Je, umewahi kujiuliza kuhusu ukimya wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na uuzwaji wa Bandari za Tanganyika?

Je, umewahi kujiuliza kuhusu ukimya wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na uuzwaji wa Bandari za Tanganyika?

Ni kweli Kuna mushkeli
-Kwani huyu Hamza Johari,yupo Ofisi ya Mwenasheria Mkuu? Au
-Kama hayupo ofisi ya Mwanasheria Mkuu Kwa nini alichaguliwa kuwa MwenyeKiti wa timu ya majadiliano badala ya Mkuu wa kitengo cha Mikataba ya kimataifa baina ya nchi mbili ambaye yupo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu?
-Kwa kutomshirikisha Mwanasheria Mkuu, ambaye ametamkwa kwenye Katiba JMT,na kuwekwa Mwanasheria Mwingine,katiba yetu,haijavunjwa? -Mwanasheria Mkuu wa Serikali/Mwakilishi wake,hakupaswa kuhudhuria tukio la uwekwaji sahihi kwenye hiyo MOU huko Dubai?
-Mwakilishi wa Mwanasheria Mkuu ni miongoni mwa wajumbe wa timu ya majadiliano?

Ushauri:
-Mamlaka husika itoe ufafanuzi wa maswali mengi ya wananchi.
- Wahusika wajitafakari na wachukue maamuzi sahihi,haijakaa vizuri.
 
Watz wapo macho na wanajua wanachokitaka
Hao wanaotoa mchango kwamba mkataba unamapungufu makubwa ni Watz pia na wana haki ya kusikilizwa. Au kwa upande wako hao Watz unaosema wako macho wana haki kuzidi wangine?
 
Katika kichwa chako cha habari ondoa neno "UUZWAJI" Hakuna bandari inayouzwa unachofanya ni uchonganishi kwa umma.
Kukubaliwa Kumiliki kitu kwa muda usiojulikana ni maana yake nini? Kumbuka wanaosema wapewe hao wawekezaji wapya wana zungumzia kupata mapata ya fedha maradufu ya sasa. Kwa hiyo, in away Kuna exchange of right katika misingi ya fedha.

Kama hiyo ngumu, Sawa wamepewa na hawatanyang'anywa hiyo bandari!
 
nenda kwenye hoja tafadhali madalali wa mali rasilimali za mama Tanganyika, jifunze kwanza namna ya kutumia neno majungu, kama kiwahili ni shida utaweza mkataba tata ulioandikwa kwa legal jagon, ulioandikwa kidhungu na kisheria? , habari ya kuuzwa nilishaijibu sirudii, Mimi ni Mtanganyika, period, kaa na profesa wako haniusu.
Hakuna hoja wala hakuna madalali na wala hakuna Tanganyika kwa sababu ilishazikwa. Lete mjadala wenye tija kwa taifa letu la Tanzania. Umeelewa wee mjombaake Mwanyiru wa Panda hill?
 
achana nae bado anadhani, akiwa tayari atatujibu
Sasa ajibu nini wakati mambo yote yako shwari hakuna cha kuuzwa bandari wala boti? Wanaosema kuna mauzo ya bandari ni wanufaikaji wa mfumo wa hovyo wa sasa na wanaogopa mwarabu akiwekeza mpunga wa kutosha na akanyoosha administration basi watakosa makombo waliyokuwa wakiambulia.
 
Kama kwenye ule mjadala wa juzi sikuona chochote cha maana alichosema Rostam, heri kutila mkumbo ni mwanasiasa, lakini Rostam hakustahili kuwa pale , aheri wangemuweka lema au zitto.
Hv kuwa na hela ni kuwa na AKILI Nchi ina Watu wapumbavu sana hii,hata wezi wana hela lkn sio lazima wawe na Akili,mnamwita rostam kwenye mjadala kweli?
 
Hv kuwa na hela ni kuwa na AKILI Nchi ina Watu wapumbavu sana hii,hata wezi wana hela lkn sio lazima wawe na Akili,mnamwita rostam kwenye mjadala kweli?
Rostam ni mtaalaam nguli wa mijadala kama hii yenye mrengo wa kibiashara. Hawezi kuachwa kando. Hoja nyingine tafadhali!
 
Back
Top Bottom