Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Tunaomba utudadavulie zaid ili tuelewe vizur chief
Kuna baadhi ya mazingira uswahilin wanaishi kizamani umwinyi mwingi,

Yaani wew henyeka ila faida mnagawana
Unakuta biashara unafanya faida huvuni ukiwa na imani kwamba biashara mtaji utaongezeka lakini matokeo ni tofauti
hapa kidogo lazima uweke biblia chini maana nguvu ya upande wa giza imebisha hodi
Na inabidi upambane la sivyo utarudi kwa mguu nyumbani
 
Mkuu umenifanya nicheke sana.
 
Duh!
 
Kuna watoto wa miaka mitano wanakuzidi akili.
 
Mawazo ya kiafrica.
 
Hapana hujasoma biblia vizur! Utajir ni mali ya Mungu aliye hai shetani hana utajili wowote ule! Sitaki kuandika mengi Ila watakuja walio na ufahamu zaidi ya Mambo ya rohoni watakufafanulia kuna memba humu anaitwa "kalunya" huwa namfatilia anaweza akakufungulia code za rohoni kwa ufahamu wake!
 
Pesa huja kwa kufanya kazi na kuwa na nidhamu na pesa.
 
Ukimuomba Mungu utaambiwa maisha ni mafupi hapa duniani, tafuta kwanza ufalme wa Mbinguni. Naona uzame tu kwa shetani ili uishi kwa raha hapa duniani. Siku ya mwisho huenda unaishia kama wanyama na vyote vyenye uhai, hakuna cha Mbinguni wala motoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mithali 8:18, Mungu anajifunua kupitia neno lake kwamba ukiutaka utajiri na heshima uko kwake.
Heshima anamaanisha kazi, cheo etcView attachment 2005354
hapo sawa naona ulitaka kupingana ma maelezo yako hapo mwanzo kuwa shetani ana utajiri! nataka nikuhakikishie Shetani hana hata utajiri na hatoi utajili...Huo alionao anaowapa watu wake ni kiini macho tu na ndo maana mtu akikosea masharti tu huwa unapukutika na kumwacha mtu fukara wa kutupwa kama sio Mauti!

Mungu alivyomtupa duniani hakumnyang'anya nguvu na ndo hizo anatumia kupotosha watu..Ila kama hujajiungamanisha na shetani Mshukuru sana Mungu.

Na nikuhakikishie shetani hana urafiki na binadamu!
 
Hizo ni imani tu, inategemea mtu anaamini kipi kati ya giza au mwanga.
 
Du kwa hiyo matajiri wote hela zao za mashetani? Mbona wengine ndo viongozi church kwangu
 
Niwape ushuhuda ulionitokea ktk kabiashara kangu ka stationery! kuna mteja mmoja ilikuwa akifika yeye kupata huduma jioni nikifunga hesabu zangu nakuta kuna upungufu wa pesa! ikawa hivyo kwa takribani miezi miwili kila anapokuja yeye tu kupata huduma hesabu zangu hazikai Sawa!
Nikamshirikisha rafiki yangu mmoja juu ya hilo, akanicheka sana akaniambia "kuibiwa kwa nguvu za giza kupo na huyo anakuibia kwa nguvu hizo ila ntakusaidia" kesho yake akanipa kitu flani ktk bahasha akaniambia nikiweke ndani ya droo nnapoweka pesa za mauzo, huwezi kuamini toka nimeweka hicho kitu yule mteja amekatika kabisa kuja bandani kwangu anapita kwa mbaali[emoji3][emoji3], nikagundua hakuwa mtu mwema!
 
🤣🤣🤣🤣
 
Ushakuwa mshirikina tayari
 
🤣🤣🤣
 
Lyamba lya mfipa sio mji kwanza
 
Mtumishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…