Je, mtu huyu nimfungulie kesi ya aina gani?

Je, mtu huyu nimfungulie kesi ya aina gani?

Habari za shughuli ndugu zangu,

Naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa mwanzoni mwa mwaka huu
Atasimamiaje mtu mwingine mirathi ya mke wako? Usingekubali upuuzi huo.

Amandla...
 
Mikataba walioandikiana itakuwa ina maelezo tofauti, Mpangaji mwenye akili huwezi kumpa notes kirahisi hivyo.
Ni kweli kabisa mkuu,hata haitakuwa hekima kumfuata mpangaji ambaye hata hakujui na kumpa notisi,atakuona kichaa.
 
Ndoa ya kanisani,na vyeti vyote viwili ninavyo,sasa nimejua kuwa kumbe ni hitaji la kisheria ukoo au familia kukaa kikao baada ya mazishi na kumpendekeza msimamizi wa mirathi,na anaweza kuwa yeyote mwenye uchungu na Mali za marehemu,tatizo lililojitokeza hapa ni tamaa,asante mkuu
pole pambana upate haki za watoto,wajomba watafute za kwao
 
Pole sana Mkuu na msiba.na maswahibu unayopitia kwa sasa.

Sijaweza kusoma comment zote ila kama kutakuwa na comment ambayo imesema nitakayokueleza basi naungana nayo.

Haya twende kazi...
Mahakamani atakuwa hajenda huyo maana lazima mashihidi wangeitwa mahakani wawepo ambao ndio wahusika wa karibu watoto na mume wa marehemu kuridhia kwamba musika apewe usimamiza wa mirathi.

Kama ameenda basi kwa kufoji kuleta mashahidi wa kuchonga ambalo ni kosa lingine la kumfunga hilo.
 
Hiyo shemeji yako NAYE MJINGA alikubaligi KUSIMAMIA mirathi ya dada yake wakati we upo...... mirathi ulitakiwa usimamie wewe kama mume wa marehemu pole sana KUMBE ATA WANAUME tunatapelewa Mali za wenza wetu

TAFUTA wakili ukafungue SHAURI la kubadilisha msimamizi wa mirathi ya MKE WAKO na uzuri vielelezo unavyo kama Cheti Cha ndoa
 
Huyu jamaa anatia aibu Sana,

Inaonekana familia ya mke imeona kabisa jamaa hafai kusimamia Mali zilizoachwa na marehemu mkewe au vipi...
Mkuu nakazia kauli yako hii ya jamaa kali mke anakufa kinakaa kikao cha mirathi? Ninavyojua mimi mume akifa ndio vinakaa vikao vya namna hiyo
 
Wewe mtu katoka kufiwa tena mkewe mpendwa angepata wapi hizo nguvu? Msipende kulaumu tu..pole sana@capt tamar..nenda kwa wanasheria watakusaidia
Kwa hiyo mimi mke wangu akifa atatokea mtu wa kuongoza mali nilizochuma mimi na mke wangu? Acha kumuonea huruma kama anayosema ni yakweli basi ni mpumbavu kabisa na kama aitaki hiyo sifa inampasa ajirekebishe achukue mamlaka yake ya Uanamume
 
Kufiwa na mke si jambo rahisi kaka,hata mimi huwa najiuliza nilikubalije?I wish ungekuwepo siku hiyo,maybe ungekuwa msaada kwangu,nahitaji kutoka hapa sasa,msaada tafadhali.
Tengua msimamizi, sababu ni hukuwa na ridhaa kwsbb moja ya vigezo vya ridhaa halali ni pamoja na kuwa akili timamu/sawa.

Wakati haya yanatendeka akili yako haikuwa sawa kutokana na tukio la kufiwa. Then with time umekuwa sawa kiakili ukagundua hilo jambo halikuwa halali.

NB: wanasheria watakuongoza vyema ktk hilo.
 
Habari za shughuli ndugu zangu,

Naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa mwanzoni mwa mwaka huu...
Kosa kubwa ulilifanya! kwanini asimamie mirathi wakati wewe upo? nenda kaweke pingamizi la huyu shemeji kufungua mirathi....then mengine yatafuata. Nenda ka wakili mzuri,
 
Asante,ila hujagusia kuhusu uwezekano wa yeye kupata hati nyingine ya kifo tofauti na hii niliyonayo,au kama anaweza kuthibitishwa na mahakama pasipo kupeleka hati hiyo,na pia nimeambiwa kuwa kwa ndoa za kiislamu na kimila mirathi inafunguliwa mahakama ya mwanzo,na kwa ndoa ya kikristo na ambapo thamani ya mirathi haizidi tsh 100,000,000 basi ni mahakama ya wilaya,au mahakama kuu ikiwa thamani ya Mali itazidi kiwango hicho,niweke sawa kwa hili pia mkuu,nashukuru mno brother.

Sawa Mkuu,

Kwenye swala la hizo nyaraka uwezekano haupo labda kama atatengeneza feki au kwa mazingira yasiyo rasmi ambayo yataangukia kwenye jinai tu, ila hapa barudia lazima uwe na uhakika 100% kwamba alifungua mirathi, sasa bahati mbaya hakuna sehemu unasema kama una huo uhakika.

