Je, nani anapokea mahari kwa binti aliyelelewa na mama pekee?

Je, nani anapokea mahari kwa binti aliyelelewa na mama pekee?

Kuna umri unakulimit kujuwa baadhi ya vitu, subiri ukikuwa wala hutohitaji kuambiwa na mtu utaijuwa dunia Kwa mapana yake.

Omba Mungu akupe miaka mingi ya kuishi.
Kwa majibu haya nitakuwa sahihi kusema ya Kwamba mahari imegeuzwa ibada, kundi kubwa linaabudu mahari na halijui ni kwa sababu zipi.

Kiujumla hakuna hasara yoyote itakayopatikana kwenye ndoa endapo mahari isipotolewa

Pia hakuna faida yoyote itakayopatikana kwenye ndoa endapo mahari itatolewa.
 
Kuna vitu vingine havihitaji degree kutoa maamuzi .
Binti tangu azaliwe mpaka anakuwa mkubwa hajalelewa na baba wala ndugu wa upande wa baba hawamfahamu! Moja kwa moja mahari inaenda kwa mama au wajomba.
Halafu mbona mnawadharau sana wanawake? Mama amemlea binti yake kwa Hali na mali bila uwepo wa baba mzazi halafu suala la mahari unataka upeleke kwa upande usiowajibika kwa lolote!!!
Labda tu nikueleze kitu ambacho huwezi kuamini kama kipo.

Kuna jamii hapa Tanzania mpaka leo hazijui kunya kwenye choo, nilipata tabu sana nilipokwenda trip kwenye jamii hizo tena siyo porini ni vijiji viko ziwani na watu wapo smati kabisa.

Sasa jamii za aina hiyo usitegemee wawe waelewa kwenye mambo ya Ki jamii, hawaelewi lolote ni primitive society.
 
Kwa majibu haya nitakuwa sahihi kusema ya Kwamba mahari imegeuzwa ibada, kundi kubwa linaabudu mahari na halijui ni kwa sababu zipi.

Kiujumla hakuna hasara yoyote itakayopatikana kwenye ndoa endapo mahari isipotolewa

Pia hakuna faida yoyote itakayopatikana kwenye ndoa endapo mahari itatolewa.
Vijana wengi waliozaliwa miaka ya 2000 wamezaliwa na roho lakini hawana nafsi, tunawaangalia tu ulimwengu ndio Mwalimu bingwa kabisa hapa duniani, utawafunza Kwa njia ngumu sana.

Asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu, weka hili akilini.
 
Huyu binti kalelewa na mama yake pekee yake. Baba yake yupo hajafa ila binti hajawahi kukutana ana kwa ana na baba yake wala katika upande wa baba yake hamjui ndugu yeyote.



Je, kwa scenario kama hiyo binti anafaa kutolewa mahari na kuolewa?



Na taratibu za mahari zipoje? Kwani navyojua mahari ni ya baba na kama baba hayupo mahari ipokelewe na yeyote upande wa baba yaani shangazi au baba mdogo au m
Wajomba
 
Vijana wengi waliozaliwa miaka ya 2000 wamezaliwa na roho lakini hawana nafsi, tunawaangalia tu ulimwengu ndio Mwalimu bingwa kabisa hapa duniani, utawafunza Kwa njia ngumu sana.

Asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu, weka hili akilini.
Umekosa hoja za kutetea mahari umekuja na vitisho hewa.

Jambo sahihi hujitetea lenyewe, faida zake hulitetea jambo husika.

Mahari ni biashara ambayo sasa inaonekana wazi, sababu zote zinazotolewa hazina mashiko na hazina faida kwa wanandoa.
 
Kikurya baba hata kama hamuelewan kias gan lazima aje akae hapo kama pambo apokee kisha awape aondoke kama baba kafa baba wadogo
Wakirya mama au wajomba hawawez kupokea mahali ni aibu kubwa sana
 
Kama binti amelelewa na upande wa mama yake pekee, kuna wajomba wataenda kuipokea hiyo mahari kisha watakuja kukabidhi kwa dada yao. Kumbuka mahari ni zawadi ya wazazi (balashishi), inaweza kutolewa ama isitolewe. Mbona wengine walilelewa na wajomba zao na majina ya ubini wakatumia ya wajomba na sio ya baba!
 
