Je, sisi Waafrika hatuna akili?

Je, sisi Waafrika hatuna akili?

Ni sahihi kwa kiasi fulani anachokisema but Tatizo la Africa si watawala tu hata watawaliwa ni tatizo pia. Nikimuona Mwigulu, kibajaji, musukuma etc ninajiona mimi, nakuona wewe utofauti ni mdogo sana kati yetu. Mambo aliyoyataja mleta mada ndiyo msingi wa matatizo yetu kwa kiasi kikubwa.
 
Heri ya siku ya Uhuru Watanganyika wote.

Habari za saa wanachama wote natumai ni njema, moja kwa moja niende kwenye dhumuni la mada hii.

Mada hii inazungumzia Muafrika na akili , kama ambavyo kichwa cha mada kiulizavyo. Je, waafrika hatuna akili ?kweli au sikweli jibu langu kama mleta mada ni sikweli.

Sikweli kwamba waafrika hatuna akili, jambo ni kuwa waafrika tuna akili Ila sababu kuu ambayo inatufanya sisi waafrika tuonekana hatuna akili ni ā€œKukosa uhuru wa kuhoji mambo mbalimbaliā€.

Hari ya sisi waafrika kukosa uhuru wa kuhoji mambo mbali mbali inaathiri mpaka uwezo wetu wa kufikiri, uwezo wa kufikiri ukiisha athirika usitegemee jamii hiyo kuwaza vitu mbalimbali kitofauti kulingana na jamii inavyo vitafsiri.

Uwezo wa kuhoji wa waafrika waliowengi umeathiriwa na mambo yafuatayo:-
i, Elimu isiyo bora
ii, Dini/ kasumba ya dini
iii, Tamaduni mbalimbali
iv, Mifumo ya Kiutawala

Haya ni baadhi ya mambo makuu yanayo minya uhuru wa kuhoji wa mwafrika kitu ambacho hupelekea kuathiri uwezo wa kufikiri wa mwafrika na kupelekea kuonekana kama ni mtu asiye na akili.

Mpaka sasa waafrika hatujawa tayari kupambana na haya mambo yanayo minya uhuru wetu wa kuhoji kitu ambacho kina athiri uwezo wetu wa kufikiri kwa kiwango kikubwa.

Jamii yoyote inayo kosa uhuru wa kuhoji baadhi ya mambo ni ngumu kutambua baadhi ya mambo kwa kina na kwa ubora zaidi.

Waafrika tuta endelea kutambulika na jamii mbalimbali za duniani kama ni watu tulio kosa akili kama hatuta kubali kubadilika na kubadili misimamo yetu juu ya hayo mambo mbalimbali niliyo orodhesha yanayo minya uhuru wetu wa kuhoji.

Elimu tupatayo imeshindwa kumuweka mwafrika kuwa huru kuhoji mambo, tamaduni nazo zina minya uhuru wa kuhoji uhalali wa baadhi ya mambo, dini ndio kabisa zina tengeneza kizazi cha hofu kuliko kizazi cha kuwa huru kuhoji mambo, tawala nazo zina minya kwa kiwango kikubwa uhuru wa kuhoji.

Tuna safari ndefu sana kujenga kizazi bora cha mwafrika kama hatuta taka mabadiliko kwenye hayo mambo baadhi niliyo orodhesha ambayo ni kikwazo kwetu.

Karibuni kwa maoni yenu wadau.
Akili zetu ni kuwaneemesha mataifa mengine si sisi
 
Mifumo inatugandamiza tuonekane hatuwezi au hatuna uwezo...
 
Ni sahihi kwa kiasi fulani anachokisema but Tatizo la Africa si watawala tu hata watawaliwa ni tatizo pia. Nikimuona Mwigulu, kibajaji, musukuma etc ninajiona mimi, nakuona wewe utofauti ni mdogo sana kati yetu. Mambo aliyoyataja mleta mada ndiyo msingi wa matatizo yetu kwa kiasi kikubwa.
Nakuunga mikono na miguu
Nasisitiza hapa "Tatizo la Africa si watawala tu hata watawaliwa ni tatizo pia."
 
Kwa akili mmm tunazo zakuvukia barabara si vinginevyo, na mara nyingi huwa tunategemea anayenda shule akija atatutoa sehemu moja kwenda sehemu nyingine lakini uwiii[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24] ni afadhali hata waliishia kidato cha nne nakuanza kujitafutia riziki
 
Kutokana na experience, udumavu wa akili wakati mwingine tunautengeneza (create) wenyewe. Sijuwi kwa jirani zetu; Kenya, Uganda, na wengineo, lakini kwetu sisi Watanzania, mtu halijuwi jambo fulani, lakini anajifanya anajuwa.

Tabia hii imetamalaki sana miongoni mwetu, hasa vijana. Unakuta mtu hajuwi jambo fulani, na wakati huohuo yuko mtu anayelijuwa jambo hilo, badala ya kuuliza ili tujuwe, mtu anaona ataonekana mshamba na hivyo kuendelea kubaki nalo moyoni mwake na kutolijuwa jambo hilo.

Nimekaa katika vijiwe mbalimbali, mtu (mwerevu) akiuliza jambo fulani, vijana wa pale kijiweni wanaanza kimzomea na kumcheka huku wakisema 'hata hili hujuwi?'. Kwa mtindo huu, utakuta vijana wengi wanaingia woga wa kudadisi mambo, kwa kuogopa kuchekwa na kuzomewa.

Kwa wenzetu wenye akili zao, hakuna jambo dogo wala kubwa katika kuuliza; jambo lolote analotaka kujuwa anauliza ili apate maarifa. Kila siku tunasema kuuliza sio ujinga, lakini hatujuwi maana ya sentensi hii. Na kwa maana hii, hatutakuja kuerevuka kamwe, tutabaki na ujinga wetu mpaka kiama!
Ahsante mkuu kwa madini mazuri.
 