Swala la Mahakama ipi nalo lipo hivi,

Kwa ndoa za kikristu ambazo ndio zinatumia sheria ya india ya mirathi pamoja na sheria yetu hapo moja kwa moja nenda Mahakama Kuu sababu ndio Mahakama yenye mamlaka.

Mahakama ya wilaya haiwezi sikiliza wala kuteua msimamizi wa mirathi, huwa kuna mtu anaitwa district deligate kama sijakosea na huyu sio Mahakama bali ni Hakimu anaweza kuwa Mahakama ya wilaya / Hakimu Mkazi. Hapa huwa watu wanamchanganya na Mahakama ama ya Wilaya/ Hakimu Mkazi.

Mahakama ni mbili tu ya Mwanzo au Kuu kwenye maswala ya mirathi Mkuu. Sasa kwa wakristu ndio wanaenda Mahakama Kuu. Kuna ambao wanaenda Mahakama ya Mwanzo pia ila huwa haipo clear mitazamo inakinzana sana hapo ila uhakikazaidi ni Mahakama Kuu.
 
Sawa Mkuu,

Kwenye swala la hizo nyaraka uwezekano haupo labda kama atatengeneza feki au kwa mazingira yasiyo rasmi ambayo yataangukia kwenye jinai tu...
Kuhusu yeye kufungua maombi ya usimamizi wa mirathi sina hakika nalo kwa asilimia 100,na ndiyo nikasema nina mashaka kuwa hakwenda mahakamani, kwa kuwa huko angetakiwa kwenda na vielelezo ambavyo hana, alichonacho ni barua ya muhtasari wa kikao cha familia tu na je naweza kwenda mahakamani kuuliza kama alikwenda kufungua shauri hilo?
 
Kutokutaka shari pamoja na kuepusha migogoro ya kifamilia, vifo n.k mali za mwanamke uza mgawane; we ubaki na mali zako tu na upambane na watoto wako.
 
Watoto ninaishi nao mimi,na kuhusu ufujaji na hayo mengine sina kabisa mkuu,ndiyo maana nimeweza kuwekeza vitega uchumi na kuilea familia yangu vyema kabisa mkuu,ushauri nimeuzingatia na nitaufanyia kazi haraka, asante
If is that so mkuu punguza upole wanakuchukulia poa kwa sababu ya pole wako hao sisi tuna gues ila issue kamili unaijua wewe.

Imezoeleka wababa wadogo kujiingiza kwenye usimamizi wa mirathi pindi kaka zao wanapo fariki hili la mjomba na huku mume yupo tena wa ndoa na watoto punguza upole wanakuchukulia poa sana.
 
If is that so mkuu punguza upole wanakuchukulia poa kwa sababu ya pole wako hao sisi tuna gues ila issue kamili unaijua wewe. Imezoeleka wababa wadogo kujiingiza kwenye usimamizi wa mirathi pindi kaka zao wanapo fariki hili la mjomba na huku mume yupo tena wa ndoa na watoto punguza upole wanakuchukulia poa sana.
Kweli mkuu.
 
Nimepata naye watoto wawili,mmoja ana miaka 9 na mwingine 5,nimeishi na mke wangu kwa miaka 9,ni hivyo mkuu
Kama usemayo ni kweli tafuta mwanasheria atakusaidia ila kama ni mimi hatua ya kwanza nafukuza wapangaji wote naweka wengine hizo ni mali zangu ni wao ndio wataenda mahakamani kama nimewadhulumu

Ila ujajibu swali langu hizo nyumba zina jina lako,lake au majina yenu wote wawili na kama lina jina lake kwa sababu gani?
 
Nilijaribu kuyamaliza polepole,ila sasa nalazimika kutumia nguvu,ushauri please.
Tafuta mwanasheria akusaidie hii mambo siyo ngumu.

Naona huyo shemeji yako ni limbukeni hajui hata maana ya usimamizi wa mirathi.

Upo mkoa gani,nikupe mwanasheria?
 
Kama usemayo ni kweli tafuta mwanasheria atakusaidia ila kama ni mimi hatua ya kwanza nafukuza wapangaji wote naweka wengine hizo ni mali zangu ni wao ndio wataenda mahakamani kama nimewadhulumu

Ila ujajibu swali langu hizo nyumba zina jina lako,lake au majina yenu wote wawili na kama lina jina lake kwa sababu gani?
Jina ni la mke wangu, inakuwa ngumu kuwafukuza wapangaji kwa kuwa hata hawanijui,nilishaenda kwa mwenyekiti wa mtaa huo akanitaka nimwagize huyo shemeji yangu awaondoe au anitambulishe kwao,kitu ambacho huyo mvamizi hakuwa tayari,nadhani mahakama ndiyo itatoa suluhisho once and for all,asante
 
kama alithibitishwa na mahakama baada ya kikao cha familia nenda ukaweke pingamizi ya yeye kuwa msimamizi wa mirathi
 
Back
Top Bottom