Kwa majibu haya nitakuwa sahihi kusema ya Kwamba mahari imegeuzwa ibada, kundi kubwa linaabudu mahari na halijui ni kwa sababu zipi.Kuna umri unakulimit kujuwa baadhi ya vitu, subiri ukikuwa wala hutohitaji kuambiwa na mtu utaijuwa dunia Kwa mapana yake.
Omba Mungu akupe miaka mingi ya kuishi.
Labda tu nikueleze kitu ambacho huwezi kuamini kama kipo.Kuna vitu vingine havihitaji degree kutoa maamuzi .
Binti tangu azaliwe mpaka anakuwa mkubwa hajalelewa na baba wala ndugu wa upande wa baba hawamfahamu! Moja kwa moja mahari inaenda kwa mama au wajomba.
Halafu mbona mnawadharau sana wanawake? Mama amemlea binti yake kwa Hali na mali bila uwepo wa baba mzazi halafu suala la mahari unataka upeleke kwa upande usiowajibika kwa lolote!!!
Vijana wengi waliozaliwa miaka ya 2000 wamezaliwa na roho lakini hawana nafsi, tunawaangalia tu ulimwengu ndio Mwalimu bingwa kabisa hapa duniani, utawafunza Kwa njia ngumu sana.Kwa majibu haya nitakuwa sahihi kusema ya Kwamba mahari imegeuzwa ibada, kundi kubwa linaabudu mahari na halijui ni kwa sababu zipi.
Kiujumla hakuna hasara yoyote itakayopatikana kwenye ndoa endapo mahari isipotolewa
Pia hakuna faida yoyote itakayopatikana kwenye ndoa endapo mahari itatolewa.
WajombaHuyu binti kalelewa na mama yake pekee yake. Baba yake yupo hajafa ila binti hajawahi kukutana ana kwa ana na baba yake wala katika upande wa baba yake hamjui ndugu yeyote.
Je, kwa scenario kama hiyo binti anafaa kutolewa mahari na kuolewa?
Na taratibu za mahari zipoje? Kwani navyojua mahari ni ya baba na kama baba hayupo mahari ipokelewe na yeyote upande wa baba yaani shangazi au baba mdogo au m
kubwa.
Umekosa hoja za kutetea mahari umekuja na vitisho hewa.Vijana wengi waliozaliwa miaka ya 2000 wamezaliwa na roho lakini hawana nafsi, tunawaangalia tu ulimwengu ndio Mwalimu bingwa kabisa hapa duniani, utawafunza Kwa njia ngumu sana.
Asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu, weka hili akilini.
Kama sio mke mwema achanae babu, kama unajua sio mke mwema kilichokufanya ulete thread ni nini ?Tatizo siyo kupokea mahari bali ni kwanini binti hajui ndugu yake yeyote upande wa baba? Unadhani huyo binti anaweza kuwa mke mwema?
Wewe unafikiri ni kosa la nani? Umempenda binti au umeupenda ukoo wake upande wa baba?Tatizo siyo kupokea mahari bali ni kwanini binti hajui ndugu yake yeyote upande wa baba? Unadhani huyo binti anaweza kuwa mke mwema?
Katika uislaam mahari ni ya bint mwenyewe...na anaweza pokea mwenyewe mbele ya mashahidi...ila atakayemuozesha ni IMAM WA MSIKITI KAMA HANA NDUGU UPANDE WA BABA MWANAUME.Huyu binti kalelewa na mama yake pekee yake. Baba yake yupo hajafa ila binti hajawahi kukutana ana kwa ana na baba yake wala katika upande wa baba yake hamjui ndugu yeyote.
Je, kwa scenario kama hiyo binti anafaa kutolewa mahari na kuolewa?
Na taratibu za mahari zipoje? Kwani navyojua mahari ni ya baba na kama baba hayupo mahari ipokelewe na yeyote upande wa baba yaani shangazi au baba mdogo au mkubwa.
Bora na ww umejb swal wengne wanaropoka kama ugomvi[emoji1787]Kwenye hii scenario upande wa baba hauhusiki kwenye hiyo mahari wala haihitaji mjadala.
Naongezea atafute hela,huwezi ukawa na hela alafu ukataka kufatilia mpaka hela ilikoenda,kama mtoto amelelewa ujombani unachouliza hapa ni nini?Komeni kuwaandama single mothers, ni ukosefu wa nidhamu na ni kinyume na utu.
Unasema mahari ipokelewe na baba ambaye hata hamjui binti. Hapo kuna baba kweli.
Unasema binti hafahamiani hata na ndugu mmoja upande wa baba, hapo undugu uko wapi?
