Je, kuna filamu nyingine kama hii unaijua!? Kwenye vitabu je?

Je, kuna filamu nyingine kama hii unaijua!? Kwenye vitabu je?

Ambivert88

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2022
Posts
3,609
Reaction score
6,388
FB_IMG_1736173471512.jpg

Ni filamu inayosimulia kisa cha msafiri anayejaribu kumshawishi kimafia afisa mmoja wa usalama kitengo cha Transportation Security Administration(TSA) ili akubali kupitisha kifurushi flani hatari kwenye ndege siku ya mkesha wa Krismasi.

Fikiria unatazama filamu, iwe peke yako na familia au umewa’downlodia watoto, halafu katikati unaona mwanaume anasema kwa kulalama, “My husband. He took him from my house and he gave me that case.”

USHOGA KWENYE FILAMU

Inaitwa CARRY-ON, ilitoka rasmi juzi tu, Disemba 13, 2024, imeongozwa na Jaume Collet-Serra na kuandikwa na T.J. Fixman, ina muda wa takribani dakika 119, na hayo maneno niliyoandika hapo juu utayaona kuanzia muda wa 1:09:03 mpaka 1:10:25.

Katika pirikapirika hiyo, star wa filamu Ethan akicheza kama afisa usalama, (Jina halisi Taron Egerton) anakutana na Bwana Mateo Flores (ambaye ndiye aliyebebeshwa kifurushi hatari na anatakiwa akipitishe kama abiria wa kawaida kwenye mlango aliopo Ethan). Mateo aliingizwa kinguvu kwenye mpango huu na mwamba Jason Bateman (The traveler).

Eti sasa, kilichosababisha Mateo Flores aingizwe kinguvu ni baada ya ‘The traveler’ kumteka nyara mume wa Mateo anayeitwa Jesse….. ambaye pia ni mwanaume. Sasa hiyo para ya kwanza hapo juu ndio analalamika akiwa na Ethan walipokutana kwenye heka heka hiyo kuwa mumewe katekwa akiwa kwenye nyumba yake.

Mateo na Jesse baadae walikuja kuzungumza kwa njia ya simu walipounganishwa na ‘The traveler’ na kumhakikishia Mateo kuwa mumewe Jesse atakuwa salama ikiwa mpango wake utakamilika, kuanzia muda wa 1:18:07 mpaka 1:18:34.

Sasa ndio umekaa nyumbani na mtoto au watoto mnatazama filamu kama hii, halafu wanauliza inakuwaje mwanaume anamwita mwanaume mwenzake mume wake? Tuweni makini, mbinu ni nyingi siku hizi.

Je kuna filamu nyingine kama hii unaijua!? Kwenye vitabu je!?
 
Anha nimekupata Mkuu.

Kwa movies kwenye tv unaweza ukaweka "parental guidance", au ukaangalia rate yake ya umri kama chaneli husika wameweka.

Ila siku hizi kuna internet, ni ngumu sana kuwadhibiti huko.
Kumbe umenielewa mkuu agenda ya movies/vitabu km hivyo ni kueneza
 
View attachment 3194283

Ni filamu inayosimulia kisa cha msafiri anayejaribu kumshawishi kimafia afisa mmoja wa usalama kitengo cha Transportation Security Administration(TSA) ili akubali kupitisha kifurushi flani hatari kwenye ndege siku ya mkesha wa Krismasi...
Mtfanywa sana Mashoga kwa kuangalia sinema za mashoga.
 
Hii dunia imekuwa ya hovyo sijui tuwafiche wapi watoto??
Kwenye nyumba za ibada tunakokutegemea nako kushaharibika 😥
 
filamu nyingi sikuhizi zina haya mambo tena nyingi za uingereza!, wanaharibu jamii tu hawa mazwazwa wanapandikiza hichi kitu kionekane cha kawaida nafikiri kuna ajenda fulani
Waingereza wapuuzi sana. Hata game of thrones kuna ushoga sana mule. Watu huwa wanatupia lawama ushoga zaidi, ila pia kuna hawa lesbians nao ni janga sana kwa sasa. Series kama FROM, mambo haya yapo ya wanawake kushiriki mapenzi ya wao kwa wao pia.
 
Siku hizi hadi cartoon ziko na hayo mambo pia... Kwahiyo kama baba au mama unatakiwa uwe makini Kila mahali and ni vyema kupitia program zote ambazo watoto wanafuatilia kabla yao.
 
Back
Top Bottom