Hao kwa wastani wa bei wapoje kwenye jeans na cadet?Nunua maduka ya Woolworths (Posta au Mlimani City au Mikocheni - Kwa Warioba) hutajutia. Mimi nina uniform dress code yaani navaa nguo za aina moja kila siku na sio nguo nyingi ila huwa zinadumu muda mrefu sana.
Ulishamwambia Mama J?
🤣🤣🤣🤣🤣Tatizo lako wewe Ni seremala hivyo lazima nguo zichakae
Ushauri tafuta kazi ya kipupwe
Umeishia hapo ili uulizwe bei sio?Nimewahi nunua Cadet Splash 2017 hadi leo ipo, kosa nilinunua nyeupe. Ila imedumu sana miaka 6 sasa
Tatizo lao ni bei yao ukienda Mtumbani wapata cadet 7 hadi 10
Umemshauri vzr Sana huu ndio ushauri mzuri niishie hapo kusoma comment,Ongeza idadi ya nguo ,ukiwa na nguo nyingi nguo Moja inachukua siku nyingi hadi kuirudia hivyo idadi ya kufuliwa na kupigwa na jua inapingua kama mfuko hauruhusu usijipinde sana kununua za duka .
Tafuta mtumba uchanganye na za duka
Wew Ni hasara tupu ucheze umeme Lisa kikadeti Cha elf 17Tumia Sabuni za kipande hazina acid Nyingine ambazo unaweza kufulia na kuogea, usifulie MAJI ya chumvi, usiache Nguo juani kutwa nzima ikiwezekana anima kuani mda mfupi MAJI yakichuja zianike kimvulini zikauke kwa upepo utaratibu, nimeshawahi kukausha Nguo kwaupepo wa feni Nguo inakauka vizuri, pia wakati wa kunyosha tanguliza kitambaa Juu ya Nguo unayonyoosha na Pasi inazuia Nguo kupauka haraka, ni hayo tuu nawasilisha
Na watu wa Viwango TBS wapo wakiangalia watu wanavyoibiwa upo sahihi mkuu...Wewe nguo za akina Mr kadeti sjui vunjabei , unasema kuna nguo hapo au ni kusitirika tuu uonekane haupo uchi
Midosho ni tatizo asee , kama kariakoo nimekata tamaa kabisa kununua nguo , midosho tupuAchana na midosho
Duka lao lipo wapi??
Nguo kama ni qualify hazipauki kirahisi, , miaka ya nyuma kariakoo kulikuwa na Duka kuitwa Cadbury, jamaa alikuwa analeta nguo first class kutoka USA na Vietnam, , kuna t shirts nilivaa miaka 4 , na nikaja kuuza kama mtumba mbeya huko.Ongeza idadi ya nguo.
Nguo za mitumba cadet hiyo hiyo imetumika ulaya na hapa utavaa kufua na kuanika bila masharti .Cadet na Jeans zina kanuni zake za utunzaji!
Wewe bila shaka ulizianika kwenye jua, ulizifua kwa kutumia sabuni ya unga, unatakiwa uzipige pasi nje ndani(naamini hukufanya hivyo), ulitumia maji ya chumvi kuzifua, ulizikamua na kuzikung'uta!
Zitatamanikaje sasa...!?
UKWELI machungu, Tatizo ubishooNunua suruali za kitambaa
Tano hazipauki pia Bei nzuri
Nimeachana na kadet kabisaa. Nanunua za vitambaa kama waimba kwayaKuna kale karaha mtu upo huko katika shughuli zako umevaa nguo bado zipo fresh, Sio unapita sehemu nguo imepauka / rangi zimefifia yani hata mtu akikuangalia mara mbili unajua tu hapa kipengere ni nguo.
Nilinunua jeans 2 na cadet 2, kwa ufinyu wa bajeti yangu nilinunua jeans elf 25 kwa pair na cadet zilikuwa elf 28 kwa pair.
Nilitegemea walau zinivushe huu mwaka lakini hali imekuwa ndivyo sivyo, Kwa sasa naanza kuona hata soo kuzivaa.
nawaza hapa nikanunue cadet na jeans aina ipi ambazo zitaweza kunivusha salama huu mwaka na pia nizitunze vipi.
Jamani nguo zinanipasulia bajeti naombeni ushauri please.