Je, sheria inaruhusu kumuua mtuhumiwa wa ujambazi asiye na silaha anayewakimbia Polisi?


Kama uko serious kwa hiki ulichoandika weka kifungu cha sheria kinachoelekeza namna ambavyo polisi ata deal na mtuhumiwa anayekimbia au matumizi ya silaha kwa polisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Adhabu ya kukimbia sio kifo Ila mazingira ya kukimbia yanaweza kupelekea kifo.

Sent using Jamii Forums mobile app
But is it necessary katika mazingira niliyotaja? mtu hana silaha na anakimbia away from you, why kill him? na kwanini walivyomtoa kituoni hawakumfunga pingu mikono kwa nyuma? mtu aliyefungwa pingu anaweza kukushinda mbio? balance ya kukimbia anatoa wapi? Hii ishu ina maajabu mengi sana, tutajua tu ukweli
 
Kwahiyo mtuhumiwa ameshageuka jambazi tena? Hivi maana ya mtuhumiwa ni nini? Na hata kama ni jambazi, adhabu ya kukimbia ni kifo? kwa hukumu ya mahakama ipi?

Raia mwema kwa kawaida huwa hawezi kukimbia akiamriwa na askari mwenye silaha. wengine hata haja ndogo huwatoka wanapoamrishwa hivyo.

Miaka mingi iliyopita nikiwa ninaendesha gari maeneo ya mwananyamala nilitoka kwenye starehe na nikamsindikiza rafiki yangu nyumbani kwake.

Kabla sijafika mbali nilisimamishwa na askari wa doria ambao walikuwa na Landrover 110. Nilisimama lakini mitutu ya bunduki kama 10 hivi ilikuwa imelengwa kwangu. Nilitoka mikono ikiwa juu [pombe zote ziliyayuka]. Wakanihoji kitemi kabisa nami niliwajibu kistaarabu wakaomba kadi ya gari pamoja na kitambulisho changu nikawapo. Baada ya ukaguzi huo waliniomba radhi na kuniruhusu kuondoka.

Baadaye nilikuja fahamishwa kuwa walikuwa wamemlia dago mtaalam mmoja wa ujambazi ambaye alikuwa na gari iliyofanana sana na yangu.[Siku ya pili nilipomhadithia rafiki yangu aliniambia kuwa jana yake baada ya kuachana nami risasi zilirindima eneo lilie kwani na kuna jambazi ambaye alikuwa anatafutwa, kwa siku nyingi aligoma kusimama na kujaribu kukimbia basi wakaamua kumwasha kwa risasi na alifia hapo hapo..
 


Asee ulivyo simama ndo ilikuwa pona yako, mara nyingi watu wanakufa kufungwa bila hatia.
 
Kwa nchi zenye utawala wa sheria haitakiwi kumpiga risasi mgongoni
ila kwa asshole nations inaruhusiwa japo sio kisheria
 
Kwa nchi zenye utawala wa sheria haitakiwi kumpiga risasi mgongoni
ila kwa asshole nations inaruhusiwa japo sio kisheria
Waambie hivyo wamarekani[ambapo wengi wenu mnasifia demokrasi yao] hivyo nao watakwambia 'you are a dead horse'
 
Sasa angekimbia si angeendelea kufanya uhalifu.
Inawezekana amekuwa msumbufu anakamatwa na kuachiwa wakaona story isiwe ndefu bora kumaliza mchezo

Hit direct to the Ntonku
 
Waambie wewe

Mimi sipo Marekani
nipo Mbezi kwa Msuguri
Umezungumzia nchi ambazo wewe unaziona zinatumia utawala wa sheria nami nikakueleza kistaarabu kuwa hata Marekani Ujerumani n.k jaribu kukimbia wakati umesimamishwa na askari mwenye silaha.
 
Ni kosa kubwa kumuuwa
Kama ni mtuhumiwa kwanini asifungwe pingu?
Hili wanalijua kabisa kuwa pingu ni moja ya zana walizopewa kuzitumia sasa iweje hazitumiwi? Au kama ile staili ya USA
Mtu mweusi anaulizwa kitambulisho akiingiza mkono mfukoni wanamuwasha risasi
Kesi: He was reaching for a gun


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Polisi hataki kutoka jasho kukimbizana na mwizi.. Ukikimbia unakula shaba tu wakati huo yee yupo juu ya difenda katuloa tu
 
Umezungumzia nchi ambazo wewe unaziona zinatumia utawala wa sheria nami nikakueleza kistaarabu kuwa hata Marekani Ujerumani n.k jaribu kukimbia wakati umesimamishwa na askari mwenye silaha.
Nitajaribu usiku huu hapa maeneo ya Magogoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…