Je, Rais Samia kutoa kauli ya "Mwanaume ni yule anayejiamini" ni kijembe Kwa Hayati Magufuli?

hahahahahaba ni Jf tuu ndio unaweza kukuta mada kama hii! Yani uwambie watu unakuja kuwaadithia adithi ya “Magufuli ajiamini” lazima wakucheke hata Samia mwenyewe anajua hilo bila kumsahau Mbowe…wote waliufyata mtu pekee ambaye alikuwa anakwenda sambamba na Magufuli ni Lissu pekee wengine wote ni kuufyata kama mbuzi😂😂😂😂
 
Mareem alikuwa hajiamini katika kushindanisha hoja ndomana hakutaka hata ushauri toka kwa wenye maarifa bali alitumia mabavu mengi na akili kidogo! Hakujiamini maskini, aliamini kwenye kutumia cheo alichobahatisha
 
Kama ni hivyo basi na yeye ni mwoga..kwanini arushe vijembe kwa mtu aliyekufa?? Mleta mada ACHA ramli za uchonganishi
 
Hebu jaribuni kumwacha huyu mtu apuumzike basi na yeye anafamilia huku alikoacha! si busara kumuhusisha Rais na Magufuli kwa wakati huu.
Hebu tuishi leo tunaweza kusonga mbele kuliko kuwainulia hasira na visasi kila kukicha vya hawa Watanganyika ambao kila kukicha wanaporwa kila kitu chao zikiwemo ajira na raslimali walizojaliwa na MWENYEZI MUNGU na madalali wanasimamia ni kati ya watu tuliowaamini na kuwapa madaraka
 
Mkuu masuala mengine yapotee! Ikiwa kila suala (hoja) unataka tukutane hapa tulijadili hata lile dogo kama hili "haipendezi". Lete HOJA mzito tuzijadili kwa faida ya Nchi.
Lema aliondoka Nchini kutokana na mazingira yaliyokuwepo wakati huo akaona inamlazimu kuusalimisha uhai wake. Bwana Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, inawezekana na yeye alibanwa vilivyo lakini ndio Kiongozi Mkuu wa chama kinacho lengwa ili kisiwepo katika ardhi ya TZ; ana kiachaje na yeye ndie Jemedari Mkuu. Mwengine ni wewe na mimi wenye majina butu humu JF tunachangia hoja kwa kificho, haya kuna walionunuliwa na kupewa vyeo na wengine hawa wa "19 members" Haya wewe kwa mtazamo wako nani "MWANAUME ANAYEJIAMINI"
 
Kwani magufuli ndo alihamia huko kanada
 
Mwanaume aliyeogopa mikutano ya siasa ni mwanaume wa ajabu sana.
 
Then akavuna Tril 199
😅😅
 
Linapokuja swala la kulinda madaraka hakuna anayejiamini.

Hata yeye alimpa za uso Ndugai ,pole pole, lukuvi na prof. Kabudi.

Kalemani nae akala buyu.

Wote hao ni woga tu.

Sisi wenyewe hapa tunaandika tu lakini tunasali yasije tukuta siku moja.
Ila jpm woga ulizidi kiwango. Akajikuta anataka vyombo vyote vimsaidie
 
hiyo haina mantiki yoyote kuhusu jpm mtoa mada umeipachika kwa nguvu tu ili usikie watu wasio kuwa na akili wakimchambua jpm, mh samia alikuwa anamaanisha lema kuwa anajiamini alipoambiwa arudi asiwe na hofu akarudi sio
lissu
 
Kufuru aliyofanya jpm itabaki kwenye historia
 
Ukiacha tu kujiamini alikuwa na msimamo kitu ambacho wengi hawana
 
Kuwa makini na maneno yako nisijelazimika kufungulia mchwa na nguchiro!
 
Mkuu wewe nikisoma mada zako ambazo hazina mlengo wa kisiasa huwa uko vizuri sana na wajua mambo mengi, lakini unapomzungumzia jiwe yani nikama wajizima data. Hivi unajua kweli ujinga aliofanya kwenye nchi hii??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…