Je, kila nafsi itaonja mauti?

Je, kila nafsi itaonja mauti?

Hakuna nafsi ya kuonja mauti wala mboga.

Kwasababu nafsi haipo.

Upo wewe na mimi.

Kifo kipo, ni nature na ndio sifa ya kiumbe hai lazima kipitie njia hiyo.

Japo wanasayansi wanaamini kuwa miaka ya mbeleni huko kunaweza kupatikana ufumbuzi wa kurudisha uhai kwa mtu aliyekufa.

Na ndio maana wanajaribu kuhifadhi miili ya watu isiharibike kwa lengo la kuja kuiwekea uhai huko mbeleni itakapopatikana suluhu.

Ha ha ha ha duuu
 
1Wakorintho 15:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; HATUTALALA SOTE, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.

Hapo 👆 aliposema kwamba hatulala wote bali wote tutabdilika maana yake ni kwamba hatutakufa wote bali wote tutabadilika.
Kwa nini tuamini ufufuo wakati Paulo katika Warumi 3:7 anakiri kwamba anadanganya ?
7 Lakini, ikiwa kweli ya Mungu imezidi kudhihirisha utukufu wake kwa sababu ya uongo wangu, mbona mimi ningali nahukumiwa kuwa ni mwenye dhambi?
 
Wadau, habari ya majukumu bila shaka muwazima wa afya, kama na wale wenye changamoto ya afya, niwaoe pole.

Bila kupoteza muda, twende kwenye mada husika. Hili neno "kila nafsi itaonja mauti," kiuhakika, halijaandikwa kwenye Biblia. Nadhani ni utashi tu wa mwadamu ameamua kutumia hili neno. Sasa turudi kwenye swali letu: Je, ni kweli kila nafsi itaonja mauti?

Kwenye kitabu cha Ufunuo, kinasema parapanda itakapolia, wafu waliolala watafufuliwa kwanza ndipo wataungana na hawa walioko hai kwa wakati huo, ndipo watapaa mawinguni kwenda kumlaki Bwana mawinguni. Sasa, kama tunasema kila nafsi itaonja mauti, na Biblia nayo inasema parapanda itakapolia itakuta kuna binadamu ambao wapo hai watasubiri kwanza wafu wafufuliwe ndipo waungane nao kwenda kumlaki Bwana mawinguni, je, kwanini hiyo kuna baadhi ya watu hawataonja mauti?
Hakuna nafsi ya kuonja mauti wala mboga.

Kwasababu nafsi haipo.

Upo wewe na mimi.

Kifo kipo, ni nature na ndio sifa ya kiumbe hai lazima kipitie njia hiyo.

Japo wanasayansi wanaamini kuwa miaka ya mbeleni huko kunaweza kupatikana ufumbuzi wa kurudisha uhai kwa mtu aliyekufa.

Na ndio maana wanajaribu kuhifadhi miili ya watu isiharibike kwa lengo la kuja kuiwekea uhai huko mbeleni itakapopatikana suluhu.


Mbona huku Tumeambiwa mengine ??

Marko
23 Basi jilindeni; Nimewaambia yote kabla ya wakati wake (ona pia Luka 2:52: MUNGU alimsamehe Yesu).

24 Lakini katika siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake;

25 nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na viumbe vya mbinguni vitatikisika. [4]

26 “Wakati huo watu watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.
27 Naye atawatuma malaika zake na kuwakusanya wateule wake kutoka pepo nne, kutoka mwisho wa dunia hadi mwisho wa mbingu.

28“Sasa jifunzeni jambo hili kutokana na mtini: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.

29 Vivyo hivyo, mwonapo mambo hayo yakitukia, tambueni kwamba yu karibu, mlangoni.

30 Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakika hakitapita mpaka mambo hayo yote yatimie.

31Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.


