Je, kila nafsi itaonja mauti?

Je, kila nafsi itaonja mauti?

Ulianza vizuri ukaja kuharibu mwishoni

Uhai kiimani ndio nafsi, roho nk........Hivi vitu havipo

Kiumbe kuwa hai ni state ambayo viungo vyote vina coordinate kumuwezesha kiumbe kuishi
Kufa ni pale viungo vinaposimama kufanya kazi kwa pamoja

Sasa unaposema uhai utunzwe utatunzwa wapi?
Utarudi kulekule kwenye nafsi na roho
Wapi nimeandika uhai unatunzwa?
 
Sijakupata mkuu hebu jazia nyama kidogo
Yaan lita pulizwa Mara mbili

Ambapo mara ya kwanza kuna watu bado watakuwepo hai kwahiyo likipulizwa Mara ya kwanza watu ambao wako hai wote watakufa.

Halafu ndio lita pulizwa tena Mara ya pili sasa ndio wote tena watafufuka kuanzia mtu wa kwanza kufa.
 
Kama una mwamini Yesu, jibu lako hili hapa:
Yohana 8:51
Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele.
 
Siyo tu kitabu cha Paulo ndicho chenye mkanganyiko, Biblia almost yote ina mkanganyiko,, na unaposema Paulo hapaswi kuaminiwa, you're wrong brother coz Paulo hakujiandikia tu kama unavyofikiri bali lile ni neno lililotoka kwa Mwenyezi Mungu mwenyewe.

Je, haya ni maneno ya Paulo au Ufunuo wa Kimungu wa MUNGU Mwenyezi?

Wanatheolojia wa Kikristo wameunda uwongo na hadithi kuhusu Biblia kuwa ni Maneno ya Mungu .

Wacha tuone jinsi dai hili la uwongo kama lina ukweli wowote

2 Timotheo 4:9-13

9 Jitahidi kuja kwangu upesi,

10 kwa maana Dema ameniacha kwa kuupenda ulimwengu huu akaenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.

11 Luka peke yake ndiye aliye pamoja nami. Mchukue Marko uje naye, kwa maana ananisaidia sana katika huduma yangu.

12 Nilimtuma Tikiko Efeso.

13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo kule Troa, na hati-kunjo zangu, hasa zile za ngozi.


Tito 3:12-14

12 Mara nitakapomtuma kwako Artema au Tikiko, jitahidi sana kuja kwangu Nikopoli, kwa maana nimeamua kukaa huko wakati wa baridi.

13 Fanya yote uwezayo kumsaidia mwanasheria Zena na Apolo katika safari yao na kuhakikisha kwamba wana kila kitu wanachohitaji.

14 Watu wetu lazima wajifunze kujitoa wenyewe katika kufanya lililo jema, ili wapate mahitaji ya kila siku na si kuishi maisha yasiyo na matokeo.
 
Siyo tu kitabu cha Paulo ndicho chenye mkanganyiko, Biblia almost yote ina mkanganyiko,, na unaposema Paulo hapaswi kuaminiwa, you're wrong brother coz Paulo hakujiandikia tu kama unavyofikiri bali lile ni neno lililotoka kwa Mwenyezi Mungu mwenyewe.

Kuna mistari inayoonyesha kwamba Paulo alikuwa akihubiri Injili yake mwenyewe...

Warumi 2:16

16 Hili litatukia siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama Injili yangu inavyotangaza.

Warumi 16:25

Basi atukuzwe yeye awezaye kuwathibitisha ninyi kwa Injili yangu na uhubiri wa Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyofichwa tangu zamani za kale;

Kuna mistari inayoonyesha kwamba Paulo alikuwa akihubiri Injili ya Mungu...


Warumi 15:16

16 niwe mhudumu wa Kristo Yesu kwa watu wa mataifa, mwenye wajibu wa ukuhani wa kutangaza Habari Njema ya Mungu, ili watu wa mataifa mengine wawe dhabihu inayokubalika kwa Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.

2 Wakorintho 11:7

7 Je, ni dhambi kwangu kujishusha ili nipate kuwainua ninyi kwa kuwahubiria Habari Njema ya Mungu bila malipo?

Kuna mistari inayoonyesha kwamba Paulo alikuwa akihubiri Injili ya Kristo...

1 Wakorintho 9:13

Lakini hatukutumia haki hii. Badala yake, tunavumilia chochote badala ya kuizuia Injili ya Kristo. 13 Je!