Tatizo siyo kupokea mahari bali ni kwanini binti hajui ndugu yake yeyote upande wa baba? Unadhani huyo binti anaweza kuwa mke mwema?
Wewe unafikiri ni kosa la nani? Umempenda binti au umeupenda ukoo wake upande wa baba?

Binti anaweza kuwa na majibu mazuri kwa nini hamjui ndugu yeyote upande wa baba hivyo aulizwe yeye humu hutapata majibu. Na ni vizuri kujua historia nyuma ya pazia kutoka kwa familia ya binti itakusaidia kufanya maamuzi..

Lakini kuwa mke mwema si wakati wote kunategemea mtu amelelewa na nani. Na malezi ya single mother hayamtengenezi mke wa hovyo, wapo mabinti ni wake bora japokuwa wamelelewa bila wazazi wote. Jambo la msingi ni kujua sababu za msingi kwa nini baba asihusishwe na unapaswa kuheshimu hilo kama unampenda huyo binti. Wapo wanaume wamekataa watoto wao wa nje wala wasihusishwe nao kwa sababu ya status zao kwenye jamii au kulinda ndoa na kitendo cha wewe kuliibua hili unaweza kuletea mtafaruku mkubwa uliokwepwa zamani.

Mambo haya hayahitaji kutumia nguvu wala maamuzi kurupushi. Ni hekima kidogo tu na kuwa muelewa wa mambo.
 
Huyu binti kalelewa na mama yake pekee yake. Baba yake yupo hajafa ila binti hajawahi kukutana ana kwa ana na baba yake wala katika upande wa baba yake hamjui ndugu yeyote.

Je, kwa scenario kama hiyo binti anafaa kutolewa mahari na kuolewa?

Na taratibu za mahari zipoje? Kwani navyojua mahari ni ya baba na kama baba hayupo mahari ipokelewe na yeyote upande wa baba yaani shangazi au baba mdogo au mkubwa.
Katika uislaam mahari ni ya bint mwenyewe...na anaweza pokea mwenyewe mbele ya mashahidi...ila atakayemuozesha ni IMAM WA MSIKITI KAMA HANA NDUGU UPANDE WA BABA MWANAUME.
 
Komeni kuwaandama single mothers, ni ukosefu wa nidhamu na ni kinyume na utu.

Unasema mahari ipokelewe na baba ambaye hata hamjui binti. Hapo kuna baba kweli.

Unasema binti hafahamiani hata na ndugu mmoja upande wa baba, hapo undugu uko wapi?

Halafu taratibu za mahari za kwenu ni tofauti na watu wengine. Upande wa bi harusi ndio unaoandaa taratibu zote za mahari na namna gani mahari ipokelewe, sio wewe unayepanga.
Naongezea atafute hela,huwezi ukawa na hela alafu ukataka kufatilia mpaka hela ilikoenda,kama mtoto amelelewa ujombani unachouliza hapa ni nini?
 
Hiyo ilikuwa zamani ambapo mtoto analelewa na Extended Familia.

Siku hizi Watoto wengi wanalelewa na One man/woman show.

Mantiki ya Mahari ilikuwa ni Zawadi Kwa Kumlea Binti. Hivyo ilitolewa Kwa Walezi.

Hasahasa Baba ambaye ndiye alikuwa anasimamia show nzima ya kumlea Mama na watoto.

Siku hizi Wababa wengi tumekimbia majukumu, Watoto wanalelewa na Mama zao au Ndugu upande wa Mama. Hao ndio wenye mamlaka na umiliki WA huyo Mtoto.

Hao ndugu, kina shangazi, Bibi, mjomba sijui Babu na Ndugu wengine wataingia kwenye protocol za kupewa sehemu ya Mahari ikiwa walishiriki kumtunza huyo Binti iwe Kwa kumsaidia Mama Yao au Baba Yao katika malezi ya huyo Binti.
Je, uoni umuhimu wowote upande wa baba kushiriki katika kupokea mahari?

