Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Waulize wakubwa kiumri waliokuwepo wakati huo ili uweze kupata kuyajua mengi yenye manufaa.

Tulikuwa na dunia mbili ndani ya moja, ile ya kibepari na kijamaa na zote zilikuwa na mivutano mingi.

Walipoamua kuungana walitazama masuala kama hayo. Haikuwa dunia kama hii ya sasa ya simu za viganjani.

Kwa akili gani walizonazo kuwa wao wajichukulie tu maamuzi ya nchi zote bila ya kushauriana na wengine?
 
Kakuhadithia nani hili jambo?

Unajua kuwa Zanzibar na Oman walivunja undugu baada ya kifo cha Seyyid Said? Wapi na wapi Oman walitaka kumsaidia Jemshid? Kakaa miaka na miaka Uingereza hakurudi Oman ila majuzi tu halafu useme alitaka kumsaidia?

Tuseme tu, Karume alikuwa na khofu matokeo yake kajiingiza mtegoni maskini, nchi ndo imeenda kudidimia kwenye Muungano.

Mkuu huyo dada yetu mchukulie poa tu, Sijui kadanganywa na nani kabisa hizo pumba, msamehe tu
 
Kwa akili gani walizonazo kuwa wao wajichukulie tu maamuzi ya nchi zote bila ya kushauriana na wengine?
Mkuu mwaka 1964 nchi hii ilikuwa bado ni pori.

Hakukuwa na hizi taasisi za kidemokrasia kama za leo. Pia nchi changa zilikuwa haziwezi kupinga matakwa ya wakoloni.

Tukijiweka katika nafasi za Nyerere na Karume ndio tunaweza kuelewa maana ya maamuzi ya kuwa na muungano.
 
Mkuu mwaka 1964 nchi hii ilikuwa bado ni pori.

Hakukuwa na hizi taasisi za kidemokrasia kama za leo. Pia nchi changa zilikuwa haziwezi kupinga matakwa ya wakoloni.

Tukijiweka katika nafasi za Nyerere na Karume ndio tunaweza kuelewa maana ya maamuzi ya kuwa na muungano.

Kushindwa hata kushauriana na Mabaraza ya mawaziri?

Hawa walikua ni Madikteta tu mkuu, acha kuwatetea
 
Kushindwa hata kushauriana na Mabaraza ya mawaziri?

Hawa walikua ni Madikteta tu mkuu, acha kuwatetea
Ndio maana nikakwambia dunia ile sio hii ya leo.

Kumbuka kulikuwa na ushawishi mkubwa wa mataifa yaliyotutawala na tulikuwa ndio tunaanza kujitawala. Hizi taasisi Za leo hazikuwepo, hao wasomi wenyewe hawakuwepo sembuse wenye mawazo yenye kuweza kuleta tija za kitaifa!.

Halafu visiwani na huku bara watu ni wale wale asili zao ni zile zile usidanganywe na hizi serikali ukadhani watu ni tofauti.

Waliojaa unguja na pemba ni wamakonde, wanyamwezi na watu wa asili ya mwambao wa pwani.
 
Ndio maana nikakwambia dunia ile sio hii ya leo.

Kumbuka kulikuwa na ushawishi mkubwa wa mataifa yaliyotutawala na tulikuwa ndio tunaanza kujitawala. Hizi taasisi Za leo hazikuwepo, hao wasomi wenyewe hawakuwepo sembuse wenye mawazo yenye kuweza kuleta tija za kitaifa!.

Halafu visiwani na huku bara watu ni wale wale asili zao ni zile zile usidanganywe na hizi serikali ukadhani watu ni tofauti.

Waliojaa unguja na pemba ni wamakonde, wanyamwezi na watu wa asili ya mwambao wa pwani.

Kuwa ni watu wenye asili moja sio hoja ya kulazimishwa kuwa lazima wawe taifa moja
 
Ndio maana nikakwambia dunia ile sio hii ya leo.

Kumbuka kulikuwa na ushawishi mkubwa wa mataifa yaliyotutawala na tulikuwa ndio tunaanza kujitawala. Hizi taasisi Za leo hazikuwepo, hao wasomi wenyewe hawakuwepo sembuse wenye mawazo yenye kuweza kuleta tija za kitaifa!.

Halafu visiwani na huku bara watu ni wale wale asili zao ni zile zile usidanganywe na hizi serikali ukadhani watu ni tofauti.

Waliojaa unguja na pemba ni wamakonde, wanyamwezi na watu wa asili ya mwambao wa pwani.

Unakimbia uhalisia mkuu, Nyerere na Karume walikua na madikteta. Sijui kwa upande wa bara Lakini Zanzibar kulikua na wasomi wa kutosha wakutoa maarifa na wengi walionekanwa wazi kutokubaliana nalo tokea mwanzoni. Jaribu kusoma historia vizuri.
 
