Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Kuna vitu haviwezi kubadilika. Kwenda shopper kuna husiana nini na kuheshimu mwanaume au kupenda mke.

Ukiona mwanamke hakuheshimu basi ujue shida ni ww mwanaume ila because ww ni mwanaume uwezi kujiuliza ndio tatizo linaanzia hapo

Mwanamke ni kama Kioo, ukicheka kinacheka ukilia kinalia

Wanawake wa zaman hata ukizaa nje walikuwa hawana shida, wanabeba Mtoto anatulia

Mwanamke wa sasa ukizaa nje basi ujue mimba ijayo sio yako
 
Nakuelewa sana.

Maisha hatufanani mazingira.

Wazazi wametuachia vijana jukumu kubwa hili la kutafutana mke na mume kwenye dunia iliyochafuka. Washenzi wengi kuliko wastaarabu. Chuo ni sehemu nzuri sana ya kupata mwenza. Shida ajira siku hizi tunachelewa kuzipata na bila ajira kuoa ngumu maana tunatokea familia maskini. Hivyo spouse wa chuo hamtoboi..

Kuna watu wanakulia mazingira ambayo wanapata spouse kwa jirani zao tu nyumba ya pili

Kuna watu wanapata ajira zinazowafanya wawe wanakutana na watu wengi wapya wanaotafuta wenza kila siku yao ya kazi.

Mwanamke mstaarabu na mwanaume mstaarabu kukutana ni ngumu sana zama hizi kama sio majirani, ama hamjasoma shule ama chuo pamoja.

Nje ya hapo hata mkikutana mnakuwa hamna imani maana hamjuani. Kitu kidogo tu mnaachana
Umeongea uhalisia mtupu, from my experience mpaka leo hii nimeshindwa kupata mke wa kuoa sio kama hawapo, lkn imekuwa kama ile kutafutana kwa kuviziana, pia machaguzi yamekuwa kikwazo, unaweza kupata mtu wa uhakika wa kuoa/ kuolewa lkn nyodo zako zikampeperusha, tusichague sana
 
Now Maisha yamechange Sana, sio kama zaman
Watu wengi wa zaman kuanzisha family ilikuwa easy Tu ndio maana walikuwa wanazaa Sana

Mtoto anaweza Kula hata Kwa Jirani, unaweza kusafiri mwez mzima na watoto ukawaacha Kwa rafiki yako,

Kwa sasa hayo mambo hamna, watoto hawachezei tena udongo wanachezea tablet haha

So before ujapanga kuwa na family kwanza jiangalie mwenyewe na jifanyie tathimin je Una uwezo wa kulea familia?

Ela unayo bank?

Una kazi mzuri?
Facts
 
Saw we Germanchaga, sasa kama shule haipandi mtu atalazimisha tu kusoma?? Unaweza ku force shule mwishi wa siku ukazekea huko, halafu uje humu jukwanii muanze kuharibu na kuwaaminisha wengine kuwa maisha yanaanza at 40yrs.
Ushauri wako nitawapa wanangu maana mimi huko shuleni kulishanishinda.
Kama shule haipandi kuna skills kibao za kujifunza sio lazima ushinde ofisini. Unakuta kijana analalamika hakuna ajira hata kufuga kuku hajui. Dunia ya leo utakula, utalipwa na utaheshimiwa kwa lipi kama hauna skills. Lakini kusema shule haipandi napingana nalo kwa sababu hio. Hakuna binadamu ambae akili yake haiwwezi kujifunza kitu kipya ndio maana kila mtu anaweza kwenda chooni mwenyewe, na pia naweza kumbatona na kula. Kama uliweza ukajifunza hivi vitu hauwezi kushindwa kujifunza taaluma mbalimbali za maisha. Vilevile kuna scholarship nyingi sana tumepewa watanzania hatuzitumii. Maisha yapo easy sana ukiwa na elimu. Elimu ni ngumu na si lele mama, lakini ukishaelewa na kujua kuitumia maisha yanakuwa marahisi sana.
 
