Je, ni kweli kuwa Dodoma CBD inaipiku Mwanza CBD?

Safi sana ata mimi huwa najifikiri kuhusu hii kitu nazidi kuwaza muda mwingine naona wakazi karibu wote wa Dodoma ni maskini ndo maana hakuna project za mtu binafsi au taasisi kwasababu kila kitu wanajengewa na serikali iwe makazi ya kuishi, hotel etc je siku hizi miradi ikiishi dodoma itapata kweli mtu au watuwakuindeleza, Dodoma kwa Mwanza bado wanasafari ndefu, nawapongeza kwa kujengewa miundombinu ya barabara tu wanaweza kuwa better kwa baadae.
 
Leta project za dodoma ambazo hazifadhiliwi na government nikuumbue, dodoma ni jiji la omba omba wanaotegemea fadhila za serikali.
 
And vise versa is true, Dodoma inaibeba sana Mwanza kulinganishwa nayo kitu ambacho Mwanza haistahili hata ukucha kupata sifa hizo.
Huwa nakuona una akili ila kila muda unavyoenda nakuona unaupungufu fulani.
 
Dodoma ambako wana njaa ya kutupa mpaka wanashindia ubuyu ulinganishe na Mwanza ambapo mazao yote yanastawi na michembe ni chakula cha asili wala sio shida kuwa nayo.
Ukame wa Dodoma ni janga ukipita njia ya Iringa ni aibu kwa kweli
Swali dogo tu kati ya Dodoma na Shinyanga au Simiyu unadhani ni mkoa gani kati ya hiyo ni mzigo kwa nchi linapokuja suala la tishio la uwepo wa baa la njaa? Au ni mkoa gani hapo uwa ndo unatangulia kuisi makali ya njaa mpaka ng'ombe wanaishia kula vumbi?
 
Mwanza ndiyo Jiji kubwa Tanzania ambalo halijaendelea kwa kutegemea miradi ya serikali. Jiji la watu.
La pili ni Mbeya.

Mwanza na Mbeya ndiyo majiji wanaume wapiganaji yasiyoendelezwa na baraza la Mawaziri.
 
Aseme hapa Mwanza kuna garden gani au Arusha
 
mkuu shinyanga nimekaa mitaa ya LIGA shinyanga nimekuta wasukuma washamba hata daladala hamna wanapanda baiskeli tu
Sio washamba..ni nyenzo za usafiri..shinyanga ni tambalare..pia shinyanga sio kubwa ni ndogo haata population sio kubwa kivile kuleta daladala za gari mjini.

Halafu kuwa na dalaladala na kugombania usafiri hadi wengine wanakufa huo ndio ujanja?

#MaendeleoHayanaChama
 
Msikariri kuwa maendeleo lazima yafanywe tu na wakazi,afu pili kuishi kwenye makazi ulojenga mwenyewe pia nikipimo cha umasikini tu wakushindwa kuafford kurent au kununua nyumba katika viwanja vilivyopimwa na vyenye miundombinu bora.

Majiji mengi mazuri duniani watu binafsi na serikali wameshirikiana kujenga nyumba nyingi za kupangisha(estates) pamoja na miundombinu mingi bora na ya kisasa na wengi wa wakazi katika majiji hayo makubwa hawa-wish kujenga tena bali kupanga au kununua kwa kuwa kipato chao kinaruhusu kufanya hivyo ndiyo maana leo utajiri wa jiji la Dar in terms of GDP haukai meza moja na Nairobi sababu ni hii.

Kwahiyo kulingana na style modern ya ujenzi wa jiji la wagogo na uwekezaji heavy uliopo haijalishi kawekeza nani kikubwa maendeleo tangible yanaonekana ground ni soon tu Mwanza itakaliswa pembeni kuanzia GDP, purchasing power na mzunguko wa pesa,miundombinu, viwanda na job creation,uzuri wa jiji na huduma muhimu hivyo usishangae wanaoona future bright ya Dodoma wakimuona mpinzani wake ukanda huu kuwa ni Nairobi.
 
Mwanza ndiyo Jiji kubwa Tanzania ambalo halijaendelea kwa kutegemea miradi ya serikali. Jiji la watu.
La pili ni Mbeya.

Mwanza na Mbeya ndiyo majiji wanaume wapiganaji yasiyoendelezwa na baraza la Mawaziri.

Majiji ya nyumba za mabati na tope zisizo na mpangilio, hizo sifa za kutokuendelezwa na serikali ndo zinawaponza mnaonekana hoya hoya! wenzenu wajanja wanazidi kula na serikali yao nyie mnabakia kuwa wapiga kura nambari moja na kwa jinsi mnavyozaliana na hamjali maendeleo ya miji yenu wala nchi wanawachabo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…