Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Kwa vile thamani ya kipande (Net asset value per unit) hukokotolewa kila siku kwa kila mfuko wao, unaweza kukokotoa thamani ya uwekezaji wako kila utakapo.

Mimi kwa mfano huwa ninakokotoa thamani ya uwekezaji wangu mara 1 kila wiki. Unaweza kukokotoa hata kila siku.

Thamani za vipande siku kwa siku zinapatikana katika website ya utt, kwenye application ya utt ukiwa nayo, na mara nyingine huchapwa katika baadhi ya magazeti.
Yaani unamaanisha licha ya gawio la at least 10% kwa mwaka, hivyo vipande vinapanda thamani pia? Yaani kama hisa?
 
Yaani unamaanisha licha ya gawio la at least 10% kwa mwaka, hivyo vipande vinapanda thamani pia? Yaani kama hisa?
Kupanda thamani ni at least (si chini ya) 10% kama ulivyandika. Yaweza vary hadi say 13%. Hivyo ukigawiwa mathalan 10%, kuna growth kutokana na kile kinachozidi hapo. Namna sahihi ya kujua thamani halisi ni kutumia thamani ya kipande inayotangazwa.

Ukokotoaji huo wa thamani hata hivi ni muhimu zaidi kwa mifuko kama Liquid ambayo fedha huchukui regularly bali unachukua pale unapoamua.

Kwa mifuko unayochagua kulipwa say kila mwezi (kama bond), ni wazi long term growth ya thamani ni ya polepole sana. Ni halali kwa vile unachukua gawio.
 
Nashukuru sana mkuu kwa huu uzi, nimepata elimu nzuri kwangu
 
Samahani..hii Liquid unakokotoa vipi riba yake kila siku?
Thamani ya kipande hukokotolewa na kutangazwa na utt kila siku ya kazi. Kwa mfano leo wanatangaza thamani kipande ya jana. Hivyo kwa vile utakuwa unajua idadi ya vipande vyako unazidisha na kupata ongezeko la uwekezaji wako.

Ukishanunua vipande mfuko wowote wa utt unashauriwa kujiunga na app ya utt ambapo thamani ya kipande utaiona kwenye simu janja yako kila siku. Pia idadi ya vipande vyako utaiona.
 
Hukunielewa. 60m nilikua nazo nikaweka Jikimu wakati naendelea KUTAFUTA nyingine. Zilipofika 100m (yaani nilikua NAONGEZEA, sio faida ya jikimu) nikafikiria nijenge au niziache tu jikimu, jibu likawa faida ya kuziacha ni kubwa. Nafikiri tumeelewana sasa.
[emoji112][emoji112][emoji112]
 
Habari mkuu, namimi niliweka liquid account mwaka jana, naomba unielekeze unaonaje ongezeko la pesa kila siku? asante
Bila shaka unajua idadi ya vipande ulivyònunua. Kama hujui, omba statement utt kwa kwenda ofisini kwao au kwa kuwaandikia email.

Sasa ukishajua idadi ya vipande, kila bei ya kipande inapotolewa wewe unazidisha tu.

Kwa mfano bei ya tarehe 6/4/2022 Liquid ilikuwa Tsh 313.3518 kwa kipande. Zidisha mara vipande vyako.

Vinginevyo download/ jiunge na app ya utt ambapo utaweza kuona directly bei za vipande kila mara, na pia thamani ya uwekezaji wako.
 
Bila shaka unajua idadi ya vipande ulivyònunua. Kama hujui, omba statement utt kwa kwenda ofisini kwao au kwa kuwaandikia email.

Sasa ukishajua idadi ya vipande, kila bei ya kipande inapotolewa wewe unazidisha tu.

Kwa mfano bei ya tarehe 6/4/2022 Liquid ilikuwa Tsh 313.3518 kwa kipande. Zidisha mara vipande vyako.

Vinginevyo download/ jiunge na app ya utt ambapo utaweza kuona directly bei za vipande kila mara, na pia thamani ya uwekezaji wako.
Asante mkuu kwa ufafanuz zaid.
 
wakuu,hivi vita vya Russia na ukrain haviwezi kuathiri faida kwenye hii mifuko?
 
Back
Top Bottom