Habari ya weekend great thinkers?

Maisha yananipa experience tofauti, Sikuwahi kufikiria kama ningefika third floor bila kuwa na familia wala watoto, kuna muda nahisi kupanic nahofia watoto wasije kuniita bibi badala ya mama, au kukosa kabisa sababu ya umri mkubwa🤔

Enzi hizo nilikua nashangaa mtu hasa mdada unafikaje hadi 30s huna familia, aisee kumbe ni kweli now ni mimi mwenyewe.

Mlioanza familia mkiwa 30s je ni kweli au mnaona dalili za watoto wenu kuwaita bibi au babu? Vipi changamoto za uzazi sababu ya umri mkubwa?😔

Nipo tayari kwa comments zote.

Happy valentine's day in advance 👏
 
Habari ya weekend great thinkers?

Maisha yananipa experience tofauti, Sikuwahi kufikiria kama ningefika third floor bila kuwa na familia wala watoto, kuna muda nahisi kupanic nahofia watoto wasije kuniita bibi badala ya mama, au kukosa kabisa sababu ya umri mkubwa🤔

Enzi hizo nilikua nashangaa mtu hasa mdada unafikaje hadi 30s huna familia, aisee kumbe ni kweli now ni mimi mwenyewe.

Mlioanza familia mkiwa 30s je ni kweli au mnaona dalili za watoto wenu kuwaita bibi au babu? Vipi changamoto za uzazi sababu ya umri mkubwa?😔

Nipo tayari kwa comments zote.

Happy valentine's day in advance 👏🥰
Na hamu Sana ya kuingia 3rd floor naisubiri Kwa hamu kubwa
 
Kuna kitu nahitaji kuwafunza mabinti ambao hawajafika 30.

Ukipata mpenzi ukamuona ana hofu ya Mungu, maisha yake yapo wazi hasa tabia zake, anakupenda kwa dhati, yupo tayari kukutambulisha kwa ndugu zake na kwa familia yake.

Yamkini asiwe na kipato kikubwa sana ila ana uwezo wa kufanya wote mle na mkalala, ISHI HAPO.

Acha tamaa za kutaka uolewe na mwanaume mwenye pesa, anayefanya kazi TRA, bandari, mfanyabiashara mkubwa, mwenye muonekano fulani n.k mwisho mtakuja kuangukia kwa wanaume za watu au kwa wanaume ambao wataishia kukuchezea. Kumbuka sehemu kubwa ya mwanaume mwenye pesa, ngono anachukulia starehe tu, kwahiyo atakuchukua na kukutumia baada ya kukutamani akijua anapiga na kupita zake.

Binti yangu, huyo mwanaume wa mtu unayemuona ana pesa, hazijaja tu hivi hivi, alianza chini kabisa kama huyo kijana ambae kwa sasa wewe unamdharau.

Kama umewahi kumnyanyasa kijana wa watu kisa masikini, yeye sijui hana umbo zuri n.k moyo wake ukaumia, katafute suluhu naye sababu huenda kuna mambo yako yakafunguka.

Mabinti sio kwamba mnakosa watu wa kuwaoa ila tamaa za maisha zimekuwa zikiwatesa wengi. Mnapenda smartphones, kila wiki msuke, utolewe out n.k mnaishi maisha ya udangaji kisa mna uzuri wa sura au mna matako makubwa, kwa bahati mbaya sana, ukishazoea kudanga, mwanaume yeyote atakujua tu, udangaji ni kama ngozi, HAIJIFICHI na hata ukijitahidi, mtu atasikia tu stori zako.

Sasa hivi kijana wa 30, 31, 32 ambapo kwa sehemu kubwa ndo vijana wengi walau kwa sehemu wanaanza kuona mwanga ktk eneo la uchumi hawezi kuwa na mwanamke wa 30, lazima atafute wa 24, 25 au 26 unless awe mpumbavu.

