Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Sizungumzii kwa wengine, ila kwangu binafsi.

Nafanya biashara ya kifedha (za mtandao na benki). Mwaka 2018 nilipigwa tukio na wakulungwa wakaondoka na 28+ Million cash, simu na mashine za benki.

Nilimpigia simu mama yangu kumueleze maswaibu yaliyonipata. Alishangaa sana nimesurvive vipi zaidi ya miaka 5 bila kuzindika eneo langu la biashara.

Akanitaka niende nyumbani kwa mwitikio wa haraka. Baada ya kuandika maelezo polisi, jioni nikazama nyumbani.

Akanipeleka kwa mzee mmoja. Wala siyo mchawi, ila ni mtaalamu wa kuzindika.

Kuzindika siyo uchawi. Nikampeleka mjini. Akafanya yake akarudi.

Nimeshakosa majaribio matatu ya kuvamiwa.

Na ripoti zote nazipata kutoka polisi. Wakivamia na kukamatwa, wakihojiwa wanasema walipanga kuja kuniibia. Ila mikakati yao inafeli.

Zindiko ni muhimu sana.

Huu ni utopolo.
 
Kaka mali ya duniani yote ni ya shetani, huu ni ukweli mchungu.
Hao mabilionea lazima uingie makubaliano na shetani au Mungu ili uwe bilionea.
Kwamba ile top ten ya dunia yotee ina makubaliano?

#YNWA
 
Ngoja nikupe elimu kidogo kuhusu utajiri
Kwanza kuanzia Leo utambue hili, Mungu alipomuumba Adam na Eva aliwapa utajiri wote wa duniani na fahari zake wazimiliki, lakini walipohasi kwa Mungu kwa kumsikiliza shetani, utajiri wote wa duniani ukawa ni Mali ya shetani, wanadamu hatumiliki tena utajiri wa hapa duniani.
Sasa ili kuwa tajiri una options mbili tu
(1) umuombe shetani akupe sehemu ya utajiri anaomiliki, hii inawezekana kama ukikubaliana na masharti yake, na siku ukienda kinyume anakunyang'anya.
(2) umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani, na hii inawezekana kama utakuwa muombaji sana na mtakatifu haswa, kumyang'anya shetani sehemu ya utajiri wake si rahisi kihivyo.

Usijidanganye kama unaweza kuwa tajiri kwa kufuata seminar za motivation speaker peke yake, utajiri wote anao shetani, ni either uungane naye au upambane kumyang'anya.


Umesema "umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani" kwanini asikupe tu hadi umuombe?

Huyo Mungu wenu anazidiwa nguvu na shetani? Sasa mnamuabudu wa nini?

Huu ulioandika ni utopolo na kwa akili hizi inabidi muanze kulipia tozo uzwazwa wenu.
 
Umesema "umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani" kwanini asikupe tu hadi umuombe?

Huyo Mungu wenu anazidiwa nguvu na shetani? Sasa mnamuabudu wa nini?

Huu ulioandika ni utopolo na kwa akili hizi inabidi muanze kulipia tozo uzwazwa wenu.
Soma Mathayo 4 : 8-10
Shetani alimwambia Yesu ukinisujudu nitakupa Mali zote hizi, Hapa shetani anajigamba mbele za Yesu Mali zote za hapa duniani ni zake.
Uliona Yesu akimbishia, zaidi ya kukataa kumsujudia?
Ongeza maarifa kijana
Screenshot_20211110-152703_Biblia.jpg
 
Sizungumzii kwa wengine, ila kwangu binafsi.

Nafanya biashara ya kifedha (za mtandao na benki). Mwaka 2018 nilipigwa tukio na wakulungwa wakaondoka na 28+ Million cash, simu na mashine za benki.

Nilimpigia simu mama yangu kumueleze maswaibu yaliyonipata. Alishangaa sana nimesurvive vipi zaidi ya miaka 5 bila kuzindika eneo langu la biashara.

Akanitaka niende nyumbani kwa mwitikio wa haraka. Baada ya kuandika maelezo polisi, jioni nikazama nyumbani.

Akanipeleka kwa mzee mmoja. Wala siyo mchawi, ila ni mtaalamu wa kuzindika.

Kuzindika siyo uchawi. Nikampeleka mjini. Akafanya yake akarudi.

Nimeshakosa majaribio matatu ya kuvamiwa.

Na ripoti zote nazipata kutoka polisi. Wakivamia na kukamatwa, wakihojiwa wanasema walipanga kuja kuniibia. Ila mikakati yao inafeli.

Zindiko ni muhimu sana.
Kweli aisee.
Nakumbuka nilipofungua Duka siku za nyuma kuna Dawa nilipewa na Shangazi yangu toka Tabora. Alisema nikiichimbia nje kwenye kona zote za Duka langu, hakuna mwizi atakaeiba kitu na hata akiiba nitamkuta hapohapo mlangoni akiwa amebeba hichokitu alichoiba, Ila akikiacha kitu cha wizi ndio anaweza kutoka.

Sasa nilikuja kuiamini ile dawa, kuna siku wezi walivunja milango na kuiba vitu kwenye eneo lile ila kwenye Duka langu nilikuta milango imevunjwa ila hakuna kitu kilichoibwa. Majirani zangu wote waliibiwa vitu.
 
