Je, ni kweli hii inapunguza gharama za ujenzi?

Je, ni kweli hii inapunguza gharama za ujenzi?

Asante kwa mchanganuo mkuu.

Nilipo cement ni 16,000
Tofali ni 900 na usafiri inakua 1000.
Ratio ya tofali 40 kwa mfuko nadhani sio mbaya.
Sitatumia mixer na vibrator.Tutaenda manual.
Vijana huku wanalipwa hadi 4000 kwa mfuko kwa kazi kubwa
Nami nilitaka kukuambia uende manual, ukisema ununue mixer+vibrator gharama iko pale pale, utaokoa ratio tu. Kwa ratio ya 35, hata ukienda manual bado tofali zitakuwa imara tu coz utazimwagia maji ya kutosha.
 
Habari waheshimiwa.

Nina kaproject kanakohitaji kama tofali 20,000 hivi kakamilike.

So far nina tofali 3000 ila nimepiga hesabu nikaona zikizobakia nikifyatua mwenyewe nitaokoa kama 40% ya pesa ya kununulia ila mafundi wananikatisha tamaa kuwa nitapata hasara tu ni bora kununua.

Naomba kujua kama yupo aliyefanya hii kitu matokeo yalikuaje.

Natanguliza shhkrani🙏🙏

Habari!

Hapa vitu vingi vinategemeana/sehemu ulipo.

1: Je ubora wa tofali unazopata haulingani na ubora wa mradi wako?
Hili utaweza kulitatua kwa kusimamia wewe binafsi kwa ukaribu uliotukuka.

2: Unahitaji kuokoa pesa
Tafakari juu ya sehemu ulipo:
A: Gharama ya upatikanaji wa mafundi bora kwenye ufyatuaji.

B: Gharama ya upatikanaji wa mashine ya kufyatua au cha kufanana nacho.

C: Gharama ya maji

D: Gharama ya mchanga

E: Gharama ya cement ununuzi na kufikisha site/kama unaweza kupata kwa bei ya jumla pia

F: Gharama ya umeme/ukitumika.

G: Gharama ya wewe kufika eneo la tukio kama si sehemu unayoishi.

H: Gharama ya mlo wako kwa siku kama si nyumbani na itaongezeka kutoka kwenye ule wa kila siku.

I: Thamani ya uwepo wako muda wote/reflect kwenye pesa utakayoiokoa.

3: Tofali iliyotayari:
A: Ubora
B: Ununuzi +kupakia +kushusha+ usafiri

Jibu la mwisho ni: 3 - (1+2)
 
Asante kwa mchanganuo mkuu.

Nilipo cement ni 16,000
Tofali ni 900 na usafiri inakua 1000.
Ratio ya tofali 40 kwa mfuko nadhani sio mbaya.
Sitatumia mixer na vibrator.Tutaenda manual.
Sawa, karibu mkuu

Kwa ushauri tu:
Ratio ya 40 sio mbaya ila inatoa tofali la kawaida sana lisilo imara kivile hata maengineer huwa hawayakubali

Mashine ya bam bam (ya mkono) haitoi tofali nzuri kwa sababu mshindilio wake ni mdogo tofauti na ya umeme. Tena ukizingatia umepanga kutoa ratio ya 40!

Na utatumia mchanga gani?
 
Kuna muda wa usimamizi, vitendea kazi vya kufyatua,kulipa mafundi, maji, mchanga, simenti, usumbufu na mafundi, kutokumaliza kwa wakati n.k
 
Nami nilitaka kukuambia uende manual, ukisema ununue mixer+vibrator gharama iko pale pale, utaokoa ratio tu. Kwa ratio ya 35, hata ukienda manual bado tofali zitakuwa imara tu coz utazimwagia maji ya kutosha.
Mkuu Soma pm basi au mpaka nikubembeleze 😏
 
mchanga bora ni ule usio na vumbi jingi au hauna vumbi la udongo kabisa unapatikana mtoni au kwenye vijito au clashing dust za kokoto ni bora sana kama utazipata kwa tofali ..mchanga bora kwa tofali ni ule wenye punje kubwa na uwe una dust kidogo upatikane mtoni sehemu ambazo hazina chumvi au magadi...huo ndio mchanga bora kwa tofali...
mchanga bora kwa plasta uwe laini au punje ndogo usiwe na vumbi la udongo kabisa kama ni wakuchimbwa uchimbwe kwenye ardhi isiyo na asili ya chumvi ama magadi...ni hayo tu wataongeza wengine...wajenzi ama wajuvi....
Asante sana mkuu kwa darasa hakika umeongeza uelewa wangu.

