Je, ninunue gari gani kati VW Tuareg, VW Tiguan, Audi Q5 ama Toyota Fortuner?


Chief kaangalie zile fortuner za petrol thailand au japan utaelewa bei uliyotaja
 
Yes, lengo langu ni SUV, siwezi kununua sedan kwa sababu ya body size yangu.

Nilikua nataka WV ila naona Audi imevuta hisia zangu ghafla.
Changamoto ya European cars kwetu ni Mafundi VW zipo mjini muda mrefu ukilinganisha na Audi hivyo naamini mafundi wapo wengi na spare parts zinapatikana kwa urahisi so kwa kuzingatia hilo mie ningenunua VW au Fortuner.
 
Chief kaangalie zile fortuner za petrol thailand au japan utaelewa bei uliyotaja
Ok Mkuu mimi nanunulia SA za petrol bei ipo chini zaidi ya diesel na kwa Nchi za SADC kuna karatasi ukiipata ya export and trade wanatolea pale Sunnyside Pretoria ni bure ila ukamilishe document zote za gari ukiipata hiyo unapata kodi nafuu hautalipa kama Japan au Dubai...Fortuner ni gari ambayo haina bei ikipita miaka kadhaa ni kama Benz tuu maana unakuta yametoka matoleo mengi..
 
We juzi ulikuwa unalalamika Kodi ya nyumba imepanda na biashara zako haziko vizur leo unakuja na upuuzi wa kusumbua watu hapa?
Aaarghhh. Eti fortuner?
Wewe allllaaaaaaa nitakupiga kofi mm!!
 

Hivi bei za SA kwa BMW X5 diesel ya mwaka 2008 mpaka 2012 ni bei gani mpaka dar+tax?

Na vp kuhusu ishu za udanganyifu nasikia kuna baadhi wanauza halafu ukishaisajili huku wanareport kule imeibwa, interpol wanakudaka, hiyo imekaaje, yaani kuna magari ya wizi pia mengi kutoka SA.

Za uingereza ghali sana yaani CIF inaanzia USD 12,000 bila kodi halafu ni zaidi ya km 100,000.
 
Kuhusu bei ingia bmw X5.olx.co.za au gumtree bmw x 5.co.za au cheki minada ya SA BMW auction...minada ipo mingi utachagua ya Gauteng Johannesburg na Pretoria...mtu akuuzie harafu baadae aseme ameibiwa hicho kitu hakipo hadithi za zamani gari zote zinatoka lazima zifutwe au uuziwe la wizi ambalo kutoka kwake bora utafute harali tuu lisilo na mashaka maana Botswana ni mawakala wa kukamata hizo gari wakikudaka ni ndani na gari imepotea...BMW zipo nyingi sijafanya usajiri hizo gari muda mrefu sana cheki na mtandao wa TRA harafu unapunguza sijajua asilimia ngapi maana nyingi ni za made SA kwa hiyo kodi inapungua tofauti na za Japan au UK..sema kwa BM huwa nashauri mtu anunue ambayo atleast isiwe imezidi miaka 7 au 8 kutokana na kupunguza Usumbufu hasa hizo 5 na 6...
 
Wakenya wengi sasa hivi wananunua magari South; yaani wamejua kutumia unafuu wa kodi kea kutumia SADC. Hebu tupe shule kidogo hapa.
 

Mkuu Isanga, naomba web ya wauza magari esp x3 sport, alafu kuna namna ingine ya kusafirisha kutoka south kama meli au ni lazima liendrshwe hadi tz?


Pia nipe link ya wauzaji wa fortuner wa kueleweka!
 
Mkuu Isanga, naomba web ya wauza magari esp x3 sport, alafu kuna namna ingine ya kusafirisha kutoka south kama meli au ni lazima liendrshwe hadi tz?


Pia nipe link ya wauzaji wa fortuner wa kueleweka!
SMD car sales smd.co.za hapo gari aina zote unachagua unayotaka ila hapo ni mnada sijajua ukiwasiliana nao ukiwa Tanzania wanafanyaje na City deep auto hao sio mnada utaangalia kwa brand pia ni vizuri kuwasiliana nao kwa namba za +2711 kwa Johannesburg namba za ofisi ndio wakupe namba za mkononi maana mitandao inachezewa ila hawachezei namba za simu za ofisi..gari unaweza ukalipia ikabebwa wabebaji wapo wengi hapo Kerk Street...wanachaji usd 1500 kuendelea inategemeana na aina ya gari...Smd wanauza gari nyingi sana ukiweza kununua mara moja ukapata uanachama unaweza kununua na kulipakia ukiwa Tanzania...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…