Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Wewe una maarifa upande wa pili.
Kwa upande wa Mungu mafanikio yanawezekana kama ukiwa muombaji na mtoaji na utakatifu, inawezekana kabisa.
Bila Baba yangu mzazi(marehemu sasa) alikuwa mchungaji, yeye nilipomwambia nataka niwe mjasiriamali, aliniambia kabisa mwanangu please kaajiriwe, sababu utaashia kuwa mshirikina tu, na itakuwa aibu mtoto wa mchungaji kuwa mshirikina.
Nikamwambia baba sitaenda kwa mganga.
Akaniambia ukitaka kuwa mfanyabiashara inabidi uache huo ulokole wa kusali jumapili, inabidi uwe muombaji wa kila siku.
Nikaanza biashara na ulokole wa kuunga unga kilichonipata, niliuza mpaka gari yangu, kiwanja changu nilivyovipata kwenye ajira, baba yangu akaniambia, nilikuambia mwanangu rudi kwenye ajira, biashara inahitaji uchawi sana au muombaji sana.
Kwa mara ya kwanza nikaanza kufunga na kuomba.
Unajua Nini nilifunga siku 30 ili nirudi kwenye biashara again....
Nilifanikiwa lakini ilinichukua almost 3 years kurudi kwenye ramani.
Leo hii, mimi siwezi kufungua duka bila kupitia Kijitonyama KKKT, kusali misa ya asubuhi. Ijumaa lazima niende kwenye mkesha, yale yale aliyoniambia baba yangu ilinidi nikubali ili biashara iende
Kumbe kkkt mpo vizurii hivoo nilifikiri huwa hamnaga maombii ya hivo
 
Hayo magari ya mizigo unayoyaona na mabasi ya abiria unayoyaona kuna 90% wamiliki wake NI matajiri wa WAGANGA.
Sawa mganga wao ila kama ni nadharia ni vyema ukajituma tu kufanya kazi kwa bidii. Hivi vitu vinafanywa bila ndumba mkuu
 
Limbwata sio uchawi wa kumtanya mwanamke apate mume, lah hasha. Limbwata anafanyiwa mume awe bwege, asitamani mwanamke mwingine,mshahara wote apewe yeye mwanamme.
Liko aina tofautitofauti kutokana na sehemu tofauti.
Ni kulishwa uchafu tu usiozingumzika hapa.
Kuna mtu aligundua alichokishwa kidogo atapike Hadi maini
Jua tu wanawake sio watu.
Huo uchafu unaufanyaje mwili mpk u akua Zuzu?
 
Kwenye maandiko kuna sehemu wanasema wakati mwana wa adamu amezaliwa, kuna nyota ilikuwa inang'aa juu upande wa mashariki; na watu mbalimbali walikuwa wakiifuatilia ile nyota ili waweze kumfikia mtoto aliyezaliwa. Wanachofanya wakulungwa ni kukutengeneza wewe kuwa kama ile nyota, na matokeo yake hela zinakuwa zinakutafuta wewe popote ulipo na si wewe kuzitafuta hizo hela. Kumbuka zile hela zinazokuja kwako kuna sehemu zinakuwa zimepungua, yaani mwingine anapoteza mwingine anapata. Swali la kujiuliza, zinatokajetokaje huko ziliko na kuja kwako?
Ile c elimu ya unajimu tu ambayo haina uchawi wala nini, ni elimu ya nyota just about Outer Space! So, sioni uchawi wowote hapo.
 
Sizungumzii kwa wengine, ila kwangu binafsi.

Nafanya biashara ya kifedha (za mtandao na benki). Mwaka 2018 nilipigwa tukio na wakulungwa wakaondoka na 28+ Million cash, simu na mashine za benki.

Nilimpigia simu mama yangu kumueleze maswaibu yaliyonipata. Alishangaa sana nimesurvive vipi zaidi ya miaka 5 bila kuzindika eneo langu la biashara.

Akanitaka niende nyumbani kwa mwitikio wa haraka. Baada ya kuandika maelezo polisi, jioni nikazama nyumbani.

Akanipeleka kwa mzee mmoja. Wala siyo mchawi, ila ni mtaalamu wa kuzindika.

Kuzindika siyo uchawi. Nikampeleka mjini. Akafanya yake akarudi.

Nimeshakosa majaribio matatu ya kuvamiwa.

Na ripoti zote nazipata kutoka polisi. Wakivamia na kukamatwa, wakihojiwa wanasema walipanga kuja kuniibia. Ila mikakati yao inafeli.

Zindiko ni muhimu sana.
Vp milioni 28 uliipata au walisepa nazo mazima
 
Mkuu biashara nyingi zimezindikwa na zimepigwa kalilio la kivutia wateja, hakuna biashara mjini zinaenda kwa uzoefu . Mjini kuzito sana ,
acha fix ndugu, mbona mimi biashara zangu zinasonga vizuri tu na wala situmii hayo unayotaka kuwaaminisha watu.
 
