Je, kuna baadhi ya Familia zimebarikiwa?

Mtambachuo

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2023
Posts
1,907
Reaction score
3,560
Habari Wakuu.

Hivi inakuje kuna baadhi ya familia unakuta watoto wote wana akili, wamesoma mpaka level za juu kabisa. Au unakuta familia nyingine karibu wote wana uchumi mzuri, wana biashara kubwa na mafanikio kede kede.

Kwa upande mwingine unakuta familia nyingine watu karibuni wote hawaja fanikiwa kielimu wala kiuchumi. Wana umasikini uliotopea.

Je, hizo familia zinazo kuwa na watu wengi walio fanikiwa ni kuwa wamebarikiwa au ni genetics au nini ndugu wajumbe.

Karibuni kwa michango yenu.
 
Hiyo ni impact ya structural arrangement
 
Maagano ya mababu zao yalikuwa vizuri.
 
Hata mm nasubiri michango ya wadau
 
Kuna familia ya kina Kijazi, Mwapachu.

Hawa kina Kijazi mimi nawaitaga vijaza post zao huyu utaambiwa katibu mkuu wa wizara, huyu Mkurugenzi Tanapa huyu siyo katibu mkuu wa nini, hawa nimewavulia kofia.
 
Katika mafanikio kuna mambo mengi. Umezaliwa wapi, umekulia wapi, umekutana na nani shule, etc.
Lakini kwa hili la familia mchango mkubwa sana unatoka kwa wazazi, jinsi walivyowalea watoto wao, jinsi walivyo wasimamia katika mambo ya shule, na jinsi wanavyo waongoza kwenye mambo mbalimbali.
Familia nyingi hutelekeza watoto wakimaliza shule either darasa la 7 au fom 4. Hivyo watoto hujikuta wakijifanyia mambo bila mpango na hatimaye kuishia kutokufanikiwa.
 
Maana yake Mambo mema yote yanakufuata na kukutokea katika maisha,
Kwamba hawafanyi jitihada zozote yanakuja Tu mema na hawana trial and errors

Kwanza kufanikiwa ww upima kulingana na nini kuwa na fedha, nyumba na magari au kuwa na furaha na amani kwenye familia

Halafu pia mafanikio nini hatua moja kwenda nyingine sasa Mtu ikiwa unatoka hatua moja kwenda nyingine ni mafanikio hata ikiwa ni kidogo Sana

Pia mafanikio sio general Sana kama wengine wanavyoona Kwa nje Lazima iwe kuna Mtu mmoja anaplay hiyo part na yeye kwake ni kama anarudi nyuma sababu anavuta wengi wengine wengi wanaotegemea connection yake..

Pia inafaa ujue hakuna watu wanafanikiwa siku zote kuna wakati wanaanguka vibaya mno

=====================
Muh 9:11 Nimeona jambo lingine chini ya jua, ya kwamba sikuzote si wenye mbio wanaoshinda mbio, wala wenye nguvu hawashindi vita, wala wenye hekima hawapati chakula sikuzote, wala werevu hawawi na utajiri sikuzote, wala wenye ujuzi hawafanikiwi sikuzote, kwa sababu wakati na matukio yasiyotarajiwa huwapata wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…