2 Wakorintho 2:12

12 Nilipokwenda Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nikaona kwamba Bwana amenifungulia mlango.

2 Wakorintho 9:13

13 Kwa sababu ya utumishi mliojionyesha wenyewe, watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utii unaoambatana na kukiri kwenu Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wenu katika kushiriki pamoja nao na pamoja na watu wengine wote.

2 Wakorintho 10:14

14 Hatuendi mbali sana katika kujisifu kwetu, kama ingekuwa hivyo kama hatungekuja kwenu, kwa maana tulifika kwenu kwa Habari Njema ya Kristo.

Warumi 1:9

9 Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuihubiri Habari Njema ya Mwana wake, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka ninyi daima.

Mstari wa mwisho unaonyesha tofauti kati ya Mungu na Mwana wake (ikimaanisha Yesu).

Je, Paulo alikuwa akihubiri injili yake mwenyewe, injili ya Yesu au Injili ya Mungu?

 
Je, haya ni maneno ya Paulo au Ufunuo wa Kimungu wa MUNGU Mwenyezi?

Wanatheolojia wa Kikristo wameunda uwongo na hadithi kuhusu Biblia kuwa ni Maneno ya Mungu .

Wacha tuone jinsi dai hili la uwongo kama lina ukweli wowote

2 Timotheo 4:9-13

9 Jitahidi kuja kwangu upesi,

10 kwa maana Dema ameniacha kwa kuupenda ulimwengu huu akaenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.

11 Luka peke yake ndiye aliye pamoja nami. Mchukue Marko uje naye, kwa maana ananisaidia sana katika huduma yangu.

12 Nilimtuma Tikiko Efeso.

13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo kule Troa, na hati-kunjo zangu, hasa zile za ngozi.


Tito 3:12-14

12 Mara nitakapomtuma kwako Artema au Tikiko, jitahidi sana kuja kwangu Nikopoli, kwa maana nimeamua kukaa huko wakati wa baridi.

13 Fanya yote uwezayo kumsaidia mwanasheria Zena na Apolo katika safari yao na kuhakikisha kwamba wana kila kitu wanachohitaji.

14 Watu wetu lazima wajifunze kujitoa wenyewe katika kufanya lililo jema, ili wapate mahitaji ya kila siku na si kuishi maisha yasiyo na matokeo.
Briefly kama unaisoma Biblia as if ni kitabu cha hadithi au magazeti kamwe hutokuja kuielewa.
 
Briefly kama unaisoma Biblia as if ni kitabu cha hadithi au magazeti kamwe hutokuja kuielewa.
Mbona hujaniwekea mfano wa aya kuonyesha naisoma biblia kama kitabu cha hadithi au magazeti ?? unao ushahidi ??

Mimi nimenukuu tu aya zilivyoandikwa , sijatia langu
 
Je, Paulo alikuwa akihubiri injili yake mwenyewe, injili ya Yesu au Injili ya Mungu?
Unaandika maelezo marefu sana yasiyokuwa na mantiki ya aina yoyote ile.

Kwanza kabisa inaonekana neno la Mungu hulijui vizuri, cha kukusaidia ni kwamba Mwenyezi Mungu ni mgawanyiko wa nafsi kuu tatu (3)
1. Mungu Baba.
2.Mungu Mwana.
3. Mungu roho Mtakatifu.

Paulo alikuwa anahubiri injili kwa ajili ya Mungu mwenyewe (Mungu Baba) kwa ufunuo wa roho Mtakatifu, sijui kama utanielewa???
 
Mbona hujaniwekea mfano wa aya kuonyesha naisoma biblia kama kitabu cha hadithi au magazeti ?? unao ushahidi ??

Mimi nimenukuu tu aya zilivyoandikwa , sijatia langu
Huko kunukuu mistari ya kwenye Biblia bila ya kuisoma na kuielewa,, ni kutafuta kuchoshana tu hapa,, maana hatuwezi kuelewana..
 
Huko kunukuu mistari ya kwenye Biblia bila ya kuisoma na kuielewa,, ni kutafuta kuchoshana tu hapa,, maana hatuwezi kuelewana..

Hiyo mistari imeandikwa kwa kiswahili na mimi ni mswahili sasa kama hizo aya zina maana nyengine niletee biblia yenye kuelezea maana ya hizo aya
 
Unaandika maelezo marefu sana yasiyokuwa na mantiki ya aina yoyote ile.

