Je, mamlaka husika zinatoa majibu ya uongo kwa wanaopima Covid 19?

Je, mamlaka husika zinatoa majibu ya uongo kwa wanaopima Covid 19?

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Hizi tuhuma zimekuwepo kwa muda mrefu kuwa watanzanzania au raia wa nje wanapotaka kwenda nje hutakiwa kupima Covid-19 na kupatiwa cheti kuonyesha kuwa hawana maambukizi.

Lakini kumekuwa na na tetezi zinazogaa mitandaoni kuwa mamlaka husika hapa Tanzania hazitoi majibu sahihi. Na mara zote watu wakipima wanaambiwa hawana maambukizi. Ila wakienda nje ya nchi wanapopimwa wanakutwa na maambukizi.

Hivi mamlaka husika mnaficha ili iweje? Kwamba Tanzania kutokuwa na maambukizi ndio sifa?

Leo hii kuna watanzania watatu huko Angola wameonekana na maambukizi,ina maana hapo maabara kwenu hamkugundua? Au mnataka kusema maabukizi wameyapata huko Angola?

Mnadhani UK ilikosea bahati mbaya kupiga marufuku watanzania kuingia huko kwao?

Kuweni wakweli maana mmeanza kuaibika.
 
Kuna mwingine nimeona analalamika anasema kapimwa akawa negative ila the next day kaanza kuugua safarini. Ila MTAGA hapa watakuambia hao wamepata njiani[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Sijui tunajukuta nani yaani.. ila taratibu tu tutaelewana maana ushaanza kufika walikodhani hautafika.
 
Kuna mwingine nimeona analalamika anasema kapimwa akawa negative ila the next day kaanza kuugua safarini. Ila MTAGA hapa watakuambia hao wamepata njiani[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Sijui tunajukuta nani yaani.. ila taratibu tu tutaelewana maana ushaanza kufika walikodhani hautafika.
Hii kuugua safarini ndio utata mkubwa
 
Time will tell.kama ipo ipo kama haipo haipo
 
sitoshangaa kama kuna kofoji majibu ili ku clear jina la nchi. ila sasa down the road itaonyesha mamlaka zetu haziko serious.. hii itatuchafua zaid kimataida.
just praying hizi tuhuma si za ukweli?
Mnakumbuka hili suala mwaka jana lilileta sintofahamu kubwa na Kenya? Madereva walikuwa wanapimwa Tanzania wanaambiwa hawana virus wakitaka kuingia Kenya wakipimwa mpakani wanakutwa na virus. Nchi ya masongombwingo!
 
Mnakumbuka hili suala mwaka jana lilileta sintofahamu kubwa na Kenya? Madereva walikuwa wanapimwa Tanzania wanaambiwa hawana virus wakitaka kuingia Kenya wakipimwa mpakani wanakutwa na virus. Nchi ya masongombwingo!
Hii inakuwaje mpaka inatokea? Kwamba vipimo vya Tanzania ni bora zaidi ya vile vya wenzetu?
 
Uk imewapiga marufuku Rwanda, SA na nchi kibao. Je nao wanadanganya vipimo?
 
Hii inakuwaje mpaka inatokea? Kwamba vipimo vya Tanzania ni bora zaidi ya vile vya wenzetu?
Inaweza kuwa ni combination ya sababu nyingi.

1. Upimaji wetu siyo makini eg hawana ujuzi au ni wazembe (note maabara zetu haziaminiki sana).

2. Wamepewa maelekezo maalum ili tusionekane tuna maambukizo. (fikiria implication za watalii wamekuja wazima halafu wakati wa kurudi waambiwe wana virus).

3. Corruption inahusika. Samples hazipelekwi kupimwa kunakohusika ili wapate nafasi ya kupiga dola 100 zinazochajiwa kwa kila mtu. Kumbuka chances za mtu kukutwa ni positive ni ndogo hivyo it worth to risk.
 
Inaweza kuwa ni combination ya sababu nyingi.
1. Upimaji wetu siyo makini eg hawana ujuzi au ni wazembe (note maabara zetu haziaminiki sana)
2. Wamepewa maelekezo maalum ili tusionekane tuna maambukizo. (fikiria implication za watalii wamekuja wazima halafu wakati wa kurudi waambiwe wana virus)
3. Corruption inahusika. Samples hazipelekwi kupimwa kunakohusika ili wapate nafasi ya kupiga dola 100 zinazochajiwa kwa kila mtu. Kumbuka chances za mtu kukutwa ni positive ni ndogo hivyo it worth to risk.
1&2 upo sahihi kabisa.
Hiyo ya tatu ni ngumu kufanyika maana siku hizi malipo yanafanyika kwa electronic na yanatumbukia hazina.
 
Back
Top Bottom