FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 38,920
- 44,970
- Thread starter
-
- #101
Tung’ang’anie kwa faida ipi wakati wewe umeshindwa kutaja hata faida moja ambayo Tanganyika inapata, ila mserereko wote wanaupata wala urojo? Hapa suala ni kujadili ili hoja ikionekana kupitia huu mjadala basi wenye maamuzi bungeni na serikali kuu wachukue hatua. Ni bora tuungane tuwe serikali moja au unyonyaji na utegemezi wa wala urojo ukome!Bora Kurudi kwetu mbona tunaomba kila siku lkn Tanganyika vinganganizi
Uchaguzi wa mwakani uwe kama Kura ya maoni wasiotaka muungano wachague upinzani wanaotaka muungano wachague CCM
Aliyeipokonya Tanganyika identity yake ni nani ??Tanganyika imepokonywa ‘identity’ yake wakati Zanzibar imeachiwa utambulisho wake, kwa sasa Tanganyika imefunikwa na shuka la Tanzania, ila kwa kuwa Zanzibar ni nchi, kinachobaki chini ya mwavuli wa Tanzania ni Tanganyika pekee. Hivyokinachoitwa Tanzania bara ni Tanganyika.
Muungano tulionao ni wa kipekee kabisa duniani. Na unafahamika zaidi kama Muungano wa changu changu, chako changu.
Yaani Zanzibar ina haki ya kufaidi raslimali za Tanganyika, ila Tanganyika hairuhusiwi kufaidi chochote kutoka Zanzibar kwenye huo Muungano. Maajabu ya karne haya!!
Hao Wazanzibari wenyewe sasa walio wengi!! Kila siku ni kulia kulia, kudeka, kulalamika, na kunung'unika tu! Hata wapewe nini, huwa hawatosheki! Wanajifanya hawautaki huo Muungano unao wafaidisha zaidi wao! Ukiwaambia wajitoe; hawataki!!
Mpaka hapo kwa mawazo yangu nadhani muungano ubaki tu kwa raia, kila nchi ijimiliki yenyewe, ila sisi raia tuwe free na undugu wetu,
Zanzibar iwe na uhuru wake nasi Tanganyika tuwe na uhuru wetu
Mali ya zanzibar iwe yao hata kama ni kijiko
Vivyo hivyo nasi pia
Kwanini Mzanzibar Shaka Hamdu Shaka ni Mkuu wa Wilaya bara, na Zanzibar hakuna Mtanganyika anayeongoza?
Mnakubali vipi Mzanzibari kuongoza Bara, Tuanze na Shaka hamdu Shaka mkuu wa wilaya ni Mzanzibari mbona Zanzibar hakuna mtanganyika anayeongoza?www.jamiiforums.com
Kwanini Mtangayika haruhusiwi kumiliki ardhi Zanzibar wakati Mzanzibari anamiliki ardhi Tanganyika?
Wakuu waliotunga Sheria ya Mtanganyika kutoruhusiwa kumliki ardhi Zanzibar wakati wazanzibar wanarusiwa kumliki ardhi Bara waliwaza nini? Kuna jamaa amekaa Zanzibar miaka miwili na kapata kiasi kadhaa akataka anunue eneo ajenge kibanda chake nje ya mji, amechoka maneno ya wenye nyumba. Cha...www.jamiiforums.com
Hapa dawa ni kuwa na muungano wa kweli chini ya Rais mmoja
Katiba / mkataba wa MuunganoAliyeipokonya Tanganyika identity yake ni nani ??
Hahaha, kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, Raia wa Tanganyika hawezi kuwa Rais Zanzibar, labda kwa kubumbaKwanini Mwinyi Mtanganyika kutoka Mkuranga ni Raisi Zanzibar na aliwahi kuwa Mbunge wa Mkuranga kabla na kwa sheria za uchaguzi hawezi kugombea Zanzibar msikilize huyu Ali Karume
View: https://youtu.be/C8SWv9uxpoo
Sawa, ni either hivyo, au tuungane tuwe nchi moja chini ya Serikali na Rais mmoja.Muungano hauna haja ya kuwepo kila mtu aende mambo yake , kwani huwezi kuunganisha nchi ya watu karibu milioni 60 ukaungana na watu milioni 2 hawafiki ,
Sawa, ni either hivyo, au tuungane tuwe nchi moja chini ya Serikali na Rais mmoja.
Ilijiandika yenyeweKatiba / mkataba wa Muungano
Utakuwaje na Makao ya Rais wa Muungano sehemu ambapo tayari kuna makao ya Rais mwingine?, utawekaje makao ya wizara ya Muungano sehemu ambapo tayari kuna makao ya wizara nyingine? Utawekaje makao bunge la Muungano sehemu ambapo kuna makao ya bunge lingine?Tuwe nchi moja sawa kwa kugeuza Zanzibar kuwa Tanganyika yaani hivi ilivyo Sasa kwa Tanganyika kuvaa jojo la Muungano , Sasa iwe zamu ya Zanzibar kulivaa joho, kwa kuweka makao ya serikali yawe Zanzibar na wizara zote Za muungano ziwe na makao Makuu Zanzibar yaani wizara Za Zanzibar ziwe Za Muungano, bunge la Zanzibar ndio liwe bunge la Muungano na makao yake yaweko Zanzibar. Raisi wa Zanzibar ndio awe Raisi wa Muungano. Tanganyika ipoteze kila kitu Kama ilivyopoteza Zanzibar hivi sasa
Iliandikwa wakati huo, na ndio maana sisi wa wakati huu tunaomba ifanyiwe mabadiliko.., katiba sio biblia..Ilijiandika yenyewe
Huyo ndiye aliyeandika ?Iliandikwa wakati huo, na ndio maana sisi wa wakati huu tunaomba ifanyiwe mabadiliko.., katiba sio biblia..
Utakuwaje na Makao ya Rais wa Muungano sehemu ambapo tayari kuna makao ya Rais mwingine?, utawekaje makao ya wizara ya Muungano sehemu ambapo tayari kuna makao ya wizara nyingine? Utawekaje makao bunge la Muungano sehemu ambapo kuna makao ya bunge lingine?
Utakuwaje na maRais wa Muungano Wawili tena wote wametoka Zanzibar?
Ukifanya hivyo italazimu sasa Tanganyika nayo iwe na serikali yake isiyo ya Muungano, means serikali 3, ambayo itakuwa ni ukichaa..
Suluhisho, Tuwe na nchi moja chini ya Rais mmoja au kila mtu awe kivyake pasiwe na unyonyaji na utegemezi..
‘huyo’ unamaanisha nani sasa? Bila kujali aliandika nani, sisi tunahitaji katiba ibadilishwe juu ya hiki kinachoitwa Muungano..Huyo ndiye aliyeandika ?