Je, Katiba yetu inamruhusu Rais Samia kukaa miaka 15 Ikulu?

Haimruhusu kugombea zaidi ya mara moja kwa miaka mitano tangu alipochukua kijiti kutoka kwa rais halali aliyechaguliwa kwa kura.
 
Haimruhusu kugombea zaidi ya mara moja kwa miaka mitano tangu alipochukua kijiti kutoka kwa rais halali aliyechaguliwa kwa kura.
Hakuna sehemu katika katiba ambapo unaweza kutoa "reference" ili kuonyesha usahihi wa hoja yako ambayo ni nzuri au ni mawazo yako mazuri tu.
 
Ni kweli na ni logical ulichokisema. Awamu ya kwanza ya SSH ni miaka 4 (na nusu). Awamu yake ya pili itakuwa miaka 5 yaani 2025 - 2025.

Ni bahati nzuri (? mbaya) kwamba awamu yake ya kwanza ni miaka 4 na ushee aliyobakiza mtangulizi wake. Sasa kwa mfano mtangulizi wake angekuwa kabakiza miezi 6 au mwaka mmoja ina maana bado awamu yake ya kwanza ingalikuwa miezi 6 au mwaka mmoja tu? Nadhani utata uko hapo. Katiba inasemaje hapo? Ni sawa kwamba awamu ya kwanza inaweza kuwa hata ya mwezi mmoja tu?
 
Mkuu,
Kweli watu wanatoa point nzuri, na wengine kejeli lakini "reference" ya ibara ya katiba ndo inakosekana. Inakuwa ni kama stori za utashi binafsi maana unapoelezea suala la kikatiba ni utaratibu kurejelea ibara ili kutoa mantiki katika hoja ya kikatiba lakini wakuu wangu wengi wao wana hoja zenye mashiko kabisa ila ibara ya kurejea ndo shida....
 
Tena viazi kweri kweri!
 
Nadhani utata uko hapo. Katiba inasemaje hapo? Ni sawa kwamba awamu ya kwanza inaweza kuwa hata ya mwezi mmoja tu?
Mkuu Dr Akili, kiukweli kabisa, kwenye hili, hakuna utata wowote. Ndio maana kule mwanzo nilisema elimu ya katiba inahitajika sana kwa Watanzania wengi. Katiba imeandikwa kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili ila watu ni wavivu kusoma, hawasomi katiba na very unfortunately katika mitaala yetu hakuna somo la katiba!. Tumewaachia wanasheria kitu ambacho sio right, sio fair. Kila mtu anapaswa kusoma katiba na kuijua katiba.

Mambo ya haki ya kuchaguliwa tena kwa kipindi cha pili kwenye nafasi ya uraisi wa JMT yanaongozwa na ibara ya 9 kufungu cha 15 cha sheria namba 34 ya mwaka 1984 iliyofanyiwa mapitio mwaka 1994 na kuingizwa kwenye Ibara ya 40 ya Katiba ya JMT ya mwaka 1977, kwenye kifungu kidogo cha 4, imeelekeza vizuri na wazi kabisa na bila utata wowote.
4) "Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa
mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama akishika kiti cha Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu".

Hii maana yake, kwa vile Samia anashika madaraka kwa kipindi cha zaidi ya miaka mutatu, hivyo hii inahesabiwa ndio awamu yake ya kwanza, bado anayo fursa ya awamu nyingine moja ya mwisho.

Endapo JPM angechomoka baada ya kutumikia urais kwa miaka 2 na nusu, hivyo Samia kushika kwa kipindi kisichozidi miaka 3. Then kipindi hicho Samia angehesabiwa kuimalizia ngwe ya JPM, hivyo Samia angekuwa na fursa za kugombea awamu zake zote mbili, kuanzia 2025-2035.
Hivyo hakuna awamu ya less than 3 years .
P
 
Kwa sasa katiba iko eda.
 
Kumbe katiba yetu ni nzuri sana. Hao wanaotaka tuifumue yote na kuweka ile ya Waryoba lazima kutakuwa na kitu kimepungua kwenye medulla oblongata zao.
 
Akienda znz itawezekana
 
Alikaimu hakugombea kama mgombea uraisi alikuwa akimsindikiza raisi kamili yeye kama makamo.

Unataka nambia wakati wa uchaguzi focus ilikuwa ni yeye au magufuli, na je katika ile karatasi ya kupigia kura, ungeweza kuselect magu halafu ukachagua makamo katika box nyingine?!

So technically samia ni kaimu raisi. Sijui why mnapenda kupotosha uma wa watanzania kwa hoja dhaifu.

Mara oooh hii ni awamu ya sita. Hii inakuwaje awamu ya sita kwa uchanguzi upi ?!
 
SSH amemkaimu nani?

Na huyo aliyekaimiwa yupo wapi, na anatarajia kurudi lini kwenye kiti chake?!

Anyway, SSH hajakaimu bali ni Rais Kamili kwa mujibu wa katiba yetu!!
Unajua maana ya neno Kaimu?! Acheni kupotosha jamii. Mbona wasomi mnakuwa na vichwa vizito hivi?!
 
Samia amekaimu nafasi kwa kipindi ambacho atabidi kuwapo katika uongozi kwa muda zaidi ya miaka mitatu.

Kwa mujibu wa katiba, makamo akikaimu nafasi kwa muda pungufu ya miaka 3 then atakuwa na chaguzi mbili za kuteuliwa agombee tena na wapinzani. But kama alikaimu nafasi kwa kipindi zaidi ya maika 3 yaani mitatu kwenda juu (kama Samia) then technically anakuwa na ruhusa kugombea awamu moja tu yaani kuingia uchaguzi mkuu mara moja tu na si zaidi.

Hii ni kwa mujibu wa katiba yetu ya sasa. Sasa kuna wanywa KVant kwa makusudi kabisa au kwa kukosa ufahamu wanapotosha kuwa bi mkubwa anaweza kugombea mara mbili yaani uchaguzi wa 2025 na wa 2030 hiyo si ukweli na ni upotoshaji wa makusudi kabisa.

Katiba inamuelekeza bi mkubwa mwisho wake kuwa 2030 kisha anakaa benchi kilazima hata kama chama chake kitasema aendelee itakuwa ni kinyume na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tz.
 
Ni kweli kabisa Samia hakaimu Urais lakini ni kweli kabisa kuwa katiba haijaweka wazi kwa mtu anayeapishwa baada ya Rais aliyemtangulia kufa kabla ya muda wake kufa, je ndiyo muhula wake wa kwanza au anakamilisha muhula na baada ya hapo ataanza kuwania muhula wake wa kwanza?
 
Paskali...lugha uliyotumia haijawa ya staha...wewe ni Mutu mnene Sana!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…