Je, ni Speed gani kubwa zaidi ushawahi kutembea na gari au pikipiki?

Je, ni Speed gani kubwa zaidi ushawahi kutembea na gari au pikipiki?

Muwe mnaacha na wosia kabisa maana tunasumbuka kugawa Mali zenu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23]
Juzi kuna jamaa yangu alikuwa na Kluger yake mbichi DYX katoka kupiga tungi huko kajiachia chuma si ikahama njia kaenda kupita na nguzo ya umeme kaondoka nayo kabisa. Nimekuja kuonana nae miguu imemvimba kama anaumwa matende, na gari haifai kabisa na engine ilipasuka palepale.
 
Hii gari uwe nayo makini sana, maaana unakwenda speed kubwa halafu hata huoni speed kubwa.

180 KPH. BMW X5. I-95.
Ila kutunguka kuna raha yake mkuu, tena haswa chuma iwe na pulling.
 
Jamaa ana shift gears kama umeme, watu wanahisi mguu wake na clutch vimeunganaga [emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23]
Ila kuna watu wanapiga gear sio poa mkuu, mie mwenyewe watu wa home huwa wananiogopaga sana nikishika sterling, sasa huwa wengne wananiiga. Mwshowe kuna ndugu zangu niliwapa Gx100 wakaenda kuimwaga kwa kuiga navyojitupaga.View attachment 2291804View attachment 2291806View attachment 2291805
20210726_183757.jpg
 
Nakumbuka kuna siku natoka Arusha kwenda Moshi mjini niko na BMW 5 Series.

Hicho kipande cha Arusha Moshi sipendi kuendesha bila kumkimbiza Prey (kwa tuliosoma Wildlfe Prey animal (mfano Swala) ni wanyama wanaoliwa na predator).

Nimeendesha mpaka maeneo ya KIA sijapata changamoto yoyote ya maana ya kufukuzana, Kuna mjinga wa Land cruiser Hardtop nilimprovoke tukimbizane akanitolea nje.

Nikawa naendesha mdogo mdogo kusubiria prey mwingine, eeh bana ikapita Gx 100 kibati.

Nikamwacha anipoteze kabisa asinione ili ajisifu. Nikatupia kitu kwenye sport mode.

170 huyu hapa, jamaa anahangaika kucheki kwenye rear mirror, mbele kulikuwa na mteremko fulani, nikasema nikimpita hapa atasingizia mteremko.

Nikashuka naye kitu kinasoma 180, na jamaa alitegemea kwenye mteremko atachanganya zaidi aniache, akicheki niko nyuma yake, tukakamata tambarare, nikawasha indicator nataka kuchomoka.

Jamaa akapaniki zaidi akaniwashia indicator ya kushoto kuniruhusu nipite halafu huku anaendelea kukanyaga kibati kisiri siri 180.

Nikampita na lengo jamaa asione kabisa break light baada ya kilometa kadhaa nikasimama nikojoe nimsubirie jamaa apite nimfukuze tena.

Hahaha jamaa alisimama akaniambia kaka nimekubali mziki, naomba niangalie dash board hii mashine inasoma ngapi.

Siku nyingine gari ilifungwa spea pump flani nikasema wacha niende barabara ya ngaramtoni nikatest hiyo pump kama inapiga kazi vizuri.

Eeh bana natiririka na 170 kurudi town, ghafla kwa mbele naona fuso linatolewa gereji linasukumwa barabarani liwake.

Wale jamaa waliokuwa wanasukuma walivyoona nakuja kwa moto mkali wakaacha gari wakakimbia kunusuru maisha yao.

Nilimwambia Mungu pokea roho yangu.

Usinitanie nikaingiza gari shambani. Nikala shamba la mahindi kama movie vile.

Nyingine natoka Arusha kwenda mto wa mbu mida ya saa 2 usiku. Nakimbia kumtafuta prey huko mbele mara Hilux double cabin yeboyebo hii hapa.

Kwa kweli jamaa alikuwa anafukia sio mchezo, nikasema huyu nisimpite nimchoshe hapo nyuma 170/180/190

Jamaa akawasha indicator anaingia kulia kama vile amefika. Nikasema huyu usikute amedhani majambazi ananikataa kijanja.

Kweli baada ya kukata kulia akasimama akawa ananisikilizia. Nikasepa zangu mdogo mdogo namuona anakuja nyuma yangu, nikimsubiria apite hapiti. Nikachimba zangu.
[emoji23][emoji23][emoji23]
Daaaah! Ukavuna mahindi shambani.
 
Back
Top Bottom