Mkuu biashara nyingi zimezindikwa na zimepigwa kalilio la kivutia wateja, hakuna biashara mjini zinaenda kwa uzoefu . Mjini kuzito sana , last weekend nilitembelea night club flan hivi chugga nilishangaa nilipoingia mwili ulisisimka sana hata watu niliowakuta hawakuwa wakawaida na cha kushangaza club nzima nilikutana na sura ngeni halafu zinafanana we acha tu. Kipindi nipo mwanza niliwahi kuwa na mwenyeji alinisimulia mambo mengi kuhusu biashara na nguvu za Giza zinavyotumika . Duniani ni mapito tu kila mtu ashinde mechi zake kwa juhudi au kubebwa.Mjini kuzito sana , nenda kwa mfano hapa Arusha , soko kuu, Kilombero au maduka ya stendi ndogo Kama uko vizuri na Kinga za jadi utaona mengi . Wamama wa Kilombero ni nomana hata wale wauza matunda Kilombero .
kwenye masoko ndo balaaa, uchawi unatumika sana
 
Ungewaona wamama wanaotuuzia vitafunio wanavyotufanyia walah tungekua tunakula mikate tu.
Kama amem target mteja Fulani Basi baada ya kupika Ile chapati ya kwanza anavua chupi na kuiweka Ile chapati kwenye kigoda chake na kuikalia akiwa hajavaa chupi Wala Nini. Kaka hiyo chapati ukiila umekwisha.
Kuna msomi mmoja mzuri tu alimuachia mkewe msomi mwenzake na kumuoa mdada aliyekua anahudumu kwa mamake mama ntilie.
 
Binafsi nilipomaliza chuo nilikuwa na wasiwasi sana juu ya kazi.Hali hii ilinipelekea kupata mawazo na kukosa amani.Siku moja niliamua nijikite katika maombi. Nilianza kusali asubuhi kabla ya kuamka ,mchana nikipata nafasi baada ya kazi za kawaida na jioni kabla ya kulala.Niliendelea kusali muda kama mwezi mmoja.Lakini pia hapo ikumbukwe natuma cv za kuomba kazi.Siku moja mama aliniambia ameota nipo ofisini na bosi wangu ni mhaya. Haikuchukua muda sana kuna sehemu niliapply wakanipigia simu niripoti kwa ajili ya usaili wa kazi.Nilifunga safari kwenda kuanza usaili bahati nzuri nilipita kwenye usaili na kupewa mkataba.Kwa mshangao pia nilikuta bosi ni mhaya kama mama alivyoniambia.Inawezekana kufanikiwa kupitia sala Mungu yuko juu ya watu na viumbe vyote
Baada ya kupata kazi uliendelea kumcha bwana na kudumu kwenye maombi kama awali? Au ndio Wagalatia 3:1
 
Binafsi sipingani na wanaokubaliana kuwa uchawi ndo kila kitu ktk biashara...
Ni vigumu sana mtu kukuelezea A to Z vile anavyozimudu na kuendesha biashara zake zaid ya kukupa maneno yaleyale ya akina motivational speakers....

Binafsi nnaendesha vijimiradi vyangu kwa namna isiyo ya kawaida. Na hio ndo njia pekee inayonifanya nipige hatua.

Then si wote wanatumia ndumba ktk biashara kwa sababu tunatofautiana kimalengo.
 
Binafsi sipingani na wanaokubaliana kuwa uchawi ndo kila kitu ktk biashara...
Ni vigumu sana mtu kukuelezea A to Z vile anavyozimudu na kuendesha biashara zake zaid ya kukupa maneno yaleyale ya akina motivational speakers....

Binafsi nnaendesha vijimiradi vyangu kwa namna isiyo ya kawaida. Na hio ndo njia pekee inayonifanya nipige hatua.

Then si wote wanatumia ndumba ktk biashara kwa sababu tunatofautiana kimalengo.
Naomba kujua hiyo namna isiyo ya kawaida.
 
Kwenye hii Dunia kama hujawahi kutwa na mauza mauza.Kaa kimya kula Ubwabwa kojoa ukaoge ulale furahia maisha yako.

Usijikute mtafitiii mwenye maneno mengi ambayo hujawahi ona wala kukutana na madhila ya hii Dunia chafu ya watu.
 
Ungewaona wamama wanaotuuzia vitafunio wanavyotufanyia walah tungekua tunakula mikate tu.
Kama amem target mteja Fulani Basi baada ya kupika Ile chapati ya kwanza anavua chupi na kuiweka Ile chapati kwenye kigoda chake na kuikalia akiwa hajavaa chupi Wala Nini. Kaka hiyo chapati ukiila umekwisha.
Kuna msomi mmoja mzuri tu alimuachia mkewe msomi mwenzake na kumuoa mdada aliyekua anahudumu kwa mamake mama ntilie.
Hivi haya ya kweli? Bado sioni nini kinamvuta... Huo ni uchafu ka takataka nyingine
 
Naomba kujua hiyo namna isiyo ya kawaida.
Ni hicho hicho unachokiwaza ww.

Haijawah kuwa rahisi kupata ukweli ndo maana nmetumia neno "namna isiyo ya kawaida"...

Inaweza ikawa n ndumba au isiwe...

Ila namna hio inaleta mvuto juu ya kile nnachokifanya, inazuia vijicho, inazuia chuma ulete, na inalinda biashara.

Watu ni wabaya
 
Back
Top Bottom