Yesu hakuahidi tu kwamba saa ingekuja kabla ya kizazi alichokuwa akiishi kati yao kupita katika kitabu cha Marko, lakini pia alitoa ahadi hiyo hiyo katika kitabu cha Luka:

"Kisha akawaambia wote, "Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwa maana yeyote anayetaka kuokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
Yafaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, na huku akijipoteza au kujipoteza mwenyewe?
Mtu ye yote akinionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na utukufu wa Baba na wa malaika watakatifu.
Amin, nawaambieni, baadhi yao katika papa hapa hawataonja mauti hata kabla ya kuuona ufalme wa Mungu.” (Kutoka Biblia ya NIV, Luka 9:23-27).

Sawa na Marko 13:1-37 kama inavyoonyeshwa hapo juu, Yesu katika Luka 9:23-27 bado anatoa ahadi nyingine kwamba saa ingekuja kabla ya kizazi alichokuwa akiishi kati yake kupita.

Sasa ni zaidi ya miaka 2,000 baada ya Yesu na kizazi alichokuwa akiishi kati yao kufa, na bado, Saa haijafika bado!
 
Kwa nini tuamini ufufuo wakati Paulo katika Warumi 3:7 anakiri kwamba anadanganya ?
7 Lakini, ikiwa kweli ya Mungu imezidi kudhihirisha utukufu wake kwa sababu ya uongo wangu, mbona mimi ningali nahukumiwa kuwa ni mwenye dhambi?
Sijakuelewa mkuu, hemu fafanua hapo.
 
nafsi ni nini exactly



BISMILLAH!

Mwanadamu ni mchanganyiko wa vitu vitatu:

1.الجسد Mwili au kiwiliwili

2. الروح Roho, na

3.النفس Nafsi, ambayo ndio kiini cha Uwanadamu wake, ألإنسان ذاته . Vile Roho ndiyo uhai wake. Ikitolewa roho hana uhai; anasalia na umbo tu, الجسد ambalo halikawii kuoza na kusambaratika. Mzoga, tu جيفة.
Kiwiliwili ni umbo, tu, lenye kuibeba hiyo nafsi, na uhai wake. Na ni NAFSI, kwa maana hiyo, ndiyo mwanadamu mwenye majukumu, myenye dhamana na dhimma, myenye kuamini au kukufuru.
Nafsi, kwa mujibu wa Qur'ani, zipo za aina tatu.

(A) Kwanza ni Nafsi yenye kuamrisha maovu tu. Na hii ndiyo nafsi za watu wengi miongoni mwetu wanadamu. Mwanadamu ni mbinafsi sana; mroho sana; mbaguzi sana, isipokuwa akihisi . Na anapenda kujifurahisha na kujishibisha kwa kila aina ya kila kitu kilicho mbele yake. Hivyo, shauku yetu na matamanio yetu, kila mmoja, ni kushibisha matamanio ya nafsi yake tu. Mwenyezi Mungu ameielezea hulka hii ya manadamu kuwa: إن النفس لأمارة بالسوء Hakika nafsi, katika asili yake, inapendelea kuamrisha maovu tu.

Mwenyezi Mungu ameielezea nafsi hii, kupitia Ulimi wa Nabii Yusuf, kwa kusema:


وَمَا أُبَرِّئُ نَفْسِي ۚ إِنَّ النَّفْسَ لَأَمَّارَةٌ بِالسُّوءِ إِلَّا مَا رَحِمَ رَبِّي ۚ إِنَّ رَبِّي غَفُورٌ رَّحِيمٌ (يوسف 12 :53 )

¬_ Na mimi sijitoi lawamani, Kwa hakika nafsi ni yenye kuamrihs sna maovu, isipo kuwa ile ambayo Mola wangu ameirehemu. Hakika Mola wangu ni Maamehevu Mwingi wa kurehemu._ (Yusuf, 12:53)

Kwa mfano:
Wakati wa swala, kwa mfano, unaweza kuadia, lakini nafsi yako ikakwambia: “Ahh acha! Sasa hivi unaangalia mpira wa timu fulani na fulani, ukiondoka utakosa kuona mbabe wake fulani anavyo funga goli!”
Basi unajiambia: Ukimalizika mcheo tu nitaenda kuswali.