Ukiona mtu amepita na chuma kipya utafikiri kimetoka kiwandani leo, Jiulize
Ukiona kwa siku mtu anauza milioni 100, 200 n.k jiulize
Ukiona mtu tajiri anavaa rafu rafu, jiulize
Ukiona mtu tajiri, biashara zake zinakuwa na misimamo, mara siku x au muda x sifungui,jiulize
Ukiona tajiri anafanya sherehe sherehe za kuchinja wanyama nyakati fulani, jiulize
Ukiona tajiri ana watoto wachache, jiulize n.k
Kuna viashiria vilivyo wazi ambavyo huwezi jiuliza mara mbili kuwa flani utajiri wake ni wa nguvu za giza. Ila usisahau pia kuna walio na ratiba zao juu siku flani kutofanya kazi; kwa mfano usishangae msabato kutofungua biashara zake Jumamosi au mkristo flani kutofungua J'pili au kwa muislamu siku ya ijumaa.
Kwa mwenye utajiri wa kichawi lazima kutakuwa na la ziada tu
 
Umesema "umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani" kwanini asikupe tu hadi umuombe?

Huyo Mungu wenu anazidiwa nguvu na shetani? Sasa mnamuabudu wa nini?

Huu ulioandika ni utopolo na kwa akili hizi inabidi muanze kulipia tozo uzwazwa wenu.
Mburura hawaishagi ndg yng, Mara Mungu Mara shetani... Wapi na wapi?
Kwa nini Mungu asitoe utajiri tu mpk masharti kibao?
 
Unachopaswa kujua tu ni kwamba inapoishia sayansi ndio uchawi unaanzia hapo kwenda mbele.
Hata huo uchawi ni sayansi sema code of universe pia tunaziita pia uchawi, mfano hata kutumia maji ya baraka au mtu achukue chumvi au mawe ya mvua aogee ataambiwa uchawi, mchawi ni mtu anayedhuru wengine iwe kwa kupata Mali au kujifurahisha huyo mtu hatakiwi kuishi anatakiwa kuuwa ila sayansi ya code of universe siyo uchawi.
 
Umesema "umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani" kwanini asikupe tu hadi umuombe?

Huyo Mungu wenu anazidiwa nguvu na shetani? Sasa mnamuabudu wa nini?

Huu ulioandika ni utopolo na kwa akili hizi inabidi muanze kulipia tozo uzwazwa wenu.
Niliwahi soma mahali kwenye kitabu kitakatifu, panasema '" vyote viijazavyo nchi ni mali ya Bwana"', sasa huyu shetani anaingiaje tena?
 
Ngoja nikupe elimu kidogo kuhusu utajiri
Kwanza kuanzia Leo utambue hili, Mungu alipomuumba Adam na Eva aliwapa utajiri wote wa duniani na fahari zake wazimiliki, lakini walipohasi kwa Mungu kwa kumsikiliza shetani, utajiri wote wa duniani ukawa ni Mali ya shetani, wanadamu hatumiliki tena utajiri wa hapa duniani.
Sasa ili kuwa tajiri una options mbili tu
(1) umuombe shetani akupe sehemu ya utajiri anaomiliki, hii inawezekana kama ukikubaliana na masharti yake, na siku ukienda kinyume anakunyang'anya.
(2) umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani, na hii inawezekana kama utakuwa muombaji sana na mtakatifu haswa, kumyang'anya shetani sehemu ya utajiri wake si rahisi kihivyo.

Usijidanganye kama unaweza kuwa tajiri kwa kufuata seminar za motivation speaker peke yake, utajiri wote anao shetani, ni either uungane naye au upambane kumyang'anya.
Kama nakusoma iviii
 
Kwenye biashara sijui Ila kwenye ndoa nakuhakikishia LIMBWATA lipo.
Ukila nyama iliyowekwa maskani kwa masaa kadhaa lazima uwehuke tu....
 
Niliwahi soma mahali kwenye kitabu kitakatifu, panasema '" vyote viijazavyo nchi ni mali ya Bwana"', sasa huyu shetani anaingiaje tena?
The universe has its own code,issue za shetani na Mungu ni man made kwa ajiri ya civilization code.na Siku civilization code imefunguka ndio utakuwa mwishi hii dunia maana haitatawalika tena.
 
k

kabla hujaomba Mungu alikua hajui

kuamini imani za kijinga za kishirikina ndio kujua vitu vingi,sumbawanga kuna matajiri wangapi
Huko sikunasifika kwa uchawi, na wachawi hawatakiwi kuishi maana wanachawia wenzao wasifanikiwe kwa chochote.
 
Kupambana na shetani ili umnyang'anye utajiri wake ni sawa na kulazimisha ngamia kupita kwenye tundu la sindano. Jibu lipo pale shetani alipompandisha Yesu mlimani na kumuonyesha utajiri wa dunia, enyi binadamu, mnahangaika nini?? Basi mtumikie shetani upate utajiri , "Amen".
 
""Africa tuko kwenye rank za juu kabisa katika mabara yenye imani za kishirikina, lakini hatujaweza kutoa hata mchawi mmoja kwenye top 10 ya mabilionea""

Mchawi ni nani? hao wachawi hua unawatambua? Kwamba maisha yao kiuchumi yapoje..?
Mchawi ni mchawia wenzake hatakiwi kuishi hata kama ni mama au baba yako atakuchawia usiendelee kwa uchawi wake.
 
Hata huo uchawi ni sayansi sema code of universe pia tunaziita pia uchawi, mfano hata kutumia maji ya baraka au mtu achukue chumvi au mawe ya mvua aogee ataambiwa uchawi, mchawi ni mtu anayedhuru wengine iwe kwa kupata Mali au kujifurahisha huyo mtu hatakiwi kuishi anatakiwa kuuwa ila sayansi ya code of universe siyo uchawi.
Code of universe inatofauti gn na Uchawi?
Naomba elezea mechanism of action Yake
 
Back
Top Bottom