Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Tanganyika
Mungu wangu...

Sikujua hela ya Tanganyika inaenda kununua meli za Zanzibar
 
Usinipangie cha kufanya, hii nchi ni yetu sote.
Kwani ni nani aliitisha referendum kuhusu muungano wetu kupata popular puplic opinion? Yupo?

Tanzania ya 1961 sio ya sasa, wengine hatukuwepo, tuna haja ya kuhoji
Nikuulize swali dogo tu, Ulishawahi kwenda Zanzibar hasa pale unguja na sio kule pemba na ukakaa japo mwezi mmoja? Ukinijibu hili ntakuuliza lingine
 
Muungano wa JMT (wa “Tanzania bara” na Zanzibar) ni muungano wa kipekee duniani. NA kwa msimamo wa Serikali na chama tawala, ni tunu muhimu ya taifa la Tanzania. Watanzania “wazalendo” hawapaswi kuhoji tunu hii.

Mkuu uliyoandika hapa yanaeleweka vizuri sana tangu enzi na enzi. Wako wengi waliojaribu kuhoji mikingamo ya muungano huu kama wewe. Tafuta walihitimishaje hizo juhudi zao na wao waliishia wapi. Juzi hapa VP katoa angalizo kwa wanaotaka “kuchezea” muungano.

Kwa kifupi, hakuna mjadala wenye tija unaoweza kufanyika kuhusu mambo ya muungano wa JMT. Hivyo, FACT ni kuwa STATUS QUO inabakia kama ilivyo. SSH ndiye Rais wa JMT hadi (hatujui lini) na ana madaraka yote (absolute power) juu ya mambo yote ya Tanzania isipokuwa yale exclusive kwa Zanzibar pekee. Hakuna nchi inayoitwa “Tanganyika” duniani.

Iko hivi, hatuwezi kuacha kuhoji mambo ya muungano kwa vitisho kutoka Serikalini.

Jambo la msingi tuhoji kwa hekima na busara. Kwani huu Muungano umekua Biblia au Msahafu kwamba usihojiwe??

Huyo VP mwenyewe ametokana na Katiba ambayo ndiyo tuna raise query zake hapa.

Uzalendo sio kuogopa kuhoji mapungufu yaliyopo waziwazi.

No, Never
 
Rais Mh Mama Samia hajaanza kuongoza Tanzania leo. Amekuwa kiongozi mkubwa namba mbili Tanzania takriban miaka sita sasa.
Hapakuwa na swali wala figusi kipindi chote hicho.
Amepanda kuwa namba moja sasa maneno yamekuwa mengi mnoo..
Kipindi chote cha nyuma mlikuwa wapi? Au kwa vile haja toka kanda iliyo haribu tasnia na utu wa Watanzania?
Kwa taarifa tuu, Mama Samia ni Rais HALALI wa Tanzania. Kama mlitegemea genge la Wasukuma poleni sana.
Miaka mitano ilikuwa kama tuko jehanam.
Sasa mama kaja kutupa tabasamu mmeanza na uchokonozi.
Tulieni Mama Samia atupeleke Kaanan nchi ya maziwa na asali.
Mungu wanMbinguni amkinge Mh. Samia na macho ya husda.

Hakuna anayempinga Mama kutawala, jielekeze kwenye hoja. Je? Kuna mahala nimeongea uongo?
 
Je, anakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye ni Mzanzibari au kwa sababu yeye ni Mtanzania?

Anyway, tusichoshane kwa maswali... hapa sio bungeni!

Kwanza, tuweke pembeni suala la kuwa rais kwa sababu alikuwa makamu wa rais! Umakamu wake wa rais ulitokana na Uzanzibari wake!

Lakini hapa tunaujadili urais, ambao mtu haupati kwa Uzanzibari wake bali kwa Utanzania wake! Na tunaposema Utanzania, tunazungumzia jamhuri ya muungano!

Sasa kwavile umeshasema mambo yasiyo ya muungano kwa Tanzania Bara yanashughulikiwa na serikali ya muungano; serikali hiyo ya muungano rais wake ndo huyo Samia, ambae, kimsingi urais wake hautokani na Uzanzibari wake bali na Utanzania wake!!!

Na kwavile urais wake unatokana na Utanzania wake, hakuna shaka kwamba, ana haki na mamlaka ya kusimamia yale yote yanayopaswa kusimamiwa au kushughulikiwa na serikali ya muungano!!

Hoja yako ni mufilisi. Huwezi kutenganisha Urais alioupata Samia bila kuweka Uzanzibari wake.