Kwa sasa nitafanya haya mambo kwa kuzingatia haya maelezo yako.

Hivi kwa Dar (Pwani) kuna sehemu inatoka mchanga wenye magadi au chumvi?
 
Una machine ya tofali?
Mchanga?
Cement za kutosha?
Umeme?
Maji yapo au ni ya kununua?
Mafundi unawalipaje?
Wabebaji je?
Ukijumlisha hizo gharama unakuta gharama inakuja pale pale bora ununue uokoe muda na gharama zako
Sikweli
 
Nami nilitaka kukuambia uende manual, ukisema ununue mixer+vibrator gharama iko pale pale, utaokoa ratio tu. Kwa ratio ya 35, hata ukienda manual bado tofali zitakuwa imara tu coz utazimwagia maji ya kutosha.
Kabisa mkuu.
Na uzuri maji hapo ni uhakika.
Cha msingi niwepo kuhakikisha vijana hawafanyi janja janja
 
Habari!

Hapa vitu vingi vinategemeana/sehemu ulipo.

1: Je ubora wa tofali unazopata haulingani na ubora wa mradi wako?
Hili utaweza kulitatua kwa kusimamia wewe binafsi kwa ukaribu uliotukuka.

2: Unahitaji kuokoa pesa
Tafakari juu ya sehemu ulipo:
A: Gharama ya upatikanaji wa mafundi bora kwenye ufyatuaji.

B: Gharama ya upatikanaji wa mashine ya kufyatua au cha kufanana nacho.

C: Gharama ya maji

D: Gharama ya mchanga

E: Gharama ya cement ununuzi na kufikisha site/kama unaweza kupata kwa bei ya jumla pia

F: Gharama ya umeme/ukitumika.

G: Gharama ya wewe kufika eneo la tukio kama si sehemu unayoishi.

H: Gharama ya mlo wako kwa siku kama si nyumbani na itaongezeka kutoka kwenye ule wa kila siku.

I: Thamani ya uwepo wako muda wote/reflect kwenye pesa utakayoiokoa.

3: Tofali iliyotayari:
A: Ubora
B: Ununuzi +kupakia +kushusha+ usafiri

Jibu la mwisho ni: 3 - (1+2)
Asante kwa ushauri mkuu.

Jana nimeongea na mafundi wakubwa wawili juu ya ya wazo langu majibu yao yanaonesha iwapo nitasimamia vizuri kuepusha mafundi kufanya uchakachuzi nitaokoa fedha na kupata tofali imara kulinganisha na za kununua
 
Utaokoa gharama kwa kiasi kikubwa, mashine unakodi Bei 5000 kwa siku. Maji unanunua kwa wenye magari makubwa makubwa, tofali 20000 kwa kununua Bei ya chini ni Kama 800 jumla milioni 16 Ila hautapata tofali Bora.
 
Sawa, karibu mkuu

Kwa ushauri tu:
Ratio ya 40 sio mbaya ila inatoa tofali la kawaida sana lisilo imara kivile hata maengineer huwa hawayakubali

Mashine ya bam bam (ya mkono) haitoi tofali nzuri kwa sababu mshindilio wake ni mdogo tofauti na ya umeme. Tena ukizingatia umepanga kutoa ratio ya 40!

Na utatumia mchanga gani?
Nimekupata mtaalam.

Kwa vile uwezo wangu kiuchumi ni mdogo itabidi tu nitumie hiyo ya mkono halafu iwe 35 blocks kwa mfuko kama mlivyoshauri.

Mchanga nitanunua kwa kufuata maelezo ya mkuu shanature hapo juu.
Au wewe ulikua unashaurije mkuu?
 
Back
Top Bottom