Unajua umuhimu wa pande zote mbili kushiriki kamuozesha binti?
 
Duuuh mbona una hasira sana, tumefika hatua jamii imeacha kabisa misingi ya kiimani na hata Mila na desturi zinatazamwa kwa macho ya makengeza, katika mazingira ya namna hiyo katu hatuwezi kutoboa!

Mtoa mada nimemuelewa na amelenga jambo jema tu ila mnavyomshambulia inaonyesha wazi namna mlivyojaa hasira vifuani mwenu, si desturi zetu kuozesha binti au kijana kuoa kama kuuza au kununua mapapai, kuna taratibu zake na moja ya taratibu ni pamoja na wazazi wa pande zote kufahamiana na kutengeneza undugu Kwa kadri ya taratibu za Kila jamii, baada ya hapo wanandoa wapya wanapaswa baraka za wazazi wao na kuendelea na maisha!

Kwa maelezo ya mtoa mada, baba wa binti ni mpuuzi tu kama walivyo wapuuzi wengine, Kwa kumtelekeza bintiye hata asijue alipo, (amemtwisha mzigo mzito binti yake na itamtesa sehemu kubwa ya maisha yake) japo haiondoi DNA zake kwa huyo mtoto! Hivyo muoaji kuuliza ana maana nzuri mnooo... (Ila ukiangalia kwa jicho la nyama hwezi kuona)

Nawakumbusha watu wenye jazba kama wewe, kwamba biblia takatifu haijabadilika, na maandiko hayabadilishwi na nyakati na kuyafanya yawe yanaendana na "situation" nooo!, tumeamriwa kuwaheshimu baba na mama, ili tupate maisha marefu na heri duniani, hakuna clarification ya aina ya baba au mama wa kumheshimu!

Katika uumbaji Mungu aliumba mtu ke na me, na Kila mmoja alipewa wajibu wake, Kwa namna yoyote iwayo hakuna excuse ya kufanya hayo mambo interchangeably, hakuna! Japo kupitia feminism movements uhalisia huu unafifishwa na tunaacha miongozo ya kiimani na desturi zetu badala yake tunaangalia Mila, tamaduni na desturi za wengine, TUTAFELI SANAAA, that is why ka kadri muda unavyokwenda watoto wengi wa kiume wanaolelewa na mama tu utawaona wakiwa na tabia za kike kike tu, na watu tunaona sawa, mwisho wa siku idadi ya mashoga na wasagaji inaongezeka kwa kuwa uanaume umepuuzwa!
Umeeleweka kiongozi, hao wanaopinga ni kwamba hawaoni mbali na hawajui misingi ya familia. Na asilimia kubwa ni wadada ambao wamezalishwa na kukimbiwa kwa makosa yao wenyewe na sasa wanalea binti zao bila kushirikisha upande wa baba na wakitegemea binti zao watakua na kuozeshwa. Na wanasahau ya kwamba maji ufuatao mkondo, kama binti umemlea mwenyewe naye atafanya chini juu alee watoto wake mwenyewe.

Mwanamke hata kama amezalishwa na akakimbiwa, ni jukumu lake kuhakikisha mtoto wake anamjua baba yake na ndugu zake upande wa baba. Hilo ni jukumu la mama kuwa daraja la kuunganisha ndugu za mtoto pande zote mbili.
 
Hivi muoaji mambo ya kwamba nani anapokea mahari yanakuhusu nini?

Wewe peleka mahari ,, wakupokea mahari hawez kukosekana.
Wee hujui nini maana ya kuoa. Ndo maana familia hazidumu siku hizi. Inamaana unaweza kuoa binti ambaye unajua ndugu zake wa upande wa mama pekee yake?
 
hapo inategemea na nature ya kabila husika, coz issue yenyewe ya mahali imekaa kitamaduni.
 
jitahidi tupate kabila la huyo mwanamke upande wa mama na wa baba.
 
Back
Top Bottom