mwenyewe , wewe ulichoweka hapo Ni historia ya usajili wa SDA, lakini pia William Miller hakuwahi kuwa SDA,

Watunza sabato wapo karne na karne , wamekuwa wanapitia transition period ,


Unawajua WAWALDENSIA ? Papa aliwaua na wengi walikimbilia milimani


Yesu aliwafundisha mitume wake kwamba hawatakiwi kufanya lolote siku ya Sabato lakini kilichoamuriwa “kisheria.” Mathayo 12:12.

Aliwaelekeza mitume wake kwamba Sabato kwa maombi ilipaswa kuangaliwa miaka 40 baada ya ufufuo wake. Mathayo 24:20 (kukimbia kwao kulitokea mwaka 66 BK).

Wanawake watauwa waliokuwa wamekaa pamoja na Yesu kwa uangaifu walitunza siku ya saba baada ya kifo chake. Luka 23:56.

Miaka thelathini baada ya ufufuo wa Kristo, Roho Mtakatifu kwa wazi anaiita “siku ya Sabato.” Mdo 13:14.

Paulo, mtume kwa Mataifa, aliita “siku ya Sabato” mwaka 45 BK. Mdo 13:27. Je, Paulo hakujua? Au tuwaamini walimu wa kisaa, wanaodai kwamba ilikoma kuwa Sabato wakati wa ufufuo wa Kristo?

Luka, mwanahistoria wa Kikristo aliyevuviwa, akiandika baadaye mwaka 62 BK, anaiita “sikuya Sabato.” Mdo 13:44.

Waongofu Mataifa waliita Sabato. Mdo 13:42.

Katika Baraza kuu la Kikristo, mwaka 52 BK, mbele ya mitume na maelfu ya wafuasi, Yakobo anaiita “siku ya Sabato.” Mdo 15:21.

Ilikuwa ni desturi kuwa na mikutano ya maombi katika siku hiyo. Mdo 16:13.

Paulo alisoma maandiko katika mikutano ya hadhara katika siku hiyo. Mdo 17:2-3.

Yalikuwa ni mazoea yake kuhubirikatika siku hiyo. Mdo 17:2.

Kitabu cha Matendo ya Mitume hutupatia kumbukumbu ya yeye kuendesha mikutano themanini na nne katika siku hiyo. Angalia Mdo 13:4, 44, 16:13, 17:2, 18:4, 11.
The Seventh-day Adventist Church had its roots in the Millerite movement of the 1830s to the 1840s, during the period of the Second Great Awakening, and was officially founded in 1863. Prominent figures in the early church included Hiram Edson, Ellen G. White, her husband James Springer White, Joseph Bates, and J. N. Andrews. Over the ensuing decades the church expanded from its original base in New England to become an international organization. Significant developments such the reviews initiated by evangelicals Donald Barnhouse and Walter Martin, in the 20th century led to its recognition as a Christian denomination.

Yaani mwanzilishi wenu unasema hakuwahi kuwa msabato bila yeye wewe ungeijua hiyo dini
 
Mleta uzi uko sahihi.

Kwa usahihi zaidi.

Milima saba ni falme saba: Egypt, Assyria, Babylon, Medo-Persia, Greece, Rome, Papacy. In the days when apostle John received the Revelation: five have fallen (falme 5 zimeshaanguka/zimeshapita); Egypt, Assyria, Babylon, Medo-Persia, Greece; the one is (this is Rome); the other is not yet come (this is the papacy). When he comes he must continue a short space (1,260 prophetic days which is equal to 1,260 years).

Revelation 17:11 And the beast that was, and is not, even he is the eighth, and is of the seven, and goeth into perdition. Huyu beast ambae ni the eighth and is of the seven, ni upapa "uliofufuka" baada ya kejeruhiwa mwaka 1798 (mwisho wa ile miaka 1,260). Jeraha la upapa lilianza kupona kwa kiasi fulani in 1929. Jeraha la upapa limepona kabisa after 2020 (222 years after 1798).

So the woman who sits on the seven mountains is spiritual Babylon. Spiritual Babylon ana sit on Egypt, Assyria, Babylon, Medo-Persia, Greece, Rome, Papacy (including the resurrected Papacy).

The great red dragon (wa Ufunuo 12) ni Satan. Note that ana seven crowns on his seven heads. The seven heads are Egypt, Assyria, Babylon, Medo-Persia, Greece, Rome, Papacy (including the resurrected Papacy). Satan huwa anaitwa the prince of this world. Satan yuko nyuma ya falme za dunia ambazo zina mwasi Mungu wa Biblia. Spiritual Babylon ana sit kwenye hivyo vichwa saba.