Kwanza kabisa inaonekana neno la Mungu hulijui vizuri, cha kukusaidia ni kwamba Mwenyezi Mungu ni mgawanyiko wa nafsi kuu tatu (3)
1. Mungu Baba.
2.Mungu Mwana.
3. Mungu roho Mtakatifu.

Paulo alikuwa anahubiri injili kwa ajili ya Mungu mwenyewe (Mungu Baba) kwa ufunuo wa roho Mtakatifu, sijui kama utanielewa???


Una ushahidi wa kuthibitisha kuwa huyo paulo alikuwa anahubiri ufunuo wa roho Mtakatifu ??
 
Unaandika maelezo marefu sana yasiyokuwa na mantiki ya aina yoyote ile.

Kwanza kabisa inaonekana neno la Mungu hulijui vizuri, cha kukusaidia ni kwamba Mwenyezi Mungu ni mgawanyiko wa nafsi kuu tatu (3)
1. Mungu Baba.
2.Mungu Mwana.
3. Mungu roho Mtakatifu.

Paulo alikuwa anahubiri injili kwa ajili ya Mungu mwenyewe (Mungu Baba) kwa ufunuo wa roho Mtakatifu, sijui kama utanielewa???

Imani ya utatu mtakatifu inaweza kuwa msingi mkuu wa imani ya Ukristo lakini haina ukweli au msingi wowote kutoka kwenye Maandiko Matakatifu - imani yote imeundwa na mwanadamu kwa asili yake.

Huu ni mfano - mwingine wa kwamba ni jinsi gani imani za kipagani zilivyoingizwa kwenye ububusa wa ukristo ili kuufanya ukristo ukubalike zaidi kwa wapagani.


Wakristo walio wengi, wanapoombwa kuielezea imani hii (ya utatu), hawawezi kutoa jibu lolote isipokuwa kusema:

"Ninaamini hivyo kwa sababu niliambiwa niamini hivyo". Wanalielezea kwamba "Ni siri ya Mungu - hakuna mtu anayejua" ingawa Biblia inasema katika Wakorinto wa kwanza 14:33 kwamba:
"Mungu sio mwanzilishi wa utatanishi na migongano".

Hata aliyeipa nguvu na kuihimiza imani hii ya utatu aliona ugumu mkubwa katika kuielewa imani hii.

Inasemekana kwamba Athanasius, askofu aliyeitwa na kuitangaza rasmi imani hii ya utatu, alikiri kwamba alivyokuwa akizidi kuandika juu ya imani hii, ndivyo uwezo wake wa kuielezea imani hii ulivyokuwa ukizidi kupungua.
 
Mbona huku Tumeambiwa mengine ??

Marko
23 Basi jilindeni; Nimewaambia yote kabla ya wakati wake (ona pia Luka 2:52: MUNGU alimsamehe Yesu).

24 Lakini katika siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake;

25 nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na viumbe vya mbinguni vitatikisika. [4]

26 “Wakati huo watu watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.
27 Naye atawatuma malaika zake na kuwakusanya wateule wake kutoka pepo nne, kutoka mwisho wa dunia hadi mwisho wa mbingu.

28“Sasa jifunzeni jambo hili kutokana na mtini: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.

29 Vivyo hivyo, mwonapo mambo hayo yakitukia, tambueni kwamba yu karibu, mlangoni.

30 Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakika hakitapita mpaka mambo hayo yote yatimie.

31Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.


Yesu hakuahidi tu kwamba saa ingekuja kabla ya kizazi alichokuwa akiishi kati yao kupita katika kitabu cha Marko, lakini pia alitoa ahadi hiyo hiyo katika kitabu cha Luka:

"Kisha akawaambia wote, "Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwa maana yeyote anayetaka kuokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
Yafaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, na huku akijipoteza au kujipoteza mwenyewe?
Mtu ye yote akinionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na utukufu wa Baba na wa malaika watakatifu.
Amin, nawaambieni, baadhi yao katika papa hapa hawataonja mauti hata kabla ya kuuona ufalme wa Mungu.” (Kutoka Biblia ya NIV, Luka 9:23-27).

Sawa na Marko 13:1-37 kama inavyoonyeshwa hapo juu, Yesu katika Luka 9:23-27 bado anatoa ahadi nyingine kwamba saa ingekuja kabla ya kizazi alichokuwa akiishi kati yake kupita.