Mchezo unamalizika na unashikwa na mengine na swala imekupita kabisa.

Hawa ndio watu wengi. Na nafsi hapa ndio shetani wako. Na kama inavyosemwa: “Shetani wa mtu ni mtu.” Hiyvo, wewe mwenyewe ndiye shetani wa mwanzo wa nafsi yako.

وقال الشاعر :
والنفسُ كالطفلِ إِن تهمله شبَّ على حُبِّ الرضاعِ وإِن تفطمْهُ ينفطم
وخالفِ النفسَ والشيطانَ واعْصِهما وإِن هما مَحَضاكَ النصحَ فاتِهَّمِ

Mshairi mmoja amesema:

Nafsi ni kama mtoto mchanga. Ukimpuuza atakulia kupenda kunyonya. Na ukimwachisha ziwa ataacha.

Na pingana na nafsi yako na Shetani, na usiwatii! Na endao watakuapia kuwa wanakupa nasaha, basi anza kuwatuhumu! Si wa kweli hao!

(B) Nafsi ya pili inayotajwa na Qur'ani ni النفس اللوامة Nafsi inayo jilaumu na kujittathimini mara kwa mara. Ikifanya kosa tu, basi inajiluaumu na kutubu na kurudi kwa Mola wake. Yaani Nafsi yenye kukumbuka, mara kaw mara, majukumu yake, dhiima yake, na dhamana yake, juu yake na juu ya kila asiyekuwa yeye; khasa Mola wake. Hii ndiyo nafsi ya mwenye kumuamini Mola wake kwa dhati. Na ndiyo nafsi za waja wema wengi. Hawa ndio wale التائبون العابدون الساجدون Wepesi wa kutubu, wepesi wa kuabudu na wepesi wa kusujudu na kushukuru. Ni waja wenye kujirudi mara kwa mara.

Hawa ndio waja wema. Nao wapo wengi vile vile. Hawa ndio wale wanao zainiwa mara moja moja na Ibilisi, wakazainika, lakini hawachelewi kukumbuka kuwa wanafanya makosa, basi papo hapo huacha makosa yao hayo na kurudi kwa Mola wao.

Hawa ndio wanaopendwa na Mwenyezi Mungu. Maana hawa ndio wenye kumuabudu kwa wingi Mola wao, na, kwa kweli, Amewaumba wawe hivyo, ili wamuabudu mara kwa mara.
( C) Nafsi ya tatu inayo zunguzia Qur'ani ni النفس المطمئنة Nafsi iliyotilia tuli, haitikisiki, haizainiki, haipapariki, inamkumbuka Mola wake mara zote na inamuweka Mola wake mble yake, maana inajuwa kuwa inaonekana Naye, hata kama yeye yenyewe haimuoni. Hizi ni nafsi za Mitume صلوات الله وسلامه عليهم
Hawa siku zote wamo katika himaya na ulinzi wa Mwenyezi Mungu. Miongoni mwao wamo mawalii wa Mwenyezi Mungu, ambao hakuna awajuwao isipokuwa Yeye mwenyewe.

Hawa ndio wanao ambiwa:
﴿ يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ * ارْجِعِي إِلَى رَبِّكِ ﴾

[ سورة الفجر: 27-28]
Ewe Nafsi iliyo tua! Rejea kwa Mola wako umeridhika, na umeridhisha. Basi ingia miongoni mwa waja wangu. Na ingia katika Pepo yuangu.

Hizo ndio nafsi zilizo zungumzwa na Qur'ani.

