Je, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina mamlaka juu ya Spika?

Je, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina mamlaka juu ya Spika?

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Kwenye nchi yoyote ya kidemokrasia kunapokuwa na Katiba iliyoandikwa hiyo katiba inakuwa na mamlaka makuu juu ya Taifa zima. Sio Spika, Rais hata Jaji mkuu anaweza kuwa na mamlaka dhidi ya Katiba.

Mamlaka ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanapatikana kwenye ibara ya 64(5) ambayo yameweka bayana kuwa hakuna mtu au sheria yoyote itayotungwa itakuwa kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania.

Kama ninakosea niko tayari kukosolewa, ibara ya 71 (1) (e) imeweka bayana kuwa mbunge atapoteza ubunge wake kama uanachama wake utakoma kwenye chama kilichompa ridhaa ya kugombea ubunge. Hii ni wazi wabunge 19 wa CHADEMA waliofukuzwa sio wabunge halali hata kama waliapishwa kwa kanuni za bunge. Na spika anawatetea kwa sheria gani, au kanuni gani ambazo zinakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Pia inasikitisha sana Spika wa bunge kudharau maoni ya wastaafu. Kwani ibara ya 71(1)(e) imefutwa? Kwani hii ibara haipo kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka spika Ndugai awe anadharau maoni ya wastaafu na kudai hawajui kinachoendelea? Nini hicho kinachoendelea? Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imebadilishwa? Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina mamlaka juu ya spika?

Jambo la msingi ambalo Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatakiwa akubumke ni kuwa bunge ni wananchi, ndio maana tunatuma wawakilishi wetu huko,la sivyo kila mtanzania angekuwa mbabe na kujiamulia anavyotaka. Na hakuna mtu kwenye nchi hii aliye juu ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Alipoenda kutibiwa India akakaa sana huko nina wasiwasi na whahindi walichofanya, kuna fyuzi ziling'olewa kwa huyu baba. Yaani hana hata aibu. Lakini haya mambo yana mwisho
Ahaaa, ni ubabe tu usiofaa kabisa.
 
Mmejichangaya na mnazidi kujichanganya. Kwa mwenendo huu, hata mkipewa hizo Trilion 2 zinazowatoa roho, msipowajibika nazo hakuna atakae toa maelezo maana wote mmekua kambale wenye mashurubu huko CCM.
Mada hapa ni Constitutional Supremacy, acha upuuzi kama huna hoja nenda kanyonye.
 
Ujinga wa wazi wazi unaofanywa na ccm, sina uhakika kama tutafika 2025 salama, nchi itabaki na makovu mengi sana. ndiyo maana walikimbilia kujipa kinga
Kinga zipi bro? Acha kuropoka kama umekunywa chimpumu
 
Kwenye nchi yoyote ya kidemokrasia kunapokuwa na katiba iliyoandikwa hiyo katiba inakuwa na mamlaka makuu juu ya taifa zima. Sio Spika,Rais hata Jaji mkuu anaweza kuwa na mamlaka dhidi ya katiba...

Nadhani spika anasubiri barua rasmi kutoka kwa KM kwa kumfahamisha juu ya kupoteza uanachama kwa wanachama hao.Lakini hilo pia halimzuii Ndugai kutoa maoni yake binafsi kwa maana yeye ni mwanachama wa CCM.Nadhani CHADEMA waendelee na kufuata utaratibu.
 
Kwenye nchi yoyote ya kidemokrasia kunapokuwa na katiba iliyoandikwa hiyo katiba inakuwa na mamlaka makuu juu ya taifa zima. Sio Spika,Rais hata Jaji mkuu anaweza kuwa na mamlaka dhidi ya katiba..

Ww ndio unaamka sasa, toka awamu hii imeingia madarakani katiba imekuwa ikivunjwa wazi wazi, na baada ya kuona watanzania ni makondoo wamenajisi box la kura kimachomacho, mkawa mnawasifia eti wamechaguliwa na wananchi. Sasa hivi wanafanya lolote maana wanajua mtawasifia.

Kama wameingia madarakani kwa kubaka uchaguzi na wanaona hamna lolote wamefanywa, watafanya lolote watakalo. Kwa kiburi anasema wastaafu waachwe maana hawajui yanayoendelea sasa, kana kwamba katiba imebadilika na hao wastaafu hawana uwezo wa kujua lolote.
 
Ww ndio unaamka sasa, toka awamu hii imeingia madarakani katiba imekuwa ikivunjwa wazi wazi, na baada ya kuona watanzania ni makondoo wamenajisi box la kura kimachomacho, mkawa mnawasifia eti wamechaguliwa na wananchi. Sasa hivi wanafanya lolote maana wanajua mtawasifia. Kama wameingia madarakani kwa kubaka uchaguzi na wanaona hamna lolote wamefanywa, watafanya lolote watakalo. Kwa kiburi anasema wastaafu waachwe maana hawajui yanayoendelea sasa, kana kwamba katiba imebadilika na hao wastaafu hawana uwezo wa kujua lolote.
Ahaaaa,tindo mimi huwa sisifii upuuzi na sipendi sheria kuvunjwa nafikiri unanijua. Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
 
Ahaaaa,tindo mimi huwa sisifii upuuzi na sipendi sheria kuvunjwa nafikiri unanijua. Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.

Nakuuliza, ndio umeamka leo? Toka walivyoanza na sisi tukawa tunapiga kelele nyie si ndio mlikuwa mnasema nchi inayoonyeshwa? Toka lini genge la wezi wa kura wakaoogopa katiba?
 
Back
Top Bottom