Ukifika Ufunuo 13, utaona mnyama mwingine, ambaye ana crowns kwenye pembe zake kumi (na sio kwenye vichwa vyake saba). Note that mnyama huyu wa Ufunuo 13, ni kichwa kimoja kati ya vichwa saba (vyenye crowns) vya the red dragon. Kwenye time period ya utawala wa mnyama wa Ufunuo 13, wakati wa utawala wa zile falme 6 (vichwa 6) umeshapita. Mnyama wa Ufunuo 13 anatawala pamoja na wafalme 10 (pembe 10, ndio maana pembe zake 10, zina crowns 10). Mnyama wa Ufunuo 13 ni upapa, na pembe 10 ni falme 10 za Ulaya zinazo shirikiana na upapa (angalia pia Ufunuo 17).

Watoto wa spiritual Babylon ni spiritual Egypt, Sodom, Tyre, na miji/mataifa mingine ya kidunia yaliyo mwasi Mungu wa Biblia. Watoto wa spiritual Babylon ni pamoja na makanisa yaliyojitenga na upapa, lakini bado yanafuata mafundisho ya upapa (kama kusema siku ya sabato imebadilishwa na kuwa Jumapili, kusheherekea 25th December kama Christmas etc).

Kumbuka Babylon (Babel) ilianza toka Genesis 11. 666 ni namba ya uasi wa mwanadamu dhidi ya Mungu wa Biblia. Ni namba ya uasi wa mamlaka/ufalme wa mwanadamu dhidi ya mamlaka/ufalme wa Mungu wa Biblia. Uasi huo unakataa the holy covenant and mercy, and the gospel of Jesus Christ. Uasi huo unakataa amri za Mungu (YAHWEH), na injili ya Bwana Yesu Kristo (Bwana Yahushua Mashiach). Uasi huo unakataa sabato ya siku ya saba (Jumamosi).

Soma pia vitabu vya Ranko Stefanovic (huyu ni SDA), Revelation of Jesus Christ, na Plain Revelation (google utaviona). Ni vizuri sda wote watanzania, wanaojua kiingereza kuvisoma hivi vitabu. Ranko Stefanovic amepatia vizuri zaidi (sehemu nyingi sana) kuliko Uriah Smith (huyu nae ni SDA), kwenye kitabu chake cha Daniel and the Revelation.

Ukisoma vitabu hivyo vya Ranko Stefanovic, utaelewa vizuri sana sana sana kuhusu kitabu cha Ufunuo, na 666. Kuna sehemu chache sana ana kosea: 1) Revelation 4 ina maanisha YAHWEH yuko kwenye his holy temple in heaven, na YAHWEH anatawala, na anaabudiwa (YAHWEH reigns, and is being worshiped), so it is not necessarily a judgment scene. 2) Parapanda ya 5 ina ambatana na kuja kwa roho ya mpinga kristo duniani, pamoja na ufalme wa kiroho wa mpinga kristo (yaani ufalme wa mnyama wa Ufunuo 13, ambao ni the papacy). Parapanda ya 6 ina ambatana na ujio wa roho ya nabii wa uongo, pamoja na ufalme wa kiroho wa nabii wa uongo wa Ufunuo 13 (yaani taifa la Marekani).

3) Kuto kupatikana kwa tiara yenye title ya Vicarius Filii Dei haimaanishi kwamba title hiyo haipo. Title hiyo ni mfano wa kujikweza kwa mwanadamu dhidi ya Mungu. Kwa hiyo title hiyo ni aina ya 666. Haijalishi namba zake zinakuwa au haziwi 666 (ingawa incidentally zina kuwa 666).

Ranko Stefanovic amepatia sana zaidi ya mafundisho ya sda wenzake kuhusu story ya kuanguka kwa Shetani kutoka mbinguni. Ila naona ana ogopa kuwa muwazi kusema kwamba Shetani alianguka baada ya wiki ya uumbaji. Kwa sababu akisema wazi atakuwa anapingana na mafundisho ya sda wenzake.

Mapungufu ya mafundisho ya kanisa la sda ni haya:

1) Shetani na malaika zake hawa kuanguka kabla ya wiki ya uumbaji. Kwa sababu malaika wote (including Lucifer, ambae baadae ali muasi Mungu) waliumbwa siku ya pili ya wiki ya uumbaji.

2) Hakuna viumbe wengine kama binadamu kwenye sayari nyingine (kama sda wengi wanavyo fundisha).