Tukija upande wa moyo, basi moyon ni sehemu tu ya viungo vya mwanadamu, tofauti na nafsi na roho. Nafsi ndiyo kiini cha mwanadamu, ndiyo uwanadamu wake. Vile roho ni uhai wa mwandamu. Na moyo ni kiungo kimojawapo wa viungo vya mwili wa mwanadamu.
Ila, moyo, ndio Injini na Dira ya mwili wa mwanadamu. Ni doge la nyama tu, ndani ya mwili wake, lenye kazi maalumu mwilini mwake; kuzungusha damu mwilini mwke, na kuisafisha pamoja na viungo vengine. Ni injini ya ujasiri wa uhai wake. Likitengemaa donge hilo basi mwili wake wote utatengemaaa. Na likitetereka au kuharibika au kupootoka basi na mwiliwake wote nao hutetereka na kupotoka.

Moyo, kwa maana hiyo, ni mfano wa kinu cha taa, au Jenereta, katika mwili wa mwanadamu. Ndiyo injini ya kuendesha mwili wa mwanadamu.

Mtume ﷺ ameuelezea MOYO kuwa ni donge la damu. Likitengenea unatengemea mwili wote wa mwanadamu. Na likifisidika basi na mwili wote wa mwanadamu unafisidika. Unakufa, ha kuoza.

Halafu kuna Akili, ubongo. Ubongo ni kompyuta ya mwili wa mwandamu. Ni bohari la kuhifadhin kila kitu ndani yake. Ndiyo hard-disc la mwili na moyo wa mwadamu.

Humo huhifadhiwa maalumat yote uyajuwayo na ujifunjzayo, na hivyo ndiko kunako toka amri kukujiulisha kuwa kuna kitu kimekuuma mguni, na kutokana na muumo huo, basi huyo ni mbu, ect., ect. Mfukuze! Au muue! Maana hiyo ndiyo taafira iliyo ihifadhin katika hard-disc hilo. Vile vile ni ubongo ndio unaokuongoza kuwa ukiona X basi kuna Y inakuja. Maana hiyo ndiyo taarifa iliyo ihifadhi katika hard-disc lako.

Kwa maana hiyo, Mwenyezi Mungu amekupa siyo Nafsi, tu, ambayo ndiyo WEWE na kukupa Roho ili uwe hai, bali amekupa injini ya kukuendesha na kinu chca umema kusaidia mwili wako kufanya kazi. Na wakati huo huo, amekupa Akili, katika sura ya Ubongo, ili kukuwezesha kujuwa mema na maovu, mazuri na mabaya, na juu ya yote hayo akautumia Mitume, na kukupa kumbukumbu za Kitabu au Vitabu Vyake, kukujilisha zaidi nini anakutaka ufanye au usifanye, na kwanini.

Hivyo, mwenye kujichagulia la kufanya au kutokufanya ni WEWEW, na utalipwa kwa uamuzi wako huo. Anapo kunyima Mwenyuezi Mugu uwezo wa kuamua, kwa maana ameifanya akili yako isifanye kazi sawa sawa, basi hakupatilizi. Sisi tunakuita mwenda wazimu. Na Mwenyezi Mungu huwanyanyag'anya baadhi ya waja wake uwezo wa kupambanua jema na baya, ili watambue hivyo wenigine umuhimun wa kutumia ubongo wao sawa sawa.
Katika yote hayo: Mwenyezi Mungu amebainisha, wazi wazi, kuhusu NAFSI na vikorombwero vyake, kwa kusema:
قال تعالى :
﴿ وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَافَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَاقَدْ أَفْلَحَ مَنْ زَكَّاهَا*وَقَدْ خَابَ مَنْ دَسَّاهَا ﴾
[ سورة الشمس:7-10]

_Na nafsi na kwa aliye itengeneza! Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake. Hakika amefanikiwa aliye itakasa Na amehasirika alie iviza.

