Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Kwa mujibu wa imani ya kiislamu mtoto ambaye amezaliwa nje ya ndoa hatambuliki Kwa mujibu wa Sheria kama mtoto wa Baba husika.

Kwasababu kizazi au uzao WA familia unatakiwa upatikane ndani ya ndoa ya kisheria au ndoa iliyofungwa Kwa misingi ya Dini,na nje ya hapo huyo ni mtoto wa zinaa ambaye kisheria anatambulika kama mtoto wa mama aliye mzaa Tu.

Ingawa kikawaida atafahamika kama mtoto wa Baba Fulani lkn kidini huyo Baba hatambuliki na hivyo kuna haki Fulani ambazo Baba hawezi kumfanyia mtoto wake.

Moja wapo ni huyo mtoto hafai kuitwa Jina la ubini WA Baba yake,Hilo Jambo ni haramu Sana na Mungu ameshalikemea tayari, ingawa Kwa bahati mbaya Sana Kwa kutojua wengi wamewapa majina ya ubini wao hao watoto wa nje ya ndoa.

Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.

Lingine huyo mtoto hawezi kumrithi Baba yake kwasababu kisheria huyo mtoto sio WA huyo Baba,Bali Baba anaweza kumpa sehemu ya Mali huyo mtoto,lkn mara Tu huyo Baba anapokufa basi huyo mtoto Hana haki ya Kurithi chochote.

Lakini sio vibaya huyo Baba kumhudumia huyo kijana Kwa malezi na mahitaji mbali mbali maadam Tu yeye ndiye sababu ya kuja Hicho kiumbe hapa duniani.

Na mtoto ambaye Hana Baba kisheria anaweza kuitwa Kwa jina la mama yake, Kwa mfano ETUGRUL BEY ASHA au Kwa jina la ubini Kwa upande wa mama yake.

Kubwa ni kutambua uzao mzuri ambao hata kizazi chako kinaweza pata haki stahiki ni kizazi ambacho kinatokana na ndoa takatifu ambayo IPO Kwa mujibu wa Sheria.

Na hata wale ambao wanafunga ndoa za kiserikali basi watambue kidini Hicho kizazi Chao hakitambuliki na Sheria za Dini Kwa maana Baba Hana watoto hapo Ila watoto ni WA mama.

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
Nurain
adriz
professional Driver
baby zu
Kwa mujibu wa sheria zipi

Toa reference

Nnje hapo kitanda hakizai haramu , na mtoto akishazaliwa ni Mungu kamleta kwa njia zake
 
Kwanza nikuwepe Sawa hakuna mtoto wa haramu Sawa?

Uharamu ni zinaa iliyofanywa na hao wazazi, Yule atabakia kuwa mtoto Safi Bila shida yoyote Ile.

Hapa naweza mzungumzia Yesu hakuwa na Baba ndio maana akaitwa Kwa ubini WA mama yake.

Chief hapa hatubishani na Mimi sio mpenzi WA mabishano, kwahiyo upo huru kuamini unachoamini
Yesu hajawahi kuitwa kwa ubin wa mama yake. Yesu (ambaye habari zake zipo kwenye Biblia) aliitwa ubin zifuatazo.

1. Ubin wa Mungu - Yesu mwana wa Mungu , Son of God
2. Ubin wa Adam - Mwana wa Adam, Son of man
3. Ubin wa Babu yake, Daudi - Yesu mwana wa Daudi, Son of David


Aliyeitwa ubin wa mama ni Isa wenu, Usichanganye mambo.
 
Yesu hajawahi kuitwa kwa ubin wa mama yake. Yesu (ambaye habari zake zipo kwenye Biblia) aliitwa ubin zifuatazo.

1. Ubin wa Mungu - Yesu mwana wa Mungu , Son of God
2. Ubin wa Adam - Mwana wa Adam, Son of man
3. Ubin wa Babu yake, Daudi - Yesu mwana wa Daudi, Son of David


Aliyeitwa ubin wa mama ni Isa wenu, Usichanganye mambo.
Utake usitake au ukubali au usikubali ndio huyo huyo kwenu mnajua kama Yesu
 
Ngoja nikuelimishe kidogo kila unachokiona duniani kiko chini ya under control hata ww uko chini ya under control.