3) "The Day of Atonement" ni tofauti na "the Day of Judgment". New tastement fulfilment of the Day of Atonement inaanza baada ya kufufuka na kupaa kwa Bwana Yesu, na inaisha at the end of probation period (karibia kabisa na ujio wake wapili).

4) Wabatize kwa staili waliyoitumia mitume wa Yesu, mtu ana inama kidogo kwa mbele, huku amesimama, huku akidumbukia kabisa kwenye maji. Wasibatize kwa staili ya mtu kalala kwa mgongo, wana mshika na kumdumbukiza kwenye maji.

5) Wasi wapinge sda wenzao, wanao sema kwamba Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles. Kwa sababu kiukweli Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles.

6) Wakubali kwamba hawa hodhi ukanisa wa kweli, na kwamba endapo kuna wasabato wanaofuata biblia ambao sio sda, wasabato hao hawana tatizo.

7) Waumini wa sda wawe pia na tabia nzuri kwenye maisha yao.

8) Baadhi ya mafundisho ya mama Ellen White ni maoni yake, na sio vitu alivyo viona kwenye maono (visions). Kwa hiyo baadhi ya mafundisho yake yanaweza yasiwe sahihi. Of course mama Ellen White yuko sahihi kwenye mafundisho yake mengi.

9) Ni vizuri wakristo weusi wakajua prophesies mbali mbali za kwenye Biblia, zinazo ongelea kuhusu injili kuja Afrika. Wakristo weusi, tu avoid a white/Eurocentric view of the bible, na tuwe na a true view of the Bible, which is a biblical centric view of the bible. Wakristo weusi tujaribu pia kuwa na makanisa huru yanayojitegemea (tushirikiane na watu wengine, lakini tusiwe tegemezi kwa watu wengine).

Sda wako sahihi kabisa kabisa kabisa kwamba sabato ni siku ya saba (Jumamosi), na kwamba Bwana Yesu Kristo hakubadilisha siku ya sabato. Na kwamba mpinga Kristo ndiye aliebadilisha siku ya sabato kutoka siku ya saba kwenda siku ya kwanza ya wiki.

Moral of the story ni: Mkristo yeyote anatakiwa kusikiliza mafundisho yanayoendana na biblia, usisikilize mafundisho ambayo hayafuati mafundisho ya biblia (hata kama ni mafundisho ya dhehebu lako).

So injili ya kweli, ni kwamba Utatu Mtakatifu upo, amri 10 zipo (hazikubadilishwa), sabato ni siku ya saba (Jumamosi), tufuate mafundisho ya Bwana Yesu Kristo kama Biblia inavyosema, na Biblia ni kitabu kitakatifu cha YAHWEH (Mungu wa Biblia). Ukristo ndio dini ya ukweli, dini nyingine zote ni za uongo.

Any way tuendelee na shughuli zetu za maisha hadi siku ya mwisho ya dunia, wakati huo huo tukiendelea kumkumbuka Bwana Yesu Kristo hadi siku hiyo atakapo rudi.
 
The Seventh-day Adventist Church had its roots in the Millerite movement of the 1830s to the 1840s, during the period of the Second Great Awakening, and was officially founded in 1863. Prominent figures in the early church included Hiram Edson, Ellen G. White, her husband James Springer White, Joseph Bates, and J. N. Andrews. Over the ensuing decades the church expanded from its original base in New England to become an international organization. Significant developments such the reviews initiated by evangelicals Donald Barnhouse and Walter Martin, in the 20th century led to its recognition as a Christian denomination.

Yaani mwanzilishi wenu unasema hakuwahi kuwa msabato bila yeye wewe ungeijua hiyo dini
Unakopi Wikipedia hujui lolote kuhusu William Miller

Narudia Tena Willam Miller hakuwahi kuwa SDA Wala kusali siku ya Sabato had anakufa


Kasome vzr historia


Na nimekuwekea hapo Watunza Sabato toka Enzi na Enzi
 
Unakopi Wikipedia hujui lolote kuhusu William Miller

Narudia Tena Willam Miller hakuwahi kuwa SDA Wala kusali siku ya Sabato had anakufa


Kasome vzr historia


Na nimekuwekea hapo Watunza Sabato toka Enzi na Enzi
Dini imeanzishwa na binadamu 1863
 
Nasubiri ili ni-note kitu. kila neno yatupasa kulipima, yawezekana kuna asilimia flan za ukweli, hizo ndio nazitafuta
TUANZIE HAPA...


Tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake. Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita." (Ufunuo13:17,18)

[emoji3591]Mambo mawili makuu sana ya mamlaka hii ya Mnyama yanafunuliwa katika Ufunuo
13. "Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio
huru kwa watumwa, watiwe CHAPA [ALAMA] katika mkono wao wa kuume, au
katika vipaji vya nyuso zao; tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala
kuuza, isipokuwa ana chapa [alama] ile, yaani, jina la Mnyama yule, au hesabu ya
jina lake. Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya
Mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na
sita." Ufunuo 13:16-18.


Kwa mujibu wa Ufunuo 13:17, hesabu ya jina lake itakuwa pia ni hesabu ya
mwanadamu.

[emoji3591] Bila shaka inamhusu mtu yule anayeiongoza mamlaka ile ya Mnyama.
Njia ya zamani ya kuipata hesabu ya jina ni kuchukua thamani ya tarakimu za herufi zote na kuzijumlisha ili kupata jumla yake. Kama tunataka kutumia kipimo hicho kwa Upapa, yatupasa kupata jina la kiofisi [cheo] la Papa, ambaye ndiye kiongozi wa Kanisa hilo.

[emoji3591] Kama hiyo ni hesabu ya mtu, basi, bila shaka ingekuwa ni ya mtu yule
anayeuongoza mfumo ule [wa dini].
Ni jambo la kuvutia macho kuona kwamba kuna cheo rasmi cha Kilatini cha Papa, cheo ambacho amepewa na Kanisa lenyewe. Cheo hicho kinaonekana tena na tena
katika vitabu vya Kanisa la Roma. Lakini katika gazeti la kila juma la Kikatoliki liitwalo, OUR SUNDAY VISITOR, la Aprili, 1915, tunao usemi wa kuvutia
unaosema kwamba herufi ya cheo hicho rasmi zimeandikwa katika kofia yake ya Kiaskofu (miter or mitre).

[emoji1542] Hapa ni dondoo lenyewe: "Herufi zilizoandikwa katika kofia ya Papa ni hizi; VICARIUS FILII DEI, ambacho ni Kilatini cha 'ALIYE BADALA YA MWANA WA MUNGU' (VICAR OF THE SON OF GOD).

[emoji3591]Wakatoliki wanashikilia [wanaamini] kwamba Kanisa ambalo ni jamii inayoonekana
ni lazima liwe na kichwa kinachoonekana; Kristo kabla ya kupaa kwake kwenda
mbinguni, alimchagua Mtakatifu Petro kuwa kama Mwakilishi wake. Kwa hiyo,
Askofu wa Rumi kama kichwa cha Kanisa, alipewa cheo cha 'Aliye Badala ya Kristo'
(Vicar of Christ)." Kwa siku hizi kofia ya papa [tiara] haina cheo chake cha Kilatini,
lakini maneno hayo yanatumika katika sherehe za kumtawaza kila Papa mpya anayevikwa taji [kofia hiyo]. Basi, tukiwa na cheo hiki rasmi cha Papa mkononi mwetu, tunaweza kuendelea kutumia kipimo hiki cha Maandiko haya.

[emoji1542]Tunaipataje hesabu ya jina lake? Kwa kupata thamani ya tarakimu za Kirumi za cheo chake cha VICARIUS FILII DEI, tunaifikia hasa hesabu hiyo halisi, 666.

[emoji1542]Angalia jinsi hesabu hizo zilivyofanywa hapa
chini, kila herufi ikipewa thamani ya tarakimu yake:
[emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484]

V ................. 5 F ..................0 D ............. 500
I................... 1 I ...................1 E.................. 0
C ............. 100 L ...............50 I....................1
A ................. 0 I ...................1 501
R ................. 0 I....................1
I .................. 1 53
U au V......... 5
S ...................0
112
112 + 53 + 501 = 666

[emoji1542]Mmoja anaweza kubisha kwamba hilo linaweza kuwa ni jambo linaloweza kutokea
kwa nasibu. Tunakubali ya kwamba upo uwezekano kwa jambo kama hilo kutokea kwa nasibu tu, kama tungekuwa na pointi moja hiyo tu ya utambulisho ya
kuitegemea. Lakini, basi, ukweli ni kwamba, hiyo ni pointi ya KUMI miongoni mwa orodha ndefu ya ishara za tabia yake ambazo Biblia huzitumia kuitambulisha mamlaka hiyo ya Mnyama.

[emoji3591]Hii inaongezea tu uzito na nguvu kwa yale ambayo tayari
yamekwisha kusemwa kwa kuzitumia [ishara zile] kuionyesha mamlaka hiyo ya Papa.
Ni uthibitisho wa kilele pamoja na zile ishara nyingine zote zilizowekwa kwa wazi sana katika Maandiko.