Kwa maneno mengine:
Kila mtu ajipime yumo katika fungu gani la nafsi. Wala asimsingizie au kumtupia lawama Shetani tu, maana Shetani ni kweli atamzaini, lakini akizainika ni ubwete wake mwenyewe, maana ametumiwa Mitume, ameachiwa Kitabu, ameonya, amefunzwa, ame tahadharisha, na papo akakubali kuzainika, au akajizaini mwenyewe. Kesho hana hoja ya kujitetea. Na akimrushia lawama Shetani, basi Shetani atamjibu kwa ulimi mpana:

وَقَالَ الشَّيْطَانُ لَمَّا قُضِيَ الْأَمْرُ إِنَّ اللَّهَ وَعَدَكُمْ وَعْدَ الْحَقِّ وَوَعَدتُّكُمْ فَأَخْلَفْتُكُمْ ۖ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا أَن دَعَوْتُكُمْ فَاسْتَجَبْتُمْ لِي ۖ فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوا أَنفُسَكُم ۖ مَّا أَنَا بِمُصْرِخِكُمْ وَمَا أَنتُم بِمُصْرِخِيَّ ۖ إِنِّي كَفَرْتُ بِمَا أَشْرَكْتُمُونِ مِن قَبْلُ ۗ إِنَّ الظَّالِمِينَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ (إبراهيم 12 : 22 )
_
Na Shetani atasema itao tolewa hukumu ya mwisho: Hakika Mwenyezi Mungu alikuahidini ahadi ya kweli. Nami nilikuahidini; lakini sikukutimizieni. Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipokuwa nilikuiteni, nanyi mkaniitikia. Basi msinilaumu mimi; bali jilaumuni NAFSI ZENU. Mimi siwezi kuwa mtetezi wenu wala nyinyi hamuwezi kuwa watetezi wangu. Hakika mimi nilikataa tangu zamani kushirikishwa na Mwenyezi Mungu. Hakika madhalimu watakuwa na adhabu kali._

والله أعلم
وبالله التوفيق
 
Sijakuelewa mkuu, hemu fafanua hapo.

Kwa nini Paulo hapaswi kuaminiwa



Paulo hakuwahi kukutana na Yesu maishani mwake.

Hii ni moja ya sababu kuu ya kutomwamini na kumwamini Paulo.

Kabla ya kujidai kuwa mtume, jina lake lilikuwa Sauli na aliwahi kuwa muuaji wa waumini wa kweli.

Akiwa njiani kuelekea Damasko, akiwa kwenye mgawo wa kuwasumbua waamini wa kweli, anadai kuwa ameona maono ya Kristo, na baada ya hayo, alidai kwamba Yesu alimpa mamlaka ya kufundisha kwa jina lake.


Jee !!!!! kuna ukweli wowote hapa katika maneno yake hayo ??

Kwa vile hakuwahi kukutana na Yesu, akili ya kawaida inasema kwamba yeye hana uhusiano wowote na dini na tunaposoma anachosema tunakuta kwamba hakika yeye hana uhusiano wowote na dini ya kweli ya Nabii Isa (amani iwe juu yake). .



Hebu tuangalie ono la Paulo anapolielezea kwa watu mbalimbali, tofauti wake



1. Katika MATENDO 9:3, imeelezwa kwamba ni Paulo pekee aliyeanguka chini alipoona mwanga. Mstari wa 7 unasema kwamba wengine pamoja naye walisimama bila la kusema.

2. MATENDO 26:14 inasema WOTE walianguka chini.

3. MATENDO 9:7 inasema kwamba watu waliosafiri pamoja na Paulo hawakumwona mtu bali walisikia sauti.

4. MATENDO 22:9 inasema wale waliokuwa pamoja na Paulo waliona nuru lakini HAWAKUsikia sauti ya msemaji.

Hayo hapo juu ni mikanganyiko ya wazi

Mtu ye yote angemkataa Paulo mara moja baada ya kusoma mistari hii.

Ikiwa huu ni uwongo wa wazi tu na Paulo amesahau aliposema nini, basi si zaidi ya ujinga wake lakini ikiwa anatumia mbinu hii kwa makusudi kusimulia hadithi tofauti kwa watu tofauti, basi mbinu hii bado inatumika hata leo.