Katiba imetamka, Rais akifariki, Makamu( ambaye ni lazima atoke Zanzibar) anarithi kiti. Sasa unatenganishaje haya mawili.

Lakini hoja yangu sio Samia kuwa Rais wa JMT. Hoja yangu ni Samia kuongoza mambo ambayo siyo ya muungano as per constitution. Over!!!!!
 
Iko hivi, hatuwezi kuacha kuhoji mambo ya muungano kwa vitisho kutoka Serikalini.

Jambo la msingi tuhoji kwa hekima na busara. Kwani huu Muungano umekua Biblia au Msahafu kwamba usihojiwe??

Huyo VP mwenyewe ametokana na Katiba ambayo ndiyo tuna raise query zake hapa.

Uzalendo sio kuogopa kuhoji mapungufu yaliyopo waziwazi.

No, Never
Ndiyo maana nyie “Team Bashiru”, mulitaka mama SSH asiapishwe kuwa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Sasa ndiyo nimegundua kwanini mulitaka kufanya hivyo.

Hata hivyo, ingekuwa kinyume cha katiba kumpa urais speaker Ndugai au waziri mkuu Majaliwa kama tetesi zilivyokuwa zikisema. Nadhani tulitizame hili mama ongoze kama taasisi na siyo kuanza ubaguzi. Kama ni marekebisho, katiba mpya inaweza kusaidia kuyapata.
 
Mama ni Rais na Mungu akipenda atakuwa mwenyekiti wa kwanza wa CCM mwanamke.

Sio lazima kila kitu chetu kifanane na cha wengine duniani. Uundwaji wa muungano wetu pia hauna sababu ya kufanana na mwingine.

Kama mzee Mwinyi mzanzibari alikuwa Rais wa TZ kwanini Mama asiweze kuwa rais?.

Kama mwanae Mwinyi ameweza kuwa rais wa Zanzibar wakati angeweza kuwa makamu wa rais wa Hayati, maana yake muda huu angekuwa rais baada ya tukio la kifo.

Mama anao uhalali wa kuwa rais kama Mwinyi alivyokuwa na uhalali wa kuwa waziri wa ulinzi wa jamhuri ya muungano.

Maishani siku zote huwezi kupata ukitakacho na sio kila ukitakacho kiwe kinaweza kuja kuwa kama ulivyotegemea kukiona kikiwa.

Tujifunze kujishusha na kukubaliana na tusichokipenda, ni kielelezo cha uungwana wa hali ya juu.

Hoja ni kwamba, Tumekubaliana kuungana kwenye (mf.) Mambo ya Nje na Uhamiaji, lakini mambo ya Ujenzi na Maji hatujakubalina kuungana.

Sasa Iweje zao la muungano kutoka upande wa pili wa muungano aje kuongoza kwa mambo ya Ujenzi na Maji ambayo siyo ya muungano?

Mantiki iko wapi hapa??? Nn shida kuelewa hoja hii
 
Yeye kuwa zao la muungano haimpotezei uhuru wake wa asili wa kuwa rais wa Jamhuri ya muungano.

Alipokuwa makamu wa rais hakuwa na huo uhuru wa kushughulika na masuala yote kwa ujumla wake?.
Halafu Mama sio rais wa kwanza kutoka Zanzibar.
Haya maswali ya kipuuzi yana toka wapi leo?
 
Yeye kuwa zao la muungano haimpotezei uhuru wake wa asili wa kuwa rais wa Jamhuri ya muungano.

Alipokuwa makamu wa rais hakuwa na huo uhuru wa kushughulika na masuala yote kwa ujumla wake?.

You could have raised that query by then, ila kwa sasa usinipangie cha kuuliza. Baki kwenye hoja yangu, ila usinipangie cha kuuliza sasa au kwa nini sikuiliza kabla.
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Samia Suluhu Hassan ataongoza Tanzania kama ambavyo Mzee Ali Hassan Mwinyi alivyoongoza. Wote wana asili ya Zanzibar.

Hoja hii ingekuwa ya mjadala murua na mashiko kama ingetolewa wakati wa enzi zile za Mzee Rukhsa..kwa sasa imepitwa na wakati! Vinginevyo watu wanasumbuliwa na husda, kijicho na hiyana tu!
 
Ndiyo maana nyie “Team Bashiru”, mulitaka mama SSH asiapishwe kuwa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Sasa ndiyo nimegundua kwanini mulitaka kufanya hivyo.