Wafrika ni sahihi hawana akili na inapaswa watawaliwe, maana haiwezekani nchi inatoa madini ya Dhahabu, almasi , tanzanite, nk kwa wingi eti nchi ina baki kuwa masikini, nchi ina mito na mabwawa ya kutosha eti umeme unakuwa wa mgao, nchi ina maziwa, bahari, na mito mingi eti bado inashida ya maji, nchi inamaliasili za kutosha maeneo mengi yasio na watu eti watu bado wanaishi nyumba za kupanga na eti serikali haina majengo eti inapanga, nchi inamaliasili nyingi na rasimali nyingi eti waliosoma hawana ajira cha ajabu nchi utakuta inawekeza mambo ya maendeleo kwa wingi Kama shule na hospitali eti inajenga lakini eti walimu na madaktari hawatoshi , hospitali na mashule yanaupungufu wa walim na madaktari wakati mtaani walimu wapo na madaktari wapo, Hivi Afrika tuna nini? Au lile andiko lisemalo " Enyi wagalatia msio na akili ni nani aliwaloga" Me nahisi hapo ni nchi za Afrika.
 
Wafrika ni sahihi hawana akili na inapaswa watawaliwe, maana haiwezekani nchi inatoa madini ya Dhahabu, almasi , tanzanite, nk kwa wingi eti nchi ina baki kuwa masikini, nchi ina mito na mabwawa ya kutosha eti umeme unakuwa wa mgao, nchi ina maziwa, bahari, na mito mingi eti bado inashida ya maji, nchi inamaliasili za kutosha maeneo mengi yasio na watu eti watu bado wanaishi nyumba za kupanga na eti serikali haina majengo eti inapanga, nchi inamaliasili nyingi na rasimali nyingi eti waliosoma hawana ajira cha ajabu nchi utakuta inawekeza mambo ya maendeleo kwa wingi Kama shule na hospitali eti inajenga lakini eti walimu na madaktari hawatoshi , hospitali na mashule yanaupungufu wa walim na madaktari wakati mtaani walimu wapo na madaktari wapo, Hivi Afrika tuna nini? Au lile andiko lisemalo " Enyi wagalatia msio na akili ni nani aliwaloga" Me nahisi hapo ni nchi za Afrika.
Asante kwa mchango wako.
 
Uhuru wa kuhoji ni jambo la msingi linalo paswa kutiliwa mkazo katika jamii zetu zilizo tuzunguka.
 
Heri ya siku ya Uhuru Watanganyika wote.

Habari za saa wanachama wote natumai ni njema, moja kwa moja niende kwenye dhumuni la mada hii.

Mada hii inazungumzia Muafrika na akili , kama ambavyo kichwa cha mada kiulizavyo. Je, waafrika hatuna akili ?kweli au sikweli jibu langu kama mleta mada ni sikweli.

Sikweli kwamba waafrika hatuna akili, jambo ni kuwa waafrika tuna akili Ila sababu kuu ambayo inatufanya sisi waafrika tuonekana hatuna akili ni ā€œKukosa uhuru wa kuhoji mambo mbalimbaliā€.

Hari ya sisi waafrika kukosa uhuru wa kuhoji mambo mbali mbali inaathiri mpaka uwezo wetu wa kufikiri, uwezo wa kufikiri ukiisha athirika usitegemee jamii hiyo kuwaza vitu mbalimbali kitofauti kulingana na jamii inavyo vitafsiri.

Uwezo wa kuhoji wa waafrika waliowengi umeathiriwa na mambo yafuatayo:-
i, Elimu isiyo bora
ii, Dini/ kasumba ya dini
iii, Tamaduni mbalimbali
iv, Mifumo ya Kiutawala

Haya ni baadhi ya mambo makuu yanayo minya uhuru wa kuhoji wa mwafrika kitu ambacho hupelekea kuathiri uwezo wa kufikiri wa mwafrika na kupelekea kuonekana kama ni mtu asiye na akili.

Mpaka sasa waafrika hatujawa tayari kupambana na haya mambo yanayo minya uhuru wetu wa kuhoji kitu ambacho kina athiri uwezo wetu wa kufikiri kwa kiwango kikubwa.

Jamii yoyote inayo kosa uhuru wa kuhoji baadhi ya mambo ni ngumu kutambua baadhi ya mambo kwa kina na kwa ubora zaidi.

Waafrika tuta endelea kutambulika na jamii mbalimbali za duniani kama ni watu tulio kosa akili kama hatuta kubali kubadilika na kubadili misimamo yetu juu ya hayo mambo mbalimbali niliyo orodhesha yanayo minya uhuru wetu wa kuhoji.

Elimu tupatayo imeshindwa kumuweka mwafrika kuwa huru kuhoji mambo, tamaduni nazo zina minya uhuru wa kuhoji uhalali wa baadhi ya mambo, dini ndio kabisa zina tengeneza kizazi cha hofu kuliko kizazi cha kuwa huru kuhoji mambo, tawala nazo zina minya kwa kiwango kikubwa uhuru wa kuhoji.

Tuna safari ndefu sana kujenga kizazi bora cha mwafrika kama hatuta taka mabadiliko kwenye hayo mambo baadhi niliyo orodhesha ambayo ni kikwazo kwetu.

Karibuni kwa maoni yenu wadau.
Wazungu ndio waliokosa Akili.
Hama, nenda huko wenzio, wanakusubiri.

Asitake kula walai
Hakuna lako hapa Afrika.
 
Back
Top Bottom