Je, kukataa uteuzi wa Rais kunaweza kuchukuliwa kama uhaini?

Je, kukataa uteuzi wa Rais kunaweza kuchukuliwa kama uhaini?

..pia yuko bwana mmoja wakati wa mzee mwinyi alikuwa balozi uganda akateuliwa kuwa mkuu wa itifaki " akakataa" uteuzi huo.
Watu wa idara ya usalama kwa mfano, huwa hawastaafu, hata ukiambiwa umestaafu bado wewe ni usalama tu na unaweza kuhitajika kufanya hili ama lile.

Kama ndugu yetu kakataa uteuzi, kwangu binafsi hajatumia busara kabisa. Na jambo kama hili raisi yeyote ni lazima atalichukulia kwa uzito mkubwa.

Kwa kifupi nisipindishe maneno, huyu hata kama ana muda gani ameacha kuwa mkurugenzi, bado haifutiki kwamba amekuwa mkurugenzi. Mkurugenzi wa idara nyeti kumgomea raisi, nafikiri unaweza kupata picha maana yake nini. Hasa kwa nchi zetu ambazo idara hizo za PCCB na TISS ziko chini ya raisi.
 
Nimeona kuna baadhi ya viongozi wamekataa teuzi baada ya Rais kuwateua je hii ikoje kisheria? Kwani Rais ni mwajiri namba moja, ni utovu wa nidhamu, vilevile inakuwaje Taasisi kubwa kama Rais iteue WATUMISHI ambao ni waajiriwa wa chama cha walimu? Je, hawa waliogoma wamegoma Kwa masilahi ya Walimu? Au ukuu wa wilaya hauna ulaji? Na kule kuna ulaji? Naomba kuwasilisha.
 
Hakuna sheria yoyote inayombana mtu kwenye nafasi za kuteuliwa iwe ni lazima ukubali hiyo nafasi, ukuu wa wilaya ni nafasi ya kisiasa sio profession kama ualimu, sio kila mtu ananjaa na kubembeleza watawala Kuna wengine wanaheshimu kile walichokisomea.

Mwajiri namba moja sio Rais ni mkurugenzi maana hao ni walimu, acheni janjajanja ya kusema Rais ni Mwajiri namba moja kwenye mkataba wa ualimu Hakuna kipengere hicho, walio jaza mikataba ya ajira ya ualimu chini ya TSC inaelekezwa kuwa Mwajiri wa mwalimu ni mkurugenzi Sasa hawawezi kuwa na waajiri zaidi ya mmoja hakunaga kitu kama hicho.
 
Nimeona Kuna baadhi ya viongozi wamekataa teuzi baada Ya Rais kuwateua je hii ikoje kisheria? Kwan Rais ni mwajiri namba moja,ni utovu WA nidhamu,vilevile inakuwaje Taasisi kubwa kama Rais iteue WATUMISHI ambao ni waajiriwa WA chama Cha walimu?je Hawa waliogoma wamegoma Kwa masilahi ya Walimu?au ukuu WA wilaya hauna ulaji? Na kule Kuna ulaji? Naomba kuwasilisha
Una ushahidi kuwa wamekataa?
 
Hakuna sheria yoyote inayombana mtu kwenye nafasi za kuteuliwa iwe ni lazima ukubali hiyo nafasi, ukuu wa wilaya ni nafasi ya kisiasa sio profession kama ualimu, sio kila mtu ananjaa na kubembeleza watawala Kuna wengine wanaheshimu kile walichokisomea. Mwajiri namba moja sio Rais ni mkurugenzi maana hao ni walimu, acheni janjajanja ya kusema Rais ni Mwajiri namba moja kwenye mkataba wa ualimu Hakuna kipengere hicho, walio jaza mikataba ya ajira ya ualimu chini ya TSC inaelekezwa kuwa Mwajiri wa mwalimu ni mkurugenzi Sasa hawawezi kuwa na waajiri zaidi ya mmoja hakunaga kitu kama hicho
We jamaa ni Mwalimu kabisa
 
Nijuavyo ni kuwa hakuna Sheria ya Moja Kwa Moja inayowabana. Lakini kumgomea Rais ni jambo ambalo linatakiwa kukomeshwa na iwe mfano Kwa wengine. Uzalendo ni pamoja na kutii mamlaka za nchi bila kujali maslahi Kama alivofanya pole pole.

Hao ndugu hawatamaliza mwaka kwenye hizo nafasi zao. Hili ni kutokana na wao kuwa na makando kando kwenye taasisi hiyo. Wataonekana ni mashujaa Kwa muda lakini watasimulia mpaka wajukuu.
 
Nilivyosoma nimeelewa kwamba hawa wote ni Viongozi wa kuchaguliwa kule chama cha Walimu. Wameandika ni Mwenyekiti, Katibu na....

Binafsi naamini hawajakataa bali kuna taratibu yafaa zifanyike. Hawa huchaguliwa tena kwa gharana kubwa szna yacwawakilishi kutoka Mikoa na Wilata zote tena kila baada ya miaka 5. Kampong zao HD kushinda si mchezo, hadi kura za maruhan hutumika sometime.

Uteuzi wao wawezasababisha gharama kubwa kwa chama kufanya uchaguzi mwingine su vyovyote vile.
Naamini kwa kuwa wote wanawajibika kwa niaba ya serikali suala hili litawekwa sawa tu.

