Je, nani anapokea mahari kwa binti aliyelelewa na mama pekee?

Je, nani anapokea mahari kwa binti aliyelelewa na mama pekee?

Hakuna mila ya siku hizi, mila ni moja tu, inavyosema ndivyo itakavyofatwa.

Hakuna mahari Kwa tajiri ya baba fuatilia vizuri utagunduwa hili.

Na kama umeowa pitia upya barua ya majibu ya poss uliyomposa mke wako walipokujibu barua walikuandikia wanataka nini katika orodha.

Mtu ambaye ana pesa direct inatamkwa ni mjaja wa mama labda na pesa ambayo ni binti anayeposwa, siyo ya baba wala ya mama.

Binti ndio mwenye mandate ya kugawa posho Kwa ndugu waliokuja wanaotambulika kimila kupata chochote.
Issue ni kwamba unawezaje kutoa mahari kwa binti ambaye hujui baba wala ndugu yeyote upande wa baba yake?
 
Baadhi ya makabila hawapeleki mahari kwa mama hata ikitokea binti hajalelewa na baba yake.
Ikiwa baba hayupo mahari italipwa kwa ndugu wa baba. Baba au ndugu wa baba watagawa sehemu ya Mali na kuipeleka kwa wajomba wa binti. Tofauti na hivyo taratibu za ulipwaji wa mahari unakuwa haujakamilika.
Uo ndiyo utaratibu wa mahari, hata ukioa unajua umeoa kweli maana unajua ndugu za binti pande zote mbilina zimeshiriki kukupa mke.
 
Hizo mila za kununua watu zimepitwa na wakati, wala hampaswi kujificha kwenye mila kiujumla swala mahari halina faida yoyote kwa sasa.

Na siku zote watetea mahari wamejificha kwenye mila ila hawana sababu za msingi mahari inawasaidia nini wanandoa.

Labda namimi nikupe elimu kidogo,
Mahari ilitolewa hapo zamani kwa sababu mwanamke alichukuliwa kama kijakazi anayetoka familia yake kwenda familia nyingine kwajili ya kuzaa watoto na kuzalisha mali. (Ufugaji na kilimo)

Ilionekana ni hasara kumuoa mwanamke kwa mahari Alafu hasizae watoto wengi au kushindwa kuzalisha mali (kilimo) na huyu mwanamke alikuwa kama mtumwa.

Sasa watu kama wewe mnataka tuendeleze utaratibu kama huu kwa kichaka cha mila.

Kama mila haina faida kwa mazingira ya sasa hatunabudi kuachana nayo.
Tatizo vijana wa siku hizi mnakimbilia usasa mwingi ndiyo maana mnakataa kuoa, mnakataa kuzaa, mnakataa kuwa na familia, mnakubali jinsia moja kuoana. Taratibu zenye misingi imara mnaziita ni za zamani.

Kutoa mahari ni zaidi ya inavyoelezwa maana wewe unatafsiri ya kwamba binti ananunuliwa. Hiyo tafsiri yako siyo kweli na ina upitishwaji mkubwa sana.

Familia ni taasisi kuu na ni ya zamani ikiwa na misingi yake iliyonyooka. Ukiyumba kutekeleza misingi ya kuanzisha familia ujue hutafika mbali, baada ya miezi miwili utaanza kukataa ndoa. Kaa wa wakubwa wakufundishe.
 
Na hapo ndipo Gender Equality inatakiwa.
Haiwezekani kwenye maslahi Mwanamke asipewe kipaombele lakini kwenye majukumu ya kimalezi Watu wanamkimbia. Hiyo sio Haki.
Tatizo ni upande mmoja wa mama kupokea mahari bila upande wa pili wa baba kushiriki.

Unajua umuhimu wa pande zote mbili kushiriki kumuozesha binti?
 
Dunia yasasa,ni vigumu eti ukoo wote wa baba,kusiwe na mawasiliano,anyway hongera kwa single mother kukuza,na kufikia hatua ya kuozesha.
Ila psychologically,huyo mdada unayemuoa, uwezekano wa kuja kua single mother,ni mkubwa sana,kwasababu ana role model ambaye kamkuza.
Hapo ndo changamoto ilipo. Nitaoaje binti asiye na ndugu upande wa baba. Je mtoto wetu akija kuleta mchumba ambaye ni ndugu wa mama yake upande wa baba?
 
Lakini huo ndio mfumo wa kale, mfumo wa wazee!

Je tusiamini katika kale?
Ya kale ni dhambi, ndiyo maana generations zinaweza kuendelea. Wanaofuata usasa wamekimbia hata kuzaa, sasa next generation itatoka wapi?
 