Hata hivyo, ingekuwa kinyume cha katiba kumpa urais speaker Ndugai au waziri mkuu Majaliwa kama tetesi zilivyokuwa zikisema. Nadhani tulitizame hili mama ongoze kama taasisi na siyo kuanza ubaguzi. Kama ni marekebisho, katiba mpya inaweza kusaidia kuyapata.

Poor minds discuss’ people/ personalities, intelligents discuss’ issues, i think you belong to the prior
 
Samia Suluhu Hassan ataongoza Tanzania kama ambavyo Mzee Ali Hassan Mwinyi alivyoongoza. Wote wana asili ya Zanzibar.

Hoja hii ingekuwa ya mjadala murua na mashiko kama ingetolewa wakati wa enzi zile za Mzee Rukhsa..kwa sasa imepitwa na wakati! Vinginevyo watu wanasumbuliwa na husda, kijicho na hiyana tu!

Sasa una hakika gani kwamba nilikuwepo kipindi cha Mzee Ruksa? Au, what if IQ za watu wa sasa zimeongezeka kuliko kipindi chenu hicho?

Kama wewe mtu mzima hukuwa na akili za kuhoji kipindi hicho ukiwa kijana, ndo hutaki sisi vijana wa sasa tuhoji?

Oooh please!!!
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Kwanza nikurekebishe kitu kimoja, Tanganyika haijawahi kufutwa, na kama ilifutwa ni kwa Sheria gani na ya mwaka gani? Na hili ndio moja kati ya kero kubwa la Muungano wanalolilalamikia Wazanzibari kua Tanganyika ndio hio hio Tanzania. Sasa kama kweli Muungano huu una nia njema, ilikuwa mulione hilo Tokea mwanzo, kuwa jee ikitokea Raisi anatokea Zanzibar si Atakuwa anaendesha Mambo ya Tanganyika ambayo hayamuhusu. Lakini waswahili husema ukificha Chongo iko siku utaadhirika tu maana utapewa Barua usome na macho hayaoni. Kifo cha Magufuli kimewaweka Uchi, mulidhani Wazanzibari watabakia na Umakamo mpaka dunia imalizike. Sasa Option ni Mbili aidha Mukubali matoke mumuachie Mama Samia aongoze kama anavyopenda, au Badilisheni Katiba Zanziba iendeshe Mambo yake, na Tanganyika iendeshe ya kwake na Tukutane kwenye Bunge la Muungano, na Uraisi tutapokelezana kwa zamu
 
Hoja ni kwamba, Tumekubaliana kuungana kwenye (mf.) Mambo ya Nje na Uhamiaji, lakini mambo ya Ujenzi na Maji hatujakubalina kuungana.

Sasa Iweje zao la muungano kutoka upande wa pili wa muungano aje kuongoza kwa mambo ya Ujenzi na Maji ambayo siyo ya muungano?

Mantiki iko wapi hapa??? Nn shida kuelewa hoja hii
Unafiki wa Watanganyika hasa wana green ndiyo tatizo kubwa. Kila zilipo kuwa zikiletwa hoja za maslahi ya Tanganyika, watu walikemewa na kufungwa midomo. Watu hawa wliamini Zanzibar ni koloni la Tanganyika, na hawakutaraji kama kuna siku Rais atatoka Zanzibar.
Sasa mambo yame badilika. Hoja hizi hazitokani na nia ya kweli ya kuboresha muungano au kuhitaji uwepo wa Tanganyika, bali ni choyo na uroho wa madaraka. Kitumbua kimeingia mchanga.
Hayati mtikila alihubiri juu ya udhaifu wa muungano waziwazi lakini aliishia kuoneka mwehu.
 