Mwenyezi mungu kaumba binadamu na kamuwekea na taratibu maalumu ni namna gani aendeshe maisha yake na sio ilimradi tu anaishi.

Mfano leo ww utatafuta pesa kwa nguvu zako utanunua gari lakini hiyo gari huwezi kuiendesha barabarani mpaka upitie utaratibu fulani licha ya kwamba hakuna aliye kusaidia kununua hilo gari.

Au ukitaka kufungua biashara utatakiwa ufuate utaratibu maalumu licha ya sio kufungua kiholela holela.

Hivyo hivyo kwa mungu alikuumba akasema nendeni mkaijaze dunia lakini kaweka utaratibu wa kuzaliana na sio kuzaliana kiholela holela.

Dawa ya kuhepusha haya sio kuukimbia ukweli bali ni sisi kuacha uzinzi wa kiholela, hakika ni ukatiri na ubinafisi mkubwa kwa mwanaume kumpa binti wa watu mimba hali ya kuwa huna mipango ya kumuoa.
Haya tumeshafanya hivyo Sasa na tunaendelea kufanya. mwambie huyo kikaragosi wako aje atuadhibu.
 
Kwa mujibu wa imani ya kiislamu mtoto ambaye amezaliwa nje ya ndoa hatambuliki Kwa mujibu wa Sheria kama mtoto wa Baba husika.

Kwasababu kizazi au uzao WA familia unatakiwa upatikane ndani ya ndoa ya kisheria au ndoa iliyofungwa Kwa misingi ya Dini,na nje ya hapo huyo ni mtoto wa zinaa ambaye kisheria anatambulika kama mtoto wa mama aliye mzaa Tu.

Ingawa kikawaida atafahamika kama mtoto wa Baba Fulani lkn kidini huyo Baba hatambuliki na hivyo kuna haki Fulani ambazo Baba hawezi kumfanyia mtoto wake.

Moja wapo ni huyo mtoto hafai kuitwa Jina la ubini WA Baba yake,Hilo Jambo ni haramu Sana na Mungu ameshalikemea tayari, ingawa Kwa bahati mbaya Sana Kwa kutojua wengi wamewapa majina ya ubini wao hao watoto wa nje ya ndoa.

Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.

Lingine huyo mtoto hawezi kumrithi Baba yake kwasababu kisheria huyo mtoto sio WA huyo Baba,Bali Baba anaweza kumpa sehemu ya Mali huyo mtoto,lkn mara Tu huyo Baba anapokufa basi huyo mtoto Hana haki ya Kurithi chochote.

Lakini sio vibaya huyo Baba kumhudumia huyo kijana Kwa malezi na mahitaji mbali mbali maadam Tu yeye ndiye sababu ya kuja Hicho kiumbe hapa duniani.

Na mtoto ambaye Hana Baba kisheria anaweza kuitwa Kwa jina la mama yake, Kwa mfano ETUGRUL BEY ASHA au Kwa jina la ubini Kwa upande wa mama yake.

Kubwa ni kutambua uzao mzuri ambao hata kizazi chako kinaweza pata haki stahiki ni kizazi ambacho kinatokana na ndoa takatifu ambayo IPO Kwa mujibu wa Sheria.

Na hata wale ambao wanafunga ndoa za kiserikali basi watambue kidini Hicho kizazi Chao hakitambuliki na Sheria za Dini Kwa maana Baba Hana watoto hapo Ila watoto ni WA mama.

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
Nurain
adriz
professional Driver
baby zu
Sheikh Kuna Aya ya Qur'an inayosadikisha haya!?
 
Katika Qur'an watoto wa nje ya ndoa wameharamishwa kuitwa majina ya Baba zao

Kwa asili kitu chochote ni halali mpaka kiharamishwe,kwahiyo maadam enzi za Manabii na Mitume hakukuwa na hizo sheria basi ilikuwa ni halali.
Hakuna Aya ya Qur'an inayosema mtoto wa nje ya ndoa si mtoto wa baba
 
Ukiona hatujibu kitu ujue ni cha kipuuzi
Uzi umetembea kwelikweli, watu wamepovukwa kwelikweli, hadi nimeshindwa nichangie nini, ila nimekumbuka maneno ya Imam Aliy Ibn Abii Twaalib aliposema:-

"حدثوا الناس بما يعرفون، أتريدون أن يُكذَّب اللهُ ورسولهُ؟"
Kwamba: Wasemezeni watu kwa wanayoyafahamu, je mnataka akadhibishwe Allah na Mtume wake.