Halafu taratibu za mahari za kwenu ni tofauti na watu wengine. Upande wa bi harusi ndio unaoandaa taratibu zote za mahari na namna gani mahari ipokelewe, sio wewe unayepanga.
Sasa kama huwezi hapa unataka ushauri gani?we na binti ndo mtajua kamaNa mimi siwezi toa mahari bila kujua upande wa baba.
Je, uoni umuhimu wowote upande wa baba kushiriki katika kupokea mahari?Hiyo ilikuwa zamani ambapo mtoto analelewa na Extended Familia.
Siku hizi Watoto wengi wanalelewa na One man/woman show.
Mantiki ya Mahari ilikuwa ni Zawadi Kwa Kumlea Binti. Hivyo ilitolewa Kwa Walezi.
Hasahasa Baba ambaye ndiye alikuwa anasimamia show nzima ya kumlea Mama na watoto.
Siku hizi Wababa wengi tumekimbia majukumu, Watoto wanalelewa na Mama zao au Ndugu upande wa Mama. Hao ndio wenye mamlaka na umiliki WA huyo Mtoto.
Hao ndugu, kina shangazi, Bibi, mjomba sijui Babu na Ndugu wengine wataingia kwenye protocol za kupewa sehemu ya Mahari ikiwa walishiriki kumtunza huyo Binti iwe Kwa kumsaidia Mama Yao au Baba Yao katika malezi ya huyo Binti.
Umeeleweka kiongozi, hao wanaopinga ni kwamba hawaoni mbali na hawajui misingi ya familia. Na asilimia kubwa ni wadada ambao wamezalishwa na kukimbiwa kwa makosa yao wenyewe na sasa wanalea binti zao bila kushirikisha upande wa baba na wakitegemea binti zao watakua na kuozeshwa. Na wanasahau ya kwamba maji ufuatao mkondo, kama binti umemlea mwenyewe naye atafanya chini juu alee watoto wake mwenyewe.Duuuh mbona una hasira sana, tumefika hatua jamii imeacha kabisa misingi ya kiimani na hata Mila na desturi zinatazamwa kwa macho ya makengeza, katika mazingira ya namna hiyo katu hatuwezi kutoboa!
Mtoa mada nimemuelewa na amelenga jambo jema tu ila mnavyomshambulia inaonyesha wazi namna mlivyojaa hasira vifuani mwenu, si desturi zetu kuozesha binti au kijana kuoa kama kuuza au kununua mapapai, kuna taratibu zake na moja ya taratibu ni pamoja na wazazi wa pande zote kufahamiana na kutengeneza undugu Kwa kadri ya taratibu za Kila jamii, baada ya hapo wanandoa wapya wanapaswa baraka za wazazi wao na kuendelea na maisha!
Kwa maelezo ya mtoa mada, baba wa binti ni mpuuzi tu kama walivyo wapuuzi wengine, Kwa kumtelekeza bintiye hata asijue alipo, (amemtwisha mzigo mzito binti yake na itamtesa sehemu kubwa ya maisha yake) japo haiondoi DNA zake kwa huyo mtoto! Hivyo muoaji kuuliza ana maana nzuri mnooo... (Ila ukiangalia kwa jicho la nyama hwezi kuona)
Nawakumbusha watu wenye jazba kama wewe, kwamba biblia takatifu haijabadilika, na maandiko hayabadilishwi na nyakati na kuyafanya yawe yanaendana na "situation" nooo!, tumeamriwa kuwaheshimu baba na mama, ili tupate maisha marefu na heri duniani, hakuna clarification ya aina ya baba au mama wa kumheshimu!
Katika uumbaji Mungu aliumba mtu ke na me, na Kila mmoja alipewa wajibu wake, Kwa namna yoyote iwayo hakuna excuse ya kufanya hayo mambo interchangeably, hakuna! Japo kupitia feminism movements uhalisia huu unafifishwa na tunaacha miongozo ya kiimani na desturi zetu badala yake tunaangalia Mila, tamaduni na desturi za wengine, TUTAFELI SANAAA, that is why ka kadri muda unavyokwenda watoto wengi wa kiume wanaolelewa na mama tu utawaona wakiwa na tabia za kike kike tu, na watu tunaona sawa, mwisho wa siku idadi ya mashoga na wasagaji inaongezeka kwa kuwa uanaume umepuuzwa!
Wee hujui nini maana ya kuoa. Ndo maana familia hazidumu siku hizi. Inamaana unaweza kuoa binti ambaye unajua ndugu zake wa upande wa mama pekee yake?Hivi muoaji mambo ya kwamba nani anapokea mahari yanakuhusu nini?
Wewe peleka mahari ,, wakupokea mahari hawez kukosekana.