Hakuna anayempinga Mama kutawala, jielekeze kwenye hoja. Je? Kuna mahala nimeongea uongo?
Wewe unajikanganya hapa, kama unasema hakuna anayepinga Bi Mkubwa kutawala Tanzania hii hoja kwa nini umeileta hapa? Na kwa nini umeileta baada ya kifo cha Dikteta ?, na kwa nini hukuleta hoja sababu ipi CCM imemteua VP mwenye asili ya zanzibar, je ulikuwa hujui kama Rais atashindwa kutimiza majukumu yake kwa ugonjwa au kifo makamu wake ndiye ataapishwa kuwa Rais. Wewe hilo ulikuwa hulijui? Na kumbuka katiba ya mzee warioba ilipendekeza mfumo wa serikali tatu lakini haikupendekeza asili ya mtu ametokea wapi sababu ya kuepusha ubaguzi, kumbuka pengine labda utoto tu unakusumbua kule Zanzibar Raia wengi wana asili ya Bara ambao walipelekwa kulima mashamba ya karafuu pemba ambayo yalimilikiwa na waarabu. Kifupi Mwl. Nyerere ndiye aliyemshawishi Hayati Mzee karume waungane baada ya karume kuomba msaada wa kuunganisha tabaka mbili la wapemba na waunguja ambao wana asili ya bara, suala la vita baridi ilikuwa ni kisingizio tu. Na baada kuondolewa utawala wa sultan Jamshid bin Abdulla mwaka 1963 Mzee karume aliwataka Wazanzibar weusi na weupe (waarabu) waoane ili kuondoa chuki baina yao iliyotokana na kukandamizwa kwa watu weusi. Hivyo kwa muktadha wa huko tulikotoka hakuna mtu anayeitwa mzanzibar wala mtanganyika wote sisi ni waTz. Hoja yako haina mashiko bali unataka kutugombanisha
 
Poor minds discuss’ people/ personalities, intelligents discuss’ issues, i think you belong to the prior
Aren’t you discussing Samia instead of the president as an institution? I don’t wanna argue with a fool. This one is a jab under a belt.
 
Hoja iko wazi na inahitaji wachangiaji
Tatizo jukwaa naona limepungukiwa na watu wafuatiliaji wa mambo na wenye kuijua historia na katiba ya nchi.
Lakini kutwa wakidai katiba mpya ili hali iliyopo hawaijui.
Kwa upande wangu nakiri kabisa kuwa, licha ya ueledi mkubwa wa baba wa taifa Hayati Mwl. JK Nyerere aliokuwa nao lakini kuna sehemu alifanya pasipo kujua madhara yake hapo baadae ijapo siwezi kulaumu sana kwani huenda alikuwa na nia njema tu kwa wakati huo.
Suala la katiba hususani upande wa mambo ya Muungano, kuna pahala sijui alizidiwa kete na Mzee Karume ama ilimbidi tu akubaliane na baadhi ya vipengele kwa sababu aliihitaji sana zanzibar minimume na zanzibar kutuhitaji sisi zaidi. Ndipo akajikuta anakubaliana na huu uwenda wazimu wa baadhi ya vipengele vilivyomo ndani ya katiba.
Moja ya mambo ya hovyo kabisa pamoja na
1. umiliki wa ardhi, ajira za umma ikiwa ni pamoja na mamlaka za juu za serikali, 2.kodi na ushuru bandarini, mgawanyo wa mapato kwa usawa ili hali kuna tofauti kubwa ya idadi ya watu baina ya hizi pande mbili,
3. uwekezaji,
4. mamlaka ya uongozi wa zanzibar kwa maana ya kiti cha rais,
5. Vitambulisho vya kitaifa,
Mimi nafikiri huu muungano inaonekana wazi kabisa kuwa watanganyika ndio tunaoutaka zaidi kuliko kwa wazanzibar wenyewe na ndio maana wanaendelea kutunyonya zaidi pasipo usawa ili pengine tusalimu amri wenyewe na tuwaachie kisiwa chao wajitawale.
Hata hivyo Mama inaonekana kabisa kuwa anataka atumie mamlaka aliyo nayo kwa sasa kuinyonya Tanganyika vilivyo kwa kufanya mambo pasipo kuzingatia uwiano wa idadi ya watu baina ya hizi pande mbili za muungano.
Hata hivyo sisi watanganyika imefikia hatua sasa ya maamuzi magumu ya kujitoa katika pingu hii ya kinyonyaji ya muungano na tuwaache wajitawale wanavyotaka wao na sio kuendelea kutuona machoko tusiojitambua kwa minyororo ya baba wa taifa.
Haileti sensi mzanzibar anakuwa Rais wa JMT ili hali hajui ata tamaduni z mtanganyika na kero zake,
Anakuwa DC, RAS, DED huko karagwe, musoma ama Maswa kweli, hivi huyu anayajua matatizo ya msukuma, mjita, mkurya, mhangaza kweli? Uongo mbaya,
Ndio maana ata yeye Mh Rais SSH hana mda tena kudhurura kujichosha na na Watanganyika asio kuwa na maslahi nao.
Hapa ni kwamba kufanyike maamuzi magumu tu, hamna kukumbatia muungano usio kuwa na tija kwa watanganyika zaidi ya kunyonywa na wazanzibar wachache.
 
Back
Top Bottom