Mbinu kama hiyo imeweka msingi muhimu sana wa Kanisa, i.e. kupitisha njia inayomfaa mtu.
 
Mtoa mada achana na habari zijazo kwanza angalia hata angalia kwanza zilizopita... Kwa mujibu wa biblia Henoko hakufa na Elia pia hakufa. Kwa kuangalia hapo tu unaona huo msemo hauna maana (kwa wakristo). Nadhani waislamu wanaamini hivyo na sisi wakristo tulivyo wepesi wa kudaka vitu hata tusivyovijua tumeiga
Uislamu unaamini watu wote watakufa, hata nabii issa atarudishwa duniani aje aonje na yeye mauti, watakaokuwa hai ni malaika tu maana malaika israfil mpuliza parapanda ndiye atakaepuliza kwa amri ya Mwenyezi Mungu mara zote mbili, inamaana lazima atakuwa hai
 
Mbona huku Tumeambiwa mengine ??

Marko
23 Basi jilindeni; Nimewaambia yote kabla ya wakati wake (ona pia Luka 2:52: MUNGU alimsamehe Yesu).

24 Lakini katika siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake;

25 nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na viumbe vya mbinguni vitatikisika. [4]

26 “Wakati huo watu watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.
27 Naye atawatuma malaika zake na kuwakusanya wateule wake kutoka pepo nne, kutoka mwisho wa dunia hadi mwisho wa mbingu.

28“Sasa jifunzeni jambo hili kutokana na mtini: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.

29 Vivyo hivyo, mwonapo mambo hayo yakitukia, tambueni kwamba yu karibu, mlangoni.

30 Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakika hakitapita mpaka mambo hayo yote yatimie.

31Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.


Yesu hakuahidi tu kwamba saa ingekuja kabla ya kizazi alichokuwa akiishi kati yao kupita katika kitabu cha Marko, lakini pia alitoa ahadi hiyo hiyo katika kitabu cha Luka:

"Kisha akawaambia wote, "Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwa maana yeyote anayetaka kuokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
Yafaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, na huku akijipoteza au kujipoteza mwenyewe?
Mtu ye yote akinionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na utukufu wa Baba na wa malaika watakatifu.
Amin, nawaambieni, baadhi yao katika papa hapa hawataonja mauti hata kabla ya kuuona ufalme wa Mungu.” (Kutoka Biblia ya NIV, Luka 9:23-27).

Sawa na Marko 13:1-37 kama inavyoonyeshwa hapo juu, Yesu katika Luka 9:23-27 bado anatoa ahadi nyingine kwamba saa ingekuja kabla ya kizazi alichokuwa akiishi kati yake kupita.

Sasa ni zaidi ya miaka 2,000 baada ya Yesu na kizazi alichokuwa akiishi kati yao kufa, na bado, Saa haijafika bado!
Unamaanisha huo ulioandika ni uongo?
 
Kwa nini Paulo hapaswi kuaminiwa



Paulo hakuwahi kukutana na Yesu maishani mwake.

Hii ni moja ya sababu kuu ya kutomwamini na kumwamini Paulo.

Kabla ya kujidai kuwa mtume, jina lake lilikuwa Sauli na aliwahi kuwa muuaji wa waumini wa kweli.

Akiwa njiani kuelekea Damasko, akiwa kwenye mgawo wa kuwasumbua waamini wa kweli, anadai kuwa ameona maono ya Kristo, na baada ya hayo, alidai kwamba Yesu alimpa mamlaka ya kufundisha kwa jina lake.


Jee !!!!! kuna ukweli wowote hapa katika maneno yake hayo ??

Kwa vile hakuwahi kukutana na Yesu, akili ya kawaida inasema kwamba yeye hana uhusiano wowote na dini na tunaposoma anachosema tunakuta kwamba hakika yeye hana uhusiano wowote na dini ya kweli ya Nabii Isa (amani iwe juu yake). .