Girls kuweni makini sana na umri, uliowatupa kisa hawana ela, wakipata ela na wao watakuona wewe sio hadhi yao. Tafuta kijana mwezio mtakaopendana, mtie moyo ktk utafutaji, mpende sana na kumpa heshima hata pale ambapo anapungukiwa, mwanaume huyo hatokusahau.
Hawa wanawake wanaoolewa kwenye 30's huwa wanaolewa Na wanaume wa umri gani
 
Hilo zigo lend sisi halituhusu hauna maadili utajioa hakuoi mtu
Amka mkuu zama za kuwatishia wanawake ndoa na kuitumia kama fimbo ya kuwachapia zinaelekea ukingoni wanawake siku hizi wameshaacha kutafuta furaha kwa wanaume wanaipata kwa watoto wao, fuatilia siku hizi wanawake kuwa single mothers imeshakuwa fashion wengi hawajali tena kuhusu matusi wanayotukanwa na 'jamii' (ambayo actually ni wanaume), matokeo yake wewe usipooa humkomoi mtu endelea kununua malaya fainali uzeeni mwanamke atabaki na watoto wake wewe utabaki na malaya wako
 
Life begins @ 40.
Hii ina apply kwa wenye familia tu kama huna.

Unakuwa jitu la hovyo na lisilojielewa.

Mtu huna mke, mtoto wala familia in your 40s nje ya kuwa binadamu kama binadamu wengine una kitu gani cha kuonyesha na wewe kama ni mtu wa maana ?
 
Amka mkuu zama za kuwatishia wanawake ndoa na kuitumia kama fimbo ya kuwachapia zinaelekea ukingoni wanawake siku hizi wameshaacha kutafuta furaha kwa wanaume wanaipata kwa watoto wao, fuatilia siku hizi wanawake wengi kuwa single mothers imeshakuwa fashion na hawajali tena kuhusu matusi wanayotukanwa na 'jamii' (ambayo actually ni wanaume), matokeo yake wewe usipooa humkomoi mtu endelea kununua malaya fainali uzeeni mwanamke atabaki na watoto wake wewe utabaki na malaya wako

They love being single mothers?[emoji848]
 
[emoji38][emoji38][emoji38] sasa kama unakuja na gia za kihuni kwanini usiulizwe hata sisi tunajuaga mwanaume serious

Hivi unakuta mtu anakutafuta halafu yupo kihuni si lazima uhoji
Hakuna Cha gia za kihuni, utakuta kukufata kistaarabu, ila sababu humtaki tu huyo mwanaume, kumkomoa ndo unamuuliza namba yako ametoa wapi mamamzungu
 
Mwanaume timamu akifika 30 tu bila mtoto akili inamcheza labda useme kupagawa kunatofautiana mwanamke anapagawa sana ila hakuna binadamu ambae akili haimchezi
Sure huwezi kuwa mwanaume mwenye akili timamu na uko sawa kiafya ufike 40 huna mke huna watoto.

Unakuwa jamaa la hovyo.
 
Na mimi bado dakika kadhaa niiguse 30, sina ndoa, sina mtoto, sina demu wa maana huu mwaka nimedhamiria kumzalisha mtu aisee maana sio poa....
Hauko peke yako Mkuu....si kila familia Ni za kuunganisha nazo damu unapozaa Na MTU unakua umunganisha Damu Na yeye kupitia mtoto.......ni vyema upate watoto Na Mtu sahihi mkishaoana
 
March 07 2024 naingia third floor nipo Ingolstadt Ujerumani currently nafanya Masters in Indutrial E gineering and Management na ninafanya kazi Kiwanda cha matairi cha Continental. Sijaoa wala sina mke huku lakini nimepata demu wa kijerumani kutokana na jitihada zabgu za kufanya kazi .Lakini sijui kama nitamwoa namfikiria. Nategemea kumaliza hii masters mwezi wa kumi maana nilianza mwaka jana mwezi wa tatu. NImejifunza mengi nataka nifanye kazi mwaka mmoja baada ya kumaliza hii masters nije kupiga hela nyumbani.
Hela zipi ?
 
Back
Top Bottom