Je, uliwahi kuwa maarufu shuleni?

Endapo ndiyo. Ni kitu gani kilikupa umaarufu?
Nilipata umaarufu shuleni kwangu baada ya kushinda mashindano ya uandishi wa barua Zanzibar mzima mwaka 2004 nilipokuwa darasa la saba nilikuwa mshindi wa mwanzo kwa primary kwa shule zote na zawadi tuliitwa kwenda kuchukulia posta ya kijangwani, kwakweli nilitokea kujulikana sana kwa wanafunzi na walimu.

Nilipoingia secondary nilifanya tena mashindano kama hayo ya mwanzo mwaka 2006 baada ya kupata taarifa ya mashindano hapa sikutokea mshindi wa mwanzo lakini nilipata zawadi za ushiriki.

Kwakweli kila pakiletwa taarifa kama hiyo shuleni nikielezwa na kushiriki mpaka nilimaliza mbanda.

Umaarufu wangu ulikuja kwa mtindo huwo na mwengine kwa uchoraji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KITU kilichonipa umaarufu O-LEVEL nilipendwa na mtoto mkali kuliko wote shule nzima (baba yake alikua mhindi mama yake muarabu), walimu, mabishoo, ma genius wa shule wote walimuimbisha dogo lakini dogo aligoma akawa ananielewa mimi tu,, (Pitia ID yangu kuna uzi nimesimulia kisa hiki unaitwa "KOSA LANGU")

Kilichonipa umaarufu baada ya kupendwa na uyu mtoto mkali, ni kwamba nilikua domo zege, dogo alijilengesha lakini wapi mzee sina habari, jamaa yangu alikua anakula rafiki yake, wote wanajadili pamoja na demu mwenyewe jinsi gani niwe na mtoto lakini wapi, mzee sina habari kichwani mwangu nilikua naiwaza man u, mpira na kutumikia altare kupiga chetezo.. .

Sasa siku moja katika harakati za hapa na pale skuli natembea mara paah mtoto uyu hapa anakuja mbele yangu, mimi ni nani bwana mpaka nikutane nae, mzee uyo nikakunja njia kwenda ofisi ya waalimu ile kuingia tu ndani nikakuta kupo kimyaa kumbe kulikua na kikao, ticha mmoja akaniuliza eenh vipi? mi lile wenge nikasema mwalimu ABC kanituma chaki kumbe lile wenge yule ticha alikuepo mle ofisini sikumuona akasema we dogo mi si nipo hapa.

Basi ticha alokua anafukuzia yule dg na anajua mi ndio kikwazo akadakia show wazee fimbo nilizochezea pale kama ingekua ni mtaji basi leo hii ningekua milionea, nilivopigwa nikajua kesi imeisha kumbe wapi bwana kesho yake parade yule ticha akaja kaniita kama wewe ni kijana upo kidato cha nne na kuna demu unamuogopa yupo kidato cha kwanza njoo hapa mbele utoe morning speech, mzee nikakaza wapi ticha kanifuata kanishika mkono mpaka pale mbele akani dis kinoma afu akanipachika jina la Domo gundi, mwisho akanipa adhabu ya kutoa morning speech wiki nzima, na viranja walivokua wananiita Welcome domo gundi ilifanya niwe maarufu sana shule nzima

Ilikua mwaka 2010 au 11 kitu kama hicho, Leo hii uyo dada ni best yangu sana sema kila tuki chat ananitania sana, mwisho wa siku tumebaki kua marafiki wakubwa na mimi niliishia kua mpenzi mtazamaji lakini maarufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahahaha nimecheka kweli

Pole sana domo gundi
Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mkuu umetoa ukweli mchungu!

Always history ni heavily biased!
 
Vyote nilivisahau huko ngoja nikavirudie labda nitafanikiwa kutikisa tena

Sent using Jamii Forums mobile app

Shule ya msingi tulikuwa tunapenda kusimuliana nani mzuri wa shule, na mkienda kutembea shule hiyo mpaka mumwone.

Shuleni kwetu mzuri wetu alikuwa mchumba wangu na muda mwingi tuko naye, kwa hiyo nikapatia kaumaarufu kupitia hapo.

Mpaka maticha wananionea wivu.
 
Hahahaha
 



Sent using Jamii Forums mobile app
 
nilikuwa maarufu chuoni, mwaka wapili nilikuwa kwenye piki ya umaarufu hata mtoto wa certificate ukimuuliza fulani unamfahau napatikana a.k.a yangu ilikuwa inafahamika hadi nikawa naandika kenye daftari zangu zote had past paper, jina langu nikasahau ........maisha bana yaachekama yalivo
 
Mkuu umetoa ukweli mchungu!

Always history ni heavily biased!

Nilimwelewa sana jamaa, ilikuwa kuhusiana na bible, jinsi walivyochagua Gospels na vitabu vyote vya kuingia kwenye Bible.

Na ndipo arguments za kwa nini Vatican wamezuia baadhi ya kitabu au vingine vinakuwa destroyed. Nadhani ni kwenye vitabu vya Dan Brown, sina uhakika na title.
 
Me nakumbuka nikiwa secondary nilipata umaharufu
Ilikua ni siku ya ukaguzi pared me ndo nilkua mchafu shule nzima siku hiyo wakanipa bakora za kutosha
Nikapewa jina la tozi mchafu maana mtaan nikua tozi but shulen mchafu
Huo umaarufu ulinipa mtoto mmoja wa 4m 2 mzuri kinoma mpk form wanaume wakanionea wivu 2012 hyo niko 4m3

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umaarufu wangu ulitokana na kushika nafasi za mwisho mara kwa mara na hatimaye
kupindua meza darasa la sita na kushika nafasi ya 1 , La saba term zote nafasi 1 mtihani wa
kata ya 1 Wilaya wa 5 Mkoa nikashika no 2 tukifungana watu Wawili yule aliyeshika no
1 alifariki kabla ya mtihani wa Taifa hivyo alituachia nafasi yetu ya kuongoza mimi na yule binti
ambaye nasikitika NAYE alifariki kwa ajali ya gari Wakati akielekea shuleni Kilakala MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA.
 
Safi sana
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha primary kulikuwa na kitabu cha kiswahili chenye story ya mwanafunzi mchafu aliyeitwa cholo. Sasa kuna jamaa mmoja classmate siku yanukaguzi wa usafi alikuwa mchafu balaa. mwalimu akamwita mbele kisha akampa jina la cholo. Hadi leo tumamwitaga cholo.
 

Pole kwa kupoteza washindani mkuu.

Mimi nimepindua meza kuanzia std 5 baada ya shuleni kuhamia mchuchu nikawa nimejikabidhi, kwa hiyo nikaanza kusoma ili niwe namfundisha mimi tu. Nikashangaa kumbe vitu ni virahisi.

Ikawa kila kitu naulizwa mimi, mpaka darasani wanashangaa huyu kilaza ndo kawa mkali hivi.

Nakumbuka kata yetu ilikuwa na shule 5 mock ya kwanza nikawafunika, yule mtoto ananikumbatia mpaka nikaona aibu. Jina likabandikwa shule zote wale top 10.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…