Unakimbia uhalisia mkuu, Nyerere na Karume walikua na madikteta. Sijui kwa upande wa bara Lakini Zanzibar kulikua na wasomi wa kutosha wakutoa maarifa na wengi walionekanwa wazi kutokubaliana nalo tokea mwanzoni. Jaribu kusoma historia vizuri.
Afrika yote ya miaka ya 1960 wakati wa kupatikana kwa uhuru iliongozwa na viongozi madikteta. Tatizo mimi na wewe hatukuwepo duniani.

Ukiwasikiliza waliokuwepo kwa maana ya Baba na Mama zetu utaelewa ni kwanini iliwabidi wawe madikteta.
 
Afrika yote ya miaka ya 1960 wakati wa kupatikana kwa uhuru iliongozwa na viongozi madikteta. Tatizo mimi na wewe hatukuwepo duniani.

Ukiwasikiliza waliokuwepo kwa maana ya Baba na Mama zetu utaelewa ni kwanini iliwabidi wawe madikteta.

Hakuna sababu za msingi Zaidi ya uchu wa madaraka na kujiona bora kuliko wenzao
 
Acha ubaguzi kijana. Kumbuka ukaribu uliopo kati ya Tanga na Pemba, kati ya Dar na Unguja.

Hivi mtu kudai haki yake nalo ni ubaguzi?

Je pia unakumbuka ukaribu uliopo baina ya TZ na Kenya au Uganda mbona hakuna muungano wa nchi?
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Mara zote wanaotaka muungano uangaliwe upya huwa natamani kupata na kujua hatima ya nchi yao yaani Tanganyika. Nikiwa mtanganyika ambaye nafanya kazi Zanzibar nachelea kusema ukiwa huku ndo utajuwa kwa undani kuwa kuna Tanganyika. Kwa nini ikiwa wewe ni meneja ukamwajibisha mfanya kazi usishangae kuona kamati nzima nzima ya ulinzi na usalama asubuhi imehamia ofisini kwako. Hoja wanayokuja nayo ni nyepesi tu kuwa hutaki kufanya kazi na wazanzibar.
Kitachofuata utafuatilia mara utaambiwa siyo mtanzania na hapo ndo utashangaa kuona mzanzibar anahoji Uraia wa Mtanzania.
Ukitoa tenda kwa kampuni yenye makao yake bara utashangaa.
Maajabu zaidi ni pale utakapokamatwa kwa kuendesha gari ukiwa na leseni ya jamhuri ya muungano ili hali polisi anayekukamata amevaa crown ya jamhuri ya muungano nawe leseni yako ni ya jamhuri ya muungano. Ukiuliza hapa niko wapi? Siko ndani ya jamhuri ya muungano? Utaambiwa leseni si suala la muungano, lkn ukirudi kwenye mambo 22 ya muungano kuna usalama, polisi na usafirishaji. Leseni inaangukia kwenye hayo yote.
Huu muungano una mashaka matupu,
 
Hicho ni kiburi kinakusumbua mkuu, Dunia haipo hivo kabisa. Lolote linaweza kutokea ndani ya dunia.
Rais Samia anayo haki ya kuiongoza Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Amezaliwa Unguja ambako ni sehemu ya Tanzania.

Na leo kakabidhiwa CCM yenyewe. Mada nyingine ni kupoteza muda tu.
 
Muundo wa muungano uliopo ni kaburi kwa Tanganyika
(Umeifanya Tanganyika kuwa ya kunyonywa na kutawaliwa na Zanzibar)
  • Zanzibar haichangii gharama za uwekezaji na uendeshaji ila mgao wa mapato, faida, bakaa inapata
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kumiliki ardhi ila bara wazanzibari wanajitwalia tuu
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kuajiliwa SMZ lakini wazanzibari wanaajiliwa mpaka ualimu na ajira za kada ya afya
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kugombea uwakilishi ila bara wanagombea tuu
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anaeteuliwa kushika nafasi za uongozi kwenye serikali ya Zanzibar ila bara wanateuliwa kuwa ma DAS, DED, DC, RAS, nakadhalika
Tunalalamika sn km muungano umeanza leo.
 
Kiukweli Tanzania bara hatukuchulia hili serious ila sasa katiba imetupiga ndo tumeshtuka, iweje ss tusiwe na haki yoyote kwenye serikali ya smz ila wao wawe la loophole ya kutuongoza. Hapa umuhimu wa katiba mpya unahitajika.
 
Ningependa kujua hili.

Mh rais Samia ni raia wa nchi gani?
 
Back
Top Bottom