Watu wengi hii mada imewazidi kimo, that's why wameshindwa hata waseme nini, badala yake waneishia kuongea maneno yasiyofaa.

Lakini ukweli ni kwamba hii mada imelenga jambo ambalo linaigusa jamii moja kwa moja, zinaa ni uchafu ulioenea kiasi kwamba wengine wamefikia kuihalalisha au kuona kuwa ni dhambi ambayo haiwezi kuepukika.
Hivyo ukizungumzia uharamu/ubaya wa zinaa na madhara yake unaonekana kama unaongea vitu ambavyo haviingii akilini.

Allah atuhifadhi.
Allah akulipe kheri kaka ETUGRUL BEY
 
Uzi umetembea kwelikweli, watu wamepovukwa kwelikweli, hadi nimeshindwa nichangie nini, ila nimekumbuka maneno ya Imam Aliy Ibn Abii Twaalib aliposema:-

"حدثوا الناس بما يعرفون، أتريدون أن يُكذَّب اللهُ ورسولهُ؟"
Kwamba: Wasemezeni watu kwa wanayoyafahamu, je mnataka akadhibishwe Allah na Mtume wake.

Watu wengi hii mada imewazidi kimo, that's why wameshindwa hata waseme nini, badala yake waneishia kuongea maneno yasiyofaa.

Lakini ukweli ni kwamba hii mada imelenga jambo ambalo linaigusa jamii moja kwa moja, zinaa ni uchafu ulioenea kiasi kwamba wengine wamefikia kuihalalisha au kuona kuwa ni dhambi ambayo haiwezi kuepukika.
Hivyo ukizungumzia uharamu/ubaya wa zinaa na madhara yake unaonekana kama unaongea vitu ambavyo haviingii akilini.

Allah atuhifadhi.
Allah akulipe kheri kaka ETUGRUL BEY
Shukrani Sana Msonjo

Igawa ulisema hauna cha kuchangia lakini wallah ulicho changia ni kikubwa mno maana kimebeba au kimeelezea Hali halisi ambayo imeikumba jamii yetu kwasasa.

Zinaa inaonekana ni jambo la kawaida na ni halali kabisa miongoni mwa jamii zetu,ndio maana unakuta watu wanaishi kinyumba na kuzaa watoto kadhaa Bila hofu yoyote wakati wazazi ndugu na jamaa wanaangalia Tu.

Shukrani Sana kaka
 
IPO Zonda nitaileta inshallah
Sheikh haipo,hayo mambo tumebambikiwa na wayahudi ili kututoa kwenye Qur'an maana kuibadili hawawezi,kumbukumbu la torati 23:2 na mistari mingine zaidi ya 13 kwenye bible ndiyo inazungumzia mtoto wa nje ya ndoa,mwanaharamu(bastard)
 
Shukrani Sana Msonjo

Igawa ulisema hauna cha kuchangia lakini wallah ulicho changia ni kikubwa mno maana kimebeba au kimeelezea Hali halisi ambayo imeikumba jamii yetu kwasasa.

Zinaa inaonekana ni jambo la kawaida na ni halali kabisa miongoni mwa jamii zetu,ndio maana unakuta watu wanaishi kinyumba na kuzaa watoto kadhaa Bila hofu yoyote wakati wazazi ndugu na jamaa wanaangalia Tu.

Shukrani Sana kaka
Na huu ndio mtihani, leo zinaa imekuwa inachukuliwa kama jambo la kawaida sana, na unajua kuenea kwa zinaa ni katika mambo makubwa ambayo yanapoteza thamani za ndoa leo hii, yaani watu hawaoni faida ya kuoa au kuolewa.

Mwanaume anakwambia anataka mwanamke amzalie watoto tu basi, na mwanamke nae anataka mwanaume wa kumzalisha tu, halafu atalea mwenyewe( kumbuka mchakato wa kuyakamilisha haya ndio zinaa yenyewe)
 
Back
Top Bottom