Naongezea atafute hela,huwezi ukawa na hela alafu ukataka kufatilia mpaka hela ilikoenda,kama mtoto amelelewa ujombani unachouliza hapa ni nini?
Hela siyo tatizo. Tatizo ni kwanini upande wa pili haujahusika kuozeshwa binti?
 
Tatizo vijana wa siku hizi mnakimbilia usasa mwingi ndiyo maana mnakataa kuoa, mnakataa kuzaa, mnakataa kuwa na familia, mnakubali jinsia moja kuoana. Taratibu zenye misingi imara mnaziita ni za zamani.

Kutoa mahari ni zaidi ya inavyoelezwa maana wewe unatafsiri ya kwamba binti ananunuliwa. Hiyo tafsiri yako siyo kweli na ina upitishwaji mkubwa sana.

Familia ni taasisi kuu na ni ya zamani ikiwa na misingi yake iliyonyooka. Ukiyumba kutekeleza misingi ya kuanzisha familia ujue hutafika mbali, baada ya miezi miwili utaanza kukataa ndoa. Kaa wa wakubwa wakufundishe.
Tatizo sio vijana, tatizo ni taratibu zisizo na maana, zisizo na faida na zimepitwa na wakati.

Mimi kama kijana ninaekwenda kuanzisha familia na mwenzangu, kutoa mahari kunatusaidia nini kwa mazingira ya sasa????

Kwamba nikitoa mahari ndo utapatikana upendo, furaha na Amani ndani ya nyumba??

Mahari ni biashara iliyowanufaisha watu huko nyuma, ilikuwa ni moja wapo ya vitu vilivyoziingizia familia mali hususani mifugo, vyakula n.k. ni utaratibu uliopitwa na wakati hauna maana tena kwa maisha ya sasa.
 
Huyu binti kalelewa na mama yake pekee yake. Baba yake yupo hajafa ila binti hajawahi kukutana ana kwa ana na baba yake wala katika upande wa baba yake hamjui ndugu yeyote.

Je, kwa scenario kama hiyo binti anafaa kutolewa mahari na kuolewa?

Na taratibu za mahari zipoje? Kwani navyojua mahari ni ya baba na kama baba hayupo mahari ipokelewe na yeyote upande wa baba yaani shangazi au baba mdogo au mkubwa.
Mm ni muislamu mahari ni yangu anayepokea ni yoyote yule then napewa mzigo wangu saaafi.
 
Komeni kuwaandama single mothers, ni ukosefu wa nidhamu na ni kinyume na utu.

Unasema mahari ipokelewe na baba ambaye hata hamjui binti. Hapo kuna baba kweli.

Unasema binti hafahamiani hata na ndugu mmoja upande wa baba, hapo undugu uko wapi?

Halafu taratibu za mahari za kwenu ni tofauti na watu wengine. Upande wa bi harusi ndio unaoandaa taratibu zote za mahari na namna gani mahari ipokelewe, sio wewe unayepanga.
Lakini si tumekubaliana wajumbe tena kwa nguvu moja hakuna kuoa single mother
 
Hapa kabinti kamoja tu,kameshatandikwa mimba kanalea saa hii.
Yaani ngoja tu
 
Komeni kuwaandama single mothers, ni ukosefu wa nidhamu na ni kinyume na utu.

Unasema mahari ipokelewe na baba ambaye hata hamjui binti. Hapo kuna baba kweli.

Unasema binti hafahamiani hata na ndugu mmoja upande wa baba, hapo undugu uko wapi?

Halafu taratibu za mahari za kwenu ni tofauti na watu wengine. Upande wa bi harusi ndio unaoandaa taratibu zote za mahari na namna gani mahari ipokelewe, sio wewe unayepanga.

Hii personal attack ni Kwa ajili ya KATAJWA SINGLE MAZA au?

#YNWA
 
Mkuu naona unataka kuoa mpenzi wangu... Mm nikisha makizana nae kuhusu namna ya kumlipia mahari yake sasa wewe naona unaingilia kunichukulia mchumba wangu shauri yako
 
Hapo ndo changamoto ilipo. Nitaoaje binti asiye na ndugu upande wa baba. Je mtoto wetu akija kuleta mchumba ambaye ni ndugu wa mama yake upande wa baba?
Kwa sababu huna akili tunataka kutueleza yatima wanaolelewa kwenye vituo vya Watoto yatima hawana haki ya kuolewa Kwa sababu hawana ndugu?

Wewe ni mpumbavu wa kwanza Kwa sababu hata mpumbavu wa mwisho ana afadhali.
 
Back
Top Bottom