Hebu tuangalie ono la Paulo anapolielezea kwa watu mbalimbali, tofauti wake



1. Katika MATENDO 9:3, imeelezwa kwamba ni Paulo pekee aliyeanguka chini alipoona mwanga. Mstari wa 7 unasema kwamba wengine pamoja naye walisimama bila la kusema.

2. MATENDO 26:14 inasema WOTE walianguka chini.

3. MATENDO 9:7 inasema kwamba watu waliosafiri pamoja na Paulo hawakumwona mtu bali walisikia sauti.

4. MATENDO 22:9 inasema wale waliokuwa pamoja na Paulo waliona nuru lakini HAWAKUsikia sauti ya msemaji.

Hayo hapo juu ni mikanganyiko ya wazi

Mtu ye yote angemkataa Paulo mara moja baada ya kusoma mistari hii.

Ikiwa huu ni uwongo wa wazi tu na Paulo amesahau aliposema nini, basi si zaidi ya ujinga wake lakini ikiwa anatumia mbinu hii kwa makusudi kusimulia hadithi tofauti kwa watu tofauti, basi mbinu hii bado inatumika hata leo.

Mbinu kama hiyo imeweka msingi muhimu sana wa Kanisa, i.e. kupitisha njia inayomfaa mtu.
Siyo tu kitabu cha Paulo ndicho chenye mkanganyiko, Biblia almost yote ina mkanganyiko,, na unaposema Paulo hapaswi kuaminiwa, you're wrong brother coz Paulo hakujiandikia tu kama unavyofikiri bali lile ni neno lililotoka kwa Mwenyezi Mungu mwenyewe.
 
Hakuna nafsi ya kuonja mauti wala mboga.

Kwasababu nafsi haipo.

Upo wewe na mimi.

Kifo kipo, ni nature na ndio sifa ya kiumbe hai lazima kipitie njia hiyo.

Japo wanasayansi wanaamini kuwa miaka ya mbeleni huko kunaweza kupatikana ufumbuzi wa kurudisha uhai kwa mtu aliyekufa.

Na ndio maana wanajaribu kuhifadhi miili ya watu isiharibike kwa lengo la kuja kuiwekea uhai huko mbeleni itakapopatikana suluhu.

Ulianza vizuri ukaja kuharibu mwishoni

Uhai kiimani ndio nafsi, roho nk........Hivi vitu havipo

Kiumbe kuwa hai ni state ambayo viungo vyote vina coordinate kumuwezesha kiumbe kuishi
Kufa ni pale viungo vinaposimama kufanya kazi kwa pamoja

Sasa unaposema uhai utunzwe utatunzwa wapi?
Utarudi kulekule kwenye nafsi na roho
 
Wadau, habari ya majukumu bila shaka muwazima wa afya, kama na wale wenye changamoto ya afya, niwaoe pole.

Bila kupoteza muda, twende kwenye mada husika. Hili neno "kila nafsi itaonja mauti," kiuhakika, halijaandikwa kwenye Biblia. Nadhani ni utashi tu wa mwadamu ameamua kutumia hili neno. Sasa turudi kwenye swali letu: Je, ni kweli kila nafsi itaonja mauti?

Kwenye kitabu cha Ufunuo, kinasema parapanda itakapolia, wafu waliolala watafufuliwa kwanza ndipo wataungana na hawa walioko hai kwa wakati huo, ndipo watapaa mawinguni kwenda kumlaki Bwana mawinguni. Sasa, kama tunasema kila nafsi itaonja mauti, na Biblia nayo inasema parapanda itakapolia itakuta kuna binadamu ambao wapo hai watasubiri kwanza wafu wafufuliwe ndipo waungane nao kwenda kumlaki Bwana mawinguni, je, kwanini hiyo kuna baadhi ya watu hawataonja mauti?

Hii ni kwa mujibu wa uislam na sio ukristo
 
The fact ni kuwa hata kama utafikia level ya kutokufa mwili wa udongo hauingii mbinguni ila unabadulishwa kuwa mwili wa kiroho
 
Back
Top Bottom