Sent from my SM-G977B using JamiiForums mobile app
 
Nilivyosoma nimeelewa kwamba hawa wote ni Viongozi wa kuchaguliwa kule chama cha Walimu. Wameandika ni Mwenyekiti, Katibu na .. . Binafsi naamini hawajakataa bali kuna taratibu yafaa zifanyike. Hawa huchaguliwa tena kwa gharana kubwa szna yacwawakilishi kutoka Mikoa na Wilata zote tena kila baada ya miaka 5. Kampong zao HD kushinda si mchezo, hadi kura za maruhan hutumika sometime.
Uteuzi wao wawezasababisha gharama kubwa kwa chama kufanya uchaguzi mwingine su vyovyote vile.
Naamini kwa kuwa wote wanawajibika kwa niaba ya serikali suala hili litawekwa sawa tu.

Sent from my SM-G977B using JamiiForums mobile app
Ni Ushindi wakati wa kampeni au fedha kutumika kwa wingi wakati wa uchaguzi ndio kunafanya hawa viongozi wamgomee Amiri Jeshi Mkuu?
 
Nijuavyo ni kuwa hakuna Sheria ya Moja Kwa Moja inayowabana. Lakini kumgomea Rais ni jambo ambalo linatakiwa kukomeshwa na iwe mfano Kwa wengine. Uzalendo ni pamoja na kutii mamlaka za nchi bila kujali maslahi Kama alivofanya pole pole.

Hao ndugu hawatamaliza mwaka kwenye hizo nafasi zao. Hili ni kutokana na wao kuwa na makando kando kwenye taasisi hiyo. Wataonekana ni mashujaa Kwa muda lakini watasimulia mpaka wajukuu.
Tatizo lipo ktk mfumo wa teuzi za kisiasa za serikali hii zilizo na chembe chembe za udikteta, ubaguzi na upendeleo.

Inakuwaje ateuliwe mtu bila kupewa nafasi ya ama kukubali au kukataa kutokana na sababu zake. Ikumbukwe hiki ni cheo cha kisiasa siyo jeshini ambako ni amri.

Ama kama kweli hao viongozi wa CWT wameamua kukataa kwa nia ya dhati ya kuwatumikia walimu hapa nawapongeza, na sasa waachane na mafungamano ya kisiasa ya ccm ambayo ndiyo yamekiharibu chama chao (CWT) na kupelekea kuwa na mitifuano iliyowafanya kuacha malengo yao ya kuwatetea walimu na badala yake kuwa sabuni ya serikali. Hivi sasa chama hivi kipo dhaifu Sana huko mashuleni tofauti na kilivyokuwa na nguvu awamu ya Rais wao Mukoba.

Ni kweli huenda wanaweza kupata misukosuko kwa muda, lakini pia itakuwa imetoa funzo kwa watawala juu ya mifumo ya teuzi zao.
 
Uhaini ni kosa la jinai, kwa tafsiri nyepesi ina maana kwamba ni kosa kubwa ambalo mtu analifanya dhidi ya nchi yake na mtu anyefanya kosa hili anajulikana kama msaliti, mfano wa watu wasaliti wanaojulikana duniani ni Yuda ambaye kidini alimsaliti Yesu, mwingine ni Benedict Anold huyu jamaa aliisaliti nchi yake ya Marekani dhidi ya Mbritishi, wengine ni Vidkun Quisling, na Marshall Pe’tain.

Kisheria ukubwa wa kosa hupimwa kwa adhabu yake, kosa likiwa kubwa mtuhumiwa hutumikia adhabu kubwa vivyo hivyo kosa likiwa dogo mtuhumiwa huadhibiwa kiasi.

Kwa mujibu wa sheria ya Tanzania, mtu akifanya yafuatayo huhesabiwa kama amefanya kosa la jinai la uhaini hivyo huadhibiwa kulingana na ukubwa wa kosa hilo.

Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais.

Aidha ifahamike kuwa kwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.

Hivyo watanzania kwa umoja wetu tunapaswa kuzijua sheria za nchi yetu ili kuweza kujiepusha kutenda makosa ya jinai dhidi ya nchi yetu.

C&p
 
Ina maana tu serikali ni feki. Ina maana yule aliyeteuliwa hakuambiwa,"kesho nitakuteua kuwa Mkuu wa Wilaya".
 
Kuna baadhi ya kada huapa kiapo cha utii kwa Rais. Je iwapo ikatokea mtu mwenye kiapo hiki amegomea uteuzi alioteliwa na Rais, je anaweza kuchukuliwa kama mhaini?
Hapana. Uteuzi siyo kutumwa jambo, mtu anayeteuliwa kufanya kazi anatakiwa aridhie ule uteuzi kama yuko tayari na ana uwezo wa kutekeleza majukumu mapya. Uteuzi siyo adhabu.

Sina Katiba na vitabu vya sheria lakini kuna mahali imeandikwa kuwa Rais anaweza kumteua mtu katika nafasi yo yote mradi afanye hivyo kwa mujibu wa sheria.

Watu wengi hata washauri wa Rais huwa wanasahau au kupuuza hayo maneno ya mwisho na mpaka sasa kuna teuzi kadhaa ambazo hazipo kwa mujibu wa sheria. Lakini hii ndiyo Tanzania yetu ya sasa inabidi tuikubali.
 
Back
Top Bottom