[emoji3591]Alama Hii ----- Ni Udanganyifu Mkuu
Sasa tuko tayari kuchukua hitimisho la kilele cha udanganyifu huu kwa kadiri
mamlaka hiyo ya Mnyama huyo inavyohusika.

[emoji3591]Tayari tumekwisha jifunza ya kwamba
mamlaka hii ingeweka mafundisho mengi ya uongo kinyume na mafundisho makuu ya kweli zake Mungu. Kwamba [mamlaka hiyo] ilikuwa ni mchanganyiko wa mawazo ya kipagani na mafundisho ya dini ya Kikristo ambayo yamekusanywa pamoja kwa hali inayoleta machafuko [kuchanganyikiwa], yanayoitwa vyema kama
"BABELI" katika Maandiko.

[emoji1542]Mafundisho machache ya uongo yanaweza kuorodheshwa kama ifuatavyo: badala ya
Neno la Mungu, imeweka MAPOKEO; badala ya Roho Mtakatifu, imemweka PAPA;
badala ya toleo moja tu la Kristo, imeweka MISA [toleo la kila siku]; badala ya
ubatizo, imeweka KUNYUNYIZA; badala ya Meza ya Bwana, imeweka MKATE
UNAOBADILIKA KABISA NA KUWA MWILI NA DAMU HALISI YA YESU
(Transubstantiation); badala ya Sheria ya milele ya Mungu, imeweka SHERIA
ILIYOFANYIWA MAREKEBISHO [Amri Kumi]; badala ya Zaka; imeweka KODI
[Ushuru] na INDULGENSIA [kuuza vyeti vya msamaha wa dhambi]; badala ya
mauti, imeweka MAHALI PA KUTAKASIA DHAMBI au TOHARANI (Purgatory);
badala ya Muhuri wa Mungu, imeweka ALAMA [CHAPA] YA MNYAMA.

[emoji1542][emoji1484]Hapa tunashughulika hasa na ALAMA YA MNYAMA. Katika Ufunuo 14:9,10
tunasoma hivi, "Mtu awaye yote akimsujudu huyo Mnyama na Sanamu yake, na
kuipokea chapa [alama] katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye naye
atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo
kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake."

[emoji3591]Hili ni jambo la KUFA NA KUPONA. Ni lazima tujue kabisa alama hii ni ya kitu gani hasa na jinsi tunavyoweza
kuikwepa.
Kwanza tunaona katika Biblia ya kwamba ALAMA hii daima iko kinyume na
MUHURI WA MUNGU. Katika Ufunuo 7:2,3, tunajifunza ya kwamba Muhuri wa
Mungu unawekwa juu ya kipaji cha uso sawasawa tu na ile Alama ya Mnyama
inavyowekwa juu ya vipaji vya uso. Vitu hivyo viwili [Muhuri wa Mungu na Alama
ya Mnyama] vinaonekana kuhitilafiana moja kwa moja na kila kimoja kiko kinyume
na kile kingine. Vyote viwili vinapokewa katika kipaji cha uso na mkononi. *_>>>


NITAENDELEA (Nasumbuliwa kidogo na tonsils)
 
Huu Ni mwaka 1863 pale Israel Yerusalemu

Luka 4:16 Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; NA SIKU YA SABATO AKAINGIA KATIKA SINAGOGI KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YAKE, akasimama ili asome.
Kwa hiyo ndio Dini yenu ilipoanzishwa
 
Kwa hiyo ndio Dini yenu ilipoanzishwa
Kasome Mwanzo 1 Mungu anaanzisha Ibada ya Siku ya sabato


Mngekuwa mnasoma Biblia kwa utulivu Wala msingekuwa mnatapeliwa na kina mwamposa


Nakupa challenge hii ili ujue huko ulipo unaibiwa na kudanganywa


Mwaka 30AD Yesu alitoa utabiri huu kabla hajapaa

Mathayo 24:20

“Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.”


Huu unabii ulitimia mwaka 70AD , yaani miaka 40 baada ya Yesu kuwa ameshapaa mbinguni


Cha ajabu Sasa ,manabii kina mwamposa,Geo Devi,Mwingira , Gwajima ,n.k ,Mapadri wanawadanganyeni SABATO iliishia msalabani

Kama Ni hivo Je Yesu kwanini anatoa unabii wa miaka 40 mbele baada ya kupaa ,Je hakujua Sabato imekomea msalaban Kama Wala nguruwe kina mwamposa wanavyowadanganyeni?


Muwe mnahoji na kuuliza ,
 
Back
Top Bottom