Sasa ni zaidi ya miaka 2,000 baada ya Yesu na kizazi alichokuwa akiishi kati yao kufa, na bado, Saa haijafika bado!
Basi katika mafungu yanayofuata yesu hapo ulipoishia kwenye kitabu cha marko yesu amesema lakini hakuna ajuaye saa ya kuja kwake wala hata malaika hawaijui


Marko 13 :32 walakini habari za siku ile na saa ile hakuna aijuaye hata malaika walio mbinguni, wala mwana ila baba.
Hapa yesu amehitimisha kwamba hakuna ajuaye siku wala saa ya kuja kwake ila baba pekee, sasa alipokuwa amesema "hakika kizazi hiki hakita pita hata yote yatimie katika marko 13 :30" alikuwa anamaanisha nini?
Ukisoma kuanzia marko 13 :1 yesu alikuwa amezungumzia mateso ambayo yangewapata watu wake yani hao mitume na kwamba baada ya hayo wakati hule wa mwisho ungekuwa umekalibia lakini hakuna "hajuaye saa ya kuja kwake"
Kwa hakika aliyoyasema yesu ni yale mateso waliyo yapata mitume hao kuminambili ambao yesu aliwaacha wakahubiri injiri na hao mitume waliuwa kwa mateso kwa ajili ya jina la yesu na hapo ndipo yesu anatabiri kuwa mateso hayo aliyo yaeleza kuanzia marko13:1 mpaka 30 anasema kwamba mateso yale yangetokea katika kizazi hiko
Lakini utabiri huu ulitimia baada tu ya yesu kupaa mbinguni mitume walianza kuteswa na kuuwawa kwaajili ya ule ushuhuda waliokuwa nao kama ukipitia historia utaona kwamba kuliwai kuwa na dola la rumi ya kale ambayo ndiyo iliyo wauwa wakristo hao ambao walikuwa ni kizazi kimoja na yesu kristo
Lakini vipi kuhusu ujio wake? Licha ya yesu kutabiri mateso hayo yatakayo wapata watu wake katika kizazi hiko yani hao mitume amesema "kwa hakika hakuna ajuaye saa ile ya kuja kwake ila baba"



Hili ndiyo jibu la swali lako bila shaka nazani umeelewa fungu hilo la marko 13:30 "hakika kizazi hiki hakita pita" hata yote yatimie ni kwamba yalikuwa ni mateso ambayo watayapitia mitume kwa hakika unabii huo ulitimia na mitume waliteswa lakini hakumkana yesu walihubiri injiri wala hawakuogopa hata kufa..

Lakini je, kutumia kwa mqteso hayo ndiyo mwisho ule ungekuwa umefika jibu ni "HAPANA"

Marko 13:7 Nanyi mtakapo sikia habari za vita na uvumi wa vita msitishwe hayo hayana budi kutukia lakini ule mwisho bado.

Yesu amezungumza mambo mengi sana ikiwemo vita, matetemwko njaa n.k kiasi kwamba mtu anaweza akachanganyikiwa asielewe lakini muonapo hayo ule mwisho bado huo ni mwanzo tu,

Marko 13:8 kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme kutakuwa na matetemeko ya nchi mahali mahali kutakuwa na njaa hayo ndiyo mwanzo wa utungu.

Swali, je, hivi leo kuna taifa limeondoka kupigana na taifa?, je leo hii kuna sehemu kulikumbwa na matetemeko, je leo kuna sehemu kuna njaa? jibu ni "NDIYO" lakini ule mwisho utakuwa bado ukiyaona hayo ila ni mwanzo tu kwa maana hakuna hajuae saa haijalishi itapita miaka miaka mingapi,


Lakini katika maelezo mengi ya yesu alizungumzia pia habari za hao mitume kuminambili ambao walipewa kazi nzito ya kuhubiri injiri ambao walipitia mateso na kuuwawa lakini haikumaanisha kwamba mwisho huo ungefika katika mateso yao ila huo ni mwanzo tu kwa hakika mitume walitimiza unabii hata hivi leo uwepo wa vita na matetemeko njaa bado yanaendelea kama kawaida lakini tazama yuaja upesi na hakuna ajuaye saa haijalishi itapita miaka elfu 2000 au elfu 19000



Je, ungependa kufahamu unabii wa siku za mwisho kwa undani zaidi basi enenda ukasome kitabu chote cha danieli, alafu nenda ukasome kitabu chote cha yohana yani ufunuo usipo elewa basi nenda kwenye kanisa la waadventista wasabato kwani hao ndio pekee wanao utazamia unabii huo wa siku za mwisho kwa ukaribu sana.

Au kama unaswali lolote niulize hapa nitakujibu moja kwa moja
 
Imani ya utatu mtakatifu inaweza kuwa msingi mkuu wa imani ya Ukristo lakini haina ukweli au msingi wowote kutoka kwenye Maandiko Matakatifu - imani yote imeundwa na mwanadamu kwa asili yake.

Huu ni mfano - mwingine wa kwamba ni jinsi gani imani za kipagani zilivyoingizwa kwenye ububusa wa ukristo ili kuufanya ukristo ukubalike zaidi kwa wapagani.


Wakristo walio wengi, wanapoombwa kuielezea imani hii (ya utatu), hawawezi kutoa jibu lolote isipokuwa kusema:

"Ninaamini hivyo kwa sababu niliambiwa niamini hivyo". Wanalielezea kwamba "Ni siri ya Mungu - hakuna mtu anayejua" ingawa Biblia inasema katika Wakorinto wa kwanza 14:33 kwamba:
"Mungu sio mwanzilishi wa utatanishi na migongano".

Hata aliyeipa nguvu na kuihimiza imani hii ya utatu aliona ugumu mkubwa katika kuielewa imani hii.

Inasemekana kwamba Athanasius, askofu aliyeitwa na kuitangaza rasmi imani hii ya utatu, alikiri kwamba alivyokuwa akizidi kuandika juu ya imani hii, ndivyo uwezo wake wa kuielezea imani hii ulivyokuwa ukizidi kupungua.
Hebu niulize swali mimi kuhusu mashaka yako kuhusu hizo nafsi tatu za mungu nami nitakujibu hata kwa quran yako mwenyewe


Uyasemayo kuhusu habari za ukatoriki kuingiza ibada za kipagani kwenye ukristo ni ya kweli kwa kweli ibada hii ya kikatoliki haikuwai kufanywa na yoyote kwenye biblia wala manabii wala mitume wala yesu katoriki kulingana na historia wao walikuwa ni utawala ulio kuwako kwa karne nyingi kuanzia ile miaka ya 300 mpaka mwaka 1798 na iliitwa kama dola ya rumi nayo ilikuwa inaabudu miungu yao wenyewe tofauti na yesu kristo ila baadae ilibadirisha na kujiingiza kwenye ukristo hata hivi leo. Unaweza kupitia historia ya dola hilo kubwa lililo tawala mabara matatu kwa karne nyingi kwenye vyanzo vya kihistoria vinavyo aminika au unaweza kusearch hata Google au Wikipedia ukapata kufahamu kama unataka kuijua kweli



Lakini vipi kuhusu uislam? Kwa hakika uislam ulisikika kwa mara ya kwanza kwa Muhammad katika kipindi cha dola la rumi baadhi ya hadithi za mtume wa kiislam au hata quran yenyewe zinathibotisha kuwa kipindi cha Muhammad kulikuwa tayari kuna ukristo duniani lakini badala yake Muhammad alikuja na quran ambayo kwa hakika asilimia 80 inazungumzia zile hadithi ambazo zilikuwa zipo kwenye ukristo tayari kabla yake ambazo zipo kwenye biblia

Quran hiyo pia ilikuwa inamtaja yesu mara nyingi kuliko allah yani imejaa majina ya yesu kuliko allah unaweza kupitia mwenyewe ukahesabu


Kulingana na hadithi pamoja na mafungu kadhaa ya quran yanaitaja biblia lakini wala biblia haitambui quran lakini pia kuna fungu linasema quran na uislam ulikuja ili ushindane na ukristo ambao ulikuwepo kabla yake

Mwisho ibada za manabii wa kale kabla ya kuja kwa quran na Mohammed zinatofautiana hazifanani waislam wa sasa wanafanya ibada tofauti na ya manabik wa kwenye quran ikiwemo kuhiji, kufunga, swala tano n. K kitu ambacho hakuna aliyekuwa akikifanya kabla ya Muhammad yani akuna nabii au mtume aliye fanya hivyo.



Lakini pia, kulingana na quran mungu wa waislam ameruhusu kuuwa, kusema uongo ili kuutetea uislam, kupigana n.k


Sipo hapa kwaajili ya kubishana lakini mwenye akili na ufahamu ajitafakari kwa faida yake mwenyewe kila mtu ananafasi ya kuchugua afuate njia hipi ila nashauri tuchunguze ukweli kisha kila mmoja afuate atakacho kipenda sipo hapa kubishana ndugu zangu tujitafakari tutafute ukweli pamoja kwani sisi ni binadamu